East Coast Team yarejea kwa kasi

brigedia mafia

JF-Expert Member
Joined
Jul 21, 2016
Posts
2,260
Reaction score
2,279
Lile kundi lililotikisa miaka ya nyuma ambalo lilikuwa na wakali kama AY, king crazy GK, Mwana FA lipo mbioni kurejea kwenye gemu


Akizungumza na E newz rapper machachali ambaye pia ni hitmaker wa songi la Zigo Abwene Yessaya au AY amesema kuwa wanasubiri kauli ya mwisho kutoka kwa GK ambaye yeye ndiye Amiri jeshi mkuu wa kundi


Ay pia hakusita kutoa pongezi kedekede kwa ujio mpya wa King Crazzy GK A.K.A baba Manka







Yapi maoni yako mdau unahisi wanaweza kurejea kwenye chat kama miaka hiyoooo??

Haya ngoja niwaachie uwanja mtililike
 
najiuliza AY ataimba chorus au?jamaa siku hizi ni more of a singer than a rapper,GK naye nimemuona anaimba afro beat za naija na amekonda ova fido dido.. .
 
Niliwapenda sana hawa vijana (Mwana FA, GK, AY, Stanboy, Buff G, Zongo) na ilisikitisha wengi waliposambaratika. Ni ndoto kwa hili kundi kurejesha makali yake ya mwanzo. Kuna sababu kadhaa.
  1. Staili yao ya muziki wa majungu wasipoiacha, hawawezi kuinuka. Nyimbo kama 'Ama zangu ama zao", "Itikadi zetu" na nyingine za maudhui hayo ndizo ziliwakimbiza akina AY na FA.
  2. Ujio wa akinda Diamond, Jux, Baraka da Prince, Darasa, Yamoto, Weusi na makundi mengine yamebadili kabisa mwonekano wa bongo fleva, kiasi kwamba inawabidi wafikiri namna bora ya kuja upya. Platform waliyo enjoy miaka hiyo haipo. Wapo waliojaribu kurudi tena kama vile Wateule, Wagosi wa Kaya, BDP, Wakali Kwanza nk lakini walibanwa mbavu na vijana wapya.
  3. Baadhi ya wasanii wa ECT wamesikika wakilalamikia ubabe wa GK, ndio sababu akina Stanboy wakatimkia USA.
By the way nawatakia kila lililo jema kwenye ujio mpya
 
Na King Kiba umesahau kumtaja mkuu
 
ni coincidence tu,jana nilikuwaa youtube natazama video za ECT...ALL THE BEST...
 
Hao maveterani mziki umesha watupa mkono watafute shughuli nyingine za kufanya kama hawakuwekeza walicho kipata ndo imekula kwao!
 
warudi tu ila wasituletee mambo yao kizamani,wawe kama jaymo,wabadilike,karudi vizuri sana,sasa hv kuna wakali kama kingzillah,bilnas,byser,wazingatie ushindani kutoka kwa kizazi hicho kipya cha hiphop,watatoboa,all da best to them
 
Dhaaaaa hata wakirud hawata kuwa km zaman aiseee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…