Election Expenses Bill 2009

Election Expenses Bill 2009


Hapa rais anazungumzia mbunge mtarajiwa kumuahid kasheshe cheo, etc. kosa wapi wandugu... mbona mnaturudisha nyumba?

tatizo lako ni kuwa unafikiri siasa ni kushawishi wengi; siasa ni kushawishi mmoja mmoja. Kura inayopiganiwa siyo kura ya wengi ni kura ya mtu mmoja. Na hivyo mgombea yoyote anafanya kazi kubwa ya kupigania kura moja. Na hivyo, hawezi (kwa mujibu wa sheria hii) kutoa ahadi kwa mpiga kura mmoja ambayo itamfanya mpiga kura huyo amchague..
 
Rais akafafanua hivi vile vile:

Ndugu Wananchi,
Kwa upande wa michango ya hiyari na zawadi zinazotolewa kwa Chama na wagombea, Sheria inataka pawepo na uwazi katika utoaji wake. Sheria inaelekeza kwamba, kila chama cha siasa kilichopokea mchango unaozidi shilingi milioni moja kutoka kwa kila mchangiaji binafsi au shilingi milioni mbili kutoka kwa taasisi, kitoe taarifa kwa Msajili.

Je hii ina maana gani? na itakuwa na matokeo gani?
 
Ndugu Wananchi;
Sheria imeainisha vizuri mambo yanavyokatazwa kwa upande wa matumizi ya fedha za uchaguzi. Sheria inakataza, kwa mfano, vitendo vifuatavyo visifanyike pamoja na matumizi ya fedha kwa ajili hiyo kuzuiliwa:
1. Kufanya malipo kwa wapiga kura ili wamchague mgombea fulani;
sawa nakubali kwa 100%

2. Kuahidi kazi au cheo au wadhifa kwa mpiga kura ili amchague mgombea;

Sikubali kabisa. Nitakubali kama zaidi ya cheo na wadhifa akiweka neno kuhahidi miradi kama ya barabara , umeme kwa wapiga kura

3. Kutoa zawadi, ahadi, mkopo, au makubaliano yoyote kwa mpiga kura ili amchague mgombea;

Nakubali kwa 70% lakini ufafanuzi wa neno MAKUBALIANO unahitajika


4. Kukubali kurubuniwa kwa mambo yoyote yaliyotajwa hapo juu ili ampigie kura mgombea yeyote;

Neno KURUBUNIWA linahitaji ufafanuzi. je mwanafunzi wa miaka 18 na mtu wa miaka 45 wanawekwa kwenye fungu moja

5. Kufanya vitendo vyovyote kati ya hivyo wakati wowote kabla au hata baada ya uteuzi wa mgombea;

Hapa sijaelewa na sikubali
Mhh hapa kuna utata mfano waziri anaweza kwenda jimboni kwake akatoa ahadi kwa mgongo wa serikali na hata kabla kampeni hazijaruhusiwa. Hii inawabana zaidi wapinzani. wafafanue.KABLA NA BAADA ya uteuzi wana maana gani
.

6. Kutoa malipo kwa ajili ya takrima ya chakula, vinywaji au starehe yoyote kwa ajili ya kuwashawishi wapiga kura wamchague mgombea;


Sawa Nakubali kwa 80 %

7. Kuwasafirisha wapiga kura ili wamchague mgombea. Hata hivyo Sheria inaruhusu wapiga kura wenyewe kujilipia nauli kwenda kupiga kura au Serikali kuwasafirisha wapiga kura pale ambapo kuna shida ya usafiri;
-- Sijaelewa nakataa hii inahitaji ufafanuzi sabbu serikali ni ya chama fulani labda angesema Tume ya uchaguzi lakini mhhh

Nadahni mambo mengi yanaongeza utatata unless Muheshimiwa angefafanua zaidi labda tungepata mwanga.
 
