East African Federation (EAF) public Views

East African Federation (EAF) public Views

Nimefurahi kusoma maandishi ya Gwandu, hujambo bwana?
Kwa kweli kama kuna kitu kinanistaajabisha ni kuona eti leo hii Wakenya wanajua umoja kuliko sisi Watanzania. Watu kama Obo wamejua lini kwamba nchi hizi ni ndugu?

Wakati Nyerere anawaambia tuungane wakati wa uhuru, hawa ndugu walikataa, bado tukawabembeleza tukaunda Jumuiya mwaka 1967, wakaleta shida tupu, halfu walipofanikiwa kuivunja wakashangilia. Leo wameamka na wanajua umoja kuliko sisi? Sielewi mtu aliyemtukana Nyerere leo amepata wapi busara za umoja?

Wakenya wana tatizo na hii ndiyo sababu Watanzania wengi wanahisi balaa kwenye shirikisho. Mtu mwenye dharau, mbaguzi na anayejiona amefika mbali, hafai kukaa naye meza moja. Wakenya wana matatiz mengi na sasa wanataka kupunguzia mzigo kwetu. Kama nchi yetu ni maskini na sisi ni wajinga, kwa nini wanataka kuungana na sisi?

Nadhani wazo la Kenya kuunga na Somalia na Ethiopia na hata na Sudan ni bora sana kama lilivyo wazo na Tanzania kuunga na Msumbiji, Zimbabwe na wengine waliojazana kusini kwa bara hili. Kenya wamekuwa waongo, wezi, majambazi, wanyang'anyi, wabaguzi, wenye dharau, wenye ukabila, wenye duini (kumbuka akina Balala walivyopata shida), wana kina upuuzi. Kuungana nao ni kuleta shida.

Lazima tukubali kwamba ukichanga kizuri na kibovu, hutapata kizuri kamwe. Tuwape miaka 50 mingine wajirekebishe. hebu angalia walivyomtukana rais wetu eti kwa kuwa ameongea na Rais wa Marekani. Yaani hawajui kuwa maraias wakikutana hujadili nchi nyingine? Tena wana bahati kwamba Kenya ilijadiliwa na marais hawa, ni bahati kwao. Kiburi cha Wakenya kilijionesha siku hiyo, yaani huwezi kuamini eti Waziri mzima anahaha kushughulikia jambo kama hili?

Sijui ni ujinga wa kidiplomasia au nini? Yaani tuna kazi kweli. Sasa hii ya Wakenya kujiita super power wa EA, hawa wamewahi hata kupigana kwa siku moja hapa duniani? Jeshi lao halijawahi hata kujaribiwa, sana sana ni polisi wao tu ndio hutesa wananchi maskini. Kenya ina tatizo na EA itabeba ujinga huu tusipoangalia.

Nina shughuli nyingi, nitachangia tena. Asante.
Mobhare Matinyi,
Washinton DC.
 
Ikiudwa Shirikicho Umoja Utakuwa Na Nguvu Wa Kibihashara Na Kifedha Na Kuwe Na Sarafu Ya Umoja Huo Na Bidhaa Zita Kuwa Nadhamani Moja.
 
its amazing,

everytime the moderators realize a kenyan has contributed to this debate,they delete their post.

its funny,

for a citizenry revered for courtesy,youre full of hatred for your neighbours.

its ironic,

you think kenyans are after tanzanian wealth,and yet kenya out perfoms tanzania in every sector;socially,politcally and economically.

its shocking,

tanzanians dont understand kenyans and yet they make haste to judge them.

its surprising,

just llike arabs blame jews for everything even the most rediculous,tanzanians point their fingures on their nothern brothers for every i'll in their society.

i wonder,

instead of looking for scape goats to blame,why dont you aspire to be better,if not like kenya?

kenyans speak the same language as you;swahili.ugandans and south africans dont.kenyans have always been warmest to welcome tanzanians into their borders than any other country,the so called "polite" tanzanians spit on kenyan integrity.

you would rather south africans,westerners and indians into your border,but not "the filthy money grabbing kenyans"?

in kenyan schools we studied two plays from tanzanian authors,and this is exactly what they talked about.your hatred of your brothers,inferiority complex and blind trust for foreigners.

now,moderators.seeing im kenyan,go ahead and delete what ive written coz God forbid tanzanian readers come across this kenyan piece of propaganda.
 
its amazing,

everytime the moderators realize a kenyan has contributed to this debate,they delete their post.

its funny,

for a citizenry revered for courtesy,youre full of hatred for your neighbours.

its ironic,

you think kenyans are after tanzanian wealth,and yet kenya out perfoms tanzania in every sector;socially,politcally and economically.

its shocking,

tanzanians dont understand kenyans and yet they make haste to judge them.

its surprising,

just llike arabs blame jews for everything even the most rediculous,tanzanians point their fingures on their nothern brothers for every i'll in their society.

i wonder,

instead of looking for scape goats to blame,why dont you aspire to be better,if not like kenya?

kenyans speak the same language as you;swahili.ugandans and south africans dont.kenyans have always been warmest to welcome tanzanians into their borders than any other country,the so called "polite" tanzanians spit on kenyan integrity.

you would rather south africans,westerners and indians into your border,but not "the filthy money grabbing kenyans"?

in kenyan schools we studied two plays from tanzanian authors,and this is exactly what they talked about.your hatred of your brothers,inferiority complex and blind trust for foreigners.

now,moderators.seeing im kenyan,go ahead and delete what ive written coz God forbid tanzanian readers come across this kenyan piece of propaganda.
 
And now you're double posting Mr. Unregistered. It's not like we do not know you Kenyans.

We do know you for sure! You're proud always. You can even check what you've done above. If you speak Swahili like Tanzanians let's exchange our views in this lingo. Otherwise you're judging Ugandans wrongly.

I appreciate Kenya's efforts but we have a problem with YOU Kenyans. You may ask why but before doing so, ask yourself WHY not Ugandans being discussed that much. Therefore you can come out with something.

