Duru za Siasa: Marekani (U.S) Chini ya Donald J. Trump

Duru za Siasa: Marekani (U.S) Chini ya Donald J. Trump

Making political predictions is normal, but for some when they make bad predictions they stop predicting or at least acknowledge that they are not getting things right and they don't quickly get embroiled in making new predictions.

"I looked at the race, and I said, 'Look. Hillary Clinton is going to be hard to beat.' Another bad prediction on my part, because she's turned out a lot weaker than I thought". Mitt Romney

But when one's predictions are filled with prejudice, it is really hard to change course because certain things other than facts are in play.

"I've been wrong on everything about Trump; I've been wrong about everything on the Republican side of the ledger. But allow me - with that caveat - to made the prediction that Donald Trump will not be the president of the United States. It just will not happen". Cory Booker

Someone who can't say or write anything good about Pres. Trump, needs to get a 'lobotomy'.
 
Someone who can't say or write anything good about Pres. Trump, needs to get a 'lobotomy'.
How about someone who can't see, say, hear or write anything wrong with Pres. Donald Perfect Trump? What would he need? Come on guys let's face it, the guy is a mistake and, much to the dismay of his faithful followers, this sad truth sinks in deeper and deeper every day...and this is just the first month in office since inauguration
 
Hebu tuweke mahaba pembeni kidogo na tuongee uhalisia wa mambo. Nimesema hapo juu kwamba kupingana na maamuzi ya jaji wala sio tatizo na ana haki ya kufanya hivyo ikiwa ana hoja za msingi. Tatizo ni kutumia lugha ya dharau na kejeli kwa mtu huyu ambaye ni jaji wa mahakama kuu kwa sababu ametoa maamuzi ambayo hajakubaliana nayo... huo ni utoto wala hakuna namna nyingine ya kuuelezea. Nchi inaendeshwa kwa misingi ya kisheria na ndio maana hata amri yake imetenguliwa kwa misingi hiyo hiyo ya kisheria na yeye anabanwa kutii atake asitake.

Suala la ugaidi na wahamiaji ni pana sana pengine litahitaji uzi tofauti kulijadili lakini kwa kifupi nikuulize swali... ikiwa lengo la kutoa zuio dhidi ya raia wa nchi 7 ilikuwa ni kuzuia ugaidi kwa nini nchi ya Saudi Arabia haimo kwenye orodha wakati asilimia kubwa ya walioshambulia september 11 walikuwa wanatoka huko? Kwa nini Saudia inaachwa bila kuadhibiwa? Au kwa sababu ya uswahiba wa kibiashara?

Unaposema mtangulizi wa Trump amefanya blunders nyingi unaweza kutoa mfano wa maeneo machache ambayo amefanya blunder kubwa kiasi cha kulazimu kutekeleza hizi executive orders? Au ni chuki binafsi tu?
 
How about someone who can't see, say, hear or write anything wrong with Pres. Donald Perfect Trump? What would he need? Come on guys let's face it, the guy is a mistake and, much to the dismay of his faithful followers, this sad truth sinks in deeper and deeper every day...and this is just the first month in office since inauguration

Kama kuna kitu ambacho Trump amefanikiwa kwa kiasi kikubwa ni kujitengenezea mazingira ya u-mungu mtu... kwamba kila anachozungumza ni sahihi na kweli hata kama ni uongo wa wazi wanaita "alternative facts"

Kazi kweli kweli!
 
"Mwalimu, post: 19590575, member: 11689"]Trump ana followers zaidi ya 23M kwa hiyo suala la post kupata likes 140k sio shida. Pia kutofautiana kimtazamo na majaji nayo sio shida na inaweza kutokea mara kwa mara.
Mkuu, umesema vema, Likes kama zinatumika ku ''qualify or quantify'' kauli katika mitandao kwakweli ni hatua mpya.

Nakumbuka walioamini Obama hakuzaliwa Marekani kutokana na kauli za Trump.
Namba inayoamini hivyo ikiwekwa mtandaoni ni zaidi ya milioni.

