Elimu Tanga Kunani?

Elimu Tanga Kunani?

Kibanga Ampiga Mkoloni

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2007
Posts
18,772
Reaction score
8,939
Shule 10 za mwisho ni;
Manolo mkoa wa Tanga
Chokocho mkoa wa Pemba
Kwalugulu mkoa wa Tanga
Relini mkoa wa Dar es salaam
Mashindei mkoa wa Tanga
Njelekela Islamic Seminary mkoa wa Kigoma
Vudee mkoa wa Kilimanjaro
Mnazi mkoa wa Tanga
Ruhembe mkoa wa Morogoro
Magoma mkoa wa Tanga.
 
Mkuu it is very abnormal kwamba nusu ya shule 10 mbovu kabisa kitaaluma zinatoka huko Tanga. No wonder, Tanga inaelekea kuwa lango kuu la ugaidi Tanzania; no wonder Tanga ndio mkoa unaoichagua CCM kwa kimbunga; no wonder Tanga ndipo alipotoka Mbunge wa kwanza Tanzanaia ambaye ni mganga wa kienyeji na hafahamu chaki inafananaje.
 
Je mkoa huu unaweza kutupa kiongozi bora wa nafasi ya juu kabisa katika nchi???
Yule kijana mtangaza nia kutoka Tanga matokeo haya yanamuweka kundi gani???
Hawa wakwe hawa
 
Sioni suala la imani hapo; anyway, mwendawazimu huwezi kumzuia kufanya chochote akiamua; hata kuvua nguo hadharani ni kawaida kwa mwendawazimu. Je, si kweli kwamba Tanga imeboronga? Je, si kweli kwamba magaidi wamefurumushwa huko Tanga jana kwa mujibu wa taarifa rasmi ya Jeshi? Je, si kweli kwamba Tanga ndio mkoa unaoongoza kwa kuichagua CCM kwa mtindo wa kimbunga? Je, si kweli kwamba mganga wa kienyeji kuotoka Tanga ni Mbunge? Tanga ina tatizo na lisiposhughulikiwa litaisumbua sana nchi huko tuendako.

Ishu ya ugaidi ilikuwa ya kutengeneza japo yapo mengi mabaya Tanga lakini mazuri pia yapo tena mengi tu! Bahati mbaya umechukulia Tanga mjini/ ukanda wa pwani na viunga vyake lakini mkoa wa Tanga ni mkubwa na una mengi mazuri tu mbona hususani wilayani Lushoto ambako elimu iko juu kuna vyuo na sekondary schools nyingi tu unazifahamu Soni seminary Kifungilo girls Mazinde juu Magamba Boys ambayo sasa ni chuo kikuu cha Secuco? Chuo cha mahakama ambacho ndio kitaaluma kikubwa Africa?

Tanga mjini kuna chuo kikuu pia, kuna trade schools za Rosminian usisahau Tanga school vyuo mbali mbali vya ualimu kilimo na fani nyingine

Jamani mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni! Hata mojawapo ya ikulu kubwa za nchi hii iko Tanga Lushoto tafiti nyingi za mime na wadudu adieu zinafanyika Tanga Tanga kuna mengi mazuri kuliko inavyodhaniwa
 
Mara nyingi maeneo ambayo wazee wa balaghashia wapo ni lazima pawe hivo!!!!!!
Angali hapo kuna Pemba, tanga, kigoma, dar es salaam, moro. LAZIMA UTEGEMEE MATOKEO YA NAMNA HIYO
dudus hiki ndicho nilichokua nakiongelea
 
Last edited by a moderator:
Ishu ya ugaidi ilikuwa ya kutengeneza japo yapo mengi mabaya ...

Mkuu hakuna aliyesema Tanga haina mazuri; yapo sana tu; lakini mazuri hayo hayaondoi ukweli kwamba Tanga safari hii kitaaluma imechemsha. Turudi kwenye suala la ugaidi, kama kweli ilikuwa ni issue ya kutengeneza unadhani kwanini fabricators waliamua kucheza sinema yao Tanga? Waliona Tanga ni mandhari inayoendana na igizo lao.
 
