Edo Kumwembe: Simba inaweza kuachana na Bwalya

Edo Kumwembe: Simba inaweza kuachana na Bwalya

Wabongo aisee kwa kubadilika kama vinyonga. Huyu kuna kipindi aliimbwa sana kuwa bonge la fundi hata chama hamfikii. Na jina mkamtungia kuwa mzee wa soft tachi. Leo hii mnamuona kihande
Utoh kwa akili ndogo hamjambo.. kwani kiwango cha mchezaji kinabaki palepale kwa muda wote.. hujui kuna wakati kinapanda au kushuka?
 
Hizi hoja zenu mnapozileta kipindi kama hiki kilivyo muhimu kwa Simba mnamaanisha nini?Mmetumwa?Legeeni kuanzia migongoni kushuka chini!
 
Utoh kwa akili ndogo hamjambo.. kwani kiwango cha mchezaji kinabaki palepale kwa muda wote.. hujui kuna wakati kinapanda au kushuka?
Pitia post za humu utaona ni jinsi gani wanaongea utafikiri kwanzia asajiliwe hakuwahi kufanya lolote na kusifiwa. Aliyeandika post namba 12 ni utoh? Kiwango kushuka na kupanda kwa mchezaji ni swala la kawaida sana. Na huwa kiwango kikishuka mtu anasema fulani kwasasa hstufai kiwango kimeshuka.
Mtu anakwambia hakuwa na hadhi kuchezea simba, mwingine bwalya jina kubwa uwezo mdogo
 
Tatizo sio Bwalya wala sio Boko wala sio Kagere.......tatizo ni form ya Simba kwa sasa

Bado naamini tulifanya haraka kumtoa Da Rosa japo alianza vibaya lakini alikwisha soma kikosi na hawa akina Bwalya walikua soft touch kweli kweli

Lakini sasa mfumo wa huyu mspaniola unawanyima fursa watu kama Bwalya kuonyesha uwezo wao at the best

Ukimuuliza huyo Edo ni mchezaji gani Simba pale mbele anayefanya vizuri? Bado naamini tatizo ni mfumo wa uchezaji Simba bado haujakaa sawa
 
Wachezaji karibia wote wa hiyo timu wanaruka ruka tu uwanjani kama wanacheza kisingeli au amapiano
 
Tatizo Sio Bwalya Tatizo Kocha Anamchezesha Katika Mfumo Gani Ili Bwalya Ampe Nini? Bwalya Ni Aina Ya Mchezaji Ambaye Atakupa Msaada kulingana na Mfumo, Anapiga Shoot Nje ya 18 Zenye Maono, Je Strikers Wetu wapo Tayari kitumia Nafasi? Bwalya Ana Offer vitu vingi Kama Mfumo Utakuwa sawa.

Binafsi sina imani na Mifumo ya Pablo kwa Soka La Afrika, Pablo Ni Kocha Mzuri sanaaaaaa Nje Ya Afrika ila Ndani Ya Afrika Bado
 
EDO: SIMBA WANAWEZA KUACHANA NA BWALYA

Rally Bwalya? Huu ni mtihani.

Kipaji kipo kwa Bwalya lakini hajawahi kuikamata Simba kama inavyotakiwa. Hata walipoondoka Luis Miquissone na Clatous Chotta Chama watu wengi walitazamia Bwalya avae viatu vyao lakini hakuvaa kama inavyotakiwa.

Bwalya anacheza soka laini, hana kasi, hana uamuzi wa haraka lakini pia ameshindwa kufunga mabao mengi au kutoa pasi nyingi za mwisho kama ilivyokuwa inadhaniwa.

Simba inapotawala mechi basi na Bwalya anakuwa miongoni mwa mastaa. Inapokuwa na mechi ngumu basi na Bwalya anapotea. .

Kwa mtazamo wangu Simba ikipata kiungo mwingine mzuri zaidi katika eneo la ushambuliaji basi wanaweza kuachana na Bwalya. Kama atahitaji pesa nyingi kwa ajili ya kusaini mkataba mwingine wa miaka miwili nadhani wanaweza kutulia kwanza na kutazama jicho lao kwingine.

Hauwezi kulaumiwa na mashabiki kwa kuachana na Bwalya.” - Edo Kumwembe.

#KanunguJR

Mie nashauri simba wakusajili wewe badala ya bwalya
 
Hamna kitu pale mdhamiru....
Anacheza holding za kizamani .... Timu ikiwa inafanya buildup ya Attacking anakua ziro kabisa...
Pass accuracy 40%
Maamuzi 45℅
Anakaba vizuri .... Lakini akikamata mali ndo ohooo !!! Unapomkataa

Sent from my FTE171A using JamiiForums mobile app
Kweli kbs jamaa akiwa na mpira ni rahisi kuchoma nyumba
Anaweza akakuoffer kwa kukata umeme lkn hapohapo anahonga pasi
 
Wabongo aisee kwa kubadilika kama vinyonga. Huyu kuna kipindi aliimbwa sana kuwa bonge la fundi hata chama hamfikii. Na jina mkamtungia kuwa mzee wa soft tachi. Leo hii mnamuona kihande
Ndio unafiki wa Mashabiki wa Simba msimu huu
 
Rally bwalya kiukweli kiwango kimeshuka sana hata kagere naye kiwango kimeshuka
 
Wabongo aisee kwa kubadilika kama vinyonga. Huyu kuna kipindi aliimbwa sana kuwa bonge la fundi hata chama hamfikii. Na jina mkamtungia kuwa mzee wa soft tachi. Leo hii mnamuona kihande
Yani unataka akiwa kwenye form asifiwe na akipoteana aendelee kusifiwa. Huoni kama huo ni ukondoo?
 
Yani unataka akiwa kwenye form asifiwe na akipoteana aendelee kusifiwa. Huoni kama huo ni ukondoo?
Hivi ni sahihi kwa shabiki kutoa kauli kama hii kwa mchezaji aliyekuwa kwenye form kisha akashuka kiwango.
1)Bwalya Jina kubwa- uwezo mdogo, toka amekuja Simba hakuna kitu kikubwa amefanya.
2) Bwalya sijawahi kumkububali huyu jamaa.

Hizi kauli zinamaanisha nini kama zaidi ya kuonesha kuwa Bwalya hakuwahi kuwa msaada kwa simba tokea asajiliwe? Ndio kitu nilichokuwa nahoji maana kumbukumbu zangu nakumbuka huyu mtu aliimbwa sana mpaka kuna uzi humu wa kumshindanisha na Chama.
 
Bwalya alivyoanza kwenda sinza tu mambo yakaanza kuharibika
 
Left footer ndio mnamsimanga hiv?
 
Wachezaji karibia wote wa hiyo timu wanaruka ruka tu uwanjani kama wanacheza kisingeli au amapiano
Timu ambayo wachezaji wake wanarukaruka tu uwanjani Hadi sasa wanakiwasha kimataifa. Timu ambayo wachezaji wake wanacheza vizuri waligusa kimataifa wakabinuliwa nyuma mbele na Rivers na sasa wanacheza mechi za kimataifa na somalia na mafunzo
 
Back
Top Bottom