Kama ingekuwa na nafasi ya 'like' zingefika milioni.
Hilo lingefanya Obama asiwe rais wa Marekani! Sasa likes 140! kwakweli inatisha, tuachie hapo

Shida ya Trump ni anavyokabiliana na wote ambao wanatofautiana na yeye kimtazamo.
Kama hajakubaliana na uamuzi wa jaji haina shida lakini kufikia hatua ya kumdhihaki kwa kumwita "so called judge" ameonyesha kiwango kikubwa cha utoto kitu ambacho hakipaswi kuonyeshwa na mtu mzima yeyote sembuse rais wa taifa kubwa kama marekani. Na hii sio mara ya kwanza kufanya hivi, juzi hapa alimkatia simu waziri mkuu wa Australia baada ya kutokubaliana juu ya hoja za uhamiaji. Hakuna namna nyingine ya kuita tabia hii isipokuwa "utoto"!
Huyu ni Jaji wa pili kumdharau baada ya yule wa kesi ya chuo

Wiki iliyokwisha ali tweet Sally Yates ni Obama's AG.

Trump haelewi Jaji akishakuwa appointment anakuwa mtumishi wa umma si wa mtu.
Ni makosa kumwita Tillerson kama ''Trump's sec of state''

Republican kama akina Mitchell wanakuwa embarrassed na kauli zisizo na vipimo za Trump

Kauli hizo kwa upande mwingine zinamjengea sana heshima Obama

Juzi wakati wa black month history, Trump alikuwa busy akieleza mzozo wake na vyombo vya habari
Ni kama hakujua kwanini alikuwa pale na umuhimu wa siku hiyo

Kuna wanaosema ana uhuru wa kusema mawazo yake.

Ni kweli, lakini si Trump wa Tower au transition ni president kila analofanya liwe katika muktadha huo

Uhuru wa kusema unamweka mahali pagumu.

Aliulizwa kuhusu ushahidi wa wapiga kura haram milioni 3.5-5.

Utetezi wake ni sawa na mtu wa mtaani kwakweli. Hana back up ya suala analozungumzia

Akatoa kauli za exec order kuchunguza wapiga kura haramu.

Wenzake wakamwambia hata kama wapo hawafiki hata 5,000 kwa kuangalia kesi za nyuma

Kauli inapingwa na Republican ambao magavana wao ni wengi katika state ukilinganisha na Dem

Trump anajua hawezi kutetea hoja zake za nyuma. Anachokifanya ni kusingizia vyombo vya habari

Tatizo analoona ni vyombo hivyo kuweka kumbu kumbu naye hataki watu wakumbuke kasema nini

Kwa mfano, sasa hivi anatekeleza sera za Obama kwa Iran kikamilifu.

Huko nyuma alisema deal ni disaster akiaminisha umma ana mbadala mzuri ambao hadi sasa haupo

Ndivyo ilivyo kwa Obamacare ambayo hana karatasi hata moja aliyoandika ikaonekana hadi sasa

Usisahau suala la ukuta ambalo nalo limeshindikana na Mexico hawatalipa gharama ila wananchi wake

Katika mkutano wa mwisho na waandishi wakati wa Obama, wengi walisema watamkosa kwa utulivu, umakini na muhimu sana anavyoweza ku articulate policy na kuzi connect na public

Kinachoshangaza ni kuwa katika tweets, Trump anamsema Jaji kama kichekesho asiyejali usalama wa Taifa. Trump bado anadhani ukuu wake hauna ukomo.

Katika nchi inayoongozwa na constitution sheria ndizo zinatangulia na Jaji alisimamia hilo

Pamoja na kumkashfu bado Trump ametii amri ya Jaji kwa maana amri ya Mahakama bila shurti

Sasa anafuata mkondo wa sheria na pengine anaanza kuelewa maana ya mihimili miatatu huko US
 
"Mwalimu, post: 19595849, member: 11689"]Hebu tuweke mahaba pembeni kidogo na tuongee uhalisia wa mambo.

Nimesema hapo juu kwamba kupingana na maamuzi ya jaji wala sio tatizo na ana haki ya kufanya hivyo ikiwa ana hoja za msingi. Tatizo ni kutumia lugha ya dharau na kejeli kwa mtu huyu ambaye ni jaji wa mahakama kuu kwa sababu ametoa maamuzi ambayo hajakubaliana nayo... huo ni utoto wala hakuna namna nyingine ya kuuelezea. Nchi inaendeshwa kwa misingi ya kisheria na ndio maana hata amri yake imetenguliwa kwa misingi hiyo hiyo ya kisheria na yeye anabanwa kutii atake asitake.
Mkuu kuna mambo mengi yanashangaza. Kuna mambo mawili.

