EDO KUMWEMBE: Ndoto inayotisha dhidi ya ndoto inayosikitisha Simba, Yanga

EDO KUMWEMBE: Ndoto inayotisha dhidi ya ndoto inayosikitisha Simba, Yanga

Oldmantz

JF-Expert Member
Joined
Jan 24, 2023
Posts
704
Reaction score
1,457
NI ndoto inayotisha. Pambano la Simba dhidi ya Wydad Casablanca ya Morocco ni ndoto inayotisha. Simba wametoka kufungwa jumla ya mabao 6-1 katika mechi mbili walizocheza na Raja, timu nyingine kutoka jiji hilo lenye wakazi milioni tatu na zaidi nchini Morocco.

Lakini kuna ndoto nyingine inayosikitisha. Pambano la Yanga dhidi ya Rivers United ya Nigeria. Kwanini Yanga walikuwa wanashangilia baada ya kupangwa na Rivers? Bado sijaelewa vizuri. Kwamba ni timu rahisi? Kwamba labda Rivers wana nafuu tofauti kama wangepangwa na wakubwa wengine wa kundi kama Pyramids?

Tuanze na mechi ya Simba. Sioni nafuu. Ni ndoto inayotisha. Ninachoamini ni kwamba ikitokea Simba wakaitoa Wydad basi wataenda kuchukua taji lenyewe. Ni ngumu Simba kuwatoa Wydad kwa sababu tatu kuu.

Inawezekana pia ni ngumu Simba kuitoa timu nyingine yoyote ambayo wangepangwa nayo kando ya Wydad.
Labda tujikite kwa Wydad pekee ambao tayari wamewekwa katika mikono ya Simba. Simba watahitaji maajabu. Ukitazama namna ambavyo walitawaliwa na Raja katika mechi zote mbili kisha ukaenda kutazama msimamo wa Ligi Kuu ya Morocco utajua mazingira ya hatari ambayo Simba wapo.

Katika uhalisia wa kawaida Wydad ni timu kali kuliko Raja. Na katika uhalisia wa nje tu Wydad imeizidi Raja pointi 12 katika Ligi yao. Raja inashika nafasi ya tano wakati Wydad inashika nafasi ya pili. Inakuonyesha tu kwamba hata katika Ligi yao ya Morocco kwa sasa Wydad ni wakali kuliko Raja achilia mbali kwamba wao ni mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Lakini kuna ukweli kwamba Wydad wanacheza na Simba hii ambayo imeendelea kujitafuta. Simba ambayo haijafikia bado makali ya ile ya kina Louis Miquissone, Clatous Chama, Hassan Dilunga, Rally Bwalya. Simba hii ambayo viwango vya kina Josh Onyango vimeanza kuwatia shaka mashabiki. Wataiweza kasi ya Wydad kama walishindwa kuendana na kasi ya Raja?

Lakini sababu ya tatu ni ukweli kwamba mechi ya kwanza itachezwa kwenye Uwanja wa Mkapa pale Temeke. Simba sio tu watahitaji kushinda, lakini watahitaji kushinda mabao mengi. Hili la kushinda mabao mengi dhidi ya Wydad ni jambo ambalo litawastaajabisha watu wengi. Kuifunga Wydad ni jambo moja, kuifunga mabao mengi ni jambo jingine ambalo litastaajabisha. Simba wataweza kweli?

Ni wazi kwamba kule Casablanca Simba wanaweza kupewa ubatizo wa moto. Kama wanatamani kujaribu kupita basi kila kitu kimalizike Casablanca. Kinachoweza kuwapitisha ni kufungwa idadi ndogo ya mabao kuliko ambayo wao watakuwa wamefunga Dar es Salaam. Hili litawezekana? Naona ni jambo gumu.

Casablanca Simba watakutana na mashabiki wenye mzuka wa Wydad. Katika mechi ya mwisho waliyokwenda Casablanca walikutana na jukwaa moja la mashabiki wa Raja ambao bado waliwapa shida. Mashabiki wengi hawakwenda uwanjani kwa sababu Raja alishapita na tayari alishapata uongozi wa kundi.

