The Evil Genius
JF-Expert Member
- Mar 21, 2014
- 6,017
- 19,506
Bwana Elon Musk ambae alikua Tajiri namba 1 Duniani toka August 2021 hadi October 2022 na kisha kua tajiri namba 2 kwa muda wa miezi 4 hivi kutokana na kushuka kwa thamani ya hisa zake, sasa amerejea tena kileleni.
Elon Musk aambaeni muanzilishi na mmiliki wa makampuni kadhaa ikiwemo Tesla, Starlink, Space X, Boring