Elimu Tanga Kunani?

Elimu Tanga Kunani?

Shule 10 za mwisho ni;
Manolo mkoa wa Tanga
Chokocho mkoa wa Pemba
Kwalugulu mkoa wa Tanga
Relini mkoa wa Dar es salaam
Mashindei mkoa wa Tanga
Njelekela Islamic Seminary mkoa wa Kigoma
Vudee mkoa wa Kilimanjaro
Mnazi mkoa wa Tanga
Ruhembe mkoa wa Morogoro
Magoma mkoa wa Tanga.

Na mimi nilivyosoma nilijiuliza mwenyewe. Nashukuru kwa kuliweka wazi watu walione.
 
Mleta uzi nahisi huijui vizuri tanga. Ukiangalia vizuri hizo shule
1.Nyingi au tuseme karibia zote ni za WIALAYA YA LUSHOTO
2.Nyingi ni SHULE ZA KATA
3.Wilaya ya lushoto iko nyuma si tu kielimu lakini kwa mambo mengi tu mf.miundo mbinu ya barabara,maji safi na salama
3.Wakazi wake wengi ni wa asili ya wasambaa/wapare(hawa wamechanganyia na usambaa) ,historia ya maendeleo "ILIWATENGA" tangu zamani, tangu tupate uhuru kuna vijiji huko havijawahi kupata umeme,maji safi nk. Ni sawa na ile mikoa ya kusini "ilivyotengwa "kihistoria.
4.hali ya hewa ya lushoto ni nzuri MNO kama tu uwekezaji mzuri ungefanyika kwa upande wa serikali ,kwa kulijua hilo wajasiriamali wa shule binafsi wamekamata fursa na shule zao zilizoko lushoto zinafanya vizuri mno kama KIFUNGILO,MAZINDE JUU,SONI SEMINARI na kuna shule moja ya wakorea jina limenitoka kidogo.
kwa hiyo TUSIHUKUMU KWA KUANGALIA ATHARI(EFFECTS) Tuangalie CHANZO , kusema kuwa ni watu wa imani fulani wanakaa huko basi ndo mana wanafeli itakuwa HATUJATENDA HAKI , ieleweke kuwa ENVIRONMENTS AFFECT LEARNING. Na tunapozungumza ENVIRONMENT tunazungumza dhana pana zaidi ,
Tuache chuki na kejeli, tujadili kihoja sio kichafua hali ya hewa,haitusaidii kujenga chuki za kidini kati yetu......


Unachosema kuwa Lushoto eti imetengwa kimaendeleo sio kweli. katika mkoa wa Tanga ukiacha jiji Lushoto ndio wilaya yenye uchumi mkubwa kwa kipato cha Mwananchi mmojammoja. Lakini pia ni moja ya wilaya zilizoendelea nchini. kuhusu Lushoto kutoa shule mbili mbovu au tatu ni tatizo la kimfumo. Kama ulivyosema, shule hizi ni za kata ambapo utakuta shule ina Mwalimu mmoja utegemee nini? lakini pia ukumbuke kuwa Lushoto kwa mkoa mzima wa Tanga ndio ina shule nyingi. Hivyo hii inaonyesha kuwa kuna shule nyingi zimefunguliwa kiholela au kwa mashindano ya kila kijiji kuwa na shule yake. Hili ni tatizo.
 
Tanga ni mkoa pekee ktk nchi hii wenye aina zote za hali ya hewa ndo maana karibu mazao yote ya biashara kama katani (korogwe, lushoto), kahawa (lushoto) chai, iliki,nk na ya chakula kama mahindi, maharage, ndizi yanastawi tanga. Shida hakuna uzalendo wa kimkoa wapo viongozi na wafanya biashara wengi na hawataki kuwekeza nyumbani kwao, ni wasaliti. Mfano mkoa mmoja ambao ni kati ya mikoa midogo nchini kilimanjaro una shule nyingi za sekondari kuliko kanda nzima ya magharibi tabora,shinyanga, kigoma na katavi.
-- lazima wazawa mbali na serikali wawe na uchungu na nyumbani, na huo sio ubinafsi bali ni uchungu wa kimaendeleo
 