Mechi hii ya robo, bila ya kujali ambacho kitatokea Dar es Salaam pale Temeke, Wydad watataka kuziyumbisha akili za wachezaji wa Simba. Wale mashabiki wao vichaa wataingia uwanjani kama sherehe ya kuipeleka timu yao nusu fainali kwa mara nyingine tena huku wakiamini kwamba wanakwenda kutetea ubingwa wao kwa mara nyingine tena.

Vyovyote ilivyo, Simba wanahitaji kupambana. Kucheza kiume hasa kwa ajili ya kulinda heshima ya nchi. Watahitaji kupambana nyumbani na ugenini kwa ajili ya kulinda heshima ya nchi. Kutolewa ni jambo moja, kutolewa kifedheha ni jambo jingine.

Ninachofahamu ni kwamba Simba ikicheza mechi kama hizi huwa inabadilika zaidi. Watahitaji kubadilika zaidi.

Vipi rafiki zao Yanga? Nilishangaa kuona wanashangilia baada ya kupangwa na Rivers. Akili yangu inanituma kwamba kama Yanga hii ingecheza na Rivers ile ya miezi 24 nyuma huenda Yanga hii ingepita.

Walitolewa kwa kufungwa kwa matokeo ya aina moja ya 1-0 nyumbani na ugenini. Fiston Mayele na Khalid Aucho hawakucheza baada ya leseni zao kuchelewa.

Pia Yanga hawakuwa katika ubora kama ambao leo wanao. Hata hivyo, hii ni hadithi ya upande mmoja. Vipi kuhusu Rivers? Yanga wanajua kwamba Rivers wamekwenda juu maili ngapi baada ya kucheza nao pambano la mwisho pale Port Harcourt? Nadhani Yanga walifurahia kupangwa na Rivers kwa sababu wamewakwepa Pyramids na USM Alger.

Lakini walishangilia kwa sababu ya kuona walikuwa wamepangwa na Rivers ambayo bado ipo katika vichwa vyao. Ile Rivers ya kawaida ambayo walicheza nayo mechi mbili na kisha wakatolewa. Katika vichwa vyao wangefanya uchunguzi kwanza kujua kama watacheza na Rivers ile ile au nyingine ambayo inalisaka taji la Shirikisho.

Vile vile naamini kwamba wameshangilia kwa sababu wanajua kwamba safari hii wataanzia pambano lao ugenini kisha kumalizia nyumbani. Kwamba watafanya kila wanachoweza kupambana ugenini na kupata ushindi au sare halafu wamalize kazi nyumbani. Siamini sana katika jambo hili kwa sababu majuzi tu Waganda wametukumbusha kitu.

Taifa Stars walikwenda Ismailia wakapata ushindi dhidi ya The Cranes. Waliporudi Uwanja wa Taifa wakachapwa kwa kipigo kile kile ambacho walikitoa Misri. Ni hadithi kama ile ya Simba mwaka 1993 walipoingia fainali za CAF. Walikwenda Abidjan kucheza dhidi ya Stella wakatoka suluhu. Waliporudi nyumbani wakalala 2-0.Yanga wasishangailie sana kupangwa na Rivers.

Kikawaida tu katika heshima ya mchezo huu haupaswi kushangilia kupangwa na timu yoyote ile. Unahitaji kuonyesha heshima. Kama hauonyeshi heshima unaweza kujikuta katika ndoto inayosikitisha mbele ya safari.

MWANASPOTI
 
Ubora wa Edo katika kuandika makala umeshuka sana. Hazivutii tena makala zake,kuna kipindi nilikuwa natafuta gazeti la Mwanaspoti kumsoma tu Edo . Kwenye waandishi wa habari niliowa-follow Instagram Kumwembe ni mmoja wapo.Niliacha kumfuata Edo Kumwembe Instagram baada ya kuona ile ni kurasa ya Shabiki wa Arsenal na sio kurasa ya mwanahabari. Nyakati zinaenda kasi sana. Asante Edo kwa makala zako nzuri sana za wakati huo.
 
