Duru za siasa: Vurugu za katiba zinalinyemelea taifa. Hali si shwari

Duru za siasa: Vurugu za katiba zinalinyemelea taifa. Hali si shwari

MPANGO ULIKUWA ‘’MZURI’
JARIBIO LIKAFANYWA BILA WELEDI


CCM WANA MAMBO 2 YA KUFANYA

Mpango wa kuleta vurugu ulikuwa umepangwa ‘vizuri’ ili kumhusisha Mzee Warioba na tume yake katika vurugu. Hili lingesaidia sana kutoa picha mbaya ya iliyokuwa tume likilenga kuonyesha, inatumiwa au ina lengo la kuleta vurugu.

CCM walipanga kutumia mwanya huo kumdhalilisha zaidi Mzee Warioba na pengine kutumia slogan yao ya amani na utulivu katika kampeni zake.

Kwa bahati mbaya waliofanya mpango huo hawakuwa na weledi au walikosea kiufundi.
Mabango yaliyotolewa katika mkutano yalihusisha CCM.
Vurugu zilizotokea zilimhusisha kiongozi wa CCM bwana Makonda

Kwa kufanya vurugu, nchi na duni iliona CCM walikusudia kuleta vurugu katika mjadala ambao haukuwa na chembe za uvunjifu wa amani.

Katika mpango huo, ilikuwa almanusra Mzee Warioba na wengine wajeruhiwe au wadhurike.
CCM haikuwa imelenga huko, ilikuwa imelenga kumtia doa.

Bahati mbaya waliopewa kazi walienda mbali na kufikia hatua ya kuhatarisha maisha ya makamu wa Rais mtstaafu na waziri mkuu pamoja na wahshiriki wengine.

CCM ilitakiwa ifanya ‘damage control’ kwa kukemea tukio ikiwa ni pamoja na kuwafikisha mbele ya sheria wahusika. Aidha ilipaswa kumuadhibu au kuwaadhibu wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine.

Tatizo linaloikabili CCM ni kuwa na viwango tofauti vya maamuzi ‘double standard’
Kwa mfano, Mansour Himid wa CCM znz aliadhibiwa kwa msimamo wa S3 tu bila tusi au kunyanyua mkono.

Wanachama 6 wa CCM-znz walikataa kupiga kura au walipiga kura ya hapana katika bunge lao.
Na pia wapo watu waliopinga msimamo wa CCM kwa namna tofauti.
Hao wote hawajawahi kuchukuliwa hatua yoyote.

Kuwachukulia hatua waliovuruga mjadala kwa kutumwa inakuwa ni ngumu zaidi.
Hapa ndipo tunaona ukimya wa CCM kwasababu ni mwiba wenye pande mbili.

KWANINI WANAHUSISHWA NA VURUGU

CCM inahusishwa na vurugu kwa namna nyingi.
Kwanza, mwenyekiti wake alihusika katika kuidhalilisha tume ya Warioba alipofungua bunge.
Pili, mwenyekiti wa bunge la CCM alishiriki katika vitendo vya udhalilishaji ikiwa ni pamoja na kuruhusu makada kama Komba kuwatukana akina Warioba.

Tatu, viongozi wa CCM walishiriki kuchochea vurugu katika maeneo kama ya kanisani yakimhusisha waziri wa serikali ya CCM bw, Lukuvi.

Waziri mkuu aliwahi kutoa kauli ya ‘’wapigwe’’

Hivyo kwa Mtanzania wa kawaida haya ya akina Makonda na kundi lake yanaweza kusomeka kama utekelezaji wa maagizo ya viongozi wa CCM.

Katika hali hiyo, CCM ilikuwa na njia mbili tu

  1. Kubaki kimya umma ukiamini kuwa walihusika na tukio la uvunjifu wa amani lililolenga kudhuru watu. Kwamba, wananchi waamini vurugu nyingine za nyuma zilikuwa na mkono wa CCM. Hilo wana weza kubaki nalo wakiendelea kukaa kimya
  2. Kuchukua hatua za kukemea na hata kuwafikisha mbele ya sheria wanaohusika ili umma uone na utambue kuwa, vurugu hazikuwa za CCM.

Katika mambo hayo 2, CCM inabeba mzigo mzito sana. Leo viongozi wa CCM wanawezaje kuhubiri amani na utulivu ikiwa wao ni sehemu ya uvunjifua wa amani tena ukiwalenga makada, wazee na watu wenye heshima nchini?

CCM pia itabidi iwaeleze wananchi, wapi demkorasia na utawala wa sheria inao hubiri.
Kama Mansour alifukuzwa kwa msimamo tu bila tusi, leo kwanini walionyanyua viti na kuponda weananchi waachwe huru.

CCM imesimamia vipi utawala wa sheria ikiwa wananchi hawana nafasi ya kushiriki shughuli zao bila uvunjifu wa amani unaoletwa na CCM?

Ndio maana tunasema, jaribio la kumhusisha mzee Warioba na wenzake katika vurugu za nchi limekwama kwa gharama kubwa ya CCM.

Vipi watasema wanamwenzi Nyerere ikiwa Mwalimu alisema watu wapingane bila kupigana?
Je, ndio CCM aliotaka Mwalimu Nyerere? Na je kwa mashambulizi wanayoonyesha, ndiko kumuenzi mwalimu?

Tusemezane
Nguruvi3,

Umejadili hoja ya msingi sana, kwa kweli Kati ya jaji warioba na viongozi wa sasa wa CCM, ni dhahiri Kwamba jaji warioba ni kiongozi anayejishughulisha zaidi na kumuenzi mwalimu nyerere kuliko genge la viongozi lililochakachua mchakato wa katiba. Kwa mfano, Katika kitabu chake cha ‘TUJISAHIHISHE’ (1962), Mwalimu anasema:

[“Ukiondoa matatizo wayapatayo binadamu kwa sababu kama mafuriko, nzige, kiangazi, n.k, matatizo yao mengi hutokana na unafsi. Unafsi ni wa aina nyingi. Swali ambalo twalisikia mara kwa mara, “Hali yetu ya baadae itakuwaje?”, ni swali ambalo sina shaka kuna wanaouliza kwa nia safi kabisa. Lakini mara nyingi linatokana na unafsi. Mtu anayeuliza anafikiri TANU iliundwa kwa faida yake binafsi. Ni kama kwamba TANU ilipoundwa ilimwahidi kwamba ikiwa atakubali kuwa mwanachama, au kiongozi, basi TANU itamfanyia yeye jambo fulani kama tunzo! Anasahau kabisa kuwa TANU inajishughulisha na haja za Jumuiya kwa ujumla. Lakini kwa mtu wa aina hiyo, hata kama TANU inatimiza madhumuni yake kwa jumuiya, ataona kuwa ni umoja ambao hauna maana kwa sababu haumtimizii haja zote za nafsi yake. Huu ni unafsi. Kama wanachama wa TANU, na hasa viongozi, hawatakihukumu chama chetu kwa mahitaji na nafsi zao wenyewe, chana hakitadumu. Wanachama wa aina hiyo ni ugonjwa katika chama.