Kwanza, kesi iliyokwenda mahakamani ni kuhusu suala la visa.
Hili ndilo Jaji amelitoa uamuzi kwa kusitisha kwa muda exec order

Pili, kilichopelekwa mahakama si suala la usalama wa nchi, my foot!
Mtu akisema Jaji hakuzingatia usalama wa nchi, unamwacha tu, utaanzia wapi
ikiwa lengo la kutoa zuio dhidi ya raia wa nchi 7 ilikuwa ni kuzuia ugaidi kwa nini nchi ya Saudi Arabia haimo kwenye orodha wakati asilimia kubwa ya walioshambulia september 11 walikuwa wanatoka huko? Kwa nini Saudia inaachwa bila kuadhibiwa?
Katika hotbed za dunia unawezaje kuiacha Pakistan na Afghanistan au Egypt.
Unaposema mtangulizi wa Trump amefanya blunders nyingi unaweza kutoa mfano wa maeneo machache ambayo amefanya blunder kubwa kiasi cha kulazimu kutekeleza hizi executive orders? Au ni chuki binafsi tu?
Mkuu hili suala wanasikia tu akina Bannon na Kellyane wakisema ,hawana uhakika ni blunder gani. Kwa mfano, kama Obama alifanya blunder ya ACA, tuonyeshwe mstari mmoja hadi wa ACA nyingine.

Kumbuka ni miaka 2 na ushee si Republican wala Trump aliyeandika hata page moja

Pili, blunder wanayosema ni Iran, kama alivyosema Trump ilikuwa deal mbaya sana.
Well,Trump hana deal nyingine anatumia ya Obama kwa nguvu kuliko Obama mwenyewe

Tatu, wakasema GDP inakuwa katika kiwango kidogo.
Tukauliza wakati Obama anaingia ilikuwaje?

Kuna recession gani nyingine ukiacha ya WWII na je ndipo Trump alipokuta nchi?
Hawana jibu

Kilichonikesha ni mtu kusema jeshi lina hali mbaya! Hivi nani anajua hali ya jeshi la US?

Trump analijua sasa alipokuwa Rais, huku mitandaoni mtu anabwabwaja tu
Kuna jeshi gani finesse duniani kuliko la US na nani anajua wana kitu gani?

Atakaye kujua ukubwa wa jeshi la US awaulize EU!

Kuna vitu nasoma hadi naogopa, najiuliza kama hakuna ufahamu kuna dhambi gani kujifunza? Wamekariri tu Obama kafanya blunder, waulize ipi, hawana jibu
 
Naomba nianzie ulipoishia, sina chuki na Obama. Nilishasema toka mwanzo kuwa wakati tunaelezea upsides na downsides za Rais Trump, ingawa wengine hawaoni upsides zake, hatuna budi kufanya the same thing kwa mtangulizi wake pia.

Kabla ya January 20th, 2009, Libya ilikuwaje? Syria ilikuwaje? Iraq ilikuwaje? n.k Hizi nchi sasa hivi zikoje? Nani aliita ISIS JV (Junior Varsity) Team? Sasa hivi ISIS imeenea nchi ngapi? Nani ali-sponsor 'moderate' Syrian rebels? Nani alim-support Morsi wa Egypt? Iran amekuwa embolden kwenye utawala wa nani? Nani alijuta kumuondoa Gaddafi madarakani? List ni ndefu sana.

Katika kujaribu kutatua madhara ya hizo foreign policy blunders, Obama pamoja na Congress wakaweka nchi 7 kwenye list ya nchi zinazohitaji 'further travel restrictions' na 'countries of concern'.

Ni 'countries of concern' kwa sababu US haiamini kuwa watu wote wanaotoka kwenye nchi hizo kuja US are who they say they are. Kwa maana nyingine, hawaamini internal systems za nchi hizo kuwapa complete and reliable information kuhusu individuals wanaotoka katika nchi hizo.

Ndio maana Rais Trump aka-sign Ex. Order ya Immigration ili kuweka 'extreme vetting' (proper controls) kwa ajili ya ku-counter hizo loopholes za internal systems za nchi hizo 7.

Kwa nini Egypt, Pakistan, Saudi Arabia, Afghanistan, hawapo kwenye list? Kwa sababu Congress haikuziweka hizo nchi katika katika list ya nchi ambazo US haiamini internal systems zake. Kwa maana nyingine, US inaamini watu wanaotoka katika nchi hizo are who they say they are na wala sio sababu za kibiashara.

Mtu anaweza kuwa radicalized akiwa anaenda na kurudi kila mara katika nchi hizo 7 au akiwa within US soil/home grown (mfano online), ndio maana Rais Trump hajasema kuwa travel restrictions kwa nchi 7 ndio solution pekee ya radical islamic terrorism. Kama vetting mechanism zikiwa in place kwa hizo nchi 7, likelihood ya terror attack itapungua.