Kimsingi Simba na Yanga wote Wana kazi kubwa
Kitu pekee Edo anapswa kujua ni kuwa
"Mayele ,Musonda,Mzinze na Kaze hawakushangilia"wao walikuna vichwa pekee.
 
Ubora wa Edo katika kuandika makala umeshuka sana. Hazivutii tena makala zake,kuna kipindi nilikuwa natafuta gazeti la Mwanaspoti kumsoma tu Edo . Kwenye waandishi wa habari niliowa-follow Instagram Kumwembe ni mmoja wapo.Niliacha kumfuata Edo Kumwembe Instagram baada ya kuona ile ni kurasa ya Shabiki wa Arsenal na sio kurasa ya mwanahabari. Nyakati zinaenda kasi sana. Asante Edo kwa makala zako nzuri sana za wakati huo.
Mzee katekwa Sana na nguvu ya matajiri wa Simba na yanga sikuhiz sio Edo yule
 
Raja ana kiwango sasahivi kuliko Wydad, kwahiyo naweza sema Simba anaweza kujikongoja.. ikibidi kufanya maajabu.

Mechi ya pili Simba na Raja kama uliangalia, ni wazi lolote laweza tokea. Form ya Simba walivopigwa tatu bila ni tofauti sana kwa sasa.
 
