Nguruvi3
Platinum Member
- Jun 21, 2010
- 15,773
- 32,431
- Thread starter
- #121
Sehemu ya II
NCHI ZA WENZETU
Katika nchi za wenzetu , raia hawekwi chini ya ulinzi bila sababu za kufanya hivyo
Na anapowekwa katika ulinzi, kwa muda uliopangwa lazima asomewe mashtaka.
Hairuhusiwi kumkamata mtu bila kumweleza kwanini.
Ikitokea ni weekend au sikukuu, mtuhumiwa atasomewa mashtaka kwa muda uliowekwa.
Isipofanyika hivyo, mtuhumiwa anaachiwa huru. Haki ya dhamana ni ya hakimu
Mwendesha mashtaka ana nafasi kuzuia/kutozuia dhamana kama ilivyo kwa mshtakiwa.Mwamuzi ni hakimu au jaji anayesimamia shauri
KWA TANZANIA
Sheria tulizorithi kwa kiwango zinashabihiana na za mataifa
Inashangaza, mambo yanatendeka kana kwamba sheria ni mali za watu
Kukamata watu limekuwa jambo la maguvu sila kisheria
Imetokea karibuni kiongozi/mwanasheria alipotakiwa kuandamana na polisi.
Alipohoji ipo wapi hati ya kukamatwa, askari hawakuwa na jibu la kisheria
'Sisi tumetumwa' si jibu, kumnyang'anya mtu uhuru ni ukiukaji wa haki za mtuhumiwa
Lakini pia inawezekana kumfikishia mtu ujumbe afike kituo cha Polisi kama anahitajika
Kinachotokea, ni mtu kuitwa kwa mahojiano, kisha mahubusu.
Wapo wanaokamatwa ijumaa ilimradi tu wakalale mahabusu hadi jumatatu mahakama, kwingineko duniani shtaka litasomwa siku yoyote 'ndani ya muda uliowekwa kisheria'
Hapa ieleweke, kuambiwa tuhuma na polisi si sawa na kusomewa mashtaka kwa hakimu
Tunaona mbinu zinatumika kuhakikisha mtu analala mahabusu kama adhabu kabla ya sheria haijachukua mkondo wake
Watu kama waziri, mbunge au wana taaluma wanadhamana katika jamii 'public trust' lakini pia ni public figure
Ndiyo maana wana uwezo wa kutoa dhamana au kujidhamini kulingana na tuhuma
Wito ukitolewa,mhusika kufika anapotakiwa, kuna sababu gani za kumweka mahabusu?
Wapo wanaoambatana na wanasheria, nini kinachosukuma kuwaweka mahabusu?
Na hapa tunaongelea tuhuma au makosa yasiyo na athari za mara moja kwa jamii, usalama au amani.
NCHI ZA WENZETU
Katika nchi za wenzetu , raia hawekwi chini ya ulinzi bila sababu za kufanya hivyo
Na anapowekwa katika ulinzi, kwa muda uliopangwa lazima asomewe mashtaka.
Hairuhusiwi kumkamata mtu bila kumweleza kwanini.
Ikitokea ni weekend au sikukuu, mtuhumiwa atasomewa mashtaka kwa muda uliowekwa.
Isipofanyika hivyo, mtuhumiwa anaachiwa huru. Haki ya dhamana ni ya hakimu
Mwendesha mashtaka ana nafasi kuzuia/kutozuia dhamana kama ilivyo kwa mshtakiwa.Mwamuzi ni hakimu au jaji anayesimamia shauri
KWA TANZANIA
Sheria tulizorithi kwa kiwango zinashabihiana na za mataifa
Inashangaza, mambo yanatendeka kana kwamba sheria ni mali za watu
Kukamata watu limekuwa jambo la maguvu sila kisheria
Imetokea karibuni kiongozi/mwanasheria alipotakiwa kuandamana na polisi.
Alipohoji ipo wapi hati ya kukamatwa, askari hawakuwa na jibu la kisheria
'Sisi tumetumwa' si jibu, kumnyang'anya mtu uhuru ni ukiukaji wa haki za mtuhumiwa
Lakini pia inawezekana kumfikishia mtu ujumbe afike kituo cha Polisi kama anahitajika
Kinachotokea, ni mtu kuitwa kwa mahojiano, kisha mahubusu.
Wapo wanaokamatwa ijumaa ilimradi tu wakalale mahabusu hadi jumatatu mahakama, kwingineko duniani shtaka litasomwa siku yoyote 'ndani ya muda uliowekwa kisheria'
Hapa ieleweke, kuambiwa tuhuma na polisi si sawa na kusomewa mashtaka kwa hakimu
Tunaona mbinu zinatumika kuhakikisha mtu analala mahabusu kama adhabu kabla ya sheria haijachukua mkondo wake
Watu kama waziri, mbunge au wana taaluma wanadhamana katika jamii 'public trust' lakini pia ni public figure
Ndiyo maana wana uwezo wa kutoa dhamana au kujidhamini kulingana na tuhuma
Wito ukitolewa,mhusika kufika anapotakiwa, kuna sababu gani za kumweka mahabusu?
Wapo wanaoambatana na wanasheria, nini kinachosukuma kuwaweka mahabusu?
Na hapa tunaongelea tuhuma au makosa yasiyo na athari za mara moja kwa jamii, usalama au amani.