Economic diplomacy: Hivi Tanzania tunataka nini toka China?

Tunapaswa kushawish wachina wachukue vijana wetu weng zaid ya sasa kwenda kusoma vyuo vya China ktk masomo ya injinia na udaktar wa watu wanyama na mimea lkn pia baadh ya malighaf wachukue kwa shart ya kuziboresha hapahapa mfano mkonge,pamba ziondoke km bidhaa yaan wachukue nyuzi au kamba za katani lkn pia na sisi wenyewe tujikaze tukitegemea kila jambo kufanyiwa mwishowe tutaharibikiwa.
 
Nani kakudanganya kama China inaongoza Kwa technologia duniani?
 
Mkuu umeongea vyema, hata hiyo kuhusu hiyo la kusomesha, ukumbuke tayari tuna graduate kibao na hawana kazi wala hawawezi kujiajiri. Unasemaje kuhusu hilo?
 
Kwenye eneo la ufugaji nyuki, mtu anaweza kujiuliza kwamba kwa ni ni sasa ushirikiano kwenye eneo simple kama hilo lisilohitaji teknolojia complicated?

Ikumbukwe kuwa pamoja na kuwa 'highly mordernized' bado China ndio inaongoza kwa uzalishaji wa asali.

Tanzania pamoja na kuwa na misitu ya kutosha uzalishaji wetu uko chini sana huku vijana hawana ajira.

Hivyo tunaweza kusema changamoto kubwa kwa upande wa Tanzania ni mitaji na soko ambapo hivyo vyote wanaweza ku complement wenzetu sasa.
 
Tunahitaji technolo2rahisi ajili proceesing and final product ajili nchi sadcc eac etc....mtuwe viwanda hata 3000 kila raw material isitoke bila kuwa processed .....kuongeza thamaniii...tunahitaji wachina technology ba partnerships
 
Tunahitaji technolo2rahisi ajili proceesing and final product ajili nchi sadcc eac etc....mtuwe viwanda hata 3000 kila raw material isitoke bila kuwa processed .....kuongeza thamaniii...tunahitaji wachina technology ba partnerships
Mkuu, nadhani hizi technology tutazipata wanapowekeza na kuajiri watanzania, watakuwa wanajifunza hizo technology taratibu. Pia nadhani technology tunazohitaji ni simple tu kama za kutengeneza simple processing industries.

Technology complicated hata wakitufundisha hatutaweza kuzioperate kwenye soko la ushindani kwa faida. Kwa hiyo bora tuwaachie wenyewe tushughulike na vitu vidogo vidogo tunavyoviweza
 
Leo mnawageuka tena wakomunist wenye sifa ya kutokuwa mabeberu🤷
 
Mkuu, kupitia huo mpango wao wa "Belt and Road Initiative" wachina hawana jipya, wanatafuta tu kumiliki 'makoloni' kinyemela kupitia masharti ya mikopo yasiyotekelezeka..




 
Hatuwezi kuwa kwepa China !!
Kuwa kwepa ni kutafuta kuumia zaidi!
Tuna hitaji wawekezaji wakubwa wanao wekeza kwenye viwanda vikubwa na sio wawekezaji kwenye viwanda vinavyo fanana na viwanda ambayo wazawa wana uwezo wa kuwekeza!
Hatuhitaji kapuni za kibiasharaa (trading company) wachuuzi)
yaani wanunuzi na wauzaji kama watu wetu wanavyo fanya!
Tukiruhusu hilo tutawaumiza wa Tanzania maana watu wao wana mitaji kuliko watu wetu wata liteka soko la Kariakoo na masoko mengine ambayo ni ya watu wetu!
kama wata wekeza kwenye viwanda vikubwa vya chuma nk!
Basi viwe ni viwanda vikubwa ambavyo hakuna mtanzania ana weza wekeza kwa sasa na ambayo malighafi zake zote zina toka Tanzania!
mara nyingi viwanda ambavyo malighafi zake zina toka nje havina faida kubwa sana kwetu!!
chonde chonde wasije ruhusiwa kuanza kuuza juisi, karanga, nguo, vipuri vya magari, na viwanda vidogo na vya kati wasi ruhusiwe kufanya kabisa uwekezaji ambao watu wa ndani wana mitaji inayo tosha kuwekeza!
serekali iwajulisha Watanzania viwanda ambavyo inaona kabisa Watanzania uwezo wakuwekeza !
serekali ya China ina saidia sana sana watu wao kwenye uwekezaji! hivyo kama wata ruhusiwa kuwa wachuuzi wata waumiza watu wetu!
 