Dalili nyingine ya unafsi, na ambayo ni ugonjwa mbaya sana ni fitina. Kanuni moja ya TANU inasema hivi: “Nitasema Ukweli Daima. Fitina Kwangu ni Mwiko.” Lakini bado tunao wanachama ambao ni wafitini wakubwa bila kujitambua. Ni wa aina mbali mbali. Wengine humwona mwenzao anafanya kosa. Badala ya kumwambia pale pale kijamaa kwamba atendalo ni kosa, watanyamaza kimya. Lakini hawanyamazi kabisa. Watakwenda kumteta katika vikundi vya siri. Mateto haya si ya kumsaidia mwenzao, ni ya kumdhuru. Hii ni aina moja ya fitina. Wengine hugawa watu katika mafungu. “Fulani” japo kafanya kosa kubwa sana hasemwi. Lakini “Fulani” wa pili akifanya kosa japo dogo, kosa lile hukuzwa likawa kama mlima Kilimanjaro. Hawa hutafuta sababu ya kumtetea “Fulani” wa kwanza, au za kumaulumu “Fulani” wa pili, ambazo hazifanani kabisa na ukweli. Kwa watu wa aina hii, ukweli ni jambo ambalo hutegemea mtu, si kitu kinachojitegemea chenyewe bila kujali mtu.“Fulani” wa kwanza akisema katika majadiliano kuwa mbili na mbili ni tano, wao watakubali. Lakini “Fulani” wa pili akisema sivyo, mbili na mbili ni nne, watamwona ni mtu mbaya kabisa ambaye hastahili hata kusikilizwa. Hawa hawajali ukweli, hujali nafsi tu. Kwao, ukweli ni maoni yao na matakwa yao. Hatuna budi, hasa katika majadiliano na mazungumzo yanayohusu jumuiya, tujifunze kusikiliza hoja zenyewe zinazotolewa na wenzetu, na kuzijibu zile hoja kwa kuzikubali au kuzikataa, bila kujali kama anaezitoa ni rafiki au si rafiki. Pia wanaopingwa hawana budi wakubali kuwa kinachopingwa ni zile hoja zao, sio wao wenyewe. Bila mazoea haya, mazungumzo hayana maana; yanakuwa ni kupoteza wakati, maana huwa tumekwisha kuzihukumu hoja za mtu hata kabla hajazitamka; kadhalika, hoja zetu zikijibiwa kwa kupingwa halafu tunawakasirikia waliozipinga tunafanya mazungumzo yasiwe na maana, kwa sababu tunapenda hoja zetu zikubaliwe tu hata kama si hoja safi.

Ukweli una tabia moja nzuri sana. Haujali mkubwa wala mdogo; haujali adui wala rafiki. Kwake, watu wote ni sawa. Pia ukweli unayo tabia ya kujilipiza kisasi kama ukipuuzwa. Ukiniona nataka kulipiga teke jiwe kwa kuwa unafikiri kuwa ni dongo au mpira, natumaini utanionya. Lakini nikilipuuza onyo lako kwa sababu eti wewe ni mdogo au kwa sababu sikupendi, nikalipiga teke, basi litanivunja dole japo ningekuwa nani. Ukweli haupendi kupuuzwa.
Wakati mwingine, mtu tunayempinga huwa ana makosa kweli lakini hoja tunazozitoa ni za kinafsi na hazihusiani kabisa na hoja zake. Nikisema mbili na tatu ni sita, nakosa. Lakini ni bora kunionyesha kwamba pengine nafikiri tunazidisha kumbe tunajumlisha. Ni kweli mbili mara tatu ni sita; lakini mbili na tatu ni tano, siyo sit.a Lakini ukijaribu kuwashawishi wenzetu wakatae mawazo yangu na kukubali yako kwa kusema kuwa meno yangu ni machafu, au natoa kamasi daima, utakuwa unatumia hoja ambazo hazina maana. Huu ni mfano wa upuuzi; lakini mara nyingi hoja tunazotumia kuwashawishi watu wakatae mawazo ya wale tusiowapenda, au kukubali mawazo yetu, huwa hazihusiani kabisa na mambo tunayoyajadili.

Makosa yetu mengine hutokana na woga; woga unaotuzuia kumlaumu mkubwa japo tunajua kuwa kakosa, au unaotuzuia kumtetea mdogo anayelaumiwa na wakubwa japo tunajua hana makosa. Na msingi wa woga ni unafsi. Pengine huwa tunaogopa sisi wenyewe kulaumiwa au kupata hasara fulani. Pengine twaweza kuwa hatuna cheo chochote ambacho tunaogopa kupoteza; pengine huwa hatuna tamaa yoyote ya kupata cheo fulani. Lakini woga unaweza kutokana na tamaa ya kila binadamu kupendwa na binadamu wenzake. Sisi sote tunayo tama hii, au sivyo tusingekuwa binadamu. Woga huu huweza kumfanya mtu kuvumilia maovu, hasa kama maovu yale yanatendwa na walio wengi kwa walio wachache, au yanatendwa na wakubwa kwa wadogo. Kwa kuogopa kuwaudhi wengi tunawaacha watende makosa bila kuwasahihisha, wasije wakatuchukia. Huu ni unafsi mbaya sana Ni kweli kwamba demokrasi haiwezi kudumu ikiwa wachache watakubali matakwa ya wengi. Lakini matakwa ya wengi hujulikana katika majadiliano au mazungumzo wa wazi.

Kadhalika, matakwa ya wachache hujulikana katika majadiliano na mazungumzo. Bila wachache kusema wazi wazi matakwa yao, majadiliano hayana maana. Wakati mwingine, hata baada ya majadiliano, wachache – japo wamekubali kutii uamuzi wa wengi wanaweza kuendelea kuamini kwamba mawazo yao ni sawa, na ya walio wengi yamepotoka. Demokrasi inawapa haki, na ukweli unawapa wajibu wa kuendeleza mawazo yao mpaka wengi waone kuwa ni ya kweli. Bila hivyo Maendeleo katika mawazo hayawezekani, kwani mara nyingi wazo zuri hutokana na mtu mmoja tu. Mwanzo laweza likapingwa, pengine kwa nguvu kabisa, na walio wengi, lakini hatimaye wengi hulikubali. Huu ndio msingi wa Maendeleo katika mawazo ya binadamu.
Makosa ni makosa na dhuluma ni dhuluma, japo watendao makosa hayo au dhuluma ile ni wakubwa au ni wengi. Chama kinachopenda ukweli na haki hakina budi kiwape wanachama wake uhuru na nafasi ya kusahihisha makosa na kuondoa dhuluma. Wanachama hawana budi waone kuwa ni wajibu wao kuutumia uhuru huo, na nafasi hiyo. Wanachama wasiotumia uhuru huo na nafasi hiyo, kwa sababu ya kuogopa kuchukiwa au kupoteza nafasi zao, wanafanya kosa kubwa la unafsi, ambalo ni adui wa haki na ukweli."]

Wanaotakiwa kujisahihisha ni wale wana CCM wote ambao wanaendeshwa na uwoga na unafsi Katika suala hili la katiba mpya.









Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Last edited by a moderator:
RAIS ANAPOKEMEA ANACHOTENDA MWENYEWE
KIWEWE CHA KATIBA CHA LAZIMISHA ‘UBABE''

KATIBA YA CHENGE IMEDODA, SASA NI MAGUVU TU

Rais JK amesema muda wa kampeni za rasimu ya CCM inaoitwa ya wananchi umebadilishwa kutoka siku 60 kama sheria inavyosema na kuwa 30.
Amedai sheria inampa mamlaka ya kubadili muda.

Rais ahakutoa sababu za kufanya hivyo, na hilo linazua swali kama utawala wa demokrasia na sheria unafanya kazi. Ni madikteta peka yao wenye kutenda bila kuhojiwa, sijui kama hili haliwezi kubeba sura ya namna hiyo kwa watu wa kawaida.

Rais amepiga marufuku kampeni kuanza sasa. Wakati akaipiga marufuku, kundi la CCM analoongoza limeanza kampeni za rasimu ya Chenge Tanganyika na kule Zanzibar.
Inashangaza kuona rais anakemea kile alichokianza wakati anapokea rasimu ya Chenge, mkutano wa kupokea mwenge, juzi na wazee wa Dodoma.

Kule znz Shein amekuwa kinara wa kampeni za rasimu ya CCM na Chenge bila kukemewa au kuhojiwa. Hivyo, ni ruhusa wao kupotosha umma na marufuku wengine kuhoji.

KWANINI AMEPUNGUZA MUDA?

Ni katika hali ya kuzuia wananchi wasichambue rasimu ya CCM wanayobambikiziwa kama rasimu ya taifa. CCM na JK hawataki kabisa uozo wa mchakato, matatizo aliyozua JK nay ale ya akina Sitta kuanikwa.

Hwataki wananchi wahoji kuhusu kuondolewa kwa vifungu vya rasimu ya Warioba wanayoikataa na kuikubali kwa nyakati tofauti.

Kwa mfano, wasi wasi mkubwa ni kuhusu Watanganyika. Kwamba, watakapogundua katiba ya Chenge imewaumiza katika muungano watachachamaa na hata muungano kuvunjika.

Hawataki Watanganyika wakahoji uwepo wa taifa lao. Ndio maana utasikia rasimu imejibu kero za wazanzibar. Hii katiba si ya wazanzibar, na kwa hakika ni ya Watanganyika zaidi kuliko wznz. Vipi hawakusikilizwa kupitia tume ya Warioba?