Ili kudeal na homegrown terrorists and other forms of evil Rais Trump amesign Ex orders mbili, Enhancing Public Safety in the Interior of the United States na Border Security and Immigration Enforcement Improvements.

Kwa namna Rais Trump anavyo-deal na security threats na challenges kwenye angle tofauti tofauti ni wazi yupo focused kitimiza promise yake ya Kuweka nchi salama. Ndio maana amekuwa critical kwa watu walio 'weak' kwenye issue ya border, radical islamic terrorism, immigration, sanctuary cities n.k

Obama aliwahi ku-criticize Supreme Court Justices akiwemo Chief Justice kwenye State of the Union Address yake ya kwanza mwaka 2010. Yaani Executive leader, ali-criticize Judiciary leaders mbele ya Legislature (Congress) na Senators wa Democrats wakasimama na kupiga makofi!!!!!

Supreme Court iliamua 5-4 kwamba zuio la serikali kwenye matangazo ya kisiasa ni kukiuka uhuru wa kutoa maoni. Unaweza kusema kwamba Obama alikosea? Au Je, kwa maoni yako alikuwa sahihi?
 
How about someone who can't see, say, hear or write anything wrong with Pres. Donald Perfect Trump? What would he need? Come on guys let's face it, the guy is a mistake and, much to the dismay of his faithful followers, this sad truth sinks in deeper and deeper every day...and this is just the first month in office since inauguration

Because I am looking at the whole thing objectively, I was able to write three things in post #38 that I believe Pres. Trump should look to change as he leads the country towards prosperity, security and liberty.

The other thing I said if you go back to that post is that you can't ignore the good things that are happening in this first month.

Now, the ball is in your court, tell us where (post #) you have written anything GOOD about Pres. Trump.
 
Kama kuna kitu ambacho Trump amefanikiwa kwa kiasi kikubwa ni kujitengenezea mazingira ya u-mungu mtu... kwamba kila anachozungumza ni sahihi na kweli hata kama ni uongo wa wazi wanaita "alternative facts"

Kazi kweli kweli!

Naona unaingiza ushabiki.

Na vipi kuhusu wale wasiokubali kuwa Obama ali-fail katika maeneo mengi na failures zake hizo ndizo zilizopelekea ushindi wa Rais Trump?

Na ndio hao wanaoona kuwa kila alichozungumza Obama ni sahihi na kweli hata kama ni uongo wa wazi. Mfano, kwenye ACA aliwadanganya wananchi kuwa wanaweza ku-keep their doctors na kwamba premiums zitashuka, walidanganya kuwa shambulio kwenye ubalozi wa US Libya (Benghazi) ilisababishwa na video n.k, ila hayo hutaona wanazungumzia.
 
Kuna watu wanai-support ACA bila kuzungumzia uongo wake, huku wakiuliza kuhusu alternative health plan ya Rais Trump.

Republicans wameshasema 'Trumpcare' itapelekwa Congress mwaka huu mwishoni au mwakani mwanzoni, sasa mtu anataka aone mstari moja, funny!,wakati Democrats bado wanaleta siasa kwenye upitishwaji wa Tom Price (HHS-Sec).

Secretaries wa Treasury, Commerce, HHS, Energy, HUD, Justice (AG), Interior, Labour, Education, Veterans Affairs na Agriculture bado hawajaanza kazi, then mtu anategemea aone mabadiliko makubwa sasa hivi!!

House Republicans wanayo health plan yao hata kabla ya ACA, Tom Price anayo alternative plan (ukizingatia alikuwa critic mkubwa wa ACA) ambayo ndio Rais Trump anazungumzia. Kinachoendelea ni kuzi-merge ili kuja na comprehensive health plan inayoitwa 'Trumpcare'.

Ukweli ulio wazi ni kwamba ACA ya Obama haina mda mrefu, itakuwa historia.

Kuna mdau anasema Rais Trump 'anatumia kwa nguvu' Iran deal ya Obama!. Rais Trump alipinga Iran deal na wanasiasa wengi tu akiwemo Senator Chuck Schumer, D-New York (Senate Minority Leader).

Huwezi kuisifia UNSC 'nuclear deal' bila kujali kuwa inamruhusu Iran ku-test-fire MR ballistic missiles. Toka 2015 baada ya 'nuclear deal' Iran wame-fire ballistic missile test nyingi tu. Ndio maana UN walikuja tena na resolution ku-supplement 'deal' ya mwanzo ili kuwazuia.

