Nyani Ngabu umenitafutia ugomvi. Asubuhi hii utasikia watakavyoshuka na hoja za UKAWA, si hoja zinavyozungumzwa.
Tumeyasema sana, bahati nzuri Lissu ameyazungumzia kwa undani na ametuelewa
Tatizo letu hatutaangalia kiini na umakini wa hoja au upotofu, utasikia tu mvua za matusi na kejeli
Nikushukuru sana kwa clip ingawa imekatika wakati wa swali la mkuu wa Wilaya.
Kama una mwendelezo wake tupia hapa tena, ni mahala pake haswa
Lakini pia ninalazimika kuahirisha mjadala wa wizara ya madini na nishati kwasababu Lissu keshayasema ! kwik kwik!
Tulitaka tuonyeshe majukumu ya wizara na inaundwaje na akina nani.
Tuzungumzie mamlaka ya Bunge na jinsi yalivyodharauliwa.
Hilo linaonyesha mfumo ulivyo mbovu
Kwa fikra kidogo, hivi Rais aliyekuwa katika Bunge na Cabinet wakati suala la escrow linazungumzwa, na bunge kutoa maazimio, leo anawezaje kwenda kinyume na yale yaliyotendeka?
Rais aliyeondoka na aliyepo wanatoka chama na baraza lile lile la mawaziri
Tunapata ujumbe gani kuhusu uteuzi uliofanyika wa kurudisha waliotuhumiwa?
Kwamba, walionewa? Au bunge lilikosea? Au Rais aliyepita hakulitazama suala kwa undani! au inakuwaje!
Tatizo ni nini, watu au mfumo?
Endapo mfumo ungekuwa sawa, kuna mawili.
Moja ungejieleza wenyewe, pili, sisi majuha tusingekuwa na maswali.
Mfano aliotoa Lissu wa sheria ya wahujumu kuandikwa baada ya kutekelezwa hata wiki hii umetokea. Kwamba, marufuku ya kwenda matibabu imewekwa baada ya ''mzee''kusema 'ameumwa uchovu''
Uvunjaji nyumba umesitishwa kwasababu mfumo unatoa haki kwa wote, aliyevunjiwa na aliyevunja.
Kwa mfano, lile hekalu Mbezi kumbe kuna afisa aliingia makubaliano kinyemela bila serikali kujua.
Hivi kwa hili hatuoni tatizo kweli. Kwamba mtu anaweza kuingia makubaliano kwa niaba ya nchi na nchi isijue! Real bado hatuoni tatizo hapo, tunashangilia tu!
Watatuelewa siku moja na kujutia nafsi zao! Watatukana, kejeli n.k. hatutabadilisha maono.
Tuna maono ya keshokutwa, itakapowafikia wataungana nasi
Ahsante sana kwa video