Lakini pia hawataki kutoa muda kwa taasisi kuchunguza au kuongelea katiba yao. Wanatafuta namna ya kufunga midomo wananchi.
Huu ni ubabe wa ajabu sana. Jk amehiriki kuvuruga mchakato na sasa anashiriki kuzuia uvurugaji usijadiliwe. Haki hiyo amejipa na Shein


KAULI ILIMLENGA WARIOBA

Kauli ya kusikitisha kampeni ilimlenga Jaji Warioba na tume.
Hili ni kosa, taasisi ya Nyerere haifanyi kampeni. Inachokifanya ni elimu kwa umma.
Sheria haijazuia elimu kwa umma. Na kwanini wananchi wanaobambikiziwa katiba ya Chenge wazuiliwe kuhoji? Kuna nini kikubwa kisichotakiwa kujulikana.

Kwa mwendo huo, taasisi ya Nyerere ina haki ya kuendelea na elimu kwa umma.
Huu wasi wasi wa kuficha maouvu ni wa serikali, wananchi wanachotaka kujua ni kama katiba wanayosokomezewa mdomoni kwa vile hawana sauti ina kitu gani.

Kauli ya Kikweta inajenga mazingira tuliyosema kuwa, akina Warioba wanatafutiwa sababu. Inashadidia vurugu na vipigo vilivyotokea, ikijenga mazingira ya kuwafunga mdomo, au kuwahusisha na uvunjaji wa amani.

Kuendelea kuficha ficha kunazua maswali mengi.
Katiba ya CCM na Chenge ina kitu gani? Kwanini inafichwa hata baada ya kutolewa kutoka mafichoni?

Wananchi wameona uhuni wa akina Sitta, sasa yote yanapofichwa ili wasokomezewe katiba iliyoandikwa na Chenge kwa maoni ya tume ya Sitta iliyohoji watu 37 ni kuleta hatari kubwa sana nchini.

Vyovyote iwavyo, katiba mpya ya Watanzania inayotokana na maoni ya Watanzania itaandikwa. Hapo viongozi waliopo watageuga nyuma na kujuta jinsi walivyolihujumu taifa. Na si kujumu, bali pia kushindwa kunawa mikono itakayokuwa imejaa vimiminika vya wanadamua

Tusemezane
 
KWANINI WARIOBA AMEGEUZWA ''KONDOO WA KAFARA''?

Katika tume ya Jaji, aliyefanya uteuzi ni Mwenyekiti wa CCM.
Tunafahamu aliteua watu kutoka makundi mbali mbali wengi wao wakiegemea UCCM.

Kule znz , wajumbe 15 walikuwa katika uwiano wa CCM na CUF.
Ni haki kusema kuwa ndani ya tume ya Warioba, CCM ilikuwa na wajumbe wengi zaidi kuliko makundi mengine.

Na kubwa zaidi, wajumbe kama Salim Ahmed, Butiku na Warioba ni makada wa juu kabisa wa CCM.
Pengine wapinzani wangekuwa na hoja ya kusema, tume iliegemea upande wa CCM zaidi.

Baada ya rasimu ya kwanza ambayo Mwenyekiti wa CCM alikuwa na mawasiliano kama Rais, hali ikabadilika.
Hoja ya kwanza ya CCM ikawa muundo wa S3 utavunja muungano.
Likatengenezwa zengwe la kuanza hadaa katika mabaraza ya kata.

Pamoja na malalamiko ya wapinzani kuchezewa rafu, tume ilisimama kidete kupinga uhuni wa CCM katika mabaraza ya kata
Hapo nyongo ya CCM ikatumbuka.

Tukaanza kusikia Warioba anafanya usaliti. Haikuelezwa usaliti wa kitu gani akiwa mwenyekiti wa tume iliyosemwa na mwenyekiti wa CCM ni huru, mbali na vyama vya siasa.

Rasimu ya 2 ikatoka. Hujuma za awali zakapangwa.
1. Kwamba tume ya Warioba ivunjwe mara moja baada ya kukabidhi.
Hiki ni kinyume na uundwaji wa tume kama hizo kwingine duniani.
Lengo lilikuwa kuzuia tume isiingie katika BMLK wakati huo ili kuweza kunyonga rasimu yake.

2. Mwenyekiti wa CCM akatumia kofia yake ya Urais akishirikiana na Sitta kumtanguliza Warioba ili Rais apate nafasi ya kumkaanga. Ni kweli, kamdhalilisha mzee wa watu na tume yake.
Ikumbukwe, aliyedhalilishwa ni wazee wote wa CCM na wajumbe wa tume. Jina la Warioba ni kwa utambulisho tu.

Mwenyekiti wa CCM kupitia Ikulu akaagiza hata usafiri uliompeleka Dodoma bungeni uondolewe kwa Warioba.
Ni katika kumdhalilisha tu na wala hakukuwa na manti.

Hoja ya kuwa tume ilishavunjwa ni gharama kumhudumia Warioba kwa usafiri wa kurudi Dar, inajibiwa na biliobi 2.5 zilizotengwa na Ikulu kuhonga Wasomi na waandishi, tena Ikulu ikukubali kuwa imetoa waraka huo wa Hongo!

3.Jitihada za kuharibu bunge zikafanikiwa kwa ushirikiano wa Sitta na JK, na rasimu ya mafichoni ya Chenge ikaingia uwanjani.
Katika muda wote, ni rasimu ya Warioba iliyokuwa midomoni.
Ile ya Chenge ilipoingizwa bungeni, mjadala wa kitaifa ukafa, tukaona Sitta akitoa nafasi wajumbe wamtukane mzee Warioba.

4. Majuzi, baada ya katiba ya mafichoni ya Chenge kutolewa, hali imekuwa mbaya sana.
Hakuna anayejadili tena, imedoda.

CCM wakitaka uhalali wanasingizia ni maoni ya tume ya Warioba.
Wakitaka uhalali wa rasimu ya Chenge wanasema Warioba hakukusanya mawazo.

5. Majuzi, CCM kupitia Paul Makonda ikaanda mpango wa kuidhalilisha taasisi ya Mwalimu Nyerere.
Lengo ni kumhusisha Warioba na vurugu na wala si tume ya Warioba.

Mzee Warioba akanusurika maafa ambayo si vema kuyakumbuka.
Haya yalipangwa na CCM ili kuhakikisha mzee anadhalilika, kwa kipigo au lolote lile.

Wazee wa CCM akina Sitta na mwenyekiti wao wakatoka kushangilia tukio hilo.
Hawakukemea kwasababu ni mpango mahususi ulioratibiwa na CCM.

HADITHI IMEBADILIKA

Licha ya kudhalilishwa, CCM hawana hoja tena.
Katiba ya Chenge haijadiliki, na ikijadilika basi habari ni jinsi gani pipi na peremende zimetolewa kwa waznz.
Katiba haijadiliki hata vijiweni. CCM waliopewa kazi wanao aibu kuijadili.
Hakuna cha maana au cha ziada zaidi ya udanganyifu.

Hadithi imebadilika, sasa hivi kuna kauli za kumtaka Warioba arudishe kadi ya CCM
Kumtaka Warioba aungane na wapinzani.

Kuna makosa hapa! CCM ilimchagua Warioba afanye kazi ya taifa.
Katiba inayoandikwa si ya CCM ni ya taifa. Kitendo cha kusema Warioba amesaliti chama kinaonyesha, mzee Warioba alipewa kazi ya chama na si ya nchi.

CCM wanajichanganya, na ni ushahidi kuwa Warioba alisaliti rasimu ya mafichoni.

Kosa la pili, kama CCM wanataka Warioba arudishe kadi, basi wangemuomba Butiku, Salim Ahmed na wale wajumbe wa CCM ndani ya tume wote warudishe kadi.

Kwanini Warioba? Ikiwa kazi imehusisha wote na wamesaini.
CCM inapaswa kusema wajumbe wake ndani ya tume warudishe kadi na wala si mzee Warioba.

Hoja ya kumtaja Warioba, imelenga kumshusha hadhi na kumdhalilisha ikijua ni mzee mwenye heshima na heshima yake haihitaji pambo. Warioba ni maarufu na mwenye heshima kuliko kiongozi wowote wa CCM.