Lakini bado wanafanya, ndio maana Iran wanasema hawaja-violate 'nuclear deal' kwenye missile tests zao lakini hawasemi kuwa hawaja-break UN resolution iliyofuatia.

Rais Trump anachosema ni kuwa loopholes kama hizo na zingine kadhaa zingeweza kujumuishwa kwenye deal ili kusudi Iran iweze kudhibitiwa.

Wale ambao hawaoni kasoro za Iran 'nuclear deal' watafute maoni ya Chuck Schumer (top Senate democrat), kwanini aliipinga?

Kingine, mtu akitaka kujua kuwa Obama alifeli kwenye Economic Recovery, akasome tofauti kati ya 'Reaganomics' na 'Obamanomics'. Pia asome kwanini recovery ya Obama pamoja na ukubwa wa recession ndio the worst recovery since the great depression!

Recession ilitokea mwaka 2008 na ikumbukwe Democrats ndio walikuwa na majority kwenye House na kwenye Senate mwaka 2006.

Kuna recessions kama kumi zimetokea baada ya WW II, historia ya uchumi wa US ni kuwa 'the worse the recession the stronger the recovery'. Obama alitekeleza sera za anti-growth hata Mitt Romney alimwambia kwenye debates za mwaka 2012 na zimeishia kuwa-cost Democrats.
 
AFFORDABLE CARE ACT (ACA)

Tumezungumzia huko kabla ya uchaguzi kufuta Obamacare si jambo rahisi kama Trump alivyoaminisha wafuasi wake ataifuta mchana wa kwanza wa siku ya kwanza Oval office

Tukazungumzia jinsi ACA inavyofungamana na mambo ya kijamii na kiuchumi

Siku ya kwanza , Trump alisaini exec order isiyo na maelezo kufurahisha na kupumbaza

Wapo waliosemailikuwa kazi nzuri, ingawa hawakueleza ni nzuri kwa vipi na inasema nini

Tangu kampeni zinaendelea, tulihoji wagombea wa Rep na Dem kila mmoja alikuwa na sera hata kama haikuwa kama mtu anavyofikiri. Trump hakuwa nayo na hana hadi sasa

Kwa miaka 2 amesema Obamacare ni disaster. Hata katika interview alirudia kusema
Trump amesema itachukua mwaka au miwili kabla ya kupatikana nyingine

Hapa pamemaliza malumbano ya ACA, Trump ameona uzito wake kiuhalisia ameahirisha

Hakufuta Obamacare kama alivyosema, aliweka exec order 'fake' kupumbaza umma

Katika kipindi cha mwaka au miwili, ACA itakayokuwepo ni ya Obama, ni legacy

Hata miaka 2 , Trump hatakuja na kitu tofauti isipokuwa ACA iliyokarabatiwa

Mtihani uliomkumba ni 'reaction' anachokifanya ni kutoongeza matatizo

Mbele ya safari ana mtihani. Baada ya mwaka 1 kutakuwa na midterm mwaka unaofuata

Kuna uwezekano Obamacare ikawa 'hukumu' , hivyo inaweza isifanyike kabisa

Midterm itahusu senate na House , uwezekano wa kupoteza kimoja upo

Kwa upande mwingine, katika kipindi hicho cha mwaka au miwili, wafuasi watapoteza imani au nguvu, matarajio yao hayakufikiwa kwa muda waliotarajia

Sijambo la kushangaza kwasababu deal ya Iran nayo imefuata mkondo huo

Wengi walitaraji mvua ya mabomu,kinachofanyika ni kusimamia sera za Obama kikamilifu

Haya mawili yanalinda legacy ya Obama kwani 'kitabu' kinachotumika oval office ni Obama

