Electrical Engineer Graduate natafuta kazi

Andika barua kwa MOE,Bakhresa grouop, kampuni za bia, soda. SGR , bwawa la Nyerere,Tanesco nk.
Mkuu inabidi uwe kama mbwa koko uzunguke kweli kweli usifanye masikhara. Hata kama hutalipwa kubali tu kupata hio uzoefu hata kwa gharama zako za chakula na nauli don't be disapointed by any nonsense human.
Mwisho anza mikakati ya kuanzisha kampuni.
Rafiki zako wote uliosoma nao kuanzia primary mpaka chuo ni waajiri wako, tangaza ujuzi/huduma yako kwao, tengeneza bussiness card nzuri,vipeperushi.
Jitolee hata kutoa huduma kwa baadhi ya watu wa karibu.
 
Mkuu nimeishatuma CV kwenye hizo Company na bado naendelea kutuma ila sijibiwi. Na wengine ambao wana connection naona wanapata hata bila kutuma CV, ndipo nikagundua wengi hawaangalii ujuzi ila nani kakupeleka. Ndio maana nikalileta hili swala hapa Jamiiforums ambapo najua kuna watu wanaweza kunisaidia.
 
Hapo nimekuelewa kwa hapa ulipo kilio kikuu ni Nini?
 
Let me tell you.Ulikuwa unasoma tu proffesinal ila hukuwa unasoma kanuni za maisha kwa ujumla !

Kuna Kanuni inaitwa the 'principle of persistance' ipo katika kitabu cha Napolean hill na kiwasoki.
Kwa tafsiri yangu inaitwa 'Kanunu ya ukupe' , mkuu inabidi uwe kupe au kunguru. Yaani usimame kwenye jambo hilo mpaka kieleweke.
Kwa hio tuma tena barua huko, wasipo kujibu rudia tena na tena. Nenda physically kila unapoona hujibiwi.
(do persist on their door and knock knock knock)
Hii kanuni watu wengi hawaitumii ila huleta matumda.
Mkuu jisiomamie hakuna wa kukusimamia.
Nimekushauri utengeneze bussiness card wape rafiki zako hata kwa nijia ya wasap Jf, tweeter nk.
Markert your self and then brand youself. Mainjinia mpo wengi, bado kuna mainjinia wa mtaa wanajua A to Z ulivyovisoma wewe miaka 4. Unafikiri ni rahisi kupenya.
Hata hapa JF watu wanahitaji huduma kama tako, kwa nini hujaja kibiashara umekuja kwa unyonge wakati wewe ni graduate,
Do you have confidence ?
Simama IMARA, simama kama ENGINEER!
 
Asante mkuu kwa ushauri, kama nilivyosema hapo awali bado naendelea kutuma maombi, KUKATA TAMAA KWANGU NI MWIKO. Nisingelileta hapa JF nisingepata hata huu ushauri wako.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…