Elimu ya Sekondari Ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini

Elimu ya Sekondari Ndani ya Jimbo la Musoma Vijijini

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
ELIM
ELIMU YA SEKONDARI NDANI YA JIMBO LA MUSOMA VIJIJINI

Ukubwa wa Jimbo letu:
Kata 21 zenye vijiji 68 na vitongoji 374

Idadi ya sekondari Jimboni mwetu:

+26 za Kata zinatoa elimu
+2 za Binafsi zinatoa elimu
+3 mpya zinajengwa kwa fedha za Serikali Kuu. Wanavijiji kuchangia nguvukazi
+3 mpya zinajengwa kwa michango ya wanavijiji na viongozi wao
+6 ujenzi kuanza Julai/Agosti 2024 kwa kutumia michango ya wanavijiji na viongozi wao

(a) Uanzishwaji wa miradi ya ujenzi wa sekondari mpya Jimboni mwetu

Malengo:
+kutatua matatizo ya umbali mrefu wa kwenda masomoni
+kutatua matatizo ya mirundikano madarasani
+kujitayarisha vizuri kwenye mfumo mpya wa elimu - wanafunzi wote watakaomaliza elimu ya msingi kwenda wote sekondari

Wanavijiji wanamuomba Mbunge wa Jimbo la Musoma Vijijini washirikiane nae kuanza miradi yao ya ujenzi wa sekondari mpya.

Mbunge wa Jimbo amekubali. Miradi hiyo ni hii ifuatayo:

1. Kijiji cha Chitare:
Ujenzi wa sekondari mpya. Hii itakuwa sekondari ya pili ya Kata ya Makojo yenye vijiji vitatu

2. Kijiji cha Buanga:
Ujenzi wa sekondari mpya. Hii itakuwa sekondari ya pili ya Kata ya Rusoli yenye vijiji vitatu

3. Kijiji cha Nyambono:
Ujenzi wa sekondari mpya. Hii itakuwa sekondari ya pili ya Kata ya Nyambono yenye vijiji viwili

4. Kijiji cha Kataryo:
Ujenzi wa sekondari mpya. Hii itakuwa sekondari ya pili ya Kata ya Tegeruka yenye vijiji vitatu

5. Kijiji cha Kiriba:
Ujenzi wa sekondari mpya. Hii itakuwa sekondari ya tatu ya Kata ya Kiriba yenye vijiji vitatu

6. Kijiji cha Mmahare:
Ujenzi wa sekondari mpya. Hii itakuwa sekondari ya tatu ya Kata ya Etaro yenye vijiji vinne

SEKONDARI MPYA 6

(b) Sekondari zitakazojengwa kwa kutumia fedha kutoka Serikali Kuu.

Wanavijiji wanashawishiwa wachangie nguvukazi ili tupate miundombinu mingi ya elimu kutoka kwenye fedha hizo za Serikali Kuu

7. Kata ya Bukima:
Kijijini Butata. Hii itakuwa sekondari ya pili ya Kata ya Bukima yenye vijiji vitatu.

8. Kijiji cha Kasoma:
Kijijini Kasoma. Hii ni sekondari ya kwanza ya amali (technical?) ndani ya Jimbo letu. Itakuwa sekondari ya nne ya Kata ya Nyamrandirira yenye vijiji vitano.

Kasoma Sekondari yenye High School iko ndani ya Kijiji cha Kaboni.

9. Kijiji cha Kurwaki:
Kijijini Kurwaki. Ujenzi wa David Massamba Memorial Secondary School. Sekondari ya kumuenzi Hayati Prof Massamba.

Hii itakuwa sekondari ya pili ya Kata ya Mugango yenye vijiji vitatu.

SEKONDARI MPYA 3: zitafunguliwa Januari 2025

(c) Ukamilishaji wa sekondari zilizoanzwa kujengwa kwa michango ya wanavijiji na viongozi wao

10. Kijiji cha Muhoji
Hii itakuwa sekondari ya pili ya Kata ya Bugwema yenye vijiji vinne. Michango ya ujenzi inatoka kwa wanakijiji na viongozi wao.

+Serikali imechangia Tsh 75m
+Mzaliwa wa Muhoji, Mhe Maboto amejenga na kukamilisha darasa moja

11. Kijiji cha Nyasaungu
Sekondari mpya ambayo michango ya ujenzi inatolewa na wanakijiji na viongozi wao. Hii ni sekondari ya pili ya Kata ya Ifulifu yenye vijiji vitatu.

12. Kisiwa cha Rukuba
Ujenzi wa sekondari hii unachangiwa na wana-Rukuba, na viongozi wao. Hii itakuwa sekondari ya tatu ya Kata ya Etaro yenye vijiji vinne.

Kisiwa cha Rukuba ni kijiji kinachojitegemea.

SEKONDARI MPYA 3: zitafunguliwa Januari 2025

(d) Ujenzi na ukamilishaji wa maabara 3 za masomo ya sayansi (chemistry, physics & biology)

+Huu ni mradi endelevu hadi sekondari zote za Kata na Binafsi zitakapokamilisha maabara hizo.

+Wana-Musoma Vijijini tuendelee kushirikiana na Serikali yetu kuchangia ujenzi na uboreshaji wa miundombinu ya elimu ya Jimboni mwetu.

+Wazaliwa wa Musoma Vijijini waanze na waendelee kujitokeza kuchangia maendeleo ya vijijini kwao.

Taarifa za shule za msingi, hususani ujenzi wa shule shikizi mpya, na vyumba vipya vya madarasa zitatolewa baadae.
 
Back
Top Bottom