Elimu ya Nape Nnauye

Elimu ya Nape Nnauye

Kumbe Nape ni Mlokole safi.

Cc. Matola,
 
Last edited by a moderator:
Kamanda Mnyika ana one ya point 9, Nepi 4 ya point 29!! Huyu ni failure kabisa!! Ndo maana mpaka leo anaropoka ropoka tu!! Mimi huwa namwita VUVUZELA!!
Hapa mkuu,Mnyika ana one ya pointi 7 ila ana A tisa!
 
na katika kumjaji mtu aliyeelimika ama mwenye akili sisi hatuangalii cheti maana kuna vya kupewa tuna angalia matendo ama fikra, tafakuri yake juu ya mambo mbalimbali. unaweza kuwa na cheti lakini hakuna unachojua yani bogas per se
 
1. Shule ya msingi, John Mnyika alikuwa mwanafunzi wa kwanza kwa mkoa wa darisalama. Akachaguliwa kwenda Ilboru lakini akaamua kwenda seminari. (Naachana na hili kwa kuwa ni swala la kiimani)

2. Form 4 akapata A masomo tisa. Katika mwaka ambao matokeo yalikuwa na mushkeli kwa uvujaji wa mitihani. Angeweza kwenda shule yoyote na mchepuo wowote. Akaamua kwenda Tambaza.

3. Form 6 akapata matokeo mazuri tuu (ambayo hayakuwekwa wazi kama matokeo ya form 4)

4. University akaamua kusoma evening classes. (Hakumaliza kwa sababu alizozitaja hapo juu)

Kwa wenye busara, mlolongo wa elimu wa huyu bwana unanuka samaki aliyechina. Mimi binafsi nimesoma Tanga school, wakati wa headmaster Tetti. Wakati sisi tuko O'level pale Tanga school alikuja mwarabu mmoja kujiunga form 5 (PCM) tulikuwa tunamwita "yarabi salama". Yarabi salama yeye wakati akiwa form 5 PCM alikuwa haelewi kwa nini namba ikitoka upande mmoja wa equation na kuvuka alama ya sawasawa na kuhamia upande mwingine mwingine, basi inabidi alama yake ibadilike, kama hasi itakuwa chanya na chanya huwa hasi. Form 5 PCM huyo. Na bwana yarabi salama alikuwa amepata alama A katika hesabu O level. Baadaye ikagundulika kwamba wakati wenzake wanafanya mitihani, yeye alikuwa anazaa mitihani.

Sijui kama msamiati wa kuzaa bado unatumika siku hizi, lakini kuzaa maana yake ni kwamba kuna watu wana networks na mitihani inapotoka na wanapoingia kwenye chumba cha mtihani, hawaji kufanya mtihani ispokuwa wanakuja na "booklet" zao ambazo maswali yanakuwa tayari yameshafanywa. Sasa wakati wenzao wanafanya mtihani wao wanaandika namba yao ya mtihani tuu kisha wanazaa.

a) Sasa, najiuliza. Mnyika amesema kwamba alikuwa wa kwanza mkoa wa darisalama. (Sibishi, lakina Sijui amejuaje)
b) amepata A tisa form IV; lakini hakusema amepata A ngapi form VI. Jee inawezekana ni kwa sababu matokeo yake ya form 6 hayashabihiani na yale ya form 4?
c) A tisa, lakini hakwenda Ilboru. Kwanini mwanafunzi hodari asiwe na hamu na shauku ya kusoma na wanafunzi hodari wengine? Jee inawezekana bwana Mnyika alikuwa anaogopa "to get found out?"
d) Baada ya kupata matokeo mazuri form 6; kwanini asome jioni? Jee alikuwa anaogopa kusoma na wanafunzi hodari?
e) Mpaka leo bado hana degree. [anisamehe kama nimekosea katika hili]. Ni kweli mwanafunzi mwenye uwezo wake wa kitaaluma atakubali kuishia njiani kwa namna aliyoishia yeye?

Sasa kila nikimtafiti huyu bwana Mnyika, samahani, lakini neno kuzaa linapiga kengere zote akilini mwangu. Nadhani huyu bwana ni miongoni mwa wale wenye bahati nzuri ambao huweza kuipata mitihani kabla ya siku ya mtihani.

Mbona wewe huelezi form six ulipata ngapi?au nawe ulizaa?watu wengine mnawatafutia watu ban za makusudi,yaani Mnyika kwa maelezo yote hapo hujamwelewa unamlinganisha na mtu ambaye hatuwezi kupata uthibitisho?Mnyika angekuwa kilaza angezaje kushawishi wasomi wa mlimani wampe kura?angewezaje kuwatingisha maprofesa kama Magembe.Bila shaka wewe ndiye Yarabi Salama
 
Suala sio nani ana nini.Suala ni kwanini umtupie mwingine matongo wakati wewe mwenyewe elimu yako ni yakuunga unga.
Si bora ingekuwa ya kuunga hizo ni magumashi tu ni nyingi tu CCM,acha hiyo masters wengine ni Madokta,maprofesa,n.k Kwenye chama chao unapokewa tu hata bila kutathimini umepatapateje,wengi ni mawaziri na manaibu waziri si ndio maana tumefika hapa tulipo?una watu wenye vyeti safi kumbe cheti hakilingani na uwelewa wa huyo mtu matokeo yake ndio haya maporomoko kila sekta au umemsahau Msemakweli????aliwatungia kitabu na akawataja kwa majina wakamtishia kumfikisha mahakamani,akawaambia nendeni tutakutana hukohuko wakaufiata hadi leo.
 
