Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 2,833
- 1,301
MBUNGE DUNSTAN KITANDULA - HEKIMA ZA VIONGOZI WETU ZILITUMIKA DHIDI YA MGOGORO
"Naiomba serikali yangu itusikie, walisaini document ya makubaliano lakini baada ya makubaliano hayo Bado kumekuwa na chokochoko za jeshi la ulinzi la Kenya kuingia kwenye maeneo yetu lakini wananchi wetu walipoingia walikamatwa baharini wakaenda kufunguliwa kesi na kutaifishwa Mali zao" - Mhe. Dunstan Kitandula, Mbunge wa Mkinga.
"Tusiache kuchukua hatua watu wetu badala ya kwenda kuhukumiwa Kenya ikafika mahali vyombo vyao vikazamishwa baharini tukapoteza maisha ya watu" - Mhe. Dunstan Kitandula, Mbunge wa Mkinga.
"Changamoto ya mpaka wa Tanzania na Kenya, wenzetu wa vyombo vya ulinzi Kenya wanafika mpaka maeneo ya ndani ya Kijiji chetu wakiwa na silaha kama isingekuwa hekima za viongozi wetu tungeingia kwenye migogoro" - Mhe. Dunstan Kitandula, Mbunge wa Mkinga.