Duru za siasa: Chama cha ACT-Wazalendo Mpini wa CCM kumaliza upinzani(?)

Naona umekuja na lawama na malalamiko mengi mwisho umeweka kipande cha hotuba ya Zitto aliyoitoa Tabora kupitia YouTube Channel ten.

Hata wewe jukumu lako pia kuleta hotuba za Zitto hapa ukumbini au mwanaukumbi yoyote anayo nafasi ya kufanya hivyo siyo mimi tu.

Sijui kwa nini umeamua kumtaja Ritz peke yake au ndiyo wale wale wanaumia na ninachokiandika.

Unasema utetezi wangu unatia shaka halafu hapo hapo unasema nikuletee hotuba za Zitto aalaah!!

Kwa faida ya Wanaukumbi vunja hoja yangu ya utetezi wenye shaka kwa kuweka hizo hotuba ambazo hazina shaka ndani yake ili kukata mzizi wa fitna.
 
Last edited by a moderator:

1. Kumbe ushauri huu ukuuona !!

Yaani tupate ama audio ama video ya hotuba zote za SL pamoja na za wasaidizi wake walipokuwa ziarani na chama chao cha ACT na kuziweka hapa kwa mjadala mpana na rahisi (maana referencez itakuwa karibu) wa ACT kuwa mpini wa CCM na pia mpini wa kuligawa taifa katika misingi ya kibaguzi. Aliwahi kufanya hivyo Nguruvi3 kwenye mjadala wa Wazanzibar na haki ya kuwa taifa huru ! .

Mfano: kwenye clip hiyo niliyoweka ukianzia dk 1:49 mpaka 2.07 M/kiti ACT anasema...
" ....Tangu tupate uhuru chini yake, tulikuwa tunaheshimika duniani..." kwangu hii kauli ni tata, mwenyekiti anamaanisha watanzania tulikuwa tunaheshimika wakati tukitawaliwa na wakoloni...!?
anaongeza kusema " Watanzania wa leo tumebaki makundi tumejigawa kidini, tumejigawa kihali, kibiashara, kisiasa..." hii pia ni tata. Na utata huu unatokana na kutopata hotuba nzima. Tungepata hotuba nzima tungepunguza hata upotoshwaji wa aina yoyote.

2. Ni kweli...! Ni jukumu letu sote. Upendeleo uliopewa wa kutajwa kwa ajili/ajiri ya kuleta hapa hotuba umetokana na ujasiri wako wa kuleta sehemu ya hotuba za wanasiasia mbali mbali kwenye uzi huu kwa mtindo wa " msome kiduchu" fulani. Ukweli hili nijukumu letu sote, ndiyo maana hata mimi nimeleta hotuba za SL na M/kiti wa ACT kwa mtindo wa "mtazame na kumsikiliza kiduchu" kwenye video/clip hii.

3. Yawezekana Umejijua

4. Nimeshauri utuletee zilizokamilika/kwa kirefu tena audio ama video. Usilete zinazofanana na hizi zinazopinga na za mwenzako Adharusi. Alinda anatufahamisha kuwa umeleta 'edited version' ya andishi la SL kutoka facebook wall yake.

5. Uwezo huo sina kwa sasa ndiyo maana nimewashirikisha wana JF tuzitafute.
 
TUJITEGEMEE.

Ritz na Adharusi wamejitahidi pia kumtetea SL kuwa kauli yake haina madhara kwa kutumia namna mbalimbali za kiuandishi huku wakileta rejea zinazopishana kiasi cha kutilia shaka utetezi wao kwa SL.


Hayo maneno yako hata nikileta utaishia kuniambia hivyo bora walete wengine unaowaamini, lakini zile kauli za kusingiziwa Zitto kwa kasema Kilimanjaro na Arusha wanainyonya Shinyanga kwako haikuwa mashaka daah!! Mahaba bana.

Mkuu najua haupendezwi na michango yangu naomba univumilie tu na jifunze kusoma vitu usivyovipenda pia itakusaidia kuchangamsha fikra zako.

Ahsante.
 
Last edited by a moderator:
....hata nikileta utaishia kuniambia hivyo bora walete wengine unaowaamini,....