Sioni suala la imani hapo; anyway, mwendawazimu huwezi kumzuia kufanya chochote akiamua; hata kuvua nguo hadharani ni kawaida kwa mwendawazimu. Je, si kweli kwamba Tanga imeboronga? Je, si kweli kwamba magaidi wamefurumushwa huko Tanga jana kwa mujibu wa taarifa rasmi ya Jeshi? Je, si kweli kwamba Tanga ndio mkoa unaoongoza kwa kuichagua CCM kwa mtindo wa kimbunga? Je, si kweli kwamba mganga wa kienyeji kuotoka Tanga ni Mbunge? Tanga ina tatizo na lisiposhughulikiwa litaisumbua sana nchi huko tuendako.

Sidhani kama Tanga itashughulikiwa na Serikali ya CCM kwa sababu hali iliyoko Tanga ndio inayopendwa na CCM. Ngao kuu ya Ushindi wa CCM ni Ujinga wa Watanzania waliowengi.Uchaguzi wa Serikali ya Mitaa ulipoisha CCM ikiongozwa na Kinana walianza kuupongeza Mkoa wa Tanga.
 
Shule 10 za mwisho ni;
Manolo mkoa wa Tanga
Chokocho mkoa wa Pemba
Kwalugulu mkoa wa Tanga
Relini mkoa wa Dar es salaam
Mashindei mkoa wa Tanga
Njelekela Islamic Seminary mkoa wa Kigoma
Vudee mkoa wa Kilimanjaro
Mnazi mkoa wa Tanga
Ruhembe mkoa wa Morogoro
Magoma mkoa wa Tanga.
Watu hawataki kusoma, shule zipo tena nzuri , wanakimbilia kuweka kambi kwenye mapango ya amboni unatarajiwa watafaulu kwa miujiza?
 
dudus
Sisemi tuogope binafsi namchukia mtu mwoga mi napenda uhodari na u wazi lakini pia werevu na hekima mabaya ya Tanga ni machache mno kulingana na mazuri yake hata katika elimu! Tanga ina shule nyingi sana zilizifanya vizuri si haki hata kidogo kuhujumu kwa hizo shule tano tuuu
 
Last edited by a moderator:
Ishu ya ugaidi ilikuwa ya kutengeneza japo yapo mengi mabaya Tanga lakini mazuri pia yapo tena mengi tu! Bahati mbaya umechukulia Tanga mjini/ ukanda wa pwani na viunga vyake lakini mkoa wa Tanga ni mkubwa na una mengi mazuri tu mbona hususani wilayani Lushoto ambako elimu iko juu kuna vyuo na sekondary schools nyingi tu unazifahamu Soni seminary Kifungilo girls Mazinde juu Magamba Boys ambayo sasa ni chuo kikuu cha Secuco? Chuo cha mahakama ambacho ndio kitaaluma kikubwa Africa?

Tanga mjini kuna chuo kikuu pia, kuna trade schools za Rosminian usisahau Tanga school vyuo mbali mbali vya ualimu kilimo na fani nyingine

Jamani mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni! Hata mojawapo ya ikulu kubwa za nchi hii iko Tanga Lushoto tafiti nyingi za mime na wadudu adieu zinafanyika Tanga Tanga kuna mengi mazuri kuliko inavyodhaniwa

umemaliza kila kitu mkuu...mwenye hekima atakuelewa.
 
Sidhani kama Tanga itashughulikiwa na Serikali ya CCM kwa sababu hali iliyoko Tanga ndio inayopendwa na CCM. Ngao kuu ya Ushindi wa CCM ni Ujinga wa Watanzania waliowengi.Uchaguzi wa Serikali ya Mitaa ulipoisha CCM ikiongozwa na Kinana walianza kuupongeza Mkoa wa Tanga.

Kweli Mkuu; nakumbuka Kinana alianzia Tanga kuwapongeza kwa kuipa CCM ushindi wa "ajabu"; yaani hata CCM wanaishangaa Tanga. Limekuja suala la ugaidi ni huko huko Tanga; matokeo ya kidato cha nne 2014, Tanga bado ina-draw attention. Tanga kuna tatizo na ni lazima lifanyiwe kazi mapema kabla athari zake hazijaleta matatizo.
 
