ElimuTiba: Jinsi ya kujieleza kwa Daktari

meningitis

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2010
Posts
8,425
Reaction score
4,768
Kwa heshima na taadhima napenda kuelezea utaratibu muhimu wa kujieleza kwa daktari ili kurahisisha upatikanaji wa tiba kwa usahihi.

UTANGULIZI

Ni ukweli usiopingika kuwa wengi wetu hatujui ni jinsi gani tujieleze kwa daktari ili tuweze kupata tiba sahihi na kwa wakati.

Pia kuna wakati tunashangazwa na baadhi ya maswali tunayoulizwa na daktari ambayo kuna muda yanaonekana kuwa hayana uhusiano na tatizo linalotusumbua.

Nimeona ni vyema nikaelezea ni taarifa zipi muhimu za kumuelezea daktari ili aweze kufikia hitimisho la kubashiri tatizo lako.

1: Tatizo Kuu(main complaint)

Hapa unatakiwa kumueleza daktari ni kipi kinakusumbua mpaka ukaamua kumuona.ni muhimu sana kueleza tatizo hili limechukua muda gani.

Mfano miaka kadhaa, miezi kadhaa, wiki kadhaa au siku kadhaa au limekuwa likijirudia mara kwa mara kwa muda flani.

Kwa mfano, kukohoa kwa zaidi ya wiki mbili kunaweza kusababishwa na kifua kikuu,kansa au ugonjwa wa moyo, kukohoa kwa wiki moja yaweza kuashiria ni homa ya mapafu, kukohoa kwa masaa kadhaa yaweza kuwa umepaliwa na chakula, kukohoa mara kwa mara yaweza kuwa ni pumu n.k

2: Historia ya tatizo

Hapa unatakiwa kueleza tatizo lako limeanza vipi, linatokea wakati gani(usiku, mchana au muda wote), linahusiana na nini mfano kukohoa na kutapika au tumbo kuuma na kuharisha.

Pia eleza kama tatizo lako linaongezeka au kupunguzwa na kitu flani, mfano unakohoa sana unapolala chali au moyo unakwenda mbio unaposimama lakini unapata afadhali unapochuchumaa au kiungulia kinapungua unapomeza vidonge vya magnesium n.k.

Kwa lugha fupi ya kitabibu maelezo ya ugonjwa wako yatafuata acronym ya DOPARA(Duration, Onset, Periodicity, Associating factors, Relieving or Aggreviating factors).

3: Historia ya afya yako kwa ujumla

Hapa unatakiwa kujieleza kwa ujumla kuhusu afya yako toka uzaliwe. Je umewahi kutibiwa kwa tatizo hilo hilo? Umewahi kulazwa hospitali kwa tatizo lolote, umewahi kufanyiwa upasuaji? Usiogope kutaja hata kama ulitibiwa kwa dawa za kienyeji.

Pia ni muhimu kueleza dawa au tiba zozote ulizowahi kupata miaka kadhaa nyuma au siku chache kabla ya kufika kwa daktari anayekuona mda huo.

Mfano tatizo lako kwa sasa ni mimba kutoka na hapo hapo ukawa na historia ya kutoa mimba kadhaa hapo ulipokuwa kigoli yaweza kuelezea kuwa shingo ya uzazi imelegea. N.k

Pia ni muhimu kumueleza daktari kuwa kuna baadhi ya dawa zinakuletea mzio(allergy)

4: Historia ya kifamilia

Kuna baadhi ya magonjwa yanasababishwa na lifestyle zetu na pia kuna baadhi ya magonjwa ni ya kurithi hivyo ni muhimu kueleza masuala ya kifamilia kwa ujumla.

Mfano babu, baba, mama au bibi walikuwa na tatizo flani kuna uwezekano na wewe ukawa nalo.

Mtoto anaweza kuwa na tatizo la utapiamlo kisa mama ni mfanyakazi wa TBC na hivyo hapati muda wa kumnyonyesha au mume ni dereva wa magari ya mizigo ya kwenda zambia na hivyo kamuambukiza mke wake UKIMWI n.k.

Haya ni baadhi ya maelezo muhimu yanayotakiwa kutolewa kwa daktari ili kufanikisha ugunduzi wa ugonjwa wa mteja
aliyefika kupata huduma.

Yanaweza kubadilika kidogo kulingana na mazingira ya mgonjwa au tatizo lakini huu ndio msingi wa kujieleza kwa daktari.


Baada ya kutoa maelezo haya daktari anatakiwa kukufanyia uchunguzi wa mwili(physical examnation) ili aweze kylinganisha na maelezo yako na baada ya hapo atakuandikia vipimo(investigations) ili kupata ugonjwa halisi unaokusumbua.

Kwa leo niishie hapa...