Mkuu, Nina amini Uzi huu haujaanzishwa ili kumuonea mtu (kama alivyowahi kueleze kwa kina Nguruvi3 kwenye post zilizotangulia). Nguruvi3 anasema 'Chama cha ACT-kuwa Mpini wa CCM kuumaliza upinzani' kutokana na uchambuzi alioufanya. Wakati mjadala ukiendelea inaibuka 'sub' hoja ya kuligawa taifa letu kwa misingi ya kibaguzi (kutokana hotuba ya SL) akiwa maeneo ya kanda ya Ziwa. Uzi huu umerefuka mno kutokana na 'sub'hoja hii ya SL kuligawa Taifa kwa msingi wa kibaguzi. Hoja na 'sub'hoja zikiendelea kujadiliwa unajitokeza wewe (Ritz) kwa ujasiri na ari kumtetea SL. Utetezi wako unauleta kwa kwa mtindo wa 'msome kiduchu'. Msome kiduchu hiyo inaonekana kutokidhi matakwa ya utetezi wako kwani utaitilafiana na ule wa mtetezi mwenzio. Ilipia linazidi kukolezwa maana imegundulika (kwa mujibu wa Alinda) kuwa unaleta hotuba zilizo haririwa wali siyo halisi.

Sasa ili kuondoa kadhi hii ya kuleta hotuba zilizohaririwa (zinazotia mashaka), ninaomba mwanaJF yeyote anayeweza kutupatia 'hotuba' halisi (from antithetical source). Yaani ziletwe audio ama video. Nikatoa na mfano wa kile ninachosahuri kufanywa .

Nimeshauri hivyo ili tupate ukweli kuwa je ."Chama cha ACT-kuwa Mpini wa CCM kuumaliza upinzani?" na Je kauli za SL na wenzake huko kanda ya ziwa na kwingineo (ambazo zimezaa 'sub'hoja kwenye uzi huu ) zinalenga kuligawa taifa letu?

Ninakuomba Mkuu Ritz usisue kuleta hotuba kutoka kwa SL na wenzake (katika mfumo nilioeleza) ili iwe rahisi kwa watanzania na wengine kupata ukweli wa hoja iliyoko mezani (Chama cha ACT-kuwa Mpini wa CCM kuumaliza upinzani) na 'sub'hoja (kuligawa taifa kwa misingi ya kibaguzi) iliyotokana na kauli ya SL.

Ni ukweli tu utakao tuweka huru na utakao tuwezesha kuondoa 'sintofahamu'. Kwa uadilifu na nia njema ya kuepusha taifa hili na majanga yanayozuilika, Ndugu (Mkuu) Ritz tushirikiane kuutafuta ukweli wa hoja na subhoja hizo hapo juu
 
Ritz,

Shukran sana sasa sina sababu ya kuendelea na ubishi huu baada ya kutazama bandiko lako na Adharusi kuwa sawa kabisa japo Adharusi kachukua vipande vipande. Tazama sehemu nilizo highlight.. Ama kweli nimeamini watu wamepania kumharibia jina kwa sababu wewe umetoa hotuba kamili, Adharusi kazungumzia wapi takwimu zake zinapatikana maana waliuliza Zitto kazipata wapi kwa sababu hawakuamini. sasa wamepewa bado wamekazania kipande ambacho hakipo ktk hotuba yake.. iweje wewe na Adharusi ndio muwe na hotuba lakini hawa jamaa na madai yao hawana hotuba hiyo? Kumbe alicholinganisha Zitto ni mkoa wa Lindi na Shinyanga sio kama walivyodai eeeh...

Hotuba ya zitto uloitoa wewe;-

" Tanga ni ya 8 katika kuchangia Pato la Taifa. Pia ni mkoa wa 8 kwa kiwango cha maendeleo ya watu wake.Mikoa yenye Maendeleo zaidi ni Arusha, Kilimanjaro na Dar es Salaam. Hata hivyo Kilimanjaro ni ya 9 katika kuchangia Pato la Taifa na Arusha ni ya 7.Mikoa iliyo nyuma zaidi kimaendeleo nchini ni Kigoma, Singida, Dodoma, Kagera na Tabora. Hata hivyo Tabora ni mkoa wa 10 kwa kuchangia katika Pato la Taifa na Kagera ni mkoa wa 11 katika GDP.Mikoa yenye mchango mdogo zaidi kwenye Pato la Taifa ni Pwani (1.85%), Lindi (1.89%) na Singida (1.92%). Hata hivyo Lindi inashika nafasi ya 9 kwa Maendeleo, juu ya Shinyanga inayochangia 6% katika GDP. Dar inaongoza kwa kuchangia Pato la Taifa ambapo mchango wake kwenye pato la Taifa ni 16.9%. Inafuatiwa na Mwanza [kabla haijagawanywa] 9.2%, Mbeya 7.3%, Shinyanga 6% na Iringa 5.3%. Hata hivyo Shinyanga ni mmoja wa mikoa yenye umasikini wa kutupwa licha ya kuwa namba 4 katika kuchangia Pato la Taifa.Ndio maana ni lazima kubomoa mfumo wa sasa wa uchumi. Huwezi kuwa na mkoa unashika namba 5 kuchangia Pato la Taifa lakini unashika namba 16 kati ya mikoa 21 kwa maendeleo ya watu. Shinyanga ina migodi 2 ya dhahabu na migodi 2 ya Almasi. Shinyanga ina Ng'ombe na Pamba. Shinyanga tarehe 17 Aprili, tujadiliane jinsi ya kufanya mapinduzi ya kiuchumi mkoani mwenu.'