Usisahau degree kuna za C.H. U .P I kwa baadhi ya kina dada ambao uwezo wao wa kielimu ni mdogo kama huyu mtu aliyepata Four ya 29. Sasa sijui za mwenzetu ni za nini? Pia mwambie aje atuambie jinsi alivyopta sifa za kuingia kidato cha tano.

Jibu hili pia linamfaa dada jenifa mtodi hapo juu aliyesoma Tanga Tech shule ya wavulana
 
Kiutendaji, elimu haitusaidii sana Watz, Angalia waziri wa Elimu and PHD, lakini angalia Elimu yetu inavyoporomoka kutoka mwaka hadi mwaka. Waziri wa Ulinzi Dr. Nchimbi, anglia hali ya amani ilivyo tete nchini. Rais wako ni PHD holder, anglaia nchi ilivyomshinda vibaya. Waziri wa Nishati na madini ni Professor, Muhongo, angalia umeme unavyotutesa, angalia mikataba feki ya madini na na gesi. Waziri wa Kilimo na Mifugo huyu Professor Jumanne Magembe, eti ni professor, lakini angalia Kilimo kinavyorudi nyuma mwaka hadi mwaka na angalia migogoro ya wakulima na wafugaji inavyokuwa mikubwa bila utatuzi.

Ukweli ni kwamba JJ Mnyika hana degree, wala hata hiyo masters ya Nape, lakini angalia michango yake Bungeni na Utendaji wake Jimboni. Ni Tofauti kabisa na Utendaji wa akina Magembe na Kawambwa wenye PHD na Professors wa ccm.

Kwani akina Moringe Sokoine walikuwa na elimu gani iliyowafanya wafanye kazi kwa weledi ule uliotukuka? Huwezi kufamnanisha Mnyika na Nape Kwa lolote lile, na ukisema Nape ana Masters mbele ya watu wasomi, wakilinganisha na utendaji wake wa kazi hasa matamko anayotoa, watakushangaa sana.

Poleni wote mnaodhani kuwa John Mnyika atang'oka Ubunge kwa kigezo cha Elimu. Hiyo ni ndoto, ingelikuwa hivyo, Prof. Lipumba angelikuwa kiongozi mkuu wa Taifa hili, lakini wapi, ndoto zake zinazidi kupotea kila siku.

NSWIMA J. E.
MPANDA, KATAVI.

Mkuu Nswima hapo kwenye Red huyo mzee usimsingizie kabisaa!!! Yeye sasa hivi ni Waziri wa Maji ndo maana Mnyika alimtoa jasho bungeni mpaka Bi. Kiroboto na mwenzake ikabidi wamwokoe! Waziri wa Kilimo na Chakula sasa hivi ni Eng. Christopher Ciza (Chizza).

Kwa ufupi Mnyika yuko juu sana wala huwezi kumlinganisha na vilaza kama akina NEPI!!
 
Enzi hizo Nsumba ilikua inafaulisha sana. Ninawasiwasi kwa matokeo haya alikuwa wa mwisho darasani.
 
hapa ni sawa na kumringalisha Messi wa Barcelona na Tegete wa Yanga kwenye medani ya soka.

Hayo masomo kwenye Blue ndipo tatizo lilipo; masomo haya ni muhimu sana kwenye mawasiliano na logic. sasa nafikiri mnaona wenyewe hawa watu wawili wakiongea juu ya jambo (hoja) moja basi unapata picha mbili tofauti kabisa.

Hapo kwenye RED unataka kuharibu utamu wa hoja yako...Nadhani tu substitute hayo maneno na haya yafuatayo...Boban wa Simba. Nadhani hata Crashwise ataniunga mkono!!!
 
Last edited by a moderator:
Hahaha F ya kiswahili, F ya English! F ya maths! Zilizobaki D!!

Btw, do you know how dumb you've got to be to get an F in civics?!

Kweli nape ni kilaza now I have no doubt. Basi tu siasa za hapa kwetu zinafavor watu wajinga,ambao actually ndio majority!

Limtu kama nape ndio huwa yanajitapa mtaani kuwa pamoja na kufeli bado linaongoza akili kubwa!! Pathetic!

Haya ndiyo yanayosababisha watoto siku hizi wanahamia kwenye bongo flavor tu! Maana wanaona kama kusoma hakuna maana!!
Mkuu umesahau mara hii maneno ya Mch Msigwa mbunge wa Iringa kuwa Tanzania tuna tatizo la kuruhusu Akili ndogo kuongoza akili kubwa? Haya ndiyo aliyokuwa anamaanisha Msigwa.
Ona sasa matokeo yake,Hivi Nape anaweza kusikia uchungu wa anguko la Elimu TZ kwa zaidi ya 60% kufeli wakati naye yupo kweye kundi hilo tena yeye alisoma katika mazingira mazuri kuliko hawa wa sasa? Hawezi tena unaweza kuta kafurahi akisema heri tuwe wengi. "Akili ndogo kuongoza akili kubwa"
 
hapa ni sawa na kumringalisha Messi wa Barcelona na Tegete wa Yanga kwenye medani ya soka.

Hayo masomo kwenye Blue ndipo tatizo lilipo; masomo haya ni muhimu sana kwenye mawasiliano na logic. sasa nafikiri mnaona wenyewe hawa watu wawili wakiongea juu ya jambo (hoja) moja basi unapata picha mbili tofauti kabisa.
Na ndio maana CDM walimkataa Nape awe mgombea wa jimbo la ubungo jimbo lingeenda CCM huyo hana uwezo wa kupanga hoja kama Mnyika ni mburura tu,akiweza tumpambanishe kwenye mdaharo.
 
Back
Top Bottom