We have all rights to raise our doubts before we UNITE again. Tunataka kujua nini faida ya kuungana na watu kama ninyi ambao mwatuona hatuna maana na kujiona mko wa thamani zaidi.

These are just OPINIONS and not from the Govt of Tanzania! Just few online Citizens and almost JUST views. Someone who's doubting need explanations on wht he/she's doubting. Muhimu ni you come with your comments and if you're a ndugu then jibu as a ndugu not as a stranger mate! Hope umenielewa kwa hii SIMPO kiingereza niliyotumia ili ieleweke bayana kwako.

Thanks and YOU'RE WELCOME TO THIS BOARD. These are just views from us who are online and using this board and not the Administrators or Moderators as you said who are deleting your postings. If such a thing happened probably you might have used a bad lingo.
 
Dear Tanzanians,

Have you read that article titled XENOPHOBIA AND THE EA FEDERATION ( in The EastAfrican issue No. 626 of this week) By one, Oscar Kimanuka, in Kigali, Rwanda? If not, read it. It is a very disgusting article.

Let me just quote for you some of the paragraphs in that article:

"There is a new wave of xenophobia that is slowly creeping into the East African region that if not nipped in the bud, could undermine the ongoing efforts at political federation, the much cherished goal of our region.

"The timing of this xenophobia is unfortunate. It has come at a time when the leaders of East Africa have just launched the fast-tracking of the political federation. What is worrying is that at the official level, not much has come out by way of condemnation of these regrettable acts.

"Xenophobia should not just viewed as a dislike or fear of foreigners. It is a form of violence. People get killed and property destroyed. In recent months, thousands of Rwandans have been expelled from Tanzania where, as minorities, they have lived in harmony with locals since the 1930s.

"This is a time long enough for any foreigner to be accepted as a bona-fide resident. The fact, however is that the Rwandans returned home under harrowing conditions and dirt poor. Stories abound of their mistreatment and loss of property.

"A Tanzanian website, www.habaritanzania.com, is getting xenophobic in its postings on issues of foreigners in Tanzania. Its message is that Tanzania is for Tanganyikans only..."

These are some of the views from the man in Kigali. He is short of "talking" genocide committed by Tanzanians to Rwandans. What a pit ?

Let me ask you, Who (a tanzanian) has said that Tanzania is for Tanganyikans? So, this man in Kigali is trying to sow seeds of mistrust among Tanzanians- from the mainland and Zanzibar. Clever isn't it?

Yaani wanyarwanda wale Tanzania kinyume cha sheria sasa tunalazimishwa tuwape uraia simply because they have stayed in Tanzania for a long time! This is ridiculous. We tanzanians (we) should be aware. There is a hidden agenda in this part of Africa to "victimize" us. They want our land. Do you remember tha Bamanyamulenge saga in Eastern Congo? They wanted the same to happen here. We are awake, Tanzania is awake now.

What is this xenophobia they are talking about? Can you just go in Rwanda, Kenya and do what you want? Tanzania is for Tanzanians and not for Rwandans and Kenyans. Watanzania tumekuwa wajinga kwa muda mrefu mno, sasa imetosha. Tunawafahamu watu waliojifanya kuwa ni Watanzania, tukawasomesha, wakafanyakazi tena wengine katika sehemu nyeti hata kwenye majeshi yetu. Baada ya kinachoitwa kupata uhuru wakakimbia wakaenda kwao na huko wakapewa madaraka makubwa wakituacha tunashangaa kwamba kumbe watu hao, waliokuwa kwenye nafasi yeti nchini mwetu kama vyuoni, madaktari na hata kwenye vyombo vya dola, hawakuwa watanzania! Je, mnafahamu kwanini baadhi ya watu wa Ngara na Karagwe wanasema kuwa hawataki kuona Wanyarwanda na Warundi kuingizwa kwenye Federation? Inasekemekana kuwa wahamiaji hao huwa wanawatambia kuwa itafika siku moja wanaitawala Tanzania. Kauli hizo zinawaudhi mno watanzania wa maeneo hayo.

Je, huyo Kimanuka wa Kigali ana hoja katika mada yake hiyo kwenye The EastAfrican? Naomba maoni yenu>
 
Mimi nafikiri WTZ badala ya kuungana na Kenya na Uganda tu-concetrate kwenye SADC. Kenya na Uganda ni kuwatafutia watu mlo tu, mambo yote SADC bwana!!
 
Hili la Tanzania kujiunga na SADC mimi naliunga mkono. Ndani ya SADC kuna heshima. Kenya, Uganda na Rwanda waungane na SUDAN, SOMALIA na ETHIOPIA katika EAC. Tabia zao zinafanana. Sisi twende kusini. Hata kwenye michezo tujiunge na COSAFA, tuachane na CECAFA.
 
Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
BURIANI TANZANIA ... AU KILA LA HERI AFRIKA MASHARIKI?
Na Mlenge Fanuel

"Mtu akikushauri jambo la kijinga, huku anajua jambo hilo analokushauri ni la kijinga, na wewe ukakubali, basi atakuona, wewe zuzu!"
-- Mwalimu Julius K. Nyerere, 1994/5

Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tafadhali isome barua hii ya wazi ya kukufikishia ujumbe kwamba Tanzania haiko tayari kujiunga na Shirikisho la Afrika Mashariki (East African Federation, EAF) wala “Soko la Pamoja” la Afrika Mashariki, na kwamba Watanzania hatutaki Tanzania ijiunge na Shirikisho hilo.. Yatakuwa ni maafa makubwa kwa Tanzania na Watanzania iwapo Tanzania itajiunga na EAF hasa kwa mpangilio ulioko wa “fast track”. Ndiyo maana nimeanza na nukuu ya Mwalimu Nyerere, ambaye tayari baadhi ya watu, hasa wa nchi jirani za Kenya, Uganda na Rwanda, wameanza kumsingizia kwamba kwa kujiunga na EAF tutakuwa "tunamuenzi" Mwalimu Nyerere, huku wakijua fika ushauri wanaotupa wa kujiunga na Shirikisho na Soko la Pamoja la Afrika Mashariki hauna manufaa yoyote kwa Tanzania, wakidhania sisi Watanzania ni mazuzu tunaoendekeza wema wa mshumaa kuwaangazia wengine huku wenyewe unateketea, kwa minajil ya kupata misifa isiyo na tija.