Aksanteni!

=============
Feb 2016: Nyongeza toka kwa mdau mwingine
 
Nitaendela kuongeza maelezo hapo juu kadri itakavyohitajika na pia nakaribisha wadau wa afya kutoa maoni yao ili kuboresha hayo niliyoyataja na kuyaelezea.
 
wanasema 70% ya diagnosis hutegemea maelezo ya mgonjwa.kabla ya vipimo ni lazima ujieleze au kuchukuliwa maelezo ya daktari ili kupata the right diagnosis.
 
wanasema 70% ya diagnosis hutegemea maelezo ya mgonjwa.kabla ya vipimo ni lazima ujieleze au kuchukuliwa maelezo ya daktari ili kupata the right diagnosis.

ni muhimu kwa mgonjwa kutambua haya niliyoeleza ili aweze kunga'amua kama huduma aliyopewa ni sahihi au la
 
Somo zuri sana. Asante kwa kutukumbusha. Kuna wamama wanapelekewa watoto clinic na mahausigelo. Msome hapa!
hapo kwenye bold umegusia jambo zuri sana.kuna wakati daktari anashindwa kupata taarifa muhimu kutokana na ukosefu wa muhusika sahihi.ingawa tiba yaweza kupatikana lakini tiba sahihi na endelevu inahitaji taarifa kamilifu.
 
Thanks for the lesson maana huwa mswahili kujieleza ni ishu bora utusaidie..
 
kuna baadhi yetu tunaogopa kujieleza kwa daktari kwa kuona kuwa siri zako zitajulikana.ukweli ni kwamba daktari au mtumishi wa afya hana ruhusa ya kutoa siri zako kwa mtu yoyote bila idhini yako.
Ni mazingira adimu sana yanamruhusu kufanya hivyo mfano pale vyombo vya sheria kama mahakama vikimtaka kufanya hivyo !

Pindi unapogundua siri zako zimepelekwa kwa asiyehusika bila ridhaa yako basi una haki ya kumshitaki daktari.
 
maelezo haya niliyoyatoa yanatumika duniani kote.uwe unatibiwa Tanzania au India!
 
Kuna watu ukiwauliza unafanya kazi gani wanadhani unataka kuwakamua/kuwafuatilia. Lengo ni kujua occupation ya mtu kwani kuna occupationa diseases. Pia strategy za matibabu hazilingani kulingana na uwezo wa mtu. Kuna mtu unatamani umwandikie dawa effective ila unaona hatamudu gharama zake hivyo inabidi umwandikie dawa zetu za siku zote.
 

nashukuru sana mdau kwa kuendelea kutoa elimu.there are so many misconception huko kwa wanajamii wa kawaida na kwa bahati mbaya hakuna wafafanuzi wa mambo na hatimaye watu hupotoshwa mno.
 
Naomba na mimi nichangie hii mada nzuri, mimi ninasema tatizo la kujieleza pia huwa linatokana na baadhi ya madaktari sio wote, kuwa harsh kwa mgonjwa inawezekana kutokana na muonekano wa mgonjwa au tabia ya kuzaliwa ya daktari.

Pili kuna baadhi ya wagonjwa huwaogopa madaktari (sijui sababu ni nini) na hivyo hushindwa kujieleza kwa ufasaha/usahihi.
 
Na madaktari wengine ukianza tu kuwaambia kichwa kinaniuma kabla hujamaliza hata kusema kichwa kinaniuma keshakuandikia ukapime choo, mkojo, marelia (a.k.a. damu) kha! utajieleza saa ngapi yaani unakuwa kama unampotezea muda? hii sijui imekaaje wallah!
 
Nashukuru sana kwa elimu hii. Naomba nichangie hapa kidogo. Unajua asilimia kubwa ya watanzania hawana elimu na walio na elimu hawatoi elimu yao waliyopata kwa jamii kwa mfano somo kama hili wanaofaidika ni wachache tu (wasomi). Naomba tutumie fursa hii kama wasomi kuwapa/kupeleka elimu hii tunayoipata kwa watu wengine(jamii). Asante sana
 

chezea governmet hospital, dokta anakimbizana na mda aende kwenye private yake, tuwe waungwana jamani
 
jana nipo dental care docta ananiulza kwnn cjang'oa meno ya utotoni?mi nmeshndwa kumuelewa coz m2 huwz ktoa jno liclouma
 

ni kweli mkuu!ni muhimu kufanya jambo au mambo kwa manufaa ya watu wa kawaida.
 
ushaur wako ni mzur mi mwenyewe nasumbuliwa na tatizo la kusikia miungurumo ndan ya masikio lakin cjapata tiba stahiki labada sababu ni kutojieleza vizur kwa daktar
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…