Eddie Ganzel

Eddie Ganzel

Hajakosea mkuu.........

Hammie Rajab amefariki wiki iliyopita tarehe 21/04/2011 katika hospitali ya Amana Ilala ambako alilazwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Malaria.....Mungu ailaze Roho yake mahali pema peponi,Amina

Hata mimi nilikuwa mpenzi wa hadith zake,kazi ya Mungu haina makosa,apumzike kwa amani,AMINA.
 
kuna kitabu kilikuwa kinaitwa kambi ya makava kilihusu vita kaka yangu alikuwa anasoma halafu ananisimulia miki nikiwa std2 yeye alikuwa std 4 miaka ya mwanzo ya themanini alikuwa mwanachama pale library sumbawanga basi akinisimulia habari za vita naogopa usiku silalii mtuzi hata nimesahau. kulikuwa na vitabu vya watoto vikiuzwa pale bookshop za wakatoliki sumbawanga kikiitwa Mbuzi aliyetaka kuwa simba yaani ndani ni vichekesho mtupu huyo mbuzi alijifanya mjanja akajitengenezea ngozi akawa anafanana na simba akajichanganya na simba wiki nzima anazurula na simba siku njaa imewauma simba wakaamua kuwinda na yeye yupo pamoja na wakaua swala kimbembe kwenye kula aliponusa damu tu si akapiga chafya ile ya kimbuzi mbuzi wale simba wakashtukia yule mbuzi alipoona simba wamemshtukia akajawa na uoga akadondosha zile karanga zake mmmh! simba wakataharuki yule mbuzi akajipa courage ngoja niwatishe niungurume wajue mie simba duuu ndo akawa kaharibu kabisaa badala ya kuunguruma akatia meeeeee kilichofuata hapo ni kuwa kitoweo cha buree kwa wale simba
 
Mkuu hebu cheki tena taarifa zako. Hammie Rajab amefariki lini? Huyu nadhani bado yupo ila siku hizi anashiriki zaidi kwenye utengenezaji wa filamu na sio uandishi wa Vitabu. Kama sikosei.

Kwa kukudhibitishia Hamie Rajab ameshafariki but kuna mwanae Mohamed Hammie au Anko Mo. ndie amerithi kipaji ya baba yake, unaweka kuperuzi blog ya huyo dogo mtoto Hamie Rajab
ankomo@blogspot.com
 
Yap nami namkumbuka sana huyu mwandishi pamoja na akina Sam Kitogo, S.M.Bawji, faraj Katalambula, Agolo Andulu. kwani na hammie rajab yu wapi?
Baadhi ya vitabu nilivyosoma vya waandishi hawa ni hivi
>Roho mkononi
>Awe hai au amekufa namtaka
>Nimekoma ukuwadi na shogayo hasidi
>Njama, Kikomo, Kikosi cha kisasi & kufa na kupona
>Simu ya Kifo
>Joto la fedha

ha ha ha ilikuwa raha kwakweli wakati ule.

Duh, mmenikumbusha mbali!
 
John Rutayisingwa
Eddie Ganzel
Hammie Rajab
Elvis Musiba hawa wote walikuwa na riwaya motomoto lakini hatunao tena.mungu uwapumzishe kwa amani
Wanaoendeleza jahazi ni
Beka Mfaume na Innocent Ndayanse-
 
Kuna mwandishi niliwahi soma kitabu chake zamani hizo anaitwa john simbamwene. yupo wapi naye?
 
Vitabu vya siku hizi utaona title nakula nyama za watu, jini mahaba, etc!! Them good old days unasoma kitabu unaridhika.
 
Kuna mtunzi anaitwa anaitwa Hussein Tuwa.........Jamaa ni mzuri sana kwenye utunzi,anatunga Riwaya/Vitabu vitamu sana...