Mzee Mwanakijiji,

1.Sijaisoma sheria hiyo ila naona kuna haja ya kuipitia,itakuwa imeandikwa kimakosa sana coz si rahisi wananchi kumchagua mgombea wa chama flani bila ya kujua atafanya nini akichaguliwa kuwa Mwakilishi(mbunge).

2.Duniani kote sifa za mtu hazitoshi kuwa kiongozi mpaka aoneshe mpango mkakati wake katika kuwasaidia wananchi na kuleta maendeleo chanya.Tunafahamu wananchi wamekuwa wakipata matatizo mengi na lengo la kuchagua ni kupata viongozi bora ambao watatelekeleza shughuli za maendeleo.

3.Kama hawataki wananchi wapewe ahadi basi hakuna haja ya kuwa na uchaguzi,tunachagua nini sasa?sura?au chama? na hii inaonesha au imeamuliwa na Chama kuwa mambo mengi ambayo wamekuwa wakiyahidi hayatekelezeki hivyo wameamua kuwaamisha wananchi kuwa wanweza kutawala kwa kuwa wana uzoefu.

4.Kwanza kwanini hii sheria haikushilikisha wadau wake?au kama walishirikishwa(viongozi wa vyama vingine) walikubaliana vipi na mambo haya?hili si suala la mambo ya serikali bali ya kisiasa zaidi na ingekuwa vyema wadau wangeshiriki kikamilifu(hapa wakiwamo wananchi wenyewe).
Gembe
Mkuu emesema kweli, hawa jamaa hawajaweza kutimiza ahadi walizotoa 2005 kwa hiyo hawana cha kuahidi kipindi hiki ndio maana wanataka kukataza wenzao wasiahidi. Wanataka mje tu na bla bla za umoja na amani, chama kikongwe n.k n.k
 
Labda nitumie mfano hai:

Kule Kyela, wakati wa kura za maoni ni formula gani itatumika kugawa fedha kwa Mwakalinga, Mwakyembe, Mwakipesile, na Mwanjala? kwa sababu hawaruhusiwi kukusanya fedha zao wenyewe na matumizi ya fedha kwa kila jimbo yataamuliwa na Waziri?

a. Je wote watapewa kiasi sawa?
b. Kwa vile kampeni zote zitaendeshwa na chama, je kutakuwa na msisimko wa uchaguzi tena?
c. Kama mgombea ana fedha yake ya ziada na anajua kuwa kiasi alichotengewa na chama chake hakitoshi kufikisha ujumbe kwanini azuiwe kutumia fedha zake au kutafuta fedha zaidi?
 
Rais akafafanua hivi vile vile:



Je hii ina maana gani? na itakuwa na matokeo gani?

kuna Mfanyabiashara anaitwa kishimba wa Mwanza alimfhadili mzee mapesa( John cheyo) kwenye urais na kampeni za ubunge kanda ya ziwa.

Kilichofuata baada ya uchaguzi kuisha TRA walipiga mehasabu ya kodi zake miaka minne nyuma akaonekana anadaiwa na alikuwa anakwepa kodi.(kama ni kweli au uongo hilo ni suala lingine) alitakiwa alipe hela kibao na ndipo alianza kutetereka kidogo.

Watu wengi wenye nia njema wataogopa. Na ukizingatia kuwa sucessful kibiashara sio uwongo lazima kuna kodi kodi uzikwepe au kuzifanyia usanii. kazi ipo
 
Kwa vile michango yote sasa itakuwa inaenda kwa vyama vya siasa.. unafikiri ni chama gani kiko katika mazingira mazuri ya kuchangiwa zaidi?
 
Kwa vile michango yote sasa itakuwa inaenda kwa vyama vya siasa.. unafikiri ni chama gani kiko katika mazingira mazuri ya kuchangiwa zaidi?

Ni wazi ni CCM kitafaidika zaidi

kuwa na uwanja sawa na wa haki wa ushindani sheria inabidi itambue vyama hivi vyote havijazaliwa 1990. kuna mabadiiko mengi inabidi yaangaliwe

Kuna chama kilifaidika na kupata michango ya kukatwa kodi watanzania wote . kinahodhi rasilimali na mali nyingi za watanzaia na hata baada ya mfumo wa vyama vingi bado mali na rasilimali hizi ni za chama.

