Samedi Amba LLC
Member
- Apr 5, 2024
- 81
- 117
Habari wanajamvi,
Nimerudi tena baada ya kufika Morogoro salama. Treni iliondoka kwa wakati (saa 12:55) na kufika kwa wakati (saa 2:59). Nilichukua bajaji ya elfu 2, nikafika Msamvu nlikoacha pikipiki. Nikawasha chombo, nikajaza mafuta, nikafika home salama.
Nimekuwa na tabia ya kusoma kurasa 10 za kitabu fulani asubuhi. Nina shauku sana ya kufikia malengo makubwa ya kifedha, nitaanza na elimu ya uchumi (ambayo na mimi ilinisumbua kwa muda mrefu).
Mwaka jana, nilinunua kitabu kinaituwa FINANCIAL INTELLIGENCE (AKILI YA UCHUMI) ilo andikwa na KAREN BERMAN pamoja na JOE KNIGHT.
View attachment 3217423
Nilianza kusoma kitabu hicho na kimenibariki sana. Kuna vitu vingi sana katika kurasa za awali. Lakini kilichonigusa sana ni CASH FLOW na PROFITS.
Nilikuja kufahamu kuwa watu wengi sana sana (haijalishi kuwa amesoma au hajasoma. Hata wafanyabiashara wengi wanajikuta hapa), hawajuagi tofauti kati ya maneno haya mawili. Naomba kutumia dakika chache kuelezea.
PROFITS (FAIDA)
Profits au faida ni pesa unayoipata kwa kazi uliyofanya, baada ya kuondoa matumizi yote. Kwa mfano, ukinunua tikiti ya sh 10,000 sokoni ukatengeneza juice ya 50,000, unapata faida ya 40,000. Hii huwa the case biashara inapokuwa katika eneo moja, na una walk-in customers (wateja na kuja na kuondoka, wanaolipa fedha taslimu).
Biashara yako inapokua, unalazimika kufikiria tofauti kuhusu faida. Utakutana na wakopaji. Kwa mfano, hoteli fulani inaweza kupenda kazi yako, wakakupa tenda ya kutengeneza juice ya sh. 500,000. Utajitutumua na kutafuta tikiti ya sh. 100,000, kisha ukatengeneza na kupeleka. Faida ya 400,000, au siyo?!
Lakini je, faida hii inamaanisha una hela mkononi? Hapa ndipo suala la cash flow linapoingia.
CASH FLOW (HELA INAYOZUNGUKA)
Cash flow ni pesa ulizofanyia kazi kukufikia mkononi kwa ajili ya matumizi. Tukirejea mfano wa hapo juu, ushapeleka chakula, washakula na kusaza, umeokota makombo, na baadaye mmekaa na bosi kupiga mahesabu. Unadai LAKI 5 zako. Unaombwa uandike invoice. Unafanya hivyo. Jumatatu asubuhi na mapema, imo.
Hapo, una cash flow.
UMUHIMU WA FAIDA NA CASH FLOW
Ni muhimu kuwa na pesa mkononi. Hili ni suala linalowasumbua wafanyabiashara wengi, hasa wadogo, au wale wanaoanza.
Nimesikia vilio vingi vya ulaji wa mtaji mtaani kwetu. Uchunguzi ukaonyesha kuwa alikuwa afahamu tofauti kati ya faida na pesa mkononi.
Tafiti zinaonyesha kuwa zaidi ya 80% ya biashara ndogo hufilisika si kwa sababu ya kukosa faida, bali kwa sababu ya ukosefu wa cash flow.
Ili kukabiliana na changamoto za "pesa zisizoonekana", mfanyabiashara mdogo anaweza:
Na maneno haya sio kwa wafanyabiashara tu. Nazungumza nawe mwajiriwa, mwanafunzi, na bachela. Ni muhimu kuwa na hela mkononi kwa ajili ya dharura. Na matumizi. Na umeme, na kodi ya nyumba.
Niishie hapo. Siku nikipata muda, nitazungumzia THE SEVEN BABY STEPS TO ECONOMIC FREEDOM (Hatua 7 rahisi za kujipatia uhuru wa kiuchumi).
Hadi tutakapokutana tena, alamsiki...
Nimerudi tena baada ya kufika Morogoro salama. Treni iliondoka kwa wakati (saa 12:55) na kufika kwa wakati (saa 2:59). Nilichukua bajaji ya elfu 2, nikafika Msamvu nlikoacha pikipiki. Nikawasha chombo, nikajaza mafuta, nikafika home salama.