Ni kweli Mheshimiwa Rais umeunda Tume ya Kupokea Maoni kuhusu Shirikisho la Afrika Mashariki, lakini inatia mashaka iwapo huo siyo tu ni utaratibu uliouweka kuhalalisha maamuzi yaliyokwishafikiwa ya kuidumbukiza Tanzania kwenye EAF. Hii inatokana na muonekano kwamba Tanzania kujiunga na EAF kumeshaamuliwa tayari -- kutaka watu tujadili siyo kiinimacho tu? Mheshimiwa Rais, palikuwa na muswada uliopelekwa Bungeni wa Tanzania kujiunga na EAF, ambao Waheshimiwa Wabunge waliukataa, na serikali ikabidi iuondoe. Lakini mchakato wa Tanzania kujiunga na EAF ukaendelea tu, na kupuuza maoni ya Wabunge wetu tuliowachagua watuwakilishe. Ikiwa sikusikiliza vibaya, katika Bunge la Bajeti 2006/2007, Mheshimiwa Waziri wa Afrika Mashariki aliliambia Bunge kwamba patakuwa na KURA YA MAONI kuhusu Afrika Mashariki. Matokeo yake tumeletewa Tume badala ya kura ya maoni! Kana kwamba hiyo haitoshi, iliripotiwa kwenye vyombo vya habari kuwa wewe Mheshimiwa Rais wetu, ulimhakikishia Rais Yoweri Museveni wa Uganda kwamba utafanya kila unaloweza kuhakikisha kufanikiwa kwa Shirikisho la Afrika Mashariki, kwenye mkutano wenu uliofanyika Mwanza. Je, maoni tunayotoa Watanzania kukataa kujiunga na shirikisho si "kilio cha samaki -- machozi yanakwenda na maji?" Wenyewe "wenye nchi" mshaamua mloamua?

Pana maswali mengi mheshimiwa Rais ambayo ukitupatia majibu utakuwa umetuwezesha Watanzania tulio wengi kuelewa kuhusu mustakabala wa maisha yetu na Tanzania yetu:

* Je, Ni sera ya CCM Tanzania kujiunga na EAF au Soko la Pamoja la Afrika Mashariki?

* Je, Ilikuwa kwenye ilani ya Uchaguzi 2005 ya Chama Tawala CCM Tanzania kujiunga na EAF?

* Je, Nani aliyependekeza Tanzania ijiunge na EAF? (Inabidi tumfahamu ili tuweze kumpamba maua iwapo Tanzania itafanya tunalodhani ni kosa la maisha la kujiunga EAF kumbe ikathibitika EAF ni manufaa tele kwa Tanzania ; vinginevyo inabidi tumfahamu ili tuweze kumzomea na kumuimbia nyimbo za kumsimanga pindi machungu ya EAF yatakapoanza kudhihirika muda si muda iwapo Tanzania itafanya kosa la maisha kujitumbukiza kwenye EAF. Vinginevyo itakuwa kama mikataba ya madini -- hatuelezwi nani aliwaalika na kuingia mikataba na 'wawekezaji' kwenye migodi.)

* Rais Yoweri Museveni wa Uganda ameshajitangaza kuwa Rais wa Kwanza wa Shirikisho la Afrika Mashariki -- ikiwa na maana yote mengine yanayojitokeza sasa ni kuhalalisha na kusafisha njia ya Museveni kuwa Rais wa Kwanza wa Shirikisho la Afrika Mashariki, hasa ukitilia maanani Rais wa Kenya na wewe Rais wetu mko kimya, ikielekea mmekubaliana na matamshi ya Museveni. Si hivyo?

* Kutokana na maneno yanayosemwa na Wakenya na Waganda, Wanyarwanda na Warundi, inaonekana kama vile serikali ya Tanzania HAINA UBAVU wa kusema HAPANA kwa EAF -- kila mara Tanzania inazomewa inapohoji maslahi yake kwenye EAF -- au inapotaka kutumia uhuru wake ISIJIUNGE na EAF. Hivi karibuni Waziri wa Afrika Mashariki wa Tanzania alisemwa kwenye vyombo vya habari kwamba hahudhurii vikao vya Afrika Mashariki -- na kumfanya Mheshimiwa Waziri Mkuu ajitokeze kumtetea -- na baadaye Waziri yule akaondoshwa toka Wizara ya Afrika Mashariki kwenye mabadiliko ya Baraza la Mawaziri uliyoyafanya hivi karibuni Mheshimiwa Rais. Ina maana Tanzania ni kama mbwa anayeelekea kwenye mdomo wa chatu EAF -- amefyata mkia, anatoa kilio cha mwisho, na hana la kufanya zaidi ya kufanywa asusa na kumezwa -- au si hivyo?

* Ni kwa nini Kiswahili SIYO lugha rasmi EAC, na badala yake ni kiingereza?

* Kama shida ni ushirikiano, kwa nini Tanzania isijiunge na Msumbiji na Zambia , na kutengeneza shirikisho?

* Kwa nini EAF inaharakishwa namna hii?

* Ni nini Tanzania inahitaji kwenye EAF ambacho haiwezi kukipata bila kuwemo kwenye shirikisho hilo ? (Mbali na ngonjera za kisiasa, pengine na watu fulani kupata posho za vikao vya EAC na baadhi kuandikwa kwenye vitabu vya historia, vitu ambavyo havimsaidii Mtanzania mpiga kura wako anayesubiri neema tele na maisha bora...)

* Pana bidhaa zipi za Tanzania hazifiki kwenye soko Kenya au Uganda , ambazo EAF itazifanya zifike sokoni?

* Nani atakuwa Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Afrika Mashariki, na ni upi mchango wa EAF kwenye uvamizi dhidi ya DRC?

