E-Fm mnaboa

Clouds nao kipindi cha Leo tena kuna wakati wanaweka singeli I was like wtf is this???

Mzuka wa kusikiliza radio unakuaga unaondoka

Ila si wanapiga mda huo tuu ila hawapigi asubuh au jion pia kumbuka kicheko mtata ndo muzee ya singeli ndo maana tokea ahamie clouds huwa katka kile pindi hua singel znapigwa sana
 
Mimi nilishaacha kusikiliza maredio toka miaka ya 2002,tangu hapo Mimi nanunua TV tu wala sijawahi kusikiliza matangazo ya radio tena.
Unajiona mjanja mwenyewe kununua tv
 
Au ndio yale umekodi boda boda

Halafu anafungulia Singeli

Mi huwa namwambia achague.. kuzima huo mziki au kunisafirisha bure..
 
Nilivyosoma heading tu nikajua tatizo ni singeli.

Nilivyofungua tu kweli tatizo ni hilohilo. Hata bongo flavour walisema wakati inaanza.

Subiri utaelewa tu coz hata shule mwengine huelewa haraka mno ila mwengine ni mgumu mno kuelewa.

Skiliza unachokielewa mkuu. That's all.
 
Kuna huyu aliyepewa kipindi cha kigenge ananiboa sana tena sana.Kicheko alikuwa anakinogesha kuliko huyu anayepiga kelele kama kakabwa koo.Kila neno analoliongea anaweka neno lake la looooooo! Mpaka nakereka.Kipindi cha kigenge kimepoteza mvuto.
Mfate KICHEKO kule alikotokomea!
 
[emoji125] [emoji125] [emoji125] [emoji125] weka na Picha plz
 
Kinachoniboa Mi Ni Yule Jamaa Anayetangaza Michezo Na Kitenge. Hana Sauti Ya Utangazaji
 
Mtoa mada kama hutaki SINGELI sikiliza Radio Tz au RADIO ONE mbn wananyimbo unazozitaka so sio lazima usikilize EFM=
 
Wanasema hainaga ushemeji tunakulaaga, wanasema hainaga ushemeji tunakula..... Zamu ya nani leo zamu ya man fongo zamu yako itakuja ndugu usijari baridaa braza j kapita braza omy kapita...... Weka weka wekaaaaaaaaa hainaga kudevela devela hahahahaha............ Ebwana mie roho saaaaafi kwa hizi singeri
 
Miziki ile usikilize peke yako lkn sio ufungulie redio kwa sauti... Mi huwa naona aibu.. Jumbe za singeli hazina mantiki kabisa....Mie pia sipendi...huwa nasikiliza online ila miziki yao ikianza nasitisha
tafuta wimbo unaitwa mida ya kubeti, ndo wimbo ulionfanya nipende singeli
 
mtu ambae hapendi singeli... hajui kucheza!! .hana hobby ya kucheza kabisa.... singeli ina style zake za kucheza kistaarabu tu...
kama unapenda kucheza huwezi kukataa singeli...
mimi wqnaniachaga hoi na maneno yao.. [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]. shamila mtoto wa uswaaazi.. we tekenya tekenya tekenya ... badala ya kucheza naanza kicheka[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]!!!?
halafu kucheza kisingeli ni moja ya mazoezi..
maana nikuruka ruka mwanzo mwisho..
pia ni dawa ya stress... ukie nda kuangalia singeli .. utacheka tu au utachangamsha akili!!
mimi nikiwa na stress naenda kutazama singeli!! hio ndo faida yangu
 
tafuta wimbo unaitwa mida ya kubeti, ndo wimbo ulionfanya nipende singeli
Mimi na ule wa DULLAH MAKABILA ndio ulinifanya nizidi kuikubali zaidi na hakuna pengine pakuisikiliza singeli zaidi ya E-FM
 
Kwani singeri haipendwi na watu..? Tena kuna hii mpya ya K ni K....
Ujio mpya wa wa baghdad ft roma & Snura juu ya K.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…