Njia rahisi ya kumshusha ni kumdhalilisha. Kwa bahati mbaya kila jaribio linamuongezea umaarufu.
Ndio msingi wa Warioba kufanywa kondoo wa kafara.

Kwamba akiwa public enemy number 1 basi wananchi wataacha kumjadili na kujadili rasimu ya Chenge.

Katiba ya Chenge imedoda, hilo CCM wanalifahamu.

Kumsakama Warioba hakuondoi ukweli kuwa katiba itaandikwa tena muda si mrefu ujao.
Hii ya CCM wataipitisha kwa maguvu, ya wananchi inakuja kwa maridhiano.

Tusemezane
 
KATIBU MKUU KIONGOZI ANAPOKUWA MSEMAJI WA CCM

ADAI VURUGUKWA WARIOBA NI SAWA NA ZA MWINYI

DALILI ZA AWALI ZA MATATIZO YA MUUNGANO ZAANZA

KATIBU MKUU

Wiki hiikatibu mkuu kiongozi kajitikeza kueleza kusikitishwa na vurugu zilizofanywa kwamzee Warioba.
Katibu kongozi kadai serikali inaangalia ulinzi wa viongoziwastaafu.


Alisema,tukio la Warioba ni sawa na lililomtokea Mzee Mwinyi baada ya kupiga kibao.

Wakatikatibu mkuu akisikitishwa na hali hiyo, Rais JK hakuonekana kusikitishwa.
Alisemaanaomba mungu yasijemkuta ya Warioba. Huenda kauli ya katibu mkuu ndiyoingekuwa ya Rais.
Kwa sababu zisizojulikana Rais hakuonyesha kusikitishwa .


Raisaliungana na Sitta katika kauli zilizoonyesha kutokuona tatizo kwaWaziri mkuu mstaafu kushambuliwa. Kinaschosikitisha Zaidi ni pale viongozi waserikali wanapokwepa ukweli kuhusu ushiriki wa CCM.

Paul Makondani mjumbe na kada mwandamizi wa CCM.Vurugu ziliandaliwa na Kada huyo akishirikiana na wahuni. Hili si tatizokama lililomtokea Rais mstaafu Mwinyi. Mwinyililikuwa tukio la kiimani lililofanywa na mtu mmoja.

Penginekufananisha ni pale ulinzi unapokosekana, lakini haya ni matukio yenye pichambili tofauti.
Alichokifanya katibu kiongozi ni kujaribu kupinda ukweli kuwaCCM wameshiriki.
Ni namna hiyo pia, msajili wa vyama yupo kimya. Sijuilingefanywa na CUF au CDM hali ingekuwaje.


Katibu mkuuaache kupotosha chanzo cha vurugu na wala haisaidii kuficha ukweli.
Huyu nimtUmishi wa serikali aliyejigeuza kuwa kada wa CCM akiwa msemaji kama Nape Nnauye.


KATIBA

Wiki hiitumeshuhudia Ikulu ikitoa Baraka za hongo kwa wanahabari na wasomi.
Hilo si lajabu, duru tumeliongelea kabla ya kutokea.


Pengine chaajabu kidogo ni maandamano yaliyopangwa na Wazanzibar kushinikiza watuhumiwa waUAMSHO warejeshwe znz kushtakiwa. Madai ya wznz ni kuwa watuhumiwa wahukumiwekule tukio lililpotokea na si Dar.

Wznzhawaelewi mahakama kuu ni jambo la muungano. Rasimu ya Warioba ilitoanafasi kwa kila taifa kujitengenezea utaratibu wake na kisha kuwa na Mahakam kuumoja.

Kwa rasimu ya Chenge, wznz wataendelea kushtakiwa, kuhukumiwa nakuadhibiwa Tanganyika.
Katiba ya Chenge iliyoungwa mkono na Wazanzibar inasemahivyo.


Hii maanayake ni kuwa dalili za mkanganyiko zinaonekana hata wakati huu katiba ya Chengeikiwa imedoda. Kama itapitishwa kwa maguvu, basi ipo siku wznz au Watanganyikawataamua kuchukua hatua mikononi kama ambavyo wznz wameanza.

Hapomuungano utavunjika tu. Wananchi wanapokuwa na hasira busara huwa mbali.

La znz kama siyo ‘kifungua macho' ni ukweli unaosubiri muda tu


tusemezane
 
MATATIZOWASIYO YAONA CCM NA WAZANZIBAR

Bandikolililotangulia tumeeleza kwa ufupi tatizo la wznz kudai watu waowashtakiwe znz na si mahakama kuu ya JMT.
Hilo tu linaeleza
kutokuwepo kwa mamlaka kamili.

Na mbele yasafari watashtakiwa Zaidi, watahukumiwa na watafungwa Tanganyika.
Ndivyo katibaya 1977 ambayo Chenge ame copy inavyosema


Kibaya zaidi,Rais wa znz kuwa makamu ni kumuondolea nguvu yake visiwani ili kutekeleza matakwa ya Tanganyika.
Mh Jumbe alikuwa mwenyekiti wa baraza la mapinduzi ,Rais wa znz na makamu wa kwanza wa Rais.
Alipotenda kinyume na maelekezo yaDodoma, aliitwa na hadi leo ni hadithi.


Katiba yaChenge ndivyo inavyosema . Hivyo wznz wanaodhani Rais wa znz kuwa makamu waRais ni jambo jema, wajiulize kwa kuangalia yaliyomtokea Jumbe.

Haiwezekani Raiswa znz akawa na nguvu kuliko za umakamu wa Rais wa JMT.
Mamlaka kamili yapo wapi?

Rais Kikwete amesema, katiba ya Chenge inawapa wznz uwezo wa kupata udhamini wa mikopo namisaada wakihitaji. Ikumbukwe katiba inayowapa uwezo huo ni ya JMT ambayo ni Tanganyika.

Hivyo, wznz itabidi waje kuomba na wanaweza kuwekewa masharti kulingana na nyakati.
Watakuja kuomba wadhaminiwe na Tanganyika na wala si kuamua. Wznz wajiulize mamlaka kamili yapo wapi hapo?


Wznzwanaambiwa ruhusa kujiunga na taasisi za kikanda kama EAC,SADC n.k.
Ni lazimawaelewe kuwa ada za taasisi hizo ni jukumu lao.

Ikibidi msaada itabidi waombeTanganyika. Hivyo maamuzi yao lazima yakubaliane na Tanganyika wanapokuwa katikataasisi hzo za kikanda. Ndio lazima wakubaliane na mwenye uwezo anaywadhamini

Mamla kakamili yapo wapi?

Na katikamaamuzi, mwakilishi wa znz katika taasisi hizo ni Rais wa znz ambaye ni Makamuwa Rais wa JMT.
Wajibu wake kwanza ni kuitetea katiba na masilahi ya JMT ambayo ndiyo mwajiri na inamlipa mshahara.
Kila atakaloamua lazima akumbuke linahitaji akubaliane na Rais wa JMT ambaye ni bosi wake.
Mamlaka kamili yapo wapi?


Wazanzibar lazima wawe macho. Kuna big G wanazopewa bila kuangalia athari za muda mrefu.

Lakini piaWatanganyika lazima wajiulize. Katiba nzima ya Chenge imelenga kuwaburudishawznz kwa gharama zao.
Nini faida ya investment hiyo.

Kwanini katiba ya Chenge ambayo nitoleo la mwaka 1977 lililobadilishwa lijadiliwe achilia mbali kupiga kura ya maoni.

Wananchi wapande zote wajiulize, wanajadili kura za maoni kuhusu nini ikiwa maoni yaohayakuzingatiwa?
Je, maoni yao ni yale ya tume ya Sitta na Chenge?


Jambo moja tu la kukumbuka, katiba ya sasa ni matatizo, hiyo ya Chenge ndiyo itakayohitimisha muungano siku si nyingi.