* Mheshimiwa Rais, hivi "Usalama wa Taifa" wa Tanzania una majukumu gani makubwa zaidi ya kulinda (uhuru) "Sovereignty" ya nchi yetu? Kwa nini "Usalama wa Taifa" haukupi picha kamili ambayo itakufanya usijisumbue hata kuja kutuuliza iwapo tunataka uhuru wa nchi yetu uondoke kupitia "soko la pamoja" na "Shirikisho la Afrika Mashariki", badala yake tukaendelea kulijenga taifa "letu changa" na kuulizana maswala ya maendeleo kama vile tutanufaikaje na maliasili tulizojaaliwa nchini mwetu?

PART I
 
(Part II)
* Kwa kuitumbukiza Tanzania kwenye "Soko la Pamoja" la Afrika Mashariki, huoni kwamba utakuwa umekiuka kiapo ulichokula cha kuulinda uhuru wa, na mipaka ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ?

* Kulikuwa na sababu gani ya kupambana na Idd Amin aliyetaka kipande "kidogo tu" cha nchi yetu, ikiwa leo tunaigawa sandakarawe nchi nzima kwa kisingizio cha soko la pamoja?

* Tanzania itaondoka SADC? (Tayari nchi nyingine za Afrika Mashariki zimeanza kutuamuru tutoke SADC. SADC imeweka bayana kwamba wakati umefika wa kuchagua kati ya EAF au SADC.) Unadhani itakuwa ni busara kuondoka SADC? Kwa nini usitoe tamko kwamba Tanzania ya kesho ni ndani ya SADC?

* Je sisi wananchi wa Watanzania tutaulizwa kuhusu kujiunga na "Soko la Pamoja la Afrika Mashariki" au ni uamuzi uliofikiwa tayari kwamba tutajiunga na soko la pamoja la Afrika Mashariki?

* Huo Mkataba wa EAC/EAF uko wapi ili tuweze kuuona na kuusoma? Ni Watanzania gani waliousoma na kuuridhia kwamba SASA tunaanza kuwa kwenye mchakato wa kuelekea kwenye Shirikisho? (Inaripotiwa kwamba Tume yako ni sehemu tu ya taratibu ‘chovu' za mchakato huo...)

Watanzania tutafanyaje ili kuondoka kwenye EAF, iwapo Tanzania ijajikaanga yenyewe kwa kuingia kwenye EAF? Vipengele vya kujiondoa kwenye EAF viko wapi? Hautakuwa ni uhaini kuzungumzia kujitoa EAF, kama ambavyo si ruksa kuzungumza kujitoa kwenye Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ?

Mheshimiwa Rais Jakaya Kikwete, maswali hayo na mengine mengi yanaleta changamoto kwako binafsi kwamba zawadi kubwa kuliko zote unazoweza kutupa sisi Watanzania, ni kutukabidhi Tanzania yetu yenye "sovereignty" ileile au zaidi ya uliyokabidhiwa pale utakapoacha madaraka mwaka 2010 au 2015, panapo majaaliwa.

Kwa taarifa yako Mheshimiwa Rais , Tanzania ndiye "Mbuzi wa Shughuli" kwenye Shirikisho la Afrika Mashariki. Na mbuzi huyu amepangwa "kuchinjiwa kwenye maji" ili hata ukelele wake wa mwisho usisike. Hawatarudia makosa ya Jumuia ile iliyokufa 1977, kwa kutuacha bado tunafurukututa. Kujiunga kwa Tanzania EAF kwafanana na Punda wa kwenye hadithi moja iliyochapishwa Tanzania ambamo Simba baada ya kujeruhiwa, alishindwa kuwinda; na Sungura, Fisi na Punda wakaenda kumpa pole. Kumbe Fisi na Sungura walikuwa na lao jambo.
"Simba kwa kuwa huwezi kuwinda naomba unile mimi", alianza kusema Sungura. " Asante sana kwa kunijali, siwezi kukula wewe rafiki yangu. Sasa nimefahamu wewe ni rafiki yangu wa kweli katika kipindi hiki kigumu cha dhiki!" alijibu Simba. Fisi naye akajitoa aliwe na Simba, ambaye pia alikataa kumla, akitoa sababu zilezile.

Sasa Punda akawa njia panda: "Nikikaa kimya nitaonekana mbaya kwa Simba. Kwanza Simba mwenyewe kakataa kuwala wenzangu, na mimi atakataa... acha nijisemee tu kwamba najitolea anile..." aliwaza.
Akaropoka, "Simba kwa kuwa huwezi kuwinda naomba unile mi..." Kabla hajamaliza maneno yake alirukiwa na kuraruliwa palepale.
Kenya, Uganda , Rwanda na Burundi zina ajenda kadhaa kwenye EAF: mbali na zile "rasmi" zinazotangazwa hadharani. Ili ajenda zao zitimie, lazima "Punda" Tanzania awemo kwenye EAF ili aweze "kuliwa". Mheshimiwa Rais, ni wajibu na heshima kwako kuhakikisha Tanzania haijiungi na EAF kwa kuwa Tanzania haina ajenda mbali na ngonjera za kisiasa, pengine na posho za vikao kwa baadhi ya watu.

Kwanza Tanzania siyo lazima ijiunge au ikubaliane na kila kitu kwenye ushirikiano wa Afrika Mashariki. Wachache wanaounga mkono kujiunga na shirikisho la afrika mashariki, wanadai upo umuhimu wa kujiunga kwa vile "dunia nzima mwelekeo ni kujiunga pamoja, kama vile Jumuia ya Ulaya, EU". Kama sababu ni hiyo, kwa nini tusibakie SADC tuliko? Hivi tulipigania uhuru wa kusini mwa Afrika ili iweje? Watanzania tulitoa damu zetu, mali na uhai wetu, kukomboa Ndugu zetu walio Kusini mwa Afrika, sasa ukombozi umepatikana, pana wakati gani muafaka zaidi ya huu kuendeleza undugu wetu? Majirani zetu wa Afrika Mashariki tutaendelea kushiriana nao, kama tunavyoendelea kushirikiana na majirani zetu wengine. Kutojiunga kwenye shirikisho siyo maana yake tutakuwa maadui!