NI ndoto inayotisha. Pambano la Simba dhidi ya Wydad Casablanca ya Morocco ni ndoto inayotisha. Simba wametoka kufungwa jumla ya mabao 6-1 katika mechi mbili walizocheza na Raja, timu nyingine kutoka jiji hilo lenye wakazi milioni tatu na zaidi nchini Morocco.
Lakini kuna ndoto nyingine inayosikitisha. Pambano la Yanga dhidi ya Rivers United ya Nigeria. Kwanini Yanga walikuwa wanashangilia baada ya kupangwa na Rivers? Bado sijaelewa vizuri. Kwamba ni timu rahisi? Kwamba labda Rivers wana nafuu tofauti kama wangepangwa na wakubwa wengine wa kundi kama Pyramids?
Tuanze na mechi ya Simba. Sioni nafuu. Ni ndoto inayotisha. Ninachoamini ni kwamba ikitokea Simba wakaitoa Wydad basi wataenda kuchukua taji lenyewe. Ni ngumu Simba kuwatoa Wydad kwa sababu tatu kuu. Inawezekana pia ni ngumu Simba kuitoa timu nyingine yoyote ambayo wangepangwa nayo kando ya Wydad.
Labda tujikite kwa Wydad pekee ambao tayari wamewekwa katika mikono ya Simba. Simba watahitaji maajabu. Ukitazama namna ambavyo walitawaliwa na Raja katika mechi zote mbili kisha ukaenda kutazama msimamo wa Ligi Kuu ya Morocco utajua mazingira ya hatari ambayo Simba wapo.
Katika uhalisia wa kawaida Wydad ni timu kali kuliko Raja. Na katika uhalisia wa nje tu Wydad imeizidi Raja pointi 12 katika Ligi yao. Raja inashika nafasi ya tano wakati Wydad inashika nafasi ya pili. Inakuonyesha tu kwamba hata katika Ligi yao ya Morocco kwa sasa Wydad ni wakali kuliko Raja achilia mbali kwamba wao ni mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Lakini kuna ukweli kwamba Wydad wanacheza na Simba hii ambayo imeendelea kujitafuta. Simba ambayo haijafikia bado makali ya ile ya kina Louis Miquissone, Clatous Chama, Hassan Dilunga, Rally Bwalya. Simba hii ambayo viwango vya kina Josh Onyango vimeanza kuwatia shaka mashabiki. Wataiweza kasi ya Wydad kama walishindwa kuendana na kasi ya Raja?
Lakini sababu ya tatu ni ukweli kwamba mechi ya kwanza itachezwa kwenye Uwanja wa Mkapa pale Temeke. Simba sio tu watahitaji kushinda, lakini watahitaji kushinda mabao mengi. Hili la kushinda mabao mengi dhidi ya Wydad ni jambo ambalo litawastaajabisha watu wengi. Kuifunga Wydad ni jambo moja, kuifunga mabao mengi ni jambo jingine ambalo litastaajabisha. Simba wataweza kweli?
Ni wazi kwamba kule Casablanca Simba wanaweza kupewa ubatizo wa moto. Kama wanatamani kujaribu kupita basi kila kitu kimalizike Casablanca. Kinachoweza kuwapitisha ni kufungwa idadi ndogo ya mabao kuliko ambayo wao watakuwa wamefunga Dar es Salaam. Hili litawezekana? Naona ni jambo gumu.
Casablanca Simba watakutana na mashabiki wenye mzuka wa Wydad. Katika mechi ya mwisho waliyokwenda Casablanca walikutana na jukwaa moja la mashabiki wa Raja ambao bado waliwapa shida. Mashabiki wengi hawakwenda uwanjani kwa sababu Raja alishapita na tayari alishapata uongozi wa kundi.
Mechi hii ya robo, bila ya kujali ambacho kitatokea Dar es Salaam pale Temeke, Wydad watataka kuziyumbisha akili za wachezaji wa Simba. Wale mashabiki wao vichaa wataingia uwanjani kama sherehe ya kuipeleka timu yao nusu fainali kwa mara nyingine tena huku wakiamini kwamba wanakwenda kutetea ubingwa wao kwa mara nyingine tena.
Vyovyote ilivyo, Simba wanahitaji kupambana. Kucheza kiume hasa kwa ajili ya kulinda heshima ya nchi. Watahitaji kupambana nyumbani na ugenini kwa ajili ya kulinda heshima ya nchi. Kutolewa ni jambo moja, kutolewa kifedheha ni jambo jingine. Ninachofahamu ni kwamba Simba ikicheza mechi kama hizi huwa inabadilika zaidi. Watahitaji kubadilika zaidi.
Vipi rafiki zao Yanga? Nilishangaa kuona wanashangilia baada ya kupangwa na Rivers. Akili yangu inanituma kwamba kama Yanga hii ingecheza na Rivers ile ya miezi 24 nyuma huenda Yanga hii ingepita. Walitolewa kwa kufungwa kwa matokeo ya aina moja ya 1-0 nyumbani na ugenini. Fiston Mayele na Khalid Aucho hawakucheza baada ya leseni zao kuchelewa.
Pia Yanga hawakuwa katika ubora kama ambao leo wanao. Hata hivyo, hii ni hadithi ya upande mmoja. Vipi kuhusu Rivers? Yanga wanajua kwamba Rivers wamekwenda juu maili ngapi baada ya kucheza nao pambano la mwisho pale Port Harcourt? Nadhani Yanga walifurahia kupangwa na Rivers kwa sababu wamewakwepa Pyramids na USM Alger.
Lakini walishangilia kwa sababu ya kuona walikuwa wamepangwa na Rivers ambayo bado ipo katika vichwa vyao. Ile Rivers ya kawaida ambayo walicheza nayo mechi mbili na kisha wakatolewa. Katika vichwa vyao wangefanya uchunguzi kwanza kujua kama watacheza na Rivers ile ile au nyingine ambayo inalisaka taji la Shirikisho.
Vile vile naamini kwamba wameshangilia kwa sababu wanajua kwamba safari hii wataanzia pambano lao ugenini kisha kumalizia nyumbani. Kwamba watafanya kila wanachoweza kupambana ugenini na kupata ushindi au sare halafu wamalize kazi nyumbani. Siamini sana katika jambo hili kwa sababu majuzi tu Waganda wametukumbusha kitu.
Taifa Stars walikwenda Ismailia wakapata ushindi dhidi ya The Cranes. Waliporudi Uwanja wa Taifa wakachapwa kwa kipigo kile kile ambacho walikitoa Misri. Ni hadithi kama ile ya Simba mwaka 1993 walipoingia fainali za CAF. Walikwenda Abidjan kucheza dhidi ya Stella wakatoka suluhu. Waliporudi nyumbani wakalala 2-0.Yanga wasishangailie sana kupangwa na Rivers. Kikawaida tu katika heshima ya mchezo huu haupaswi kushangilia kupangwa na timu yoyote ile. Unahitaji kuonyesha heshima. Kama hauonyeshi heshima unaweza kujikuta katika ndoto inayosikitisha mbele ya safari.