Tusemezane
 



VURUGUZILIPANGWA KUHARIBU ELIMU YA UMMA

CCM WAANZAKAMPENI KINYUME NA MAAGIZO YAMWENYEKITI WAO

SHEINAENDELEA WILAYA 12, NAPE NA KINANA MIKOA YAKUSINI

Baada yakushambuliwa mzee Warioba, Rais ambayeni mwenyekiti wa CCM alizungumza Dodomana wazee wa mji huo. Alisema, serikaliyake ina muda uliopangwa wa kampeni yakura ya maoni ya katiba ya CCM

Wakati akisemahivyo, Rais Shein wa znzanaendelea na mikutano ya kunadi katiba ya Chenge.
Ratiba imetolewa ya Shein kuwa na mikutano na wana CCM kwa wilaya 12 za Znz.
Ndivyo ilivyo kwa Kinana na Nape kwenda mikoa ya kusini.



Hayoyanatokea baada ya Ikulu kuidhinisha fungula bilioni Zaidi ya 2 za kuhongawana habari na kununua wasomi. Fungu huendalimetoka na mikutano ya kunadikatiba ya CCM kwa wana CCM imeanza.

Ni kwa maanahiyo, tunasisitiza kuwa katiba yaChenge ni ya CCM na wana haki ya kunadikatiba yao.
Si katiba iliyotokana na maoni ya wananchi, bali katiba ya CCMinayofanyiwa hilakuwa ya wananchi.



Mikutanohiyo inafuatia kudoda kwa katiba yaChenge. Ni kama vile hakuna tukio kubwakama ilivyokuwa kwa tume ya Warioba.Hiyo nidalili kuwa wananchi hawajaridhika na wamesusa katiba ya Chenge na CCM.


WAPINZANI

Mara zotetumewaasa wapinzani kuwa katiba ni yaCCM.
Mchakato mzima haukuzingatiademokrasia achilia mbali udanganyifu hata pale CCMwalipobaki wenyewe.

Mnakumbuka Zakhia Meghji kuwa Mtanganyika katika gazeti la serikali nakuwamzanzibar wakati wa kupiga kura za BMK la CCM



Wapinzani hawapaswikuongelea kura ya maoni,kwamba watashawishi wananchi wapige kura ya hapana.Kufanya hivyo ni kutoauhalali kwa kile kisicho na uhalali tena wananchiwakionyesha kwa uwazi kabisakupinga


Wapinzaniawana hoja kubwa mbili


1. Mchakatoulivurugwa na CCM wakaimtumiamwenyekiti wao na umma uliona


2. Maoni ya wananchikwa kutumia tume ya Wariobayamedharauliwa


Hoja si kura ya ndiyo au hapana. Hojawanayotakiwakubeba UKAWA kama walinzani r ni kuwa katiba ya nchi itaandikwa.Kwamba,madai ya katiba mpya hayajatekelezwa na huo ni mwanzo wa kudai katibampya.


Ni kazi ya wapinzani kuwasaidia wananchikuelewaudanganyifu uliofanyika.
Endapo wataendelea na suala la kura ya hapana,hilohawatafanikiwa.

Ikiwa waziri mwandamizi na mzee kama Sittawamewezakujiibia kura wakiwa wenyewe bila haya, ni ngumu kwa tume ya uchaguziyataifa-CCM kutoa haki kwao.
Hivyo wasitarajie kuwa hoja ya hapana itashinda hatakama imeshinda.


Lazima wajiulize utoto uliofanywa kwa kudanganyaumma.

Ni utoto kwasababu anaposimama mtu mzimakuteteahoja ya Zakhia , au kura mbili za maruhani au wapiga kura wasiokuwepobungeni,huo hauwezi kuitwa wendawazimu.
Ni utoto na hivyo wapinzani wasidhani kunanamna wanaweza kuzuia utoto huo.


Tusemezane



 
ELIMU YA UMMA MARUFUKU
ELIMU YA KATIBA YA MAFICHONI YA CHENGE RUKSA

TUME YA WARIOBA KUBEBA LAWAMA
WAMETISHWA , KUNA DALILI ZA KUOGOPA

Suala la latiba si la wabunge ni la wananchi. Katiba ya CCM inayopenekezwa imeanza kupigiwa debe na viongozi wa CCM.
Hilo si tatizo endapo hawatailazimisha kuwa ya wananchi kama wanavyotaka.

Hadi sasa imedoda, na hakika CCM wajiulize kama hali iliyopo inajenga muafaka wa kitaifa

Vurugu alizofanyiwa Warioba zimepata Baraka za CCM na Serikali yake.
Tumeeleza jinsi katibu mkuu kiongozi alivyogeuka kuwa msemaji wa CCM badala ya kiongozi wa umma

Rais wa JMT badala ya kukemea vurugu, aliomba mungu yaliyompata Warioba yasijemapata hata kama yatawapata raia wengine.

Vurugu zile zilipangwa mahususi ili kuhakikisha kuwa tume ya Warioba haina nafasi ya kueleza, kufafanua na kubainisha uovu uliotendeka na unaotarajiwa kutendeka.

Wametumwa wahuni, hadi leo wapo mitaani tena wakiwa na nafasi zao za uongozi ndani ya CCM, ikiwa ni ishara nzuri kuwa suala hili liliratibiwa vema na CCM na serikali yake.

ILIYOKUWA TUME YATISHWA

Vurugu zililenga kuwatisha akina Warioba.
Jitihada za kuwatisha kisiasa zimekwama na sasa nguvu za kujeruhi zikatumika

Inaonekana tume ya Warioba imeanza kuahirisha mikutano yake pengine kwa hofu zaidi ya kudhurika au kudhuriwa kama ilivyotokea Ubungo plaza.

Iliyokuwa tume ililenga kutoa elimu ya umma. CCM hawataki hilo kwasababu wanataka kutumia jina la tume ya Warioba na maoni ya wananchi ili kujenga uhalali kuwa katiba ya Chenge imetokana na maoni ya tume ya Warioba.

Tume ya Warioba itakuwa imefanya makosa makubwa sana kama itaruhusu itumiwe kuhalalisha rasimu ya mafichoni ya CCM.

Maoni ya tume yametupwa, iweje tume ikubali kutumika na CCM katika kunadi katiba ya CCM?

Mbele ya safari, tume itajikuta inabeba lawama kutokana na rasimu ya Chenge ambayo haina uhusiano au maoni yanayofanana.

CCM watageuza kibao na kusema yale yalikuwa maoni ya tume ya Warioba.
Watakapofanikiwa kukungumiza katiba yao, atakayebeba lawama ni tume ya Warioba

Ni kwa msingi huo, tunasisitiza kuwa tume iendelee na kutoa maoni na kile walichokiona bila kuingilia suala la kura ya maoni ya CCM.

CCM wana haki ya kupiga kura za maoni kama ambavyo wananchi wana haki ya kudai katiba itakayoandikwa kwa maoni na matakwa yao, na wala si hii ya CCM ya mafichoni iliyoandikwa na akina Chenge

Tusemezane
 
KATIBA YA KUSHINIKIZA NA HATIMA YA TAIFA

JK HATAKWEPA LAWAMA MAMBO YAKIHARIBIKA

NGUVU ZINaZAOTUMIKA ZINACHAGIZA VURUGU BARA NA ZNZ

Rais Kikweteameendelea na shinikizo kupitisha katiba ya Chenge

Rais amejivika jukumu la tume ya uchaguzi la kutangaza utaratibu wa kura ya maoni

Rais alipiga marufuku kampeni , akiruhusu ziendelee kwa chama chake.
Hilo linashadidia ukweli,kinachoandikwa ni katiba ya CCM kwa mujibu wa taratibu zao

Kuna tartibuza kisheria zenye utata. Kura ya maoni lilipaswa kujadiliwa na Baraza lawawakilishi.
CCM imeona ni kikwazo, na hivyo kuendelea kuburuza umma ikijua ndani ya BLW hakuna uwezekano wa muafaka


Kwa mujibu wa katiba ya Zanzibar iliyofanyiwa marekebisho 2010, ili muafaka upatikane n ilazima iwepo 2/3 ya wajumbe.
Hali ya CUFna CCM kwa jinsi ilivyo, hakuna 2/3.


Hilo ndilo linawasukuma CCM kuendelea na katiba ya Chenge kana kwamba hakuna taratibu nyingine za kisheria

Wanategemea ubabe kama ule wa BMLK nakutumia vyombo vya umma kuendeleza' uhalifu' ule ule wa BMLK katika umma

Hii maana yake,katiba ya Chenge iliyosusiwa itakosa uhalali wa kisheria visiwani.