Kwa upande 1ja sheria inaweza kufanikisha kupunguza matumizi ya hela chafu ndani ya CCM lakini upande mwingine inapunguza na kudumaza demokrasioa ya kweli hasa kwa vyama vya upinzani amabavyo ni vichanga.
 
Ni wazi ni CCM kitafaidika zaidi

kuwa na uwanja sawa na wa haki wa ushindani sheria inabidi itambue vyama hivi vyote havijazaliwa 1990. kuna mabadiiko mengi inabidi yaangaliwe

Kuna chama kilifaidika na kupata michango ya kukatwa kodi watanzania wote . kinahodhi rasilimali na mali nyingi za watanzaia na hata baada ya mfumo wa vyama vingi bado mali na rasilimali hizi ni za chama.

Kwa upande 1ja sheria inaweza kufanikisha kupunguza matumizi ya hela chafu ndani ya CCM lakini upande mwingine inapunguza na kudumaza demokrasioa ya kweli hasa kwa vyama vya upinzani amabavyo ni vichanga.

Mind you, sheria ina kiwango cha juu cha matumizi ya uchaguzi kwenye jimbo... so it doesn't matter chama chako ni tajiri kiasi gani, hautaruhusiwa kutumia zaidi ya hapo.
 
Mind you, sheria ina kiwango cha juu cha matumizi ya uchaguzi kwenye jimbo... so it doesn't matter chama chako ni tajiri kiasi gani, hautaruhusiwa kutumia zaidi ya hapo.

Mhh this is interesting...I am curious serikali na washauri wake walitumia vigezo gani kuweka hicho kiwango cha juu.
 
Mind you, sheria ina kiwango cha juu cha matumizi ya uchaguzi kwenye jimbo... so it doesn't matter chama chako ni tajiri kiasi gani, hautaruhusiwa kutumia zaidi ya hapo.

Ok aksante kwa ufafanuzi lakini bado naona bila kufafanuliwa zaidi muswada huu una utata mwingi mfano

Chama cha mapinduzi kina magari au kina gari kila wilaya wakati vyama vingine havisa usafiri. Ukisema kila jimbo maximum ni shilingi 1000 hawa wengine watatumia shilingi 500 kwa usafiri na 500 kwa kazi nyingine wakati CCM tayari wana rasilimali wao watatumi 1000 zote kwenye kazi halisi za kampeni . je Kutambua kiasi gani chama kimetumia zimetumika wataingiza kwenye mahesabu mpaka asset za chama zilizotumika. kama bend za TOT na magari ?
 
Ni wazi ni CCM kitafaidika zaidi

kuwa na uwanja sawa na wa haki wa ushindani sheria inabidi itambue vyama hivi vyote havijazaliwa 1990. kuna mabadiiko mengi inabidi yaangaliwe

Kuna chama kilifaidika na kupata michango ya kukatwa kodi watanzania wote . kinahodhi rasilimali na mali nyingi za watanzaia na hata baada ya mfumo wa vyama vingi bado mali na rasilimali hizi ni za chama.

Kwa upande 1ja sheria inaweza kufanikisha kupunguza matumizi ya hela chafu ndani ya CCM lakini upande mwingine inapunguza na kudumaza demokrasioa ya kweli hasa kwa vyama vya upinzani amabavyo ni vichanga.

Heshima yako mkuu,

Hapo kwenye red, hiyo balance kuipata ni ngumu sana. Kwa kuongezea sioni kabisa uwezekano wa CCM kuwepo madarakani halafu watunge sheria ambayo kwa kiwango kikubwa inanufaisha vyama vya upinzani.

Ni realiaty ambayo ni muhimu tuikubali kuwa chama kikiwa kimeshika dola, kinakuwa na added advantage.
 