Alichoandika Adharusi:-

Nanukuu maelezo ya Zitto

"Dar inaongoza kwa kuchangia pato la Taifa
-16.9% Dar
-9.2% Mwanza kabla haijagawanya
-7.3%. Mbeya
-6%. Shinyanga
-5.3% Iringa

Hata hivyo Shinyanga ni moja ya mikoa yenye Umaskini wa kutupwa licha ya kuwa namba 4 katika kuchangia pato la Taifa,pia akasema Mikoa yenye Maendeleo Zaidi ni Arusha,Kilimanjaro na Dar es salaam.

Hata hivyo Kilimanjaro ni ya 9 katika kuchangia Pato la Taifa na Arusha ni ya 7 kuchangia Pato la Taifa.


" Zitto akasisitiza ndio mana ni lazima kubomoa mfumo wa sasa wa uchumi,huwezi kuwa na mkoa unashika nafasi ya 4 kuchangia Pato la Taifa lakini unashika namna 16 kati ya mikoa 21 kwa maendeleo ya watu,Shinyanga ina migodi 2 ya dhahabu na migodi 2 ya Almasi,ina Ng'ombe na Pamba.

Tunavita moja tu,kufanya Mapinduzi ya mfumowetu was uchumi kutoka mfumo wa kinyonyaji na kifisadi na kujenga uchumi shirikishi.

Zitto aligusia Takwimu za watu wenye elimu ya sekondari simiyu ni 3.7%, na Dar ni 29% inaongoza nchi mzima(THDR2014)
 
Ahsante, kwa taarifa ya wasomaji naomba mupuuze hiyo o hotuba ya Ritz. Ni uongo tu hakuna ukweli

1. Kwanza hakusikiliza Redio free Afrika(ushihidi upo)
2. Amesoma kipande cha hotuba hiyo May 13 hapa Duru(ushahidi upo)
3. Amebadili maneno ya hotuba iliyoletwa na mkereketwa mwenzake kwasababu ina maneno machungu(ushahidi upo)
4. Hakusoma hotuba kutoka JF, uzi upo hauna hotuba wala Riza hakuchangia (ushahidi upo)
5. Alikiri kutojua Zitto kasema nini hapa duru May 13 2015, wiki tatu baada ya su[reme leader kumwaga sumu


Kama mnafuatilia mjadala huu, kuanzia mwanzo watu wamempuuza Rutz kila alipoandika.
Tunaomba watu warejee kwenye mambo ya maana

Lengo la kutaka kuondoa watu katika mjadala kwa hoja zisizo na msingi limeanza muda mrefu
Ku entertain hoja kama hizi ni kuvuruga mjadala. Tunaomba watu waachane na ubabbaishaji unaondelea

Tunaomba mjadala uendelee

ACT MPINI WA KUMALIZA UPINZANI
 

Naona unajaribu kupindisha hoja..

Kwanza kama kumbukumbu zangu ziko sahihi hakuna mtu hata mmoja aliyeulizia sehemu alikozipata takwimu..

Pili kinachojadiliwa toka mwanzo ni hoja ya MAENDELEO VS UCHANGIAJI WA PATO LA TAIFA

Tatu. wewe ndo ulipindisha mjadala na kusema "Si kosa la Zitto kusema Shinyanga wanachangia sana lakini hawapati stahiki sahihi,

Nne: Hizo ni hotuba mbili zinazofanana lakini zenye maudhui tofauti.. Wakati ya Ritz ikilenga taifa zima ya Adharusi inalenga mkoa wa Shinyanga Vs Arusha na Kilimanjaro.. Na kudhibitisha hilo ni hizi sentensi

"Hata hivyo Shinyanga ni moja ya mikoa yenye Umaskini wa kutupwa licha ya kuwa namba 4 katika kuchangia pato la Taifa,pia akasema Mikoa yenye Maendeleo Zaidi ni Arusha,Kilimanjaro na Dar es salaam.
Hata hivyo Kilimanjaro ni ya 9 katika kuchangia Pato la Taifa na Arusha ni ya 7 kuchangia Pato la Taifa.