Tusemezane
 
Asante sana El Jefe kwa kuja! Sasa, mimi binafsi, nakupa hadhi ya kuwa mwalimu wangu wa masomo ya ziada ('Tuition'). Nguruvi3 anabaki kuwa Mwalimu Mkuu wangu wakati Mag3 akiwa mwalimu Mkuu wangu msaidizi na wengine wakiwa walimu wangu wa masomo ya hapa na pale. Jukwaa linachangamka kweli kweli, sijutii MB zangu na muda ninaotumia hapa.
====================
Wakati mjadala unaendelea; kuna habari za watabiri maarufu (siyo Soros) wa masuala ya uchumi na fedha wanasema US itaporomoka ikifika 2050 ki-uchumi.Watabiri hao ni PwC. Nashawishika kudhani kuwa kile nilichokisema kuwa Trump anaweza kuiangusha US pole pole si kubashiri kimakosa!
------------------------
Over the next three decades, the global economy will be dominated by China, and the US economy will lose steam and fall behind India, says consulting firm PricewaterhouseCoopers (PwC).
Russia will become the leading European economy ahead of Germany, UK, and Italy with GDP of $7 trillion, according to a PwC.
......................................
Nigeria has the potential to be the fastest growing large African economy and could move up the GDP rankings from 22nd place to 14th by 2050. But Nigeria will only realise this potential if it can diversify its economy away from oil and strengthen its institutions and infrastructure. Colombia and Poland also exhibit great potential, and are projected to be the fastest growing large economies in their respective regions, Latin America and the EU (though Turkey is projected to grow faster within the wider European area)
----------------
Sources: China to become #1 economy by 2050, US to fall behind India, Russia to top Europe – PwC

http://www.pwc.com/gx/en/world-2050/assets/pwc-world-in-2050-summary-report-feb-2017.pdf
 
....

Haya mawili yanalinda legacy ya Obama kwani 'kitabu' kinachotumika oval off ni Obama

...
Legacy yake inabidi ajidhatiti kweli kuilinda...maana kashifa dhidi ya utawala wake zinazidi kuibuliwa. Inasemekana serikali ya US chini ya Obama ilichakachua takwimu juu ya hatari ya ongezeko la joto duniani ili ikidhi matakwa yake katika Mkutano wa masuala ya Hali ya HEwa, kule Paris,Ufaransa mwaka 2015. Hizi tuhuma zimechapishwa na mtandao wa Urusi.
---------------
A recently-retired top scientist from the America’s National Oceanic and Atmospheric Administration (NOAA) has accused his superiors of fudging data to hide a slowdown in the rise of global temperatures ahead of the UN Climate Change Conference in 2015.
John Bates told the Mail on Sunday that Thomas Karl, the head of the climate change department at the government agency, authored a paper based on doctored data, “rushed” it into publication, and then saw his work used to make international commitments to fight global warming worth hundreds of billions of dollars.

US govt agency manipulated data to exaggerate climate change – whistleblower
 
TUJITEGEMEE kwani climate change imeanza na Obama? I mean haikuwepo kabla ya hapo?
Ilikuwepo kabla ya hapo, nadhani Clinton (Bill) ndiye aliyeishupalia sana. Kinacholeta shida, ni serikali ya US chini ya Obama kushiriki kuchakachua takwimu hili kulaghai wadau wa mazingira na hali ya hewa kutoa ela. Yaani naona kama utapeli fulani hivi!
 
Ilikuwepo kabla ya hapo, nadhani Clinton (Bill) ndiye aliyeishupalia sana. Kinacholeta shida, ni serikali ya US chini ya Obama kushiriki kuchakachua takwimu hili kulaghai wadau wa mazingira na hali ya hewa kutoa ela. Yaani naona kama utapeli fulani hivi!
Kwahiyo umehitimisha habari hizo ni kweli kabisa, na ukweli mtupu!

Pili, kama ilikuwepo kwanini unadhani ni Legacy ya Obama?
 
snapshot_chart_api.asp


Kwa ufahamisho tu...kwa siku kama mbili hivi Dow Jones imerudi pale pale ilipokuwa kabla ya Uchaguzi na inazidi kushuka...
Hivi bado una-track Dow jones? au unai-track tu ukisikia imeshuka!

YPO Global Pulse survey wametoa study yao ya CEO confidence, kwa robo moja ya mwaka US imepanda kwa 4.2 points (haijawahi kutokea).
 
Rep. Nanci Pelosi (D-Calif.) anadhani George W. Bush bado ni Rais wa US!!

Rep. Maxine Waters (D-Calif.) anadai Vladimir Putin anazidi kuingia Korea!!

Democrats sio tu wamechanganyikiwa, kuna vitu vingi hawaelewi.

 
Hivi bado una-track Dow jones? au unai-track tu ukisikia imeshuka!

YPO Global Pulse survey wametoa study yao ya CEO confidence, kwa robo moja ya mwaka US imepanda kwa 4.2 points (haijawahi kutokea).

Na wewe je, Kanye West bado anamuunga mkono Trump?
 
Back
Top Bottom