Hataikipita, kipindi cha mpito cha miaka 4 hakiwezi kutoa matokeo tofauti na sasa.

Rais aliachaznz warekebishe katiba yao 2010 katika kuwafurahisha .
Leo katiba ile ile aliyoiruhusu ina mhukumu, anajitahidiku kwepa ukweli wa mazingira tengefu aliyoyatengeneza.

Wazungu wanasema ‘what goes around comes around''


Ukweli kuwa katiba ya Chenge haikutokana na maoni ya wananchi , na wala haikufuata taratibu kama ilivyoendeshwa na Sitta, inaeleza jinsi itakavyoweza kuwa chimbuko la uvunjifu wa Amani katika nchi yetu

Kwa upandewa Tanzania bara, kuna duku duku la wananchi kususiwa maoni yao.

Haliiliyopo hasa mijini inaonyesha bila kuhitaji utafiti,
katiba iliyoandikwa na Chenge kwa mhuri wa CCMimekosa hamasa, imesusiwa na inajenga chuki katika jamii


Kwa upandewa visiwani hai ni mbaya. Upinzani usio na suluhu utachochowe na uwepo wakatiba mpya.

Ukiukwaji wa sheria na katiba ya znz utachochea matatizo makubwa.Kwanza, kuporomoka kwa serikali ya umoja wa kitaifa.

Kama itakuwepo, itakuwa ni dhaifu.

Pili, migogoro itakayohusishwa makundi hadi yadini kwa kuangalia jamii ilivyo, na mwisho kukoksekana kwa mufaka wa jambo lolote ndani ya BLW


Hivyo, anawezakushinikiza katiba ya Chenge kwa kutumia vyombo vyake kama NEC, polisi na usalama wa taifa.

Jambo atakaloondoka nalo au kumwachia atakayemrithi ni taifa lenye mashaka na pengine lenye vurugu kubwa


Vurugu za katiba zimeparaganyisha mataifa mengi.

Tusemezane
 
UTEUZI WAWAKUU WA WILAYA.NIMAANDALIZI YA ‘KURAYA MAONIYA CCM''

TAIFA NJIA PANDA, NI MAANDALIZI YA VURUGU


WAPINZANI MNATAMBUA HILO?



Yamekuwepomalalamikokutoka kwa wasomi, wanasiasana wana harakati kufuatia uteuziwawakuuwa wilaya.
Malalamiko ni pamoja nakuteuliwa kwa watu wasio na sifa au uzoefu kusimamia
Wilaya


Uteuzi wa wakuu wa wilaya umekuja takribani miezi miwili kabla ya kura ya maoni kuidhinisha katiba ya CCM

Uteuzi umelenga kuhakikisha katibaya CCM si kuwa inapita, bali inapita kwa kishindo hata kama ni hujuma ilikuueleza ulimwengu uhuni uliofanywa katika bunge la Sitta ulikuwa na uhalali

Wengi wanatoa mfano wa wakuu wa wilaya walioteuliwa kama kichekesho.
Orodha hiyo wapo watoto
wa vigogo waliotoa mchango katika kuiweka na kuitetea serikali ya CCM,ikiwa ni zawadi.


Wapo wasio na sifa za uongozi hatawa kata ambao sasa.
Mfano umnaosemwa ni
wa mkuu mpyawa wilayaya Kinondoni, Paul Makonda.


Makonda nimhamasishajiwa CCM chipukizi, ukiwa ndio wadhifa wake mkubwa aliowahi kuutumikia kisiasa.
Makonda alipata wadhifa huo kama kipoozeo
baada ya mtafaruku ndani yaUVCCM.


Katikawadhifa huo wa chipukizi, amefanikiwa kuwa msemaji wa kundi linalopingana namgombea Urais mtarajiwa EL. Makonda amemshambulia pembeni na hadharani na amekuwa chanzo cha mtafaruku wa makundi.

Lakini hichoni sehemu tu ya sababu za kupewa ukuu wa wilaya. Inategemewa, katika wadhifa huo, itasaidia kupunguza makali dhidi yaEL. Makonda atakuwa kiongozi wa chama na serikali, kauli zake zitakuwa zimefungwana miiko ya uongozi

Kubwa Zaidi nikuwa, Makonda ndiye aliyeongoza genge lililomshambulia Jaji Mzee Warioba katika ukumbi wa Ubungo plaza. Kazi ile ilungwa mkono na Rais ambaye ni mwenyekiti wa CCM kwa kusema ''warioba ameyataka, na anamuomba mungu yasije mkuta''.

Hivyou teuzi
wa Makonda una sehemu mbili katika hili la kumsahmbuliwa Warioba.
Moja, kumzawadia
kwa kufanikiwa kuzima harakatiza kamati ya Warioba.

Tangu shambulio lile kamati imekuwa kama inmeingiwa na hofu ya mashambulizi Zaidi.

Pili,Makonda anaandaliwa katika eneo la Kinondoni ili kuongoza vurugu za kura ya maoni ya katiba ya CCM inayoandaliwa kuwa ya Taifa

Na huendawakuu hao wa wilaya ni nguvu mpya ya kuhakikisha CCMinapitisha katiba yake kwa utulivu, na kwamba vijana hao wataweza kukabliana nanguvu yoyote ya kisiasa ikiwemo kuswake ndani wanasiasa. Hapo ndipo vuruguzinazolinyemelea taifa zitakapoibuka



Wapinzaniwameliona hilo?

Inaendelea ……
 
WAPINZANI MUMELIONA HILO KWA JICHO LA PILI?

Kutokanana maandalizi ya serikali katika uteuzi, ile hoja yetu ya kuwa nasihi wapinzani wasishiriki au kuzungumzia katibainakuwa na mashiko

Kuzungumzia katiba tu ni kuipa uhalali. Kushiriki ni kutoa Baraka baada ya kuipa uhalali stahiki.
Katika mazingira ya akina Makonda kuwa wakuu wa Wilaya, hakuna uwezekano wa kuzuia walichopanga


Ikiwa CCM na Samwel Sitta waliweza kujiibia kura, ni jambo la kushangaza kama Makonda aliyeongoza vurugu dhidi ya m zee Warioba, na ambaye sasa ‘ametunukiwa ' zawadi kukaa kimya.

Hakuna,tunarudia hakuna namna ambayo kura ya maoni ya katiba ya CCM inaweza kuzuiwa.

Kwa upande mmoja tume ya uchaguzi ambayo ni tawi tanzu la CCM, vipo vyombo vya dola kama Polisi kwa kutisha,usalama wa taifa n.k. ambavyo vyote ni sehemu ya CCM.
Nani anaweza kuzuia uhalifu kama ule wa mzee Sitta pale Dodoma
?

Kuliko kuingia katika ulingo wakijua kila sehemeu ya ulingo, waamuzi na watoa point ni wafanyakazi wa mpinzani wao, itakuwa ni kosa kubwa la kisiasa nakihistoria.

Lakini pia historia ina nafasi yake. Wapinzani wakisusia, historia itawatoa katika ‘pingu'zitazotokana na matatizo mazito ya katiba yanayokuja mbeleni.

Si suala lakususia katiba ya Chenge, ni suala la kutoongelea kabisa.
Hakuna uhalali wa kisiasa, kijamii au iwavyo uiojengwa na katiba ya Chenge

Wapinzaniwanapaswa kuchukua hatua madhubuti za kukaa mbali na akina Makonda
walioandaliwa kuleta vurugu. Waache CCM imalize kazi yao , na wao waanze kazi ya kudai katiba mpya ya nchi.


Tusemezane
 
VURUGUZIMEANZA HONG KONG

WANAOZUNGUMZIAHONG KONG. HOJA IPO WAPI?


NI kawaida kusikia wanasiasa wa Zanzibar wakitolea mfano wa muungano wamaeneo kama Hong Kong, Macao n.k. Hoja yao kubwa ni kuwa nchi hizo zimepewa ‘fullautonomy' mamlaka dani ya taifa la China


Wanasiasa wanaochukua hoja kwa wepesi na baadhi ya wanaduru wanadandia hoja nyepesi,leo watakuwa wamepata jibu la matatizo ya mfano wa Hong Kong

Hong Kong ni sehemu ya China inayojulikana kama ‘special administrative region'

Ukiacha ulinzi na mambo ya nje, shughuli nyingine zote zipo chini ya serikali ya HongKong.