(toa hilo neno pia akasema)

Unapata hiki, na ndicho alichokuwa ameandika katika Fb yake kabla ya kufanya "editing"

"Hata hivyo Shinyanga ni moja ya mikoa yenye Umaskini wa kutupwa licha ya kuwa namba 4 katika kuchangia pato la Taifa,Mikoa yenye Maendeleo Zaidi ni Arusha,Kilimanjaro na Dar es salaam.
Hata hivyo Kilimanjaro ni ya 9 katika kuchangia Pato la Taifa na Arusha ni ya 7 kuchangia Pato la Taifa.


Na hiki ndicho tunachojadili.. Na ninauliza ni kwanini katika hotuba nzima alichomoa hicho kipengele chenye mikoa ya Arusha/Kili vs Shinyanga??
 
Alinda , huyu anataka kutuondoa katika mada, naomba apuuzwe

Tunajadili kauli za Zitto kuanzia tarehe 5 hadi Sihinyanga. Yeye anasema tunajadili kauli ya Mwanza

Nakuhakikishia Ritz hakujua kinachoendelea hadi tarehe 13 may alipokiri mwenyewe kuwa hajui

Kusema alisoma hotuba, alisikiliza au alijadili ni ubabaishaji tu.



Naomba apuuzwe jamani, tuna mengi ya maana ya kujadili. Alipuuzwea sana huko nyuma na sasa apuuzwe tu
 
Bibie nina kumbukumbu nzuri tu za mjadala huu kwa sababu ilifikia tukajiuliza sababu ya Zitto kusema Shinyanga inachangia kuliko Kilimanjaro na Arusha kapata wapi takwimu. Mchambuzi akaja na za TRA kiasi hata mimi nikasema kama ndivyo itabidi tumuulize Zitto mwenyewe. Hata mimi sikuelewa lengo lake ilikuwa nini unakumbuka?

Mjadala ukaendelea, na ndipo Adharusi akaja kusema Zitto kazitoa HDR repoti ya mwaka 2014, ikawa ubishimwingine ambao umechukua sura hii, nami nikasema kama ndivyo hakuna ubaya maana kiongozi yeyote wa siasa lazima awe na vigezo kama hivi. JokaKuu akapinga akisema sawa unaweza tumia vigezo, lakini Zitto kuzitaja Kilimanjaro na Arusha alikuwa na sababu zake za kibaguzi. Au nakosea?..

Nilipochukua muda kuwasoma wote Ritz na Adharusi, nikaona maelezo yao yanafanana kabisa isipokuwa Adharusi kachukua sehemu zinazohusiana na mjadala kuelezea wapi Zitto katoa takwimu hizo. Ikawa kosa jingine kwa Zitto kutumia takwimu za HDR sio zake na ndio nikauliza kwani Mchambuzi alipotumia za TRA ilikuwa kosa? mbona mimi sikuona kosa. Na kama mnaziona takwimu hizo sio sawa basi wa kulaumiwa ni HDR sio Zitto, maana watakuwa wao ndio wamedanganya.

Sasa ukweli tumeupata na nadhani itakuwa vizuri jamani mnyonge mnyongeni laini haki yake mpeni! Msibadilishe maneno na kumzulia mtu uongo ili tu kuhakikisha ACT haipati kukubaliwa Kilimanjaro na Arusha. Maelezo ya Adharusi umeyaona ni kwamba amechukua baadhi ya sehemu lakini mfululizo wa Hotuba kamili kautoa vizuri tu Ritz maana ukimsoma Adharusi utaona hoja hazifuatani sawa akitumia neno pia akasema ambalo ni ongezeo la mwandishi wa makala hiyo ktk kumbukumbu zake, not exactly Zitto alivyosema, ni kiswahili rahisi kabisa.
 

Sijaona kosa la Zitto hapo, yeye kaongea kwa Takwimu nyinyi mlitakiwa mumpinge kwa Takwimu na siyo hisia. Alichokifanya ni kutoa statistical comparison ya mikoa kwa mikoa.

