Cannabis
JF-Expert Member
- Jan 20, 2014
- 11,557
- 33,535
====
Pia unaweza kusoma zaidi taarifa kutoka The East African:
Takriban Wakenya milioni 2.8 katika kaunti 23 wanahitaji chakula cha msaada kwa dharura, serikali imesema. Ingawa maafisa walisema hakuna mtu aliyekufa kwa njaa kufikia sasa, ukame unaendelea kukumba maeneo mengi ya nchi. Msemaji wa serikali Cyrus Oguna mnamo Alhamisi alisema hili ni ongezeko kutoka kwa watu milioni 2.1 ambao walikuwa na njaa Septemba iliyopita.
Hata hivyo, ripoti ya Shirika la Kimataifa la Oxfam iliyotolewa wiki jana ilionyesha kuwa idadi ya watu walioathiriwa inaweza kufikia milioni 3.1. Miongoni mwa kaunti zilizoathiriwa ni pamoja na Baringo, Isiolo, Mandera, Marsabit, Samburu, Turkana, Wajir, Kilifi, Lamu, Nyeri, Pokot Magharibi, Laikipia na Garissa, ambazo ziko katika hali mbaya ya ukame.
Hali inazidi kuwa mbaya katika maeneo ya Makueni, Taita Taveta na Tana River, huku kwa Embu, Kajiado na Narok, hali ni shwari. Meru na Tharaka Nithi wako katika hatua ya tahadhari, huku hali ikiimarika katika kaunti za Kitui na Kwale.
Chanzo: The East African