Tanzania lazima ikae mbali na EAF, hata ikibidi kwa miongo kadhaa ijayo, ikiwa si moja kwa moja. Kwanza , Muungano wetu wenyewe una "mipasuko" ambayo haijasilibwa bado. Kabla ya kuulizwa kuhusu Shirikisho la Afrika Mashariki, tuulizwe basi kuhusu Muungano wa Tanganyika na Zanzibar . Tanganyika na Zanzibar , mara baada ya kupata Uhuru, hazikutimiza miaka mitano, "zikaishia" na kuwa Taifa moja Tanzania . Sasa jamani, Tanzania hata miaka hamsini haijafikia, nayo "iishie", tena kusikoeleweka? Tanzania ina manufaa tele SADC, kuliko kwenye shirikisho la Afrika Mashariki. Hivi, wakati tulipokuwa "Mstari wa Mbele wa Ukombozi Kusini mwa Afrika", majirani zetu wa Kenya na Uganda walikuwa wapi? Leo hii tukiwakubalia kuondoka SADC, watatuona timamu kweli?

Mheshimiwa Rais Kikwete, kiasi inaeleweka ikiwa unaona pana ugumu wa wewe kuonekana unakwenda tofauti na Watawala wetu waliotutangulia, ambao huenda wanapendelea kuona EAF ikizinduliwa, Tanzania ikiwemo. Lakini mheshimiwa Rais, ndiyo maana kukawa na kikomo cha utawala cha vipindi viwiliviwili! Kwa kuwa umechaguliwa kwa ushindi "wa kishindo", imani yetu Watanzania imekuwa kwako kwamba utaweza kuipeleka Tanzania kule tunakotaka. Na tunakotaka sisi Watanzania siyo kwenye "soko la pamoja la afrika mashariki" wala EAF. Huo Muungano tu wa Forodha wa Afrika Mashariki unatekelezwaje? Matatizo na mizengwe iliyoko panaashiria nini pindi tukiwagaia nchi hii yote kwenye Shirikisho au "soko la pamoja"? Siyo maafa, Mheshimiwa Rais?

Mheshimiwa Rais Kikwete, kwenye Jumuia ya Ulaya --EU, Uingereza na Jamhuri ya Ireland SIYO mataifa yaliyoko kwenye "Mkataba wa Schengen" wa Jumuia ya Ulaya, mkataba unaoondoa mipaka na vizuizi baina ya nchi za Jumuia ya Ulaya kwenye masuala ya Uhamiaji, japo Uingereza na Jamhuri ya Ireland ni wanachama kamili wa Jumuia ya Ulaya. Hii haikuzuia Ufaransa, Uholanzi, Ubelgiji, Ujerumani na nchi nyinginezo za EU zilizokubali kusaini kuendelea na "Makubaliano ya Schengen". Kadhalika , Iceland , Norway na Uswisi zimesaini "Mkataba wa Schengen" japo nchi hizo SI zanachama Jumuia ya Ulaya. Kila taifa linaangalia maslahi yake kama taifa. . Ulipoanzishwa umoja wa Forodha wa Afrika Mashariki takriban karne moja iliyopita, Tanganyika haikujiunga mpaka ilipoona vema kwamba itakuwa ni kwa maslahi yake kujiunga.

Hii haikuzizuia Kenya na Uganda kuanzisha Umoja wao wa Forodha. Tanganyika ilijiunga baadaye! Hata ile Jumuia ya Afrika Mashariki iliyovunjika, ilianzishwa baada ya kupita MIAKA HAMSINI tangu kuanzishwa ule Umoja wa Forodha wa Afrika Mashariki, japo nchi hizi zote tatu zilikuwa zinatawaliwa na Mkoloni mmoja takriban muda wote huo. Haraka ya sasa hivi ya nini? Wanajua wakituachia muda, tukienda hatua kwa hatua, hawataweza tena kuigeuza Tanzania koloni lao.

Tanzania iendelee kuwa mwanachama wa SADC, na kuendelea kuwa imesaini kwa muda makubaliano ya Umoja wa Forodha wa Afrika Mashariki mpaka pale SADC itakapoanzisha Umoja wa Forodha wa SADC, ambapo Tanzania itajitoa kwenye Umoja wa Forodha wa Afrika Mashariki. Au busara zaidi, ni vyema Tanzania ikajitoa SASA HIVI toka Umoja wa Forodha wa Afrika Mashariki, na kuelekeza nguvu zake kwenye SADC. Kenya , Uganda , Rwanda na Burundi zinaweza kuendelea na Umoja wao wa Forodha, Soko la Pamoja na Shirikisho (waliite vyovyote wapendavyo), bila Tanzania kuwemo.

* Mheshimiwa Rais, ukubwa wa eneo la ardhi ya Tanzania ni zaidi ya Jumla ya eneo lote la ardhi ya Kenya , Uganda , Rwanda na Burundi ukizichanganya pamoja -- bila kuzungumzia rasilmali zilizoko. Halafu wanasema tuchanganye ardhi yetu na zao, halafu tugawane sawasawa kwa jina la "Soko la Pamoja la Afrika Mashariki". Hivi tukikubali ujuha huo, ni kwa nini wasituone sisi mazuzu?

Swali kuu tunaloulizwa Watanzania na Tume yako mheshimiwa Rais ni iwapo Watanzania tunaona bado kuna sababu za Tanzania kuendelea kuwa nchi huru ambayo ni "dola", wakati ambapo kuna shinikizo nchi yetu igawe uhuru wake kwa kisingizio cha "soko la pamoja" na "shirikisho la Afrika Mashariki". Tuchukulie kwa mfano, tume itawahoji na kupokea maoni toka kwa watu laki mbili. Kati yao 80% wakasema Tanzania ijiunge kwenye "Soko la Pamoja" na "Shirikisho la Afrika Mashariki", 20% wakasema tusijiunge.