Nimependa namba mbili Ila nasikia wachina wakijua unajua kichina kama ni katika mradi wanakutimua.Anayelijua hili anisaidie
 
China ni nchi ambayo kiongozi anaweza kutakatisha fedha akala mlungula bila kelele. Mfano Kenya na SGR yao; kikwete na Bandari ya Bagamoyo pamoja na bomba la gesi
 
Robot tatu ya uzi umeongea mwenyewe kwa kuuliza maswali na kujijibu hii no dalili kuwa wewe ni dalali wa wachina.

China sio nchi nzuri sana kuwekeza sera yao ya madeni ni hatari hasa kwa nchi zetu hizi ambazo hazina intelligence nzuri. Anakukopesha then anakufanyia sabotage ushindwe kulipa deni achukue miundombinu yako.

Nashauri selikari isiwekeze mradi wowote wa kimkakati na China.

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Mabadiliko na Maendeleo yanaanzia ndani...Uchumi wa kweli ni ule ulioshikwa na Wazawa.

Hizi habari za kutegemea wawekezaji then sisi tukawe wafanyakazi ni utaahira na uvivu wa kufukiri, maana ht wao hawakufanya hivyo...

Tujenge uwezo wa ndani, serikali na mabank yatoe mitaji yenye riba nafuu na isimamiwe maana usimamizi, uvivu na uzembe ndio tatzo letu kubwa...

Tupeleke nje vijana wengi sana wakasome nje, hawa ndio watakaotuletea technology ndani km wachina wanavyomfanyia mmarekani.

Na km tunataka hao wawekezaji lazima sharti la ubia na mzawa liwekwe..ila hii ya sasa muwekezaji 100% anamiliki yy, ma tax holiday juu haitatufikisha popote zaidi ya kutengeneza matabaka na kuja kuleta mtafaruku huko mbele km South Africa.

Uchumi wa kweli na wenye multiplier effects ni ule wa wazawa sio wawekezaji kutoka inje. Ht China Ma billionaire wao wote ni wazawa na sio wahindi na wazungu km huku kwetu Africa.
 
2. Tuwashawishi wawekeze mtaji kwenye ufugaji nyuki kwa kutoa vifaaa halafu watanzania wanafuga kwenye mapori yetu halafu asali tunauza China. Ikumbukwe tuna mapori ya kutosha na ufugaji nyuki hauharibu mazingira.
Hivi kweli tunahitaji watu kutoka nje kuja kuwekeza hata kwenye ufugaji nyuki?!!!

Tunao ma-graduate wengi tu wa misitu na nyuki toka SUA, hawana kazi ila elimu wanayo. Kwa nini serikali isiwape mitaji ya kuwekeza huko?
Au watumike kusimamia wafugaji wadogo.

China imepiga hatua kubwa ya maendeleo kutokana na serikali yao kusaidia wananchi wake kupata elimu, ujuzi na mitaji..
 
Mbona jibu Mama alishasema kwenye hotuba yake tunataka ajira kuwe na mzunguko wa pesa...

Ushasema kwamba watanzania tuna misitu na ardhi lakini hatuna mitaji na technology ya kuzalisha kwa wingi na ubora ilituweze kuuza nje na pia tunawasomi ambao hawana ajira, wapo tu ni watazamaji wa matukio ya maendeleo na siasa za dunia...basi sisi tuzidi kuomba Mungu tupate nchi “muwekezaji” atakae tupenda sana atutatulie tulipokwama..maana uwezo sisi hatuna sisi ni maskini....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…