Dream Queen
JF-Expert Member
- Nov 4, 2015
- 8,263
- 18,201
Mtangazaji wa Clouds FM, Paul James aka PJ ameshtakiwa mahakamani na kituo cha redio cha EFM kwa kuvunja mkataba kinyemela
Mtangazaji huyo aliondoka EFM mwanzoni mwa mwezi huu na kurejea kwenye kituo chake cha zamani, Clouds FM, alichoondoka pamoja na mwenzake Gerald Hando. EFM imefungua mashtaka katika mahakama ya kazi jijini Dar es Salaam kwa madai ya kukiuka mkataba wa kazi wa kituo hicho.
Kufuatia mashtaka hayo, EFM inadai fidia ya shilingi milioni 200 kutoka kwa mtangazaji huyo.
Inadai PJ alikatisha mkataba kiholela na kurudi tena Clouds FM bila kufuata makubaliano pamoja na sheria alizokubaliana nazo katika mkataba wake pale alipojiunga nacho.
Kesi hiyo imepangwa kusikilizwa November 23, 2016 katika mahakama ya kazi jijini Dar es Salaam.
Chanzo: Bongo5
wanachukulia ushikaji kwenye kila kitu hawa watangazaji wa hapa DAR...!!Sijui nini kinawapata watangazaji wetu? hivi kweli Pj alikuwa hafahamu kuwa kuvunja mkataba kuna taratibu zake kweli? nimesikitika sana kama kweli mtangazaji ana kurupuka tuu bila kuangalia au kusoma vipengele vya mikataba yake na mwajiri wake.
Pengine aliona kuna kipengele kinacho mruhusu kuvunja mkataba nakufanya hivyo...pengine.
Ni kweli Clouds hawakujua hilo?
Hata hivyo madai yamepelekwa kwa baraza la usuluhishi na si mahakamani.
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]kawa kama Paul Pogba, aliondoka bure baada ya mkataba kuisha, leo Clouds wanatakiwa kuvunja rekodi ya usajili
Afu nyie wanasheria wa sikuhizi mkoje??kwanini amtunzi siri za clients kwenu.!?
Sijui PJ hafahamu taratibu za kuvunja mkataba au ni jeuri ya mwajiri mpya ya kwamba anaweza kufanya atavyo kwa kuwa yuko juu ya sheria, au walifikiri E FM wataiogopa Clouds kwa wako karibu na mamlaka kuu. Ni kitu cha ajabu na wala hakiingii akilini mbona mwenzake Mzee wa Jahazi alizingatia taratibu zote za kuacha kazi na kuhamia CloudsSijui nini kinawapata watangazaji wetu? hivi kweli Pj alikuwa hafahamu kuwa kuvunja mkataba kuna taratibu zake kweli? nimesikitika sana kama kweli mtangazaji ana kurupuka tuu bila kuangalia au kusoma vipengele vya mikataba yake na mwajiri wake.
Pengine aliona kuna kipengele kinacho mruhusu kuvunja mkataba nakufanya hivyo...pengine.
Ni kweli Clouds hawakujua hilo?
Hata hivyo madai yamepelekwa kwa baraza la usuluhishi na si mahakamani.