Ok aksante kwa ufafanuzi lakini bado naona bila kufafanuliwa zaidi muswada huu una utata mwingi mfano

Chama cha mapinduzi kina magari au kina gari kila wilaya wakati vyama vingine havisa usafiri. Ukisema kila jimbo maximum ni shilingi 1000 hawa wengine watatumia shilingi 500 kwa usafiri na 500 kwa kazi nyingine wakati CCM tayari wana rasilimali wao watatumi 1000 zote kwenye kazi halisi za kampeni . je Kutambua kiasi gani chama kimetumia zimetumika wataingiza kwenye mahesabu mpaka asset za chama zilizotumika. kama bend za TOT na magari ?


Kunaweza kuwepo na "loop hole" kwenye sheria, badala ya kutoa fedha kwenye chama Wanachama wanaweza kuchangia nyenzo kama magari, kujitolea kuimba au kufanya kazi bila kulipwa..??
 
Mzee Mwanakijiji is this the so called great thinking... then tumechosha na spinning zako... Ili uelewe jambo lazima uangalie contest gani mtu huyo anaongelea.. ndio maana ukisoma vitabu vitakatifu ukitoka na mstari mmoja bila kusoma mistari ya kutosha unaweza toka na maana ambayo haijakusudia.

Would you please stop your bad intent of trying to justify everything president talk is wrong please.... wewe mkubwa sasa mkuu.

MMKJ hajakosea kitu yeye kaleta summary ya bill tuijadili hakuna ubaya wowote hata bungeni misuada hujadiliwa kabla ya kupitishwa wewe ndiye uliye na spinning umechoshwa na hoja zake kwa hiyo kila anacholeta MMKJ lazima litakukera hata hivyo hata yeye kauliza hakuja na conclusion yake
 
Tatizo halipo kwnye sheria,lipo kwenu mnaoisoma kama vile kipeperushi cha udaku! kama mtakuwa mnachukua kipande cha neno na kujengea hoja, hata vitabu vyenu vya dini mtavikosoa tafsiri sahihi. jifunzeni kusoma kabla ya kusoma. wengi wenu mnaanza kusoma sheria kabla ya kujifunza ndo matokeo yake mnajiaibisha. sheria hutungwa kwa kufuata Liberal meaning sasa nyie mkizoea kuifasiri kwa literal meaning mtaona kila sheria imekosewa kumbe wewe ndo unakosea kukosoa.Tumkosoe JK kwa lingine sio hili.
 
Tatizo halipo kwnye sheria,lipo kwenu mnaoisoma kama vile kipeperushi cha udaku! kama mtakuwa mnachukua kipande cha neno na kujengea hoja, hata vitabu vyenu vya dini mtavikosoa tafsiri sahihi. jifunzeni kusoma kabla ya kusoma. wengi wenu mnaanza kusoma sheria kabla ya kujifunza ndo matokeo yake mnajiaibisha. sheria hutungwa kwa kufuata Liberal meaning sasa nyie mkizoea kuifasiri kwa literal meaning mtaona kila sheria imekosewa kumbe wewe ndo unakosea kukosoa.Tumkosoe JK kwa lingine sio hili.


hili ndilo tatizo kwa swababu unafikiri wote tunashindwa kuelewa sheria na jinsi inavyotungwa. Tunapozungumzia Law of Unintended Consequences tunataka kuona kila ambacho sheria itafanya bila kukusudia. Sasa wewe ukitunga sheria bila kufikiria matokeo yake yasiyotarajiwa ndiyo unashindwa kuelewa kwanini wawekezaji wa Tanzania katika madini wanatangaza hasara miaka nenda miaka rudi; baadaye mnafikiria kubadilisha sheria ya madini ya 1998 kwa sababu hakumfiria matokeo yake yasiyotarajiwa. Ndiyo hilo la kweli kwenye Sheria ya Fedha na mambo ya Capital gain ya 2001 na ni kweli pia kwenye sheria ya Maadili ya Umma ya 1998 na ni kweli pia kwenye Sheria ya Usalama wa Taifa ya 1996.