Je, Mheshimiwa Rais, hiyo itakuwa na maana uamuzi utakuwa umesilibwa wa Tanzania kufikia mwisho wake, kwa kujiunga na Soko la Pamoja na Shirikisho la Afrika Mashariki? Je, hutatumia busara kama ilivyotumika kwenye Tume ya Nyalali ya Vyama Vingi pale Tanzania ilipoangalia maslahi ya taifa, na kuruhusu mfumo wa vyama vingi, bila kuangalia asilimia zilizotokana na tume? Ikiwa kweli kabisa umedhamiria kuipeleka Tanzania kwenye mwisho wake machinjioni Afrika Mashariki, kwa nini usiweke KURA YA MAONI kwa kila Mtanzania kupiga kura yake, badala ya kutumia Tume, angalau basi kuchelewesha kwa muda mauti ya Taifa Tanzania? "Soko la Pamoja" na pacha wake "Shirikisho la Afrika Mashariki" maana yake ni mwisho wa uhai wa Taifa la Tanzania .

Ikiwa Tanzania itajinyonga (Mungu apishie mbali!) kwa kusaini mkataba wa "Soko la Pamoja la Afrika Mashariki" au ule wa "Shirikisho la Afrika Mashariki", basi Watanzania tutasahau "maisha bora kwa kila Mtanzania" na itabidi tujiandae kwa "Bora Maisha kwa kila Mtanzania", na kwamba wewe Rais wetu, Jakaya Kikwete, utakuwa umefeli vibaya kabisa jukumu lako la msingi tulilokupa -- kulinda uhuru na umoja wa Taifa la Tanzania na kubakisha Taifa la Tanzania kuwa dola huru kwa manufaa ya Watanzania mpaka pale utakapomkabidhi madaraka ya Urais wa dola la Tanzania huru Mtanzania mwingine.

Kwa kuandika barua hii, imani yetu Watanzania kwako Rais wetu kwamba utaweza kuhimili mashinikizo yote ya nje, na kutusikiliza sisi raia zako, tunaotaka tubakie na taifa letu huru la dola ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania .

Mwenyezi Mungu akujalie. Amin.

Ndimi,

Mlenge Fanuel
Raia na Mwananchi wa Tanzania,
Simu: +255 75 4372902,
Email: mlenge@yahoo.com,
Dar es Salaam, Tanzania.
 
Shirikisiho la afrika mashariki siyo jambo geni, lina historia ndefu ambayo watanzania hatutakiwi kuisahau. Kunako miaka ya sitini, Nyerere alikuwa tayari kuchelewesha uhuru wa Tanganyika ili kuzisubiri Kenya na Uganda kusudi tupate uhuru kwa pamoja na kuunda shirikisho lenye usawa ambapo Nyerere alitaka Kenyatta awe rais halafu yeye (Nyerere) awe waziri wa mambo ya nje. Kulitokea kutoelewana na mwishoni ikabakia kuwa kila mtu afate lwake na hivyo sisi tukapata uhuru wetu mbele ya Kenya na Uganda.

Mara tu baada ya Muungano wa Tanzania, kukawa na effort nyingine tena za kuunganisha nchi za afrika mashariki. Effort hii nayo haikufanikiwa na mwishoni tukaishia kuunda jumuia ya kiuchumi ya afrika mashariki mwaka 1967. Jumuia hiyo ikawa na mafanikio sana; Tanzania iliziamini nchi wanachama hasa Kenya kuwa makao makuu ya tasisi nyeti za jumuia hiyo kama vile ndege, reli na bandari. Miundombinu nzito sana zilijengwa Kenya kwa kutumia mali ya Jumuia huku sote tukijua kuwa hiyo ni kwa faida ya wanachama wote. Kumbe wenzetu walikuwa na lao; baada ya shughuli za kiuchumi za jumuia kuanza kunyooka na shirika la ndege kuwa limenunua ndege kadhaa za kisasa, Kenya wakavunja jumuia hiyo bila ridhaa ya wanachama wengine mwaka 1977.

Mbaya zaidi ni kuwa baada ya kuvunja jumuia, walikalia mali zote za jumuia zilizokuwa Kenya kama vile zilikuwa zao binafsi kwa karibu miaka mitano mpaka pale benki ya Dunia ilipoingilia. Wakenya walifurahia sana utapeli huo na kuanza kutucheka watanzania. Mpaka leo sidhani kama Tanzania tulipata share yetu ya haki kwa vile wakti huo Kenye ilikuwa swahiba wa wamarekani wakati tanzania inafuata siasa ya ujamaa. Kwa hiyo kutokana na kuwa msuluhishi huyu alikuwa mmarekani, inawezekana aliwapa Kenya share kubwa zaidi.

Ndugu zanguni wabongo, sina tuna matatizo yetu mengi tu. Hatuhitaji kujiongezea mengine katika kipindi hiki. Tupambane na matatizo yetu hivi hivi lakini Jumuia siyo yetu. Ni afadhali tuendelee na utaratibu huu huu wa sasa kila watu na mambo yao tukiwa tunakutana kiujirani tu.
 
Ndugu yangu Mlenge,
Asante sana kwa maoni yako.Mimi nikiwa kama mtanzania ambaye niko masomoni nje ya nchi ni nawasiwasi sana na Tanzania kujiunga na EAF in "Fast Tracking Fashion" na agenda za Museveni and Kagame.

1) Maraisi hawa ( Museveni and Kagame) wakiwa vibaraka wa marekani walivamia nchi ya Congo na kuikalia kimabavu,huku wakitwaa rasilimali zake.Mpaka Angola ilipoamua kupambana nao kiume!!

2) Wote ni watu wenye kupenda sana madaraka. Kagame atatawala nchi ya yake kwa miongo miwili kila muongo una miaka saba so atatawala kwa miaka kumi na nne.!! na museveni naye hata sijui atatawala mpaka lini ..tayari ameshabadili katiba yao..sasa sijui hataibadili hata hiyo ya Afrika mashariki.

