Edibily Jonas Lunyamila, miguu ya Dhahabu, kichwa chenye mamlaka ya kusoma alama zote ndani ya Uwanja

Edibily Jonas Lunyamila, miguu ya Dhahabu, kichwa chenye mamlaka ya kusoma alama zote ndani ya Uwanja

Hii picha Katika mchezo wa fainali ya kombe la Hedex, uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza.
Hii ilikuwa ni muda mfupi baada ya Lunyamila kutua nchini toka nchini Ujerumani alikokuwa amekwenda kufanya majaribio ya kucheza soka la kulipwa, na siku hii akiwapiga Simba moja kati ya mabao mawili na lingine likifungwa na Bakari Malima kufuatia kona ya Lunyamila. Yanga ilishinda 3-0
1908323_880535095322358_7761619432287883378_n.jpg


Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Hii ni hazina, na ni vizuri anapata sifa zake akiwa ni hai bado, badala ya kusubiri atakapokufa ndio sifa zake zienee na michango lukuki kama ilivyo mazoea kwa Tanzania yenye unafiki.

Hongera sana E.J Lunyamila

Yanga imekuwa na hazina kubwa ya wachezaji Wazuri sana.
 
Hii ni hazina, na ni vizuri anapata sifa zake akiwa ni hai bado, badala ya kusubiri atakapokufa ndio sifa zake zienee na michango lukuki kama ilivyo mazoea kwa Tanzania yenye unafiki.

Hongera sana E.J Lunyamila

Yanga imekuwa na hazina kubwa ya wachezaji Wazuri sana.
Nakumbuka 1993, kwnye mashindano ya Challage navikiri Yanga ikicheza na AS Villa tulipiga bao 2-1 Lunya akifunga bao la pili, Kule Uganda mpka leo kuna Mabasi yammeandikwa Lunyamila

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
EDIBILY JONAS LUNYAMILA . Macho yangu yameshuhudia mengi na Moyo wangu umebahatika kujawa na hisia tosha kwa Uzalendo wa Taifa langu la Tanzania.

Miaka mingi tumekua tukiimba nyimbo za kuitukuza Nchi yetu na mashujaa na hata kuwasoma katika historia . " Tazama Ramani utaona Nchi nzuri, yenye mito na mabonde mengi ... " au hata ubeti mwingine maarufu " ... jina lako ni tamu sana, nilalapo nakuota wewe, niamkapo ni Heri Mama weee . "Hii yote ni kuipenda Nchi yetu lakini tuna mengi hatuyaimbi na kuyatukuza.

Edibily Jonas Lunyamila, miguu ya Dhahabu, kichwa chenye mamlaka ya kusoma alama zote ndani ya Uwanja, kipaji maridhawa kabisa katika ukanda huu.

Ukienda Uganda hadi leo jina La Lunyamila ni Maarufu kuliko Emanuel Okwi ni kutokana na uwezo wa maajabu wa Winga huyu .

Mwaka 1992 katika mashindano ya UMISETA kule Zanzibar kiliibuka kipaji cha Dhahabu kutoka shule ya Sekondari ya Buhangija huko Shinyanga na mwaka huo akaitwa Timu ya Taifa, bahati iliyoje.

Inasemekana Abbas Gulamali ndiye aliyekwenda kumsubiri Edibily Jonas Lunyamila mlangoni mwa chumba cha mtihani ili ampeleke Mwanza kucheza timu ya Taifa.

Nafikiri hii ndiyo sababu akacheza Yanga na mwaka 1993 akaacha alama ya Maisha yake Kule Kampala Uganda. Kwangu Mimi maisha ya soka ya Lunyamila na kipaji chake kinastahili kuimbwa kama kivutio cha Taifa na ni Hadhi ya Nyota Tano.

Nikiwakumbuka watangazaji wa zamani kina Swedi Mwinyi, Juma Nkamia, Ahmed Jongo au Charles Martin Hillary walivyokua wakitangaza soka basi mie jina linalokuja ni Lunyamila.

Unamkumbuka Edibily Jonas Lunyamila kwa lipi au nyakati gani..?
Tulisoma nae yeye anaingia F1 mi F4, lakini mechi ya Welcome F1 alitutesa sana.
 
Nahisi huyu Jamaa ndio alisababisha mm kuishabikia yanga,
Maana kipindi hicho anacheza nilikua Mdogo hata shule siajaanza , kuna mzee tulikua tunaishi nae alikua anamsifia Sana Jamaa na alikua ni yanga nikajikuta nafuata tu upepo na kua shabiki Wa yanga
 
Nahisi huyu Jamaa ndio alisababisha mm kuishabikia yanga,
Maana kipindi hicho anacheza nilikua Mdogo hata shule siajaanza , kuna mzee tulikua tunaishi nae alikua anamsifia Sana Jamaa na alikua ni yanga nikajikuta nafuata tu upepo na kua shabiki Wa yanga
Karibu tu jangwani
 
Tupe briefly habari zake mkuu

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
Lunya kama alivyopenda kuitwa ni miongoni mwa vipaji murua katika soka kuwahi kutokea nchini. Aliujua mpira nao ulimtii. Wakati wa paper ya mwisho form 4, alifanya mtihani huku akisubiriwa na gari la Gulamali nje.
Kizuri ninachomsifu Lunya ni utulivu na Nidhamu ya matumizi. Fedha aliyoipata alifanya vitu vonavyombeba Leo. Kosa kubwa katika maisha yake ya soka ni kuwa na mapenzi yaliyopitiliza kwa Yanga kwa kisingizio cha kukumbuka fadhila. Safari ya Ujerumani ilikuwa hatua ya kutokea lakini mapenzi kwa Yanga yakamwangusha.
 
Lunyamila,Kizota, Nteze na Mmachinga vipaji hivi havitatokea hivi karibuni kwenye soka la bongo
Lunyanila na Nteze....ni matunda ya umiseta.....tunapoteza vipaji vingi sana kwa kupuuzia michezo mashuleni.... siku hizi Shuleni michezo haichezwi tena Kama zamani.... serikali kwenye hili imetuangusha sana....shule inafunguliwa na vibali vyote kwenye eneo la nusu eka.....hakuna viwanja vya michezo....wanaocheza mpira siku hizi ni ambao hawajafanikiwa kwenda shule....wengi vipaji hawana wanalazimisha tu.
 
[emoji23][emoji23][emoji23] yanga wanahiki kitabia chakuwarubuni wachezaji mfn. Tegete alitakiwa na timu nyingi za nnje wakambania hadi carer yake ikaishia Yanga


hata Msuva walitaka kumbania lkn and of the day club iliyumba kifedha na Difaa walitoa Dau kubwa ikabid Msuva aondoke bila hivyo angeondoka kama mchezaj huru na club isingepata kitu

Nakumbuka kipindi kile Manji ndo anakabilia na mashtaka kedekede...pesa za Msuva zulitusaidia sana kipindi kile viongozi wayanga walimpa baraka zote
Maajabu! na hao wachezaji kwa nini wabakubali kurubuniwa?
 
Back
Top Bottom