Sheria zote hizo mmezitunga vizuri tu na with "liberal meaning" matokeo yake mmetengeneza loopholes za kutishia demokrasia na uhuru wetu kwa sababu mnafikiri watu wote hamnazo!

Ukiisoma hiyo sheria with your liberal mind. Je mtu akichangia shilingi laki 999,999 kwa chama anatakiwa kutangaza?
 
Mind you, sheria ina kiwango cha juu cha matumizi ya uchaguzi kwenye jimbo... so it doesn't matter chama chako ni tajiri kiasi gani, hautaruhusiwa kutumia zaidi ya hapo.

you can't do that!! we are in a democracy not a tyranny of the party! mimi kama nina fedha zangu za kutosha kujitangaza katika kugombea ambazo nimezipata kihalali na natangaza kuzitumia kihalali kwanini serikali iniwekee kikomo kwa sababu mtu mwingine hana kama mimi? Huu ni udikteta wa chama and you don't see any problem with that.
 
you can't do that!! we are in a democracy not a tyranny of the party! mimi kama nina fedha zangu za kutosha kujitangaza katika kugombea ambazo nimezipata kihalali na natangaza kuzitumia kihalali kwanini serikali iniwekee kikomo kwa sababu mtu mwingine hana kama mimi? Huu ni udikteta wa chama and you don't see any problem with that.

aaaaahaaaaa kumbe hujaisoma sheria/muswada....Mimi nadhani tungesoma kwanza kabla ya kupoteza muda hapa, mheshimiwa rais amegusia kwenye 3. hapa chini.
Katika kufikiria na kutayarisha rasimu ya muswada wa sheria hii, mambo saba ya msingi yalizingatiwa. Mambo hayo ni haya yafuatayo:
1. Kuutambua kisheria mchakato wa uteuzi wa wagombea ndani ya vyama vya siasa na kuusimamia kisheria.

2. Kuweka utaratibu wa kisheria utakaosimamia na kuratibu mapato na kudhibiti matumizi pamoja na gharama za uchaguzi kwa vyama vya siasa na wagombea.

3. Kuweka viwango kwa matumizi na gharama za uchaguzi.

4. Kuweka utaratibu utakaosimamia mapato na matumizi ya vyama vya siasa ikiwa ni pamoja na zawadi, misaada na michango itakayotolewa na wagombea au wahisani wakati wa kampeni za uchaguzi.

5. Kudhibiti michango na zawadi kutoka nje ya nchi.

6. Kuweka utaratibu na mfumo wa udhibiti na uwajibikaji kwa mapato na matumizi ya fedha za uchaguzi kwa upande wa vyama vya siasa na wagombea.

7. Kuainisha adhabu kwa watakaokiuka masharti yatakayowekwa na Sheria hii.

Mheshimwa Rais anaendelea

Viwango vya Gharama za Uchaguzi

Ndugu Wananchi,
Sheria ya Gharama za Uchaguzi inaweka utaratibu wa kudhibiti gharama za uchaguzi kwa kumpa mamlaka Waziri mwenye dhamana ya uchaguzi kuweka viwango vya gharama za uchaguzi. Waziri huyo atatangaza kiwango cha juu ambacho kila mgombea ataweza kutumia katika kampeni na katika uchaguzi. Kiwango hicho cha gharama kitazingatia tofauti ya majimbo, idadi ya watu, aina ya wagombea pamoja na miundombinu. Chama au mgombea atakayevuka viwango vya mtumizi alivyowekewa bila maelezo ya kuridhisha, atakuwa ametenda kosa na anastahili kuwajibishwa ipasavyo.
Utaratibu huu ni muhimu katika kujenga nidhamu na usawa miongoni mwa vyama na wagombea katika uchaguzi. Hivi sasa kwa sababu ya kutokuwepo ukomo, wako watu wenye pesa ambao wanafanya matumizi kupita kiasi. Wapo wanaopitiliza au hata kukufuru na kuwadhalilisha wenzi wao wasiokuwa na uwezo kama wao.