Katika mambo ya nje Hong Kong ina balozi zake tofauti na balozi zilipo china kwa maana kuwa zinajitegemea.
Hong Kong ni ya tatu duniani katika taasisiza kifedha ikifuatia London na New York.



Taarifa ya habari ya BBC imeonyesha vurugu kubwa zilizotokea Hong Kong.
Wananchi wamepinga wimbi kubwa la wafanyabiashara kutoka China wanao nunua bidhaa na kuzipelekaChina.

Hong Kong haina kodi za muazo'sales tax' bidhaa zake zikiwa na bei nzuri.
Wafanyabiashara kutoka China bara, hununua bidhaa na kuziuza nchini kwao kwa faida.

Halihiyo imeongeza mahitaji ya bidhaa nchini Hong Kong na kusababisha ongezeko labei' supply and demand''


Wa Hong Kong wanataka kupiga marufuku wafanyabiashara,kupunguza hal ihiyo inayowasababishia hali ngumu ya maisha

Mfumo wa muungano wa Hong Kong na China ni ‘one country, two systems' kwamba nchi mojamifumo miwili .
Hilo ndilo linaonekana kuwa hoja hapa nchini kuwa S2 ni mfano wa China


Ukiangaliakwa undani hakuna ufanano kabisa. Ni mifumo miwili iliyo na tofauti kubwa sana.

Ni kwa mtazamo huo tume ya Warioba ilibaini tatizo na kuto upendekeza kwakuzingatia mazingira yetu


Tatizo linalowakumba Hong Kong lipo nchini ingawa halisemwi. Wazanzibar huwachukiawaba bara kwa kuhisi wanawachukuliwa fursa.

Na wznz wanataka kuwa na mifumo yao ya fedha na kodi. Malalamiko yao ni kuhusu kodi zinazotoswa bidhaa zinazoingiaTanganyika. Kwamba, ni kubwa hasa tukifahamu znz inatoza kodi ndogo, na pengine kutotoza kabisa kwasababu sehemu kubwa ya mapato yake si uchumi kama HongKong, bali bakuli ‘hand outs' kutoka Tanganyika


Kwa mfumo wasasa na wa Chenge, kutakuwa na ugomvi unaohusu masilahi.

Kwanza, wznz watataka soko la Tanganyika, lakini Watanganyika hawatakubali soko lao litumiwe hovyo kwa kutokusanya kodi au misamaha isiyo na maana


Jaribio la awali lilishindikana, na matatizo yaliyopo ni makubwa kuliko Hong Kong kwakuzingatia kuwa znz ni tegemezi kwa mambo mengi kutoka Tanganyika

Hili ndilo linatusukuma kwa dhati kabisa kusema, huu muungano upo karibu sana kuvunjika kuliko ilivyokuwa huko nyuma.

Hong Kong nimfano mzuri si wa muungano bali matatizo mazito yatakayovunja muungano wa Tanganyika n zanzibar

Tusemezane
 
DALILI ZA VURUGU ZINAANZA KUAPALILIWA
BAADA YA LUKUVI, SAMWEL SITTAKASHIKA ‘KIBIRITI'

Sehemu ya I

Tunakumbuka waziriLukuvi alipokwenda kanisani kwa niaba ya waziri mkuu na kuchochoea muundo wa Serikali. Alichosema Lukuvi , S3 zitaondoa udhibiti wa Zanzibar yenye waislam wengi

Katika bungela katiba, Samwel Sitta alifanya yasiyosemeka. Aliunda tume ya maoni bila sheria,akaruhusu mahujaji wapige kura ya ‘face book' na kuchukua kura za ‘UKAWA' wawili bila kuwepo bungeni na kinyume cha utaratibu

Sitta,alimgeuza Mama Meghji kinyume cha tangazo la gazeti la serikali.
Mwisho kupitisha katiba ya Chenge hata pale idadi ya CCM waliobaki haikutimu

Sitta naLukuvi walitenda makosa katika uongozi unaojali demokrasia, utawala wa sharia na maadili, leo wasingekuwa viongozi. Walilitishia Amani na umoja wa kitaifa.

Kilichofuata ni Sitta kupewa nishani ya juu ya taifa December 9 2014, Lukuvi kubaki waziri

Sitta amekaririwa na sauti ya America (VOA) akisema, wznz waliondolewa mwaka1964 na kwenda Oman.
Kutoa Uraia pacha kutawarudisha katika na kupindua SMZ


Kauli yaSitta inashadidia aliyoyafanya BMLK kuwa ni makusudi ili kulinda mfumo wa S2,pengine kuzuia kupinduliwa SMZ.

Kauli ya mapinduzi ilitolewa pia na Rais wakati anafungua bunge la katiba ingawa yakeilikuwa ya ujumla

Kauli yaSitta ina ukweli wowote?
Hakuna ushahidi wa kuwepo na jaribio la tangu mapinduzi ya 1964.
Mapinduzi yaliyofanyika Afrika siku za nyuma yalikuwa ni mipango iliyohusisha mataifa mengine.


Mapinduzi hayahitaji mtu awe raia, yanaweza kutokea yakichochewa na chanzo chochote .
Hata hao wa oman, si lazima wawepo wakitaka.
Hoja hii haina maana na ni hatari sana kwa mustakabali wa taifa

Kwanini kauli imetokewa?

Kauli hiyoni jitihada za kuwagawa wazanzibar katika matabaka ya rangi.
Baada ya hoja ya udini kushindwa, na kwa muonekano wa katiba ya Chenge kudoda, CCM wametafutambinu mpya ya kuwagawa wazanzibar ili ,mradi wao utimie

Wanawagawa vipi na kwanini


Inaendelea……
 
Sehemu II
CCMwanatambua donda la chuki za rangi lililopo Zanzibar kwa miaka mingi.Wanatambua njia nyepesi na rahisi yakuwagawa wznz ni kuleta hisia za usultani ili kuwepo Watwana na mbawana, kwahisia tu kutokana na historia ya nyuma

CCM inatambua nguvu ya dini kama ilivyotumiwa na Lukuvi inajenga ufa si kwa wznz bali wznz na Watanganyika.
Pia wametambu kuwa udini unaweza kuwa kiungo chema kwa wznz kuliko kuawagawa


Na pia, CCMwanatambua kuwa uwepo wa serikali ya umoja wa kitaifa, ni kikwazo kikubwa cha mipango yao kutokana na kukosekana kwa 2/3 kila watapohitaji

CCM wanatambua kuwa, katika mazingira yaliyopo mswada wa kufuta serikali ya umojawa kitaifa hautafanikiwa na hivyo katiba ya Chenge itabaki kama kinyago. Na kubwazaudi, CCM wanatambua kuwa suala la katiba linawagawa wznz

Mgawanyo ni ½kutoka pemba hadi Unguja. Hivyo, hakuna uwezekano wa kupata 2/3

Hesabu za CCM ni kuwa , upo uhakika wa kupata ½ ya kundi wanalolilenga.

1/3 nyingine nilazima watie fitna ili baadhi ya watu waingiwe na hofu na kupunguza wingi wakundi jingine.
Huo ndio msingi wa kutumia maneno ya Waarabu watarudi,kupinduliwa serikali n.k. kama alivyokaririwa Samwel Sitta


Nani wakulaumiwa?
Wznz wajilaumu wenyewe. Hizi mbegu za kibaguzi walioanza kuzipanda ni wao wenyewe,wanaozimwagilia ni wao wenyewe.

Mathalan, tulitegemea wznz wa makundi yote wajitokeze na kumkana Sitta ili kukomesha tabia za uzushi. Hakuna! Na wala tusitegemee Vuai, Nahodha, Seif Idd n.k. wajitokeze kutetea umoja wao wakitaifa


Wzn asimlumu mtu, kitabu cha ubaguzi wamekandika wao kuanzia zama hizo, na hadi wakati wa chaguzi zilizomwengua Salim Ahmed kwa kutumia mbinu wanazotumia CCM.

Ni haki kusema Samwel Sitta plays the script written by znz themselves.


AsichokielewaSitta na Lukuvi ni kuwa machafuko yaktokea katika hali iliyopo, ni Watanganyika watakaobeba mzigo.

