Duuuh!! Mwacheni Nasibu aitwe 'Diamond Platinumz'

Kama ni Oman kati ya watu watatu mmoja anakijua Kiswahili na ndo maana hakuna Taifa linalozungumza Kiswahili nje ya bara la Africa zaidi ya Oman

Na nina uzoefu mmoja niliwahi kuenda bank yao moja pale 'Muscat' nikawa naongea Kiswahili na mwenyeji wangu na kuna dada alikuwa ndo atuhudumie nikashangaa yule dada nae akaunga kwa Kiswahili na nikamuuliza ana Asili ya huku akasema kafundishwa nyumbani na wazazi wake wao waliishi huku japokuwa yeye hajawahi kanyaga Africa kwa maelezo yake

Kwahiyo kama Oman lugha ya pili ukitoa kiarabu ni Kiswahili na kuna wengine wanaongea Kisukuma ( hapa refer waraabu wengi wa Oman walifikia haya maeneo ya unyamwezini na usukuman baada ya kuingilia toka Tanga na Zanzibar) pia wapo wanaoongea kihaya/ kinyambo wengi waliokaa hasa pande za Karagwe na Kirundi/Kinyarwanda kwa waliokaa nchi hizo

Oman ni nchi pekee kwa anaejua Kiswahili pekee akapata watu wengi wa kuelewana nae kuliko taifa lolote duniani nje ya Africa

Kama ni Oman kuelewa Kiswahili ni kawaida lkn jua mziki pia hauna 'Lugha' ni mpangilio tu watu wana 'enjoy'

Big up sana 'Lion' kwa kutuwakilisha na tunataka wengi waongezeke tuwape sapoti yetu isije kuwa ya marehem Kanumba kaondoka na 'bongo movies' yake we need more 'lions'
 
60% ya waoman wanakijuw kiswahili

90% ya wa oman ni wapemba na huichukulia zanzibar kama nchi yao pia.. Sultan wa Oman aliondoka na watu wake ambao pia waliacha ndugu zao huku..Oman ni zanzibar/ pemba tu ile..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…