MWANASPOTI
Edo kaathiriwa na mawazo ya kikoloni kuwa sisi hatuwezi kwa sababu siku zilizopita hatukuwa tunaweza!! Akili ya kutokuwa na uthubutu wa kujikomboa!! Waafrika wengi wameathiriwa sana na mawazo hayo mgando!! Nimkumbushe tu huyu edo nabii wa kushindwa kuwa Simba hii:
1. Ilimtoa Al Ahyl aliyekuwa bingwa mtetezi mashindano ya klabu bingwa afrika.
2. Iliongoza kundi lililokuwa na Al Ahyl ambayo baadaye ilitwaa taji la afrika.
Kwa hiyo kumfunga bingwa mtetezi haitakuwa mara ya kwanza kwa simba!
Lakini pia Simba imeifunga timu afika ya kaskazini 7-0!! Haijawahi kutokea kwenye ukanda wetu wa afrika ya mashariki kuibatiza ubatizo wa moto timu toka afrika ya kaskazini!! Kwa hiyo si ngumu sana Simba kuifunga Wydad kama ambavyo Edo anataka tuamini!!
 
Ubora wa Edo katika kuandika makala umeshuka sana. Hazivutii tena makala zake,kuna kipindi nilikuwa natafuta gazeti la Mwanaspoti kumsoma tu Edo . Kwenye waandishi wa habari niliowa-follow Instagram Kumwembe ni mmoja wapo.Niliacha kumfuata Edo Kumwembe Instagram baada ya kuona ile ni kurasa ya Shabiki wa Arsenal na sio kurasa ya mwanahabari. Nyakati zinaenda kasi sana. Asante Edo kwa makala zako nzuri sana za wakati huo.
Uko sahihi. Edo alikuwa wa moto mno. Kuna makala yake yenye kichwa cha habari kwamba Baba wa taifa angemkemea Pep Guardiola ilinifurahisha sana.. ila kwa sasa hivi haeleweki. Zamani nilikuwa namsoma Edo Kumwembe na Mzee Joseph Mihangwa. Raia Mwema na mwanaspoti nilikuwa sikosi kila wiki.
 
Ubora wa Edo katika kuandika makala umeshuka sana. Hazivutii tena makala zake,kuna kipindi nilikuwa natafuta gazeti la Mwanaspoti kumsoma tu Edo . Kwenye waandishi wa habari niliowa-follow Instagram Kumwembe ni mmoja wapo.Niliacha kumfuata Edo Kumwembe Instagram baada ya kuona ile ni kurasa ya Shabiki wa Arsenal na sio kurasa ya mwanahabari. Nyakati zinaenda kasi sana. Asante Edo kwa makala zako nzuri sana za wakati huo.
Wabongo bana!! edo alishasema yeye kama unataka usirias mfatilie ktk gazeti la mwanasport na sport arena ila Instagram kwake ni sehemu kujiburudisha na kujipa furaha wala sio sehemu ya kazi..akasema Instagram hawezi kutoa maoni au mawazo yake ya msingi na kama unataka edo aliyesiriasi kamtafute ktk makala zake za mwanasport na kamsikilize redion

Instagram ni kijiwe cha soga tu sio sehem rasmi ya watu kuleta habari, katafute makala yake moja edo inaitwa 'nani anajali"

Edo anasema alishasema ametumia muda mwingi mitandaoni kuandika mambo ya msingi ktk nchi hii ila hakuna anayejali sasa kwann yeye ajali? Na yeye ameamua kutokujali ndomana unamuona hivo Instagram ndo mambo wanayopenda wabongo ya kipumbavu
 
Wabongo bana!! edo alishasema yeye kama unataka usirias mfatilie ktk gazeti la mwanasport na sport arena ila Instagram kwake ni sehemu kujiburudisha na kujipa furaha wala sio sehemu ya kazi..akasema Instagram hawezi kutoa maoni au mawazo yake ya msingi na kama unataka edo aliyesiriasi kamtafute ktk makala zake za mwanasport na kamsikilize redion