Nimekuwa na tabia ya kusoma kurasa 10 za kitabu fulani asubuhi. Nina shauku sana ya kufikia malengo makubwa ya kifedha, nitaanza na elimu ya uchumi (ambayo na mimi ilinisumbua kwa muda mrefu).
Mwaka jana, nilinunua kitabu kinaituwa FINANCIAL INTELLIGENCE (AKILI YA UCHUMI) ilo andikwa na KAREN BERMAN pamoja na JOE KNIGHT.
View attachment 3217423
Nilianza kusoma kitabu hicho na kimenibariki sana. Kuna vitu vingi sana katika kurasa za awali. Lakini kilichonigusa sana ni CASH FLOW na PROFITS.
Nilikuja kufahamu kuwa watu wengi sana sana (haijalishi kuwa amesoma au hajasoma. Hata wafanyabiashara wengi wanajikuta hapa), hawajuagi tofauti kati ya maneno haya mawili. Naomba kutumia dakika chache kuelezea.
PROFITS (FAIDA)
Profits au faida ni pesa unayoipata kwa kazi uliyofanya, baada ya kuondoa matumizi yote. Kwa mfano, ukinunua tikiti ya sh 10,000 sokoni ukatengeneza juice ya 50,000, unapata faida ya 40,000. Hii huwa the case biashara inapokuwa katika eneo moja, na una walk-in customers (wateja na kuja na kuondoka, wanaolipa fedha taslimu).
Biashara yako inapokua, unalazimika kufikiria tofauti kuhusu faida. Utakutana na wakopaji. Kwa mfano, hoteli fulani inaweza kupenda kazi yako, wakakupa tenda ya kutengeneza juice ya sh. 500,000. Utajitutumua na kutafuta tikiti ya sh. 100,000, kisha ukatengeneza na kupeleka. Faida ya 400,000, au siyo?!
Lakini je, faida hii inamaanisha una hela mkononi? Hapa ndipo suala la cash flow linapoingia.
CASH FLOW (HELA INAYOZUNGUKA)
Cash flow ni pesa ulizofanyia kazi kukufikia mkononi kwa ajili ya matumizi. Tukirejea mfano wa hapo juu, ushapeleka chakula, washakula na kusaza, umeokota makombo, na baadaye mmekaa na bosi kupiga mahesabu. Unadai LAKI 5 zako. Unaombwa uandike invoice. Unafanya hivyo. Jumatatu asubuhi na mapema, imo.
Hapo, una cash flow.
UMUHIMU WA FAIDA NA CASH FLOW
- Faida huwa ni kipimo cha kuashiria kama biashara yako inafaa. Bila faida, biashara yako haiwezi kustahimili mwendo mrefu.
- Cash Flow (Pesa Mkononi) hukusaidia kuhandle matumizi vizuri na mapema. Biashara inaweza kuwa na faida, lakini ikashindwa kulipa bili zote kwa wakati.
Ni muhimu kuwa na pesa mkononi. Hili ni suala linalowasumbua wafanyabiashara wengi, hasa wadogo, au wale wanaoanza.
Nimesikia vilio vingi vya ulaji wa mtaji mtaani kwetu. Uchunguzi ukaonyesha kuwa alikuwa afahamu tofauti kati ya faida na pesa mkononi.
Tafiti zinaonyesha kuwa zaidi ya 80% ya biashara ndogo hufilisika si kwa sababu ya kukosa faida, bali kwa sababu ya ukosefu wa cash flow.
Ili kukabiliana na changamoto za "pesa zisizoonekana", mfanyabiashara mdogo anaweza:
- Kuwasiliana mapema na wateja kuhusu malipo
- Kutumia mikataba iliyo na masharti ya malipo ya haraka
- Kuwa na akiba ya dharura ya kifedha
Na maneno haya sio kwa wafanyabiashara tu. Nazungumza nawe mwajiriwa, mwanafunzi, na bachela. Ni muhimu kuwa na hela mkononi kwa ajili ya dharura. Na matumizi. Na umeme, na kodi ya nyumba.
Niishie hapo. Siku nikipata muda, nitazungumzia THE SEVEN BABY STEPS TO ECONOMIC FREEDOM (Hatua 7 rahisi za kujipatia uhuru wa kiuchumi).
Hadi tutakapokutana tena, alamsiki...