jayspol malika
Member
- Jan 19, 2017
- 14
- 28
Jiji la Mwanza, la pili kwa ukubwa Tanzania (The second largest City in Tanzania), sifa nyingine ni jiji lililo katikati Kati ya majiji ya Jumuiya ya Afrika Mashariki, hapa namaanisha Nairobi, Kampala, Kigali, Bujumbura. Kinshasa pote ni karibu kufika jijini Mwanza.
ELIMU YA JUU
Katika elimu ya juu hapa jiji la Mwanza limechelewa sana, yaani hakuna chuo hata kimoja kikuu cha serikali , kitu ambacho kinakichekewesha sana jiji la Mwanza kimaendeleo Kama jiji na kusomeka vizuri katika ulimwengu duniani Kama kitivo cha elimu.
Ikumbukwe jiji la Mwanza lina vyuo vikuu viwili vya binafsi vinavyomilikiwa na taasisi ya dini , amabvyo ni CUHAS ( Catholic University of Health and Allied Science) pia SAINT AUGUSTINE UNIVERSITY OF TANZANIA au maarufu Kama SAUT .
Ukiachana na vyuo hivyo Kuna taasisi tu tena ni kampasi za vyuo vya sehemu nyingine, hapa namaanisha Taasisi ya mipango vijijini (IRDP) -Mwanza, Tassisi ya uhasibu Tanzania ( TIA), College of Business Education ( CBE) - Kampasi ya Mwanza, chuo cha usimamizi wa fedha (IFM)- Mwanza Kampasi , chuo kikuu huria ( OUT) - Mwanza , Taasisi ya teknolojia Dar es salaam ( DIT) -Mwanza.
Hivyo vyuo vyote havijakidhi mahitaji ya watu wa ukanda wa ziwa na magharibi ambapo kuitafuta elimu inabidi wasafiri umbali mrefu sana, mikoa hiyo ni Mwanza , Shinyanga, Simiyu, Geita, Kagera, Mara, Tabora , Kigoma , Katavi , Rukwa n.k
Kiuhalisia wengi wanaotoka Kanda ya ziwa husoma fani za uhandisi, madini, sheria na biashara pia udaktari , katika kundi kubwa , kuipata elimu hiyo katika vyuo vikuu Hadi waende umbali mrefu sana.
Sijawahi kuona mpango mkakati wa chuo kikuu jijini Mwanza zaidi ya Kampasi tena za taasisi tu na sio vyuo vikuu.
Hapa serikali ilijisahau sana au pengine Mwanza haikupata wabunge wenye ushawishi bungeni juu ya suala la elimu , hivyo kuachwa nyuma sana.
Kama mdau wa elimu Kuna haja serikali kuweka mradi mwingine was chuo kukuu , hiki kijengwe jijini Mwanza either maeneo ya Kisesa au Wilaya ya Misungwi , kiwe Kama chuo kikuu cha Dodoma kibobee zaidi katika uhandisi , madini , biashara na masuala ya teknolojia namaanisha IT, Telecom, Computer Science na Engineering na mambo mengine mengi mazuri.
Na Kama uwezo wangu chuo hicho kiitwe University of Mwanza (UoM) . Kiendane na kasi ya mabadiliko ya ongezeko la watu, na watu wengi ukanda wa ziwa wapate elimu pia kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kati.
Viongozi wa serikali pitieni uzi huu. Naamini nimetoa mawazo yangu.
Nawasilisha wenu Malika.
ELIMU YA JUU
Katika elimu ya juu hapa jiji la Mwanza limechelewa sana, yaani hakuna chuo hata kimoja kikuu cha serikali , kitu ambacho kinakichekewesha sana jiji la Mwanza kimaendeleo Kama jiji na kusomeka vizuri katika ulimwengu duniani Kama kitivo cha elimu.
Ikumbukwe jiji la Mwanza lina vyuo vikuu viwili vya binafsi vinavyomilikiwa na taasisi ya dini , amabvyo ni CUHAS ( Catholic University of Health and Allied Science) pia SAINT AUGUSTINE UNIVERSITY OF TANZANIA au maarufu Kama SAUT .
Ukiachana na vyuo hivyo Kuna taasisi tu tena ni kampasi za vyuo vya sehemu nyingine, hapa namaanisha Taasisi ya mipango vijijini (IRDP) -Mwanza, Tassisi ya uhasibu Tanzania ( TIA), College of Business Education ( CBE) - Kampasi ya Mwanza, chuo cha usimamizi wa fedha (IFM)- Mwanza Kampasi , chuo kikuu huria ( OUT) - Mwanza , Taasisi ya teknolojia Dar es salaam ( DIT) -Mwanza.
Hivyo vyuo vyote havijakidhi mahitaji ya watu wa ukanda wa ziwa na magharibi ambapo kuitafuta elimu inabidi wasafiri umbali mrefu sana, mikoa hiyo ni Mwanza , Shinyanga, Simiyu, Geita, Kagera, Mara, Tabora , Kigoma , Katavi , Rukwa n.k
Kiuhalisia wengi wanaotoka Kanda ya ziwa husoma fani za uhandisi, madini, sheria na biashara pia udaktari , katika kundi kubwa , kuipata elimu hiyo katika vyuo vikuu Hadi waende umbali mrefu sana.
Sijawahi kuona mpango mkakati wa chuo kikuu jijini Mwanza zaidi ya Kampasi tena za taasisi tu na sio vyuo vikuu.
Hapa serikali ilijisahau sana au pengine Mwanza haikupata wabunge wenye ushawishi bungeni juu ya suala la elimu , hivyo kuachwa nyuma sana.
Kama mdau wa elimu Kuna haja serikali kuweka mradi mwingine was chuo kukuu , hiki kijengwe jijini Mwanza either maeneo ya Kisesa au Wilaya ya Misungwi , kiwe Kama chuo kikuu cha Dodoma kibobee zaidi katika uhandisi , madini , biashara na masuala ya teknolojia namaanisha IT, Telecom, Computer Science na Engineering na mambo mengine mengi mazuri.
Na Kama uwezo wangu chuo hicho kiitwe University of Mwanza (UoM) . Kiendane na kasi ya mabadiliko ya ongezeko la watu, na watu wengi ukanda wa ziwa wapate elimu pia kutoka nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki na Kati.
Viongozi wa serikali pitieni uzi huu. Naamini nimetoa mawazo yangu.
Nawasilisha wenu Malika.