Instagram ni kijiwe cha soga tu sio sehem rasmi ya watu kuleta habari, katafute makala yake moja edo inaitwa 'nani anajali"

Edo anasema alishasema ametumia muda mwingi mitandaoni kuandika mambo ya msingi ktk nchi hii ila hakuna anayejali sasa kwann yeye ajali? Na yeye ameamua kutokujali ndomana unamuona hivo Instagram ndo mambo wanayopenda wabongo ya kipumbavu
wabongo wamefanya nini? wabongo ndio wameandika comment hapa? Afanye masikhara anayotaka huko instagram mie simfuati tena kwahiyo sijali,kuna waandishi makini nimewafuata na sijuti.Hata hizo makala zake za mwanaspoti unazosema tumfuate akiwa serious hazina mvuto tena,nifuate nini? Mazoea?
 
wabongo wamefanya nini? wabongo ndio wameandika comment hapa? Afanye masikhara anayotaka huko instagram mie simfuati tena kwahiyo sijali,kuna waandishi makini nimewafuata na sijuti.Hata hizo makala zake za mwanaspoti unazosema tumfuate akiwa serious hazina mvuto tena,nifuate nini? Mazoea?
kipindi hicho nadhani unaongelea 'jicho la mwewe' mwanasport ya jumamosi,......
 
wabongo wamefanya nini? wabongo ndio wameandika comment hapa? Afanye masikhara anayotaka huko instagram mie simfuati tena kwahiyo sijali,kuna waandishi makini nimewafuata na sijuti.Hata hizo makala zake za mwanaspoti unazosema tumfuate akiwa serious hazina mvuto tena,nifuate nini? Mazoea?
kwani na yy unadhani anajali kwa wewe kutomfatilia??
 
kwani na yy unadhani anajali kwa wewe kutomfatilia??
Hao watu maarufu mtaji wao ni watu,Edo alikuwa na akaunti facebook alivyoenda Instagram akaomba watu wamfuate huko,na huko instagram kuna muda alikuja shtuka watu wanaomfuata wanapungua na alisema. Kwahiyo ukiangalia kwa mtu mmoja mmoja hawezi jali lakini kwa picha kubwa ufuasi wa watu ndio unampa ulaji watu wakimuacha kwa wingi ni tatizo kwake. Hiyo hoja hapo juu kuwa Watanzania hawajali ni hoja dhaifu,angalia mtu kama Masudi Kipanya ni mioyo ya watu wangapi anaigusa kupitia katuni zake? Hata kama kuna kundi la watu wanaopotezea kazi zake lakini haiwezekani kukakosena watu watakapata mguso chanya.
 
Ubora wa Edo katika kuandika makala umeshuka sana. Hazivutii tena makala zake,kuna kipindi nilikuwa natafuta gazeti la Mwanaspoti kumsoma tu Edo . Kwenye waandishi wa habari niliowa-follow Instagram Kumwembe ni mmoja wapo.Niliacha kumfuata Edo Kumwembe Instagram baada ya kuona ile ni kurasa ya Shabiki wa Arsenal na sio kurasa ya mwanahabari. Nyakati zinaenda kasi sana. Asante Edo kwa makala zako nzuri sana za wakati huo.
Edo yupo hivi hivi miaka yote. Inawezekana wakati unampa vyeo edo ulikuwa hauna acess na exposure ya kutosha ya taarifa za futbol. Ndio mana sasa hivi hata kununua gazeti hununui tena kwa kuwa access ya info imekuwa sana.

Ni sawa na mtoto mdogo anamuona baba ake mrefu lkn akiwa mkubwa anamuona mfupi au wa kawaida.
 
Edo yupo hivi hivi miaka yote. Inawezekana wakati unampa vyeo edo ulikuwa hauna acess na exposure ya kutosha ya taarifa za futbol. Ndio mana sasa hivi hata kununua gazeti hununui tena kwa kuwa access ya info imekuwa sana.

Ni sawa na mtoto mdogo anamuona baba ake mrefu lkn akiwa mkubwa anamuona mfupi au wa kawaida.
,😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Back
Top Bottom