Kusema kweli pwani kwà ujumla kuna balaa kwani kila mwaka kila ngazi Fulani ni lazima mikoa hii itakuwa ya mwisho na Kigoma ikiwemo
 
Kusema kweli pwani kwà ujumla kuna balaa kwani kila mwaka kila ngazi Fulani ni lazima mikoa hii itakuwa ya mwisho na Kigoma ikiwemo

Na ndiko CCM ilikotamalaki!
 
Mkuu it is very abnormal kwamba nusu ya shule 10 mbovu kabisa kitaaluma zinatoka huko Tanga. No wonder, Tanga inaelekea kuwa lango kuu la ugaidi Tanzania; no wonder Tanga ndio mkoa unaoichagua CCM kwa kimbunga; no wonder Tanga ndipo alipotoka Mbunge wa kwanza Tanzanaia ambaye ni mganga wa kienyeji na hafahamu chaki inafananaje.

P{oleni sana laiti mngelijua huyu jamaa ni Mfanya Biashara mkubwa wa madawa ya kulevya akiyabeba kupitia Tunguli zake hakika msinge mdharau.
 
Tanga imefulia almost kila sekta serikali imetusahau na wanatanga tumejisahau tanga ya sasa na ile nliosimuliwa na wazee wangu ni kama kaskazini na kusini havilingani kabisaa
 
Tanga, mkoa wangu niupendao... Inanisikitisha sana. Kuna siku nilikwenda mkutano wa Kinana pale Tangamano. Nakumbuka wakati Kinana anahitimisha na kutoa shukran kwa mahudhurio aliuliza siku akirudi Tanga, awafanyie nini watu wa Tanga kama shukrani? Amini usiamini, pamoja na matatizo yaliyopo kila sekta Tanga, wao walipiga kelele waletewe Mzee Yusuph wa taarab. Siku ile mpaka leo sitahisahau.
 
Kule tanga uchawi mwingi. Watu wapo busy kupiga ramli huo muda wa kushika kitabu hawana
 
Kule tanga uchawi mwingi. Watu wapo busy kupiga ramli huo muda wa kushika kitabu hawana

Si kweli mkuu, mambo hayo yalikuwepo long time ago, tatizo la tanga ni kupenda starehe. Mtu yupo radhi mtoto wake akose ada ya shule yeye akodishe kigodoro afunge mtaa mzima
 
Mleta uzi nahisi huijui vizuri tanga. Ukiangalia vizuri hizo shule

1.Nyingi au tuseme karibia zote ni za WIALAYA YA LUSHOTO

2.Nyingi ni SHULE ZA KATA

3.Wilaya ya lushoto iko nyuma si tu kielimu lakini kwa mambo mengi tu mf.miundo mbinu ya barabara,maji safi na salama

3.Wakazi wake wengi ni wa asili ya wasambaa/wapare(hawa wamechanganyia na usambaa) ,historia ya maendeleo "ILIWATENGA" tangu zamani, tangu tupate uhuru kuna vijiji huko havijawahi kupata umeme,maji safi nk. Ni sawa na ile mikoa ya kusini "ilivyotengwa "kihistoria.

4.hali ya hewa ya lushoto ni nzuri MNO kama tu uwekezaji mzuri ungefanyika kwa upande wa serikali ,kwa kulijua hilo wajasiriamali wa shule binafsi wamekamata fursa na shule zao zilizoko lushoto zinafanya vizuri mno kama KIFUNGILO,MAZINDE JUU,SONI SEMINARI na kuna shule moja ya wakorea jina limenitoka kidogo.

kwa hiyo TUSIHUKUMU KWA KUANGALIA ATHARI(EFFECTS) Tuangalie CHANZO , kusema kuwa ni watu wa imani fulani wanakaa huko basi ndo mana wanafeli itakuwa HATUJATENDA HAKI , ieleweke kuwa ENVIRONMENTS AFFECT LEARNING. Na tunapozungumza ENVIRONMENT tunazungumza dhana pana zaidi

Tuache chuki na kejeli, tujadili kihoja sio kichafua hali ya hewa,haitusaidii kujenga chuki za kidini kati yetu......
 
Back
Top Bottom