Baba Jenifa
Member
- May 14, 2023
- 5
- 14
Naandika nikiwa nimeketi nyuma kabisa ya darasa lenye zaidi ya wanafunzi mia moja, wote tukingoja shahada miezi kadhaa ijayo. Mbele kidogo yupo fundi wa mpira na medali zake, na mbele kabisa mwandishi wa mashairi na riwaya katupia miwani yake na tuzo za hapa na pale, na kuna mdada mmoja fundi wa kusuka aliyefungua saluni yake na mwingine mwanamitindo kiasi, kashiriki mashindano kadhaa
Tunafanana
Wote tunaingoja Novemba tuvae joho tule kiapo, turushe kofia juu na baadaye tusajiliwe na baraza tuungane na wengine mtaani wenye elimu na maarifa kama yetu. Nakumbuka mara ya mwisho kupigwa fimbo na mzee wangu alisema “nawatandika kwa sababu mnafanana tabia” nani atamkemea mwenzake au kumshauri ikiwa wote mnafanya makosa yale yale??. Basi hakuangaika na fimbo alitumia mkanda wote tukachezea. Nimekua nikatambua kufanana sana si heri bali heri ni kujua kuwa elimu inatufananisha na ujuzi, ubunifu na vipaji hututofautisha.
Mali ya umma na mali binafsi
Hapa darasani kila mtu ameweza kusoma,kuelimika na kupata maarifa mengi, kila mtu katika mia na zaidi, lakini si kila mtu anaweza kucheza mpira na kungára au kuandika na kupokelewa na wasomaji, au kubuni mitindo ya vitu, au kusuka, au kuimba, au kucheza na tukanyanyuka tumuone, au kuigiza, labda na kughani, au kushawishi na tumsikilize yeye tu, vitu vya kipekee sana hivi.
Elimu imetufananisha ni kama huduma ya umma, ujuzi na vipaji vinatutofautisha maana ni mali binafsi
Ni gharama nafuu kupata huduma kutoka katika taasisi za umma na wengi tunaweza kumudu. Kwa upande mwingine ni ghali kupata huduma kutoka katika taasisi binafsi kama hospitali, shule n.k. kwa kifupi mali binafsi ni chache na ni ghali. Uchache na utofauti huongeza thamani pia.
Katika soko la sasa shughuli binafsi zinalipa pengine zaidi ya mshahara. Kuna fursa katika uchache na upekee. Ipo fursa , ipo.
TUFANYE NINI?
Tukitazama kwa karibu tunaweza kujua upekee wa watoto wetu. Kuna mzee mmoja alimuambia mkewe “usimchape mwanao akichelewa kutoka mpirani, siku moja mfuatilie uangalie anavyocheza, pengine ni mwanasoka wa baadaye”. Pengine ni mchoraji wa aina yake, au mwanamuziki kwa sauti yake au mwandishi mchanga. Sote tunaona watoto wakiimba katika runinga, wakiandika, wakichora, wakiigiza, si muujiza bali ni jicho la mzazi. Tunaweza kupalilia talanta za watoto wetu na kuwafundisha fani mbalimbali nje ya elimu yao ya shuleni kwani uchache na utofauti huongeza thamani
Kwa maana rahisi pengine kuliko zote, mazingira ni mambo yote yanayomzunguka mtu. Kama mtu huyo ni mtoto basi mazingira ni mambo yote yanayomzunguka mtoto. Na mtu hujengwa na vitu viwili, moja ni yeye mwenyewe na pili ni mazingira yake, mazingira ya mtoto ni pamoja na mzazi, mwalimu, sanaa, ufundi, ubunifu na vinginevyo. Ni rahisi kumkunja angali mbichi, ni rahisi kumfunza
Mazingira yanayotuzunguka yanatulazimu kuchangamka, kuanza na kunyumbulika. Kuchangamka nikuongeza kasi ya kuona fursa , na fursa iliyopo ni kuwa wengi tumesoma, tuna maarifa lakini ubunifu ni hafifu sawa ulivyo ujuzi wa kufanya vitu bora, tena kwa viwango vya juu. Kuanza ni kuacha ahadi, kufungua mikono na kufanya. Kunyumbulika ni kubadilika, kuona uhitaji na kukidhi uhitaji huo.
Bwana Yule!, bibi Yule!, asee Yule jamaa noma sana, pale ofisini kwake!, alianza taratibu, akaboresha, sasa imekua tabia yake kutoa vitu bora, bora nitumie gharama kubwa kwa huduma yake. Hivi ndivyo viwango mabibi na mabwana.