Sitta amesahau kuwa znz ni pipa la petrol linalilosubirikibiriti. Na hakika CCM na Sitta wanaanza mchezo wenye mauti kwa wananchi


Vurugu wanazochochea Lukuvi, Sitta na wenzake ndizo hasa zitahitimisha muugano

Kwasasa wznz wanazidi kujenga chuki na Watanganyika, na Watanganyika wameanza kuchoka kuhusumgooro ya znz.

Muungano upo njia panda


Tusemezane
 

DALILI TARATIBU ZINAJITOKEZA
Rais aonya, watakaoletea vurugu ‘washughulikiwe'
Katibu Myeka wa Rais Nyerere atoweka nyumbani kwake
Kuna BAKWATA na ''UKAWA-Waislam''
Kuna KATOLIKI na ''UKAWA-Wakristo ''
Mwaziri kila mmoja atoka na kauli yake

Hadi hapo , watu hawaoni tatizo?
Inafuata…
 
DALILI ZIMEANZA, MBELENI KULIKONI?

Tumesisitiza kila mara kuwa kunapokosekana muafaka wa kitaifa, ni rahisi kwa nchi kuingia katika haili ya sintofahamu

Ni wazi suala la katiba mpya limeigawa taifa kwa mjia nyingi

1. Katika misingi ya kisiasa hasa vyama
2. Misingi ya dini
3. Kutoheshimiana

Tunaelewa siasa ilivyovuruga mchakato mzima wa katiba mpya.
Ni mchakato ulioandaliwa katika mazingira yasiyoruhusu sauti za wananchi bali wanasiasa.

Tulisema kuwa katiba huandikwa na wananchi, wanasiasa hutunga sheria ndogo kuhusisha sheria mama ambayo ni katiba

Wanasiasa wakaingia katika mchezo wao mchafu, kila jambo likipelekwa kisiasa na kwa kasi kana kwamba bila katiba nchi haiwezi kusimama. Kasi ilitotumika ilikuwa na sababu za ubinafsi.

Rais: Juzi akiongea na ma DC wapi Rais Kikwete ameagiza kuwashughulikia watu watakaovuruga mchakato mzima.
Haieleweki kuvuruga kuna maana gani kwasababu wanaovuruga mchakato ni wanasiasa wa chama chake

Uandikishaji wa daftari la kura una matatizo makubwa yanayoonyesha bila shaka zoezi ni tanuru la kuoka vurugu.

Hili linaonekana bara na kule visiwani ni 'bomu' linalosubiri tu sababu.

Kuna malalamiko kuhusu kuvurugwa kwa mchakato mzima na katiba ya Chenge kutotokana na maoni ya wananchi

Haihitaji degree kutambua kuwa wananchi wanaliona zoezi zima katika hali ya utapeli.

Hakuna hamasa waliyokuwa nayo kwa rasimu mbili zilizotangulia.

Ubaridi wa wananchi hauonyeshi kuridhika, unasema jambo kubwa tusilolijua. Muda unaweza kutueleza

Kauli ya Rais ililenga maeneo haya
1. Kuwapa nguvu viongozi kuhakikisha katiba wanayoitaka CCM inapita hata kama ni kutumia nguvu
2. Kuhakikisha wapinzani hawaongelei katiba ili CCM wafanye 'mambo yao kwa amani'
3. Kuwatisha wananchi kuhusu hali ya baadaye kama sehemu ya kuwanyamazisha

Muhimu ni kuwa Rais ametambua hali si nzuri, kinachofanyika sasa ni kumaliza tu zoezi na anajua fika uwezekano wa kuzuka vurugu ni mkubwa. Hivyo anajaribu kuwa mbele ya wakati kutokana na ukweli.

Inaendelea... Dini
 
Inaendelea..

DINI
Tatizo la makundi ya dini nalo llimejitokeza kwa kasi

Kuna Waislam wasiokubaliana na wenzao wanaowataja kama BAKWATA.

Wapo wakristo katika majukwaa yao wasiokubaliana na wenzao wa katoliki wakiongozwa na Pengo

Kuna tatizo kati ya dini mbili, kwamba kila mmoja anajaribu kuangalia masilahi wakigawanywa na mahakama ya kadhi

Viongozi wa dini wamekuwa mstari wa mbele kuleta pamoja pande za kijamii zinazosigishana.

Tumeona sala za kuombe taifa zikiyaleta makundi na dini tofauti pamoja, dini na serikali, watawala na wapinzani n.k

Dini ilikuwa inatumiwa kama suluhisho kwa kile kinachoitwa 'kuliombea taifa amani''

Kwa hali ya sasa, mambo ni tofauti. Kuna mtafarauku miongoni mwa makundi ya dini, serikali na wapinzani, serikali na dini n.k.

Malumbano yasiyoisha yametokea wiki hii kati ya makundi na dini tofauti na kwa kiwango kikubwa kati ya dini na serikali.

Waziri mkuu akilumbana na waislam, waziri wa sheria akisemezana na maaskofu, Bunge likiubuka na malumbano na viongozi wa dini

Katika hali hii, hakuna msuluhishi wa mgogoro. Wale viongozi wa dini wasuluhishi sasa ni sehemu ya mgogoro kwa ujumla wake

Tunauliza, nani ataongoza sala ya ''kuombea amani taifa'' ikiwa viongozi wa dini ni sehemu ya mgogoro?

Hali ipo kule znz ambako mtafaruku wa siasa ni sehemu ya maisha kwa muda mrefu na kwa historia ya visiwa hivyo

Ingawa suala la dini halionekani kwa uwazi, ukweli ni kuwa lipo likiwa limefichwa katika ubaguzi wa rangi, ubaguzi wa maeneo na ubaguzi wa hadhi ya wananchi.

Wapo wanaoona nchi ya znz ni ya wote na kila mmoja ana haki
Wapo wanaoona nchi ni mali ya kundi fulani
Wapo wenye hofu isiyojulikana inatoka wapi

Kwa pamoja wanaweza kuonekana wana imani moja, tatizo ni kuwa tofauti nyingine zikichagizwa na tafsiri za watu kiimani zinaigawa znz kuliko inavyofikiriwa.

Mfano mzuri ni Somalia ambapo asilimia 99 wana imani moja. Tofauti zao za kijamii zilkichagizwa na mitazamo tofauti ya kiiamani (iwe sahihi au la, iwe ukweli au kupotosha) zimelivuruga taifa hilo kabisa

Katika mazingira yaliyopo, ni kujidanganya kama hatukubali kuwa hali ni tete na inahitaji fikra

Nchi hii ni ya watanzania na litakapotokea lisilotarajiwa hakuna atakaye kuwa salama

Wanasiasa waelewe nchi ni mali ya watu na si kundi la watu. Ni busara kuangalia hali kuzuia uharibifu mapema.

Uharibifu hauzuiwi kwa uharibifu. Maguvu na matumizi ya vyombo vya dola hayawezi kuleta amani.
Kama maguvu yangeleta amani, basi kusingekuwa na vurugu duniani

Hali inayoanza kujitokeza ni dalili twendako tunahitaji umakini

Tunauliza, hivi nani aliyebaki atakayewaongoza watu katika 'sala ya kuombea amani taifa''

Amani si zao la maneno, ni zao la uadilifu na unyenyekevu. Mambo hayo hayapo nchini kwasasa.

Hakuna kuheshimiana, dharau, ubabe na uhuni vimetanda kila kona

Hakuna busara kati ya wananchi, viongozi wa dini au serikali.

Tumebaki kuwa kama 'wanyama' katika zizi kila mtu akikurupukia upande wake

Kwa mtazamo huu tukubaliane ipo haja ya kurudi katika ubao, tukae pamoja na kufikia muafaka

Huu ubabe na uhuni unaonendelea unajenga mazingira mazuri ya hali tete na tata katika siku za usoni

Viongozi wa kisiasa, mnaliona hili? Mnasubiri uharibifu kwanza ndipo mkae mezani?

Je, hali ya vurugu hionekani kwa kuzingatia mtiririko wa matukio yanayojitokeza?

Tunasubiri manabii au mitume watujibu kama sala zetu zimeshindikana au zimekubaliwa?

dalili zinazoendelea haziwezi kuwa tahadhari kama sehemu ya majibu ya sala 'za kuobea amani taifa'?

Tusemezane
 
Back
Top Bottom