Binafsi nimebahatika kusoma Riwaya zake kama Mdunguaji,Mtuhumiwa,Mkimbizi,Mfadhili, Bondia na Utata wa 9/12.......Jamaa anatisha hasa

mkimbizi ndo mwisho wa matatizo.naapa hakuna story niliyoipenda kama hiyo (tigga mumba
 
kikomo,njama,kikosi cha kisasi,madhambi ya Elita, pumabzo la roho ilikuwa km tunaangalia ''movie'' na hv TV hatukuwa nazo
 
Eric anaandika hadithi ndefu sana hawa magwiji waliotajwa riwaya zao hazikikuwa ndefu sana sababu walitambua hadhira yao ni wavivu wa kusoma
 
Hao jamaa walikuwa Magwiji mahiri wa riwaya za kusisimua pia alikuwapo John Rutayisingwa na Agoro Anduru
kwa sasa wanajitahidi kuendeleza fani ni Beka Mfaume na Ndalichako
huyo jamaa mwingine uliyemtaja cjui huwa anaandika nini mpaka page inajaa
Umenikumbusha John Rutayisingwa na Agoro Anduru, kwa nini waandishi wazuri maisha yao ni mafupi. RIP WOTE, AMEN
 
Uandishi haulipi niliwahi kujidanganya after being inspired nikaandika HEKAHEKA ,kashifa .hadithi zikatoka msanii miaka ya tisini malipo yakawa kidogo na sikupata mtu wa kunisponser nikaghairi.baadae nikaona nitest novel.nikaandika HÖTSOUP in the beginning.ni cha kijasusi kinahusu gulfwarone irag .nilikua bush skupata spönser miaka hyo ya tisini na tano.
Mwisho nkaandika HOTSOUP the aftermath hicho miaka 2005 after gulfwar two nikaishia chapter six nikawa nimepata ajira nikabullshit.
Kwa hapa bongo fani hailipi labda upublish na kuuzia majuu
Mkuu kweli kwa uandishi huu ulikuwa mwandishi wa vitabu za hadithi?
 
Kuna mwandishi niliwahi soma kitabu chake zamani hizo anaitwa john simbamwene. yupo wapi naye?
Hili jina lako la Masulupwete kwa mara ya kwanza nililisoma kwenye kitabu kiitwacho Mtu ni Utu. Alikuwa ni mmoja wa wahusika wakuu. Jina la mtunzi wa kitabu ni George A. Mhina.
 
Kuna kitabu kimoja nadhani kiliandikwa na mtunzi wa Rosa mystika kilikuwa kinamhusu padri in the making kinaitwa'PETE' sikumalizia kukisoma and I have often wondered about it...kama hiyo ndio correct title nijuveni
Unazungumzia Gamba la Nyoka cha Mwanafalsafa mbobezi Euphrase Kezilahabi. Padri Madevu jasusi la CIA na mjane Mama Tinda. Kazi zingine za Kezilahabi ni Kichomi na Karibu Ndani (Mashairi), Nagona na Mzingile (Novela), Rosa Mistika, Gamba la Nyoka, Kichwamaji na vingine viwili vitatu hivi nimevisahau. Kama unaweza kufikiri tafuta vinovela hivyo (Nagona na Mzingile) ujisomee halafu ulete mrejesho hapa.
 
Eddie Ganzel nimemsoma vitabu vyake, pamoja na kina Ben Mtobwa, Hammie Rajab na baba lao Eristablus Elvis Musiba.
Hivi vitabu viko bookshop gani i.e. Vya Eddie Ganzel, Agoro Anduru nk? (NB: Najua Pundit ha-exist tena ila kama yeyote mwenye jibu tafadhali!
 
Unazungumzia Gamba la Nyoka cha Mwanafalsafa mbobezi Euphrase Kezilahabi. Padri Madevu jasusi la CIA na mjane Mama Tinda. Kazi zingine za Kezilahabi ni Kichomi na Karibu Ndani (Mashairi), Nagona na Mzingile (Novela), Rosa Mistika, Gamba la Nyoka, Kichwamaji na vingine viwili vitatu hivi nimevisahau. Kama unaweza kufikiri tafuta vinovela hivyo (Nagona na Mzingile) ujisomee halafu ulete mrejesho hapa.
Sw umebobea huko nafikiri...
 
MATHIAS KABYEMERA mkuu Eddie Ganzeli ametotoka muda mrefu sana. Mola amfanyie wepesi ktk maisha yake ya kaburini. Nimejaribu kukutafutia huu upate kujiridhisha
 
Back
Top Bottom