3) Kutokana na ukubwa wake Tanzania inatamaniwa sana na maraisi hawa hasa ukiangalia taabu walizo nazo watu wa Rwanda kwenye issue ya ardhi( person per unit land),the same kuhusu Kenya,watu wengi wa kenya hawana ubavu wa kupata ardhi kwenye nchi yao( kutokana na sera za ukabila,rushwa na ubepari ndani ya Kenya) kwa hiyo kimbilio ni Tanzania.

Ushauri:
- Suala la EAF halina ubaya ila ubaya ni kwa nini muungano huu lazima ufanyike sasa hivi wakati Tanzania bado haijajiandaa kikamilifu ukilinganisha na nchi nyingine.
-Pile kwa nini iwe sasa wakati akina museveni ,kagame na kibaki bado wako madarani?. kwa nini kwa mfano muungano usiwe 2025 ou 2030 kwa mfano?
-Nchi za Uganda,Rwanda na Burundi ziko vitani ..na ni vita za wao kwa wao nani atabeba gharama zote hizo?..EAF? or ..think kama museveni au kagame watakuwa maraisi wa EAF na wakaamuru kuivamia Congo nani atasimama kuwaonya? ...wa tanzania au?

-Tribalism is still big issue in Rwanda ,Kenya na Uganda.Je watanzania watapata treatment sawa kwa mfano na watusi wa Rwanda au Wanyankole wa Uganda au Wakikuyu wa Kenya?...wake up Tanzanias leaders?...

-Tanzania imejifunza mambo mengi kuhusu muungano wetu na zanzibar.kwa kifupi muungano siyo mchezo!! unahitaji careful approach!,patience and wisdom which i don see in people like Kagame or Museveni or even Kibaki!!

-Na penda kumuonya Raisi Kikwete katika hili!..muungano siyo kukurupuka tu!..tafadhali muheshimiwa rais usidanganyike na mambo ya ..kutakuwa na soko la pamoja eti 80 milions people!..Please be careful on this...let us spend time prepare ourselves for EAF.Hakuna haraka yoyote!..globalization ipo na itaendelea kuwepo tu!.

Asanteni sana,
Mwananchi na mpenda nchi ya Tanzania.
Mungu ibariki Tanzania.
 
Sitaki kujumuishwa na Kenya na Uganda (ingiza Burundi na rwanda) katika mambo ya siasa ama uchumi!
 
mwanachi said:
Ndugu yangu Mlenge,
Asante sana kwa maoni yako.Mimi nikiwa kama mtanzania ambaye niko masomoni nje ya nchi ni nawasiwasi sana na Tanzania kujiunga na EAF in "Fast Tracking Fashion" na agenda za Museveni and Kagame.
1) Maraisi hawa ( Museveni and Kagame) wakiwa vibaraka wa marekani walivamia nchi ya Congo na kuikalia kimabavu,huku wakitwaa rasilimali zake.Mpaka Angola ilipoamua kupambana nao kiume!!
2) Wote ni watu wenye kupenda sana madaraka. Kagame atatawala nchi ya yake kwa miongo miwili kila muongo una miaka saba so atatawala kwa miaka kumi na nne.!! na museveni naye hata sijui atatawala mpaka lini ..tayari ameshabadili katiba yao..sasa sijui hataibadili hata hiyo ya Afrika mashariki.
3) Kutokana na ukubwa wake Tanzania inatamaniwa sana na maraisi hawa hasa ukiangalia taabu walizo nazo watu wa Rwanda kwenye issue ya ardhi( person per unit land),the same kuhusu Kenya,watu wengi wa kenya hawana ubavu wa kupata ardhi kwenye nchi yao( kutokana na sera za ukabila,rushwa na ubepari ndani ya Kenya) kwa hiyo kimbilio ni Tanzania.

Ushauri:
- Suala la EAF halina ubaya ila ubaya ni kwa nini muungano huu lazima ufanyike sasa hivi wakati Tanzania bado haijajiandaa kikamilifu ukilinganisha na nchi nyingine.
-Pile kwa nini iwe sasa wakati akina museveni ,kagame na kibaki bado wako madarani?. kwa nini kwa mfano muungano usiwe 2025 ou 2030 kwa mfano?
-Nchi za Uganda,Rwanda na Burundi ziko vitani ..na ni vita za wao kwa wao nani atabeba gharama zote hizo?..EAF? or ..think kama museveni au kagame watakuwa maraisi wa EAF na wakaamuru kuivamia Congo nani atasimama kuwaonya? ...wa tanzania au?
-Tribalism is still big issue in Rwanda ,Kenya na Uganda.Je watanzania watapata treatment sawa kwa mfano na watusi wa Rwanda au Wanyankole wa Uganda au Wakikuyu wa Kenya?...wake up Tanzanias leaders?...
-Tanzania imejifunza mambo mengi kuhusu muungano wetu na zanzibar.kwa kifupi muungano siyo mchezo!! unahitaji careful approach!,patience and wisdom which i don see in people like Kagame or Museveni or even Kibaki!!
-Na penda kumuonya Raisi Kikwete katika hili!..muungano siyo kukurupuka tu!..tafadhali muheshimiwa rais usidanganyike na mambo ya ..kutakuwa na soko la pamoja eti 80 milions people!..Please be careful on this...let us spend time prepare ourselves for EAF.Hakuna haraka yoyote!..globalization ipo na itaendelea kuwepo tu!.
Asanteni sana,
Mwananchi na mpenda nchi ya Tanzania.
Mungu ibariki Tanzania.


Wewe umesema kweli.

Kuungana na jamaa hawa ni karibu sawa na kupata HIV.

Kwanza kabisa , nchi hizi ambazo hazina uzoefu na mambo ya Muungano zisitushinikize kuingia kwenye Muungano ambao hatuoni manufaa yake. Sisi tumeshakuwa chini ya Muungano kwa zaidi ya miaka 40; tunajua faida na ugumu wa muungano kwa hiyo tuna kila haki kutafakario madhumuni na faida za muungano huo. Inatakiwa wao ndio watusikilize sisi kutokana na uzoefu wetu, siyo watushinikize kimbuzimbuzi tu.
 