Najua utasema makosa ya JK... lakini haya yako kwenye sheria sasa sijui alishika akili za wabunge na kalamu zao... I don't know
 
aaaaahaaaaa kumbe hujaisoma sheria/muswada.... kwa taarifa yako kuna kifungu kinasema aidha waziri mwenye dhamana au mlezi wa chama au tume ya uchaguzi itaweka kiwango cha juu kwenye majimbo kulingana na miundo mbinu, ukubwa wa jimbo etc.
Mimi nadhani tungesoma kwanza kabla ya kupoteza muda hapa!

nimeisoma.. ndio maana nimeuliza... siulizi kutoka hewani! Yaani, mtu mmoja tunampa madaraka ya kuamua nini kinafanyika kwenyejimbo? Hivi huoni kuwa unintended consequences zitasababisha baadhi ya majimbo kutengewa fedha zaidi na hilo la "etc" ndio linandokeza discretion kubwa ambayo tunataka kumpa mtu mmoja. Sheria haiweki kanuni hasa ya kugawa hizo fedha kwa wagombea au kwa jimbo. Kuna majimbo yatapata zaidi (maana yake wagombea wake watakuwa na uhuru mkubwa wa kujitangaza, na majimbo mengine yatakuwa na fedha kidogo na matokeo yake yanaweza kutabiriwa)?

Huoni kwamba katika misingi hiyo the incumbent atakuwa na unfair advantage?

Unapokubali kuwa serikali iweke mipaka ya kiasi kinachoweza kutumika kwenye jimbo, je uko tayari kuona serikali ikiweka mipaka idadi ya magari, vipeperushi, matangazo ya radio, tV n.k ambayo chama kinaweza kuyafanya kwenye jimbo ili kuleta uwiano? Je huoni kuwa inatishia uhuru wa kujieleza?
 
Wapendwa,

Tunahitaji kuwa makini zaidi tukisoma mabadiko au sheria... haiwezekani unataka ubunge unaenda kumuahidi mtu mmoja... sheria imesema mpiga kura... "singular" kiswahili "mamoja".

Usually ahadi za mbunge ni kwa huduma zinazokumba jamii nzima sio mpiga kura mmoja. hivyo ingesema ahadi kwa wapiga kura that is different.

You are right Kasheshe, make sheria ikisema mpiga kura inamaanisha mtu mmoja, na hiyo yaweza kuwa illegal, make hapo mgombea atakuwa anafanya signs za rushwa, ilitakiwa sheria itoe ujumla wa wapiga kura na sio mpiga kura, any way bwana, The Mwana Village yupo sawa, make hata ilani ya CCM tayari ikitafsiriwa inaashiria rushwa, make unawaaidi wananchi vitu ambavo havipo katika mazingira ya kawaida------ahadi lukuki, we angalia 2005 ahadi zilikuwa ngapi kutokana na ilani yao, sasa Mr President anasema sheria imekataza wagombea kutoa ahadi, ilani je, si ahadi hizo jamani, bsi waondoe hata ilani za vyama, wagombea waje na policy na strategies zilizokaa kiinchi zaidi badala ya vyama, halafu huu mfumo wa mgombea uraisi kutumia 100% ilani ya chama it is wrong, huu sio wakati wake, wakati wa chama kimoja ilikuwa ok, sasa utakujaje na ilani ya chama wakati nchi sio ya chama kimoja, so what happen hata raisi akichaguliwa kwa kishindo 80% what about 20% ambao hawakumchagua,

mimi naona 2010 wagombea uraisi waje na agenda zao at least 65% and 35% za chama, ili tujue hawa watu wana uwezo gani kufafanua policies and what kind of strategies have put on focus when elected, sio tu mtu anakuja na kuanza kuimba jukwaani kuhusu CCM, tell people the policies you have put forward, in your tenure as a president how the country is gonna move forward----badala ya ngonjera za akina Komba---ccm,ccm---what is that?????
 
Back
Top Bottom