Hata kama ni kuangalia motive yake, basi siyo rahisi Kumjengea hoja hasi kwa sababu amekuwa consistent katika mikutano yake kuelezea ugawanyaji mbovu wa keki ya Taifa kulinganisha na namna mikoa hiyo inavyochangia pato la Taifa.

Kuna watu wameamua kujitoa Ufahamu, wa kutwist kauli zake, kutake out of context maelezo yake ili kumfitinisha Zitto na Jamii. Lakini huu ni ujinga wa hali ya Juu, huwezi kupingana na Common sense.

Zitto anachokielezea kwenye takwimu hizi ni Ukweli mtupu kwamba Shinyanga inachangia Zaidi kuliko Kilimanjaro, na wala siyo scenario hiyo tu alishazungumzia na mikoa mingine pia kuwa katika setup hiyohiyo ya kuwa chini wakati wanachangia zaidi.

Mpingeni Zitto kwa Hoja na siyo Vihoja
 
Watu huwa wanakusetiri mimi sina stara na wewe kwasababu moja, mnafiki kazumngumzwa katika vitabu vya dini na kijamiii na njia nzuri ya kudeal na mnafiki ni kumwambia

Pitia uzi huu, https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...wanyo-rasilimali-za-taifa-6.html#post12518131

Ukishamaliza kusoma mabandiko kama 66 na 93 urudi


Kwanza, lazima uelewe, mjadla mzima umejikita kuanzia kauli za supreme leader, na hotuba zake

Kwa mwezi mzima umekuwa unajadili kule jukwaa la siasa na hapa duru.

Kam si upungufu ninaousema, leo unakuja na habari kuwa ulikuwa hujui kinazumzingimziwa nini.

Yaani unachangia tu hujui unatetea nini. Ndio kile nililicholuambia ukasema nimekutusi, hapana! hujatukanwa ndivyo ulivyo

Tatu, angalia maneno ya Adharusi, angali na hiyo unayosema hotuba.

Kama ungetumia sehemu kidogo sana ya fikra ungebaini matatizo makubwa

Hoja kubwa hapa ni kuwa Zitto ameleta mtafaruku mkubwa saba katika jamii

uzi huuhttps://www.jamiiforums.com/jukwaa-...wanyo-rasilimali-za-taifa-6.html#post12518131 Wtanzania wamesima bila kujali makabila, dini au itikadi zao za kisiasa kumlaani supreme leader kwa maandishi yake ya uchochezi na kuligawa taifa

Mkandara unafahamu hilo, lakini unabadili na kusema kuna watu wana chuki hapa duru.

Soma uzi mzima uone jinsi ulivyokuwa mwenyewe unampigani mhalifu peke yako miongoni mwa watanzania waliokuwa na akili zao

Tunakuambiwa wazi, mashambuliza ya zitto dhidi ya mikoa ya kaskazini na Tanzania hayakubaliki na hayatakubalika kama na watu wanaotumia akili.

Kazi yake ya kumailiza upinzani yeye na genge lake tumeibaini na tunaianika hapa

Kazi hiyo ni pamoja na ushirika wake na CCM ambao sasa anatumia ukanda kama mpini wa kumaliza upinzani

Supreme leader keshakula 'nyama ya mtu' dhambi ya migogoro inamwanadama.

Hatutakaa kimya akituleta mambo ya uhutu na utusi.
 
Mkuu sasa wewe ndio unazidi kutupotosha kabisa, fedha za TRA sio mchango wa Taifa ni sehemu tu kama vile tunapozungumzia Hotuba ya Zitto kaitaja mikoa mingi lakini watu mkanyofoa Mkoa wa Kilimanjaro kuweka hoja yenu. Hii tabia ya kunyofoa ili mjenge hoja ndio imepotosha maana, hata mimi niliingia mkenge huo kuamini mchango ulokuwa ukizungumziwa ni tax collections za kila mkoa.

Na kama unakumbuka nikasema ebu tujiulize kwanza hizo tax za Shinyanga na ruzuku ktk migodi yake hulipwa wapi? natazama katika hotuba ya Zitto inasema kumbe hulipwa Dar. Hapa ina maana hata wakazi wa Dar wanatakiwa wachukie hotuba hiyo kwa sababu anasema tax za Shinyanga hulipwa Dar!. Lakini je, kweli inatakiwa iwe hivyo? tazama Mtwara leo tax za gas zinalipwa pia Dar kweli utaweza vipikuwa na takwimu za ukweli tunapozungumzia mchango mikoa ktk mfuko wa Taifa?

