elimu ya juu

elimu ya juu

Joshua Haji

Senior Member
Joined
Nov 4, 2011
Posts
108
Reaction score
20
naombeni mnisaidie ..hichi chuo cha IFM kwanini watu hawaoni jinsi maslahi ya kipesa yalivowekwa mbele?dharau walizonazo wahadhiri ambao ni vijana tu kwa vijana wa watu waliokuja kutafuta maisha kupitia shule.nimeipata leo kwa vijana wa mwaka wa kwanza eti test ratiba imetoka na watu wameirekodi na kuifata ghafula unabadilisha muda wa mtihani jioni unauleta asubuhi na tangazo kuwekwa notice board jana yake jioni kweli sio makusudi hayo kweli??tunawapa hawa watu madaraka ya kucheza na shule ya vijana hawa kama makia?
 
pole sana,najua inauzi lakini mkuu hapa si mahara pake peleka kwenye jukwaa la elimu.pole sana kwakweli inauzi na nimekua nikikutana nayo
 
Slow learner Mmezoea kwenda kukesha disco. Mwanafunzi lazma awe active 24/7, sio unatangaziwa test wiki 3 kabla. Huo ni ujinga...
 
Slow learner Mmezoea kwenda kukesha disco. Mwanafunzi lazma awe active 24/7, sio unatangaziwa test wiki 3 kabla. Huo ni ujinga...

umeelewa alichokimaanisha?
 
Principle wa ifm hawa vijana malecture wana matatizo mengi sana nashangaa hata siku moja hawajawi kua assesiwa yani bora wazee wetu maana hawa vijana they need us to appreciate them while we need education which leads us to be innovater and discovery to our society and not their first class or others. So bored younger lecturer esp. Chuo mtajwa
 
Mheshimiwa, Kubadilika kwa ratiba ni mambo ya kawaida kabisa unless una uthibitisho usiotia shaka kuwa kulikua na malicious intention katika hilo! Wahadhiri hawa ni binadamu tu kama wanafunzi wao ambao nao pia wanaweza kuahirisha mtihani kwa sababu moja au nyingine! Sasa kama wanafunzi wanaweza ahirisha test, why not lecturers! Tena these guys wamekua waungwa kwelikweli, wametoa mpaka tangazo?! Make vijana wangeweza kukaa examination room halafu mtihani usitokee wala mhadhiri, wala excuse!
 
kila kichwa kilichojaa upumbavu hufikiria kuheshimiwa kuliko kuheshimu,wahadhili weng wa nchi hz za kimaskin huwa na mawazo butu juu ya utendaji wao kunachuo kimoja katika nchi hii ambacho mhadhil anajiita aeroplane kwamba ukichelewa kukusanya assignment saa na dakika iliyopangwa basi basi hakutambui,poleni kwa yaliyowasibu wanafunz wa chuo kitajwa ni challenge kimaisha cha muhimu ni kufikiria kesho itakuwa vp kama ikitokea hal kama hyo ila wanafunz wa nchi hii ambao tunasomea kwan hamna mtanzania anayesoma wote wanasomea ndo maana et sie tupo kwenye kilimo kwanza ambayo ilifanyika uingereza karne ya18 kama historia inavyoeleza...
 
Kuacha mambo yaende yatakavyo kama ndugu yangu anavyotaka kufanya "yangu macho" ni kutoitendea haki nchi hii! Sasa ikiwa kila mmoja wetu ataamua mambo yaende hivihivi itakuaje? Ni wajibu wetu kukemea tunapoona mambo hayaendi kama tulivyotarajia, na kuchukua hatua mahususi kila inapobidi.

Ndugu yangu thinker96 analalamika kua kuna mwalimu ukichelewa kukusanya assignment hakutambui! Mimi nadhani huyu mwalimu alipaswa kupongezwa! kwa nini usikusanye assignment kwa wakati. Tabia za uvivu na kuto meet deadline tangu tukiwa wanafunzi ndo zinasababisah hatuwezi ku meet deadline hata tunapokua kazini au tunapoendesha shughuli zetu binafsi! Matokeo yake miaka hamsini baada ya uhuru bado sisi ni maskini sana!

Ku-meet deadline ni muhimu sana katika maisha, uwe mwanafunzi, mfanyakazi na hata mkulima! Kwa mfano ukiwa mkulima na huwezi kulima na kupanda kwa wakati, nini matokeo yake? Hutapata mavuno! Hapa ninapoendesha shughuli zangu za ujasiriamali, am strict when it comes to deadline. Hii ni kwa sababu our survival depends on our customers' satisfaction. Tusipofanya hivyo wateja weatahamia kwa wachina halafu kama kawaida yetu tutabaki kulalama.
 
Back
Top Bottom