JE NINAWEZA KUFANYA NINI KWA KIWANGO CHA JUU BILA KUAJIRIWA?
Namaliza
kwa kujiuliza...
Asanteni sana
Baba Jenny..
Tunafanana
Wote tunaingoja Novemba tuvae joho tule kiapo, turushe kofia juu na baadaye tusajiliwe na baraza tuungane na wengine mtaani wenye elimu na maarifa kama yetu. Nakumbuka mara ya mwisho kupigwa fimbo na mzee wangu alisema “nawatandika kwa sababu mnafanana tabia” nani atamkemea mwenzake au kumshauri ikiwa wote mnafanya makosa yale yale??. Basi hakuangaika na fimbo alitumia mkanda wote tukachezea. Nimekua nikatambua kufanana sana si heri bali heri ni kujua kuwa elimu inatufananisha na ujuzi, ubunifu na vipaji hututofautisha.
Mali ya umma na mali binafsi
Hapa darasani kila mtu ameweza kusoma,kuelimika na kupata maarifa mengi, kila mtu katika mia na zaidi, lakini si kila mtu anaweza kucheza mpira na kungára au kuandika na kupokelewa na wasomaji, au kubuni mitindo ya vitu, au kusuka, au kuimba, au kucheza na tukanyanyuka tumuone, au kuigiza, labda na kughani, au kushawishi na tumsikilize yeye tu, vitu vya kipekee sana hivi.
Elimu imetufananisha ni kama huduma ya umma, ujuzi na vipaji vinatutofautisha maana ni mali binafsi
Ni gharama nafuu kupata huduma kutoka katika taasisi za umma na wengi tunaweza kumudu. Kwa upande mwingine ni ghali kupata huduma kutoka katika taasisi binafsi kama hospitali, shule n.k. kwa kifupi mali binafsi ni chache na ni ghali. Uchache na utofauti huongeza thamani pia.
Katika soko la sasa shughuli binafsi zinalipa pengine zaidi ya mshahara. Kuna fursa katika uchache na upekee. Ipo fursa , ipo.
TUFANYE NINI?
- Watoto wengi wana mbegu za vipaji na ni rahisi kuwapa ujuzi mbalimbali
Tukitazama kwa karibu tunaweza kujua upekee wa watoto wetu. Kuna mzee mmoja alimuambia mkewe “usimchape mwanao akichelewa kutoka mpirani, siku moja mfuatilie uangalie anavyocheza, pengine ni mwanasoka wa baadaye”. Pengine ni mchoraji wa aina yake, au mwanamuziki kwa sauti yake au mwandishi mchanga. Sote tunaona watoto wakiimba katika runinga, wakiandika, wakichora, wakiigiza, si muujiza bali ni jicho la mzazi. Tunaweza kupalilia talanta za watoto wetu na kuwafundisha fani mbalimbali nje ya elimu yao ya shuleni kwani uchache na utofauti huongeza thamani
Kwa maana rahisi pengine kuliko zote, mazingira ni mambo yote yanayomzunguka mtu. Kama mtu huyo ni mtoto basi mazingira ni mambo yote yanayomzunguka mtoto. Na mtu hujengwa na vitu viwili, moja ni yeye mwenyewe na pili ni mazingira yake, mazingira ya mtoto ni pamoja na mzazi, mwalimu, sanaa, ufundi, ubunifu na vinginevyo. Ni rahisi kumkunja angali mbichi, ni rahisi kumfunza
- Tusome kwa mikono yetu
Mazingira yanayotuzunguka yanatulazimu kuchangamka, kuanza na kunyumbulika. Kuchangamka nikuongeza kasi ya kuona fursa , na fursa iliyopo ni kuwa wengi tumesoma, tuna maarifa lakini ubunifu ni hafifu sawa ulivyo ujuzi wa kufanya vitu bora, tena kwa viwango vya juu. Kuanza ni kuacha ahadi, kufungua mikono na kufanya. Kunyumbulika ni kubadilika, kuona uhitaji na kukidhi uhitaji huo.
- Tuwe watu wa viwango
Bwana Yule!, bibi Yule!, asee Yule jamaa noma sana, pale ofisini kwake!, alianza taratibu, akaboresha, sasa imekua tabia yake kutoa vitu bora, bora nitumie gharama kubwa kwa huduma yake. Hivi ndivyo viwango mabibi na mabwana.
JE NINAWEZA KUFANYA NINI KWA KIWANGO CHA JUU BILA KUAJIRIWA?
Namaliza
kwa kujiuliza...
Asanteni sana
Baba Jenny..
Upvote
2