Tetesi: Elie Mpanzu amekamilisha usajili wa kujiunga na Simba SC, mkataba wa miaka mitatu

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Simba ilipambana sana kuisaka saini ya winga machachari aliyeitumikia AS Vita kwa mafanikio, Elie Mpanzu lakini jitihada hazikuzaa matunda baada ya mchezaji huyo wa DR Congo kutimkia Ubelgiji kwa ajili ya majaribio lakini hakufanikiwa na kurudi kwao Congo.

Taarifa mpya ni kwamba Mpanzu amekamilisha usajili wa kujiunga na Wekundu wa Msimbazi, Simba Sports Club, kwa mkataba wa miaka mitatu na atakuwepo Benjamin Mkapa Jumapili hii kutazama mchezo wa marudiano kati ya Simba Sports Club dhidi ya Al Ahli Tripoli.

Soma zaidi:
=> Nawashauri Simba SC wamrudie tena Elia Mpanzu amerudi kwao Congo, waachane na mchezaji wao wa ovyo
=> Mpanzu alilia Simba baada ya kufeli KRC Genk, hataki tena ucheza AS Vita
 
Bado tetesi until official site ikituma
 
Kwani dirisha la Usajili bado halijafungwa?

Could be best signing Simba SC had done.

Ikiwa kweli, tutaanza kuona ile Simba ya enzi ya Kagere wa moto, yaani ukikaa nchale ukichimama nchale 😅
Inasemekana si rasmi. Ni tetesi ambazo usahihi wake utakamilika kupitia taarifa rasmi na kucheza ni mpaka dirisha dogo la usajili litakapofunguliwa.

Ila recently pamekuwa na tetesi za usajili zenye uzito ilihali dirisha lilishafungwa. Mara Fei kurudi, sasa Mpanzu. Isije ikawa ni kutuliza wenye kimuhemuhe na tar 23.
 
Yeah, na hata kama amesajiliwa basi kutangazwa itabidi wasubiri mpaka Januari wakati dirisha dogo litakapofunguliwa
 
Kwani dirisha la Usajili bado halijafungwa?

Could be best signing Simba SC had done.

Ikiwa kweli, tutaanza kuona ile Simba ya enzi ya Kagere wa moto, yaani ukikaa nchale ukichimama nchale 😅
Dirisha kubwa lilifungwa, nadhani wanasubiri dogo litakapofunguliwa mwezi Januari huko
 
Elia ni striker mzuri sana, ingekuwa ni furaha sana Mtaa wa Msimbazi maana jamaa anajua boli
 
Dirisha kubwa lilifungwa, nadhani wanasubiri dogo litakapofunguliwa mwezi Januari huko
Ikawe kweli, maana hawa jamaa wa Mtaa wa Jangwani wametuonea sana

Ifike wakati tuseme enough is enough 💪
 
Ikawe kweli, maana hawa jamaa wa Mtaa wa Jangwani wametuonea sana

Ifike wakati tuseme enough is enough 💪
Yanga Walisha taarifiwa mapema Sana na uongozi wa mchezaji wakati Mchezaji na KRC Genk walipo shindwana ila kwasasa Yanga hawatumii Tena mfumo wa mawinga. mfumo wa Gamond
Mabeki wa Yanga ndio Mawinga, waka washauri wawasiliane na Simba wanaweza Fanya biashara.
 
Shukrani Kwa taarifa Mkuu

Hizi angekuwa Mjukuu wangu Nifah angesema ni exclusively info kutoka vyanzo vya ndani kabisa 🤗
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…