Mimi nadhani lengo la mjadala huu uwe kutafuta solutions sio kulalamika maana jamani tumelalamika sana na kwa miaka mingi pasipo kuelewa mzizi wa umaskini wetu upo ktk mfumo mzima wa maendeleo. Tunapojenga hoja za maana inawasaidia hata wengine pia kuelewa mfumo mbovu uliopo na sio wa CCM wala Zitto bali Kikatiba. Haya maswala hayarekebishwi na itikadi wala sera za chama bali ni maswala ya Kisheria katika ukusanyaji wa kodi na uwezeshawaji wa mikoa kimamlaka. Hivyo madai ya Zitto kufumua mfumo mzima tulokuwa nao ni ya lazima iwe kwa vyama vyote muhimu sana watambue na wafikirie hivyo.
 
Takwimu za Zitto zinatoka katika Tanzania Human Development Report 2014(THDR 2014), Je za Mchambuzi zinatoka wapi?
 

Takwimu za Zitto zinatoka katika Tanzania Human Development Report 2014(THDR 2014), Je za Mchambuzi zinatoka wapi?
 
Umeingia basi tofauti. Huko unakosema kulimalizwa siku nyingi

Pili, kauli tunazopinga hapa ni za kuligawa taifa kwa kama alivyosema kuanzia April 5 hadi Shinyanga na Mwanza.

Msome Alinda, kaweka kauli za Zitto dhidi ya mikoa ya kasakazini.

Ukisoma mjadala mzima watu kama akina Mkandara wanatetea na kusema hichoni sawa sawa.

Kwamba Zitto kurudi shambulio dhidi ya mikoa ya kaskazini ni sahihi

Tumewaeleza kuwa hakuna mkoa uliopata maendeleo kwasababu ya mkoa mwingine, na wala hakuna mkoa uliodhulumiwa na mkoa mwingine.

Maneno makali ya Zitto dhidi ya Arusha/ Kilimananjaro ni hatari sana ndiyo tunayekemea hapa

Pitia uzi huu uone watu wazima wanavymkemeasupreme leader https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...wanyo-rasilimali-za-taifa-6.html#post12518131

Supreme leader anaendeleza ukanda na ukabila kazi aliyopewa na sasa anaifanya vema

Kwasasa siasa zimemzidi anachomeka siasa za uhutu na utusi.

supreme alipaswa aelewe madhara ya kugawa taifa, na kwamba mustakabali wake kisiasa kama mtu binafasi usizue matatizo kama ya Rwanda na Burundi.

Huyu supreme alipaswa kujua hilo kwasababu anatoka Kigoma, kinyume chake anasambaza mbegu za chuki za mikoa na kanda.

Alaaniwe huyu ataliangamiza taifa.
 
Takwimu za Zitto zinatoka katika Tanzania Human Development Report 2014(THDR 2014), Je za Mchambuzi zinatoka wapi?
Rudi nyuma utaoana source, ndio maana tunasema umeingia katika katika kutetea usicho na background yake

Walitaka za Mchambuzi, zikaletwa, Mkandara naye kaja na zake. Makundi yote yaliyoleta takwimu hakuna hata aina moja ya takwimu inayomtetea Zittom hakuna.

Zote zinaonyesha amezungumza kwa hisia za kisiasa na chukio dhidi ya mikoa ya kasakazini

Historia ipo wazi, supreme leader ameanza kuichukia mikoa hiyo siku nyingi akiwa bungeni. Chuki zake zimevuka mipaka na hadi kuanza kutumia mitandao na hotuba zake kufatakanisha taifa. Akemewe huyu.

Soma bandiko la Kimweri na Geza ulole https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...wanyo-rasilimali-za-taifa-6.html#post12518131
 

Nimeisikiliza Kauli ya Zitto na Kuisoma Kauli yake, Amepresent Facts, Amesema Ukweli kuhusu ugawanyaji mbovu wa Keki ya Taifa kwa Serikali kutopeleka vipau mbele katika Mikoa inayochangia zaidi pato la Taifa, hili haliwezi kuwa kosa La Zitto kuzungumza kilichokuwa cha kweli. Ni Planing Mbovu tu ya Serikali.

Nyinyi naona mmeamua kumuattack Zitto Personally kwa kutake out of context anachokizungumza, Lakini siwashangai sana kwa sababu humu katika JF mmejipambanua kuwa Mna chuki kali kwelikweli dhidi ya Zitto. Na haya mnayoyafanya ni mwendelezo ule ule ambao hauna tija.
 
Linahusiana vipi na maendeleo ya Kilimanjaro na Arusha?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…