Suala limeulizwa kielimu sasa linapelekwa kimkoa dah,mimi wa Tanga na nilifaulu vizur tu cha kufanya vijana na wazee wa Tanga bado hawajaona umuhimu wa elimu kijana kufaulu either ni juhudi binafsi au katoka familia yenye watu waliosoma kidogo,hapo ndipo tatizo lilipo maana kama ni starehe hakuna kwenye starehe kama Dar,Arusha na Moshi kwa mikoa niliyofika TZ hii
 
Sioni suala la imani hapo; anyway, mwendawazimu huwezi kumzuia kufanya chochote akiamua; hata kuvua nguo hadharani ni kawaida kwa mwendawazimu. Je, si kweli kwamba Tanga imeboronga? Je, si kweli kwamba magaidi wamefurumushwa huko Tanga jana kwa mujibu wa taarifa rasmi ya Jeshi? Je, si kweli kwamba Tanga ndio mkoa unaoongoza kwa kuichagua CCM kwa mtindo wa kimbunga? Je, si kweli kwamba mganga wa kienyeji kuotoka Tanga ni Mbunge? Tanga ina tatizo na lisiposhughulikiwa litaisumbua sana nchi huko tuendako.

Kwenye red, usiamini habari za jeshi, hasa la CCM. Tumesikia mara ngapi Mwigulu anawasingizia wapinzani kuwa wameingiza silaha! Mabomu eti ni ya wapinzani! Aliyekwenda kuungama !!!!???.na sijui iliishia wapi? Nchi hii! ya CCM
 
Hivi Ndalichako bado katibu mkuu pale NECTA ama.....bado siielewi hiyo orodha ya hao kumi bora aisee!!
 
Tafadhali mkuu,hapo kwa Mzee Yusufu kuna ka-chumvi kidogo.
Maana haiwezekani kabisaaa
Tanga, mkoa wangu niupendao... Inanisikitisha sana. Kuna siku nilikwenda mkutano wa Kinana pale Tangamano. Nakumbuka wakati Kinana anahitimisha na kutoa shukran kwa mahudhurio aliuliza siku akirudi Tanga, awafanyie nini watu wa Tanga kama shukrani? Amini usiamini, pamoja na matatizo yaliyopo kila sekta Tanga, wao walipiga kelele waletewe Mzee Yusuph wa taarab. Siku ile mpaka leo sitahisahau.
 
Mkuu hakuna aliyesema Tanga haina mazuri; yapo sana tu; lakini mazuri hayo hayaondoi ukweli kwamba Tanga safari hii kitaaluma imechemsha. Turudi kwenye suala la ugaidi, kama kweli ilikuwa ni issue ya kutengeneza unadhani kwanini fabricators waliamua kucheza sinema yao Tanga? Waliona Tanga ni mandhari inayoendana na igizo lao.

kula gwala kamanda
 
Kwani mikoa mingine haina shule za kata,za serikali?
Shule za kata zimeenea nchi nzima.
Tukubaliane kuwa mwamko wa elimu mkoa wa Tanga bado upo chini.
Baada ya kulitambua na kukubaliana na hilo ndio tukae kutafuta sababu za mwamko wa elimu kuwa chini.
Hakuna haja ya kukashifiana na kutukanana huku tukibeza ukweli.
Nyinyi makafir nguruwe wanaharibu akili ndo maana akawa haram sasa unalinganisha shule zilizofanya vizuri za private na zilizofanya vibaya za kata kuna uwiano hapo kweli izo shule zilizoongoza ni zakulipia kwa nini usiweke za serikali kwa serikali na private kwa private tupate uwiano. Alaf izo zilizoongoza za pwani ujasema kama wakazi ni waislam. Acha chuki za kijinga
 
Kwani mikoa mingine haina shule za kata,za serikali?
Shule za kata zimeenea nchi nzima.
Tukubaliane kuwa mwamko wa elimu mkoa wa Tanga bado upo chini.
Baada ya kulitambua na kukubaliana na hilo ndio tukae kutafuta sababu za mwamko wa elimu kuwa chini.
Hakuna haja ya kukashifiana na kutukanana huku tukibeza ukweli.