Unregistered said:
Sitaki kujumuishwa na Kenya na Uganda (ingiza Burundi na rwanda) katika mambo ya siasa ama uchumi!
Huyu Raisi wetu kikwete anapenda sana sifa mananake sasa hivi anajiona kama mtu ambaye mungu wa tanzania wala ashauriki,maoni anayozungumzia kutoka kwa wananchi hiyo hakuna manake sasa hivi wanawachagua wabunge hayo maoni ni lini watu wametoa we acha wajiunge nasi tutajiunga na magaidi wa kule kwao LRA,we acha tu ,manake ndicho wanachotaka,Anashindwa kushugulikia umeme kazi kushangaa tu kwenye nchi za watu.
 
Hakuna haja ya Tanzania kujiunga na Kenya au Uganda, kwani mazingira yetu ni tofauti sana. Kenya na Uganda wameshagawana Ardhi yote, wakati huo Tanzania kupata hati ya ardhi inakuchukuwa miaka 50.
 
Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mimi ni Mtanzania ila ninasikitika sana unapotaka kuingiza Tanzania kwenye huo muungano. Sisi hatutaki kwanza Wakenya wabinafsi ile mbaya, HATUTAKI MUUNGANO WA EAST AFRICA WALA RWANDA WALA BURUNDI HATUTAKI.
 
Unregistered said:
Huyu Raisi wetu kikwete anapenda sana sifa mananake sasa hivi anajiona kama mtu ambaye mungu wa tanzania wala ashauriki,maoni anayozungumzia kutoka kwa wananchi hiyo hakuna manake sasa hivi wanawachagua wabunge hayo maoni ni lini watu wametoa we acha wajiunge nasi tutajiunga na magaidi wa kule kwao LRA,we acha tu ,manake ndicho wanachotaka,Anashindwa kushugulikia umeme kazi kushangaa tu kwenye nchi za watu.

HII NI point kubwa sana
 
Aisee, nimefurahishwa sana namna watanzania mnavyoamka. Hii kitu Federation ni ujinga mtupu. Hakua haja ya Rwanda na Burundi kujiunga na EA federation. Awali ya yote federation hii haitakuwepo. Watanzania hawatakubaliana na hili. Kwa hiyo kelele hizi zinazotoka Kenya zitaishia hivyo hivyo. Hizo ni kelele za chura mtoni.

Ni lazima tujiulize kwanini pale watanzania wanapotoa maoni yao wakenya wanapiga sana kelele? Eti watanzania wanawachukia wageni! Yaani kutoa maoni ni kuwachukia wageni? Eti watanzania hawakusoma? Sasa kama hatukusoma, kelele za nini? Kwanini wakenya mliosoma msikae wenyewe huko na usomi wenu?

Kwa kadri hali inavyokwenda ni wazi hakutakuwa na federation, hizo ni ndoto. Watanzania hatuwezi kurudia ujinga ule wa miaka ya nyuma. Kumbukeni kufanya kosa siyo kosa lakini kurudia kosa ni kosa tena basi kosa kubwa.

Yule Mwandishi wa The EastAfrican, Oscar Kimanuka, ni wa ajabu sana. Eti Wanyarwanda wale walioko Ngara, Karagwe, Biharamulo anataka wapewe uraia kwa kuwa wameishi Tanzania kwa miaka mingi. Hainiingii akilini kwamba mtu mwenye busara na akili zake anaweza kukubaliana na mtazamo huo.

jambo moja ambalo baadhi ya Wakenya na watu wengine katika eneo hili la Afrika Mashariki hawalifahamu ni kuwa watanzania wa sasa ni tofauti sana na wale wa jana na juzi. Watanzania wameamka. Uzalendo na utaifa sasa unatawala zaidi baada ya kuchezewa kwa muda mrefu. Tanzania ni ya Mtanzania na wala siyo ya Mkenya, Mnyarwanda na mtu mwingine yeyote.

Watanzania tunayo matatizo yetu lakini angalau tunaheshimiana na tunajali utu na demokrasia. Uhuru wa kusema kwetu ni mkubwa pengine kuliko nchi nyingine yoyote ile katika afrika mashariki.

Sasa Wakenya wasifanye kosa, kama wanavyojaribu kufanya, wakadhani kuwa watanzania wamelala. Hapana, watanzania wameamka. And, in fact we have nothing to loose kuwe na EA federation au isiwepo. Wakenya ndio mtapoteza. Mtalazimika kununua bidhaa zenu wenyewe mnazozizalisha kwenye viwanda vyenu. Mtalazimika kununua colgate ishirini kwa siku na pia chocolate kibao kwa kila mmoja wenu. Mkifanya mzaa wakenya ndio mtakaokuwa wenye viwanda na wakati huo huo mkawa pia wateja. Bidhaa zenu zitawadodea. Jiepusheni na kauli za shari. Kuweni waungwana kama walivyo watu wengine. Tumieni lugha nzuri. Acheni kuwa na majivuno. Kuweni wakweli. Msiwaanzishie watanzania kampeni ya kuwashambulia kwani ni nyie wakenya mtakaoumia. Na mtaumia kweli kweli. Fikirieni wenyewe. Hamna ardhi ya kutosha.

Kelele za Wakenya kwamba tanzania inawakumbatia wazungu wa afrika kusini ni za uongo. Kenya ndio iliyowekeza zaidi tanzania kuliko afrika kusini. Magazeti yenu Daily Nation, The EastAfrican yamesambaa afrika mashariki nzima. Mngekuwa waungwana mngenyamaza kusemasema ovyo, kwani mtaumia.

Mbona waganda ni watu wastaarabu na waungwana. Kwanini wakenya msiwe kama watanzania na waganda?

My final point, hakuna haja kwa Burundi na Rwanda kujiunga na EA federation kwani in the first place shirikisho hilo la Afrika Mashariki halitakuwepo.
 
Back
Top Bottom