SI KWELI Eduardo Camavinga alipata mtoto wake wa kwanza akiwa na miaka 11

SI KWELI Eduardo Camavinga alipata mtoto wake wa kwanza akiwa na miaka 11

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Kulikuwa na uvumi kuwa kiungo wa Real Madrid, Eduardo Bamavinga ana umri wa miaka 19 na mwanaye ana miaka 8. Hali inayooonesha kuwa alimpata mtoto huyo akiwa na miaka 11.

1657965215707.png

Picha1: Camavinga akiwa na mtoto aliyehisiwa ni mwanaye


1670832546824.png

Picha2: Camavinga akiwa na wazazi wake na ndugu zake
 
Tunachokijua
Mnamo Mei 28, 2022 baada ya mchezo wa fainali wa Ligi ya Mabingwa Ulaya kati ya Liverpool ya Uingereza dhidi ya Real Madrid ya Uhispania, Wachezaji mbalimbali walipata fursa ya kupiga picha za kumbukumbu na familia zao.

Eduardo Camavinga mchezaji wa Real Madrid aliyekuwa na miaka 19 wakati huo alionekana akipiga picha na mtoto wa miaka 7. Baada ya kusambaa kwa picha hiyo fununu na habari zilienea zikidai mvulana huyo alikuwa ni mtoto wa Camavinga. Mijadala mingi ilihoji inawezekanaje Camavinga mwenye miaka 19 awe na mtoto wa miaka 7, Wanajiuliza je Camavinga alimpata mtoto huyo akiwa na miaka 12?

Ukweli upoje?
Baada ya kufuatiliwa imebainika kuwa mvulana huyo aliyepiga picha na Camavinga si mwanaye bali ni mmoja wadogo zake kutoka kwenye familia yake yenye watoto watano (Tazama picha namba 2). Eduardo yupo na kwenye mahusiano na mwanamitindo wa Ufaransa na bado hawajapata mtoto.

Camavinga alizaliwa katika kambi ya wakimbizi huko Cabinda, Angola mwaka wa 2002, na wazazi wa Kongo. Ni mmoja wapo katika familia yenye watoto watano. Familia yake ilihamia Ufaransa alipokuwa na umri wa miaka 2.

Jarida la Kimtandao la Ghpluzz lilifuatilia pia habari hii na kuthibitisha kuwa anayeonekana kwenye picha ni mdogo wake Camavinga na sio mtoto wake.
Hapana yule alikuwa mdogo wake zile ni story tu za vijiweni na walionzisha ni waafrika ni kama ilikuwa utani tu kutoka kwa waafrika mwenzao ni kama wanavyomtania Vincent aboubakar kwamba ana miaka 19 it's serious.
 
Wajuzi nielewesheni. Huyu mwamba Camavinga ambaye ana miaka 20 tayari ana Mtoto wa miaka 12?
Ni kweli na imekaaje hii?
Kwa Mwafrika ni possible kabisa........kuna madingi kibao wapo kwenye public sector walidanganya umri wanaishia kusinzia tu maofisini ndiyo maana maana taasisi nyingi za serikali ziko choka mbaya
 
Inasemekana Mikel Obi ni mtoto wa kocha wa Cameroon national team
 
Kulikuwa na uvumi kuwa kiungo wa Real Madrid, Eduardo Bamavinga ana umri wa miaka 19 na mwanae ana miaka 8. Hali inayooonesha kuwa alimpata mtoto huyo akiwa na miaka 11.

View attachment 2292769
Picha1: Camavinga akiwa na mtoto aliyehisiwa ni mwanaye


View attachment 2443764
Picha2: Camavinga akiwa na wazazi wake na ndugu zake
Waliosoma Cuba ndo wanaelewa hii imekaaje kitalam
 
Back
Top Bottom