Tatizo sio uislam kama wengine wanavyodai tatizo ni serikali yenyewe imeshindwa kuzisimamia izi shule na mikoa mingi ya pwani 6oka uhuru ilinyimwa kipaumbele katika kila nyanja alafu watu wanasema hawataki kusoma wakasome wapi sasa na shule amna. Hii nchi misingi iliyojiwekea tokea uhuru kuna watu hawatakiwi kushika nyadhifa serikalini sasa kikwete anajaribu kutoa huu ndo haya leo yanayomkuta sababu anawapa elimu watu ambao hawaruhusiwi.
 
Uzuri wa mada kama hizi unasaidia kuonesha kuwa wengi wetu tu weupe.

Badala ya watu kuja na uchambuzi, wanaleta porojo na upuuzi.

Binafsi naishi Tanga na naamini Tanga siyo ya mwisho kielimu na kiuchumi. Ila katika ujumla wake, serikali ya CCM imeharibu elimu na sekta nyingine za huduma ya jamii. Kwa hali ya sasa, mkoa wowote unaweza kuwa wa mwisho. Ndiyo maana hao NECTA hawawezi kuthubutu kutuwekea matokeo kwa mchanganuo na uchambuzi unaoeleweka (mfano, private Vs government schools na trends ya kila mkoa)!
 
Kwani mikoa mingine haina shule za kata,za serikali?
Shule za kata zimeenea nchi nzima.
Tukubaliane kuwa mwamko wa elimu mkoa wa Tanga bado upo chini.
Baada ya kulitambua na kukubaliana na hilo ndio tukae kutafuta sababu za mwamko wa elimu kuwa chini.
Hakuna haja ya kukashifiana na kutukanana huku tukibeza ukweli.

Unaweza kutupa takwimu (for the past 5 yrs) kuthibitisha hayo?
 
muulizeni yule mtu anayetaka kuwa Rais na huku akishinda kwenye mitandao,cha kushangaza hata wana Tanga wenyewe hawajui mitandao
 
Uzuri wa mada kama hizi unasaidia kuonesha kuwa wengi wetu tu weupe.

Badala ya watu kuja na uchambuzi, wanaleta porojo na upuuzi.

Binafsi naishi Tanga na naamini Tanga siyo ya mwisho kielimu na kiuchumi. Ila katika ujumla wake, serikali ya CCM imeharibu elimu na sekta nyingine za huduma ya jamii. Kwa hali ya sasa, mkoa wowote unaweza kuwa wa mwisho. Ndiyo maana hao NECTA hawawezi kuthubutu kutuwekea matokeo kwa mchanganuo na uchambuzi unaoeleweka (mfano, private Vs government schools na trends ya kila mkoa)!

Babu DC, you might be right to some extent, but there are tradition that can not be denied! Look, Tanga Elimu ahera is over and above Elimu dunia. Nakubali kila mkoa unaweza kuwa wa mwisho lakini kwingine kuna vichocheo kuliko kwingine!
 
ndo kambi imara ya c.c.m,mnyime mtu elimu umtawale
 
Babu DC, you might be right to some extent, but there are tradition that can not be denied! Look, Tanga Elimu ahera is over and above Elimu dunia. Nakubali kila mkoa unaweza kuwa wa mwisho lakini kwingine kuna vichocheo kuliko kwingine!


Nitashukuru na kufurahi kama atajitokeza mtu na takwimu kutuonesha kuwa mkoa wa Tanga kweli unashika mkia kielemu. Miaka ya hivi karibuni, Shinyanga ilikuwa ya mwisho na pia kuna kipindi Kagera ilikuwa karibu na mwisho.

Zaidi ya hapo, ni jambo la kutumia nafasi (one time event) kuuponda mkoa wa Tanga. Hivi kuna mkoa Tanzania ambao hauna mila au tamaduni ambazo wengine tunaziona hazifai? Kama upo naomba kutajiwa!!
 
Unajua madhara ya comment yako ya kuweka kila kitu kwenye kapu moja?

Kwa nini usitupe takwimu za miaka 50 iliyopita kuonesha jinsi Tanga ilivyoshindwa kuwekeza kwenye elimu?

kwanini wewe usitoe hizo takwimu?au unataka kutafuniwa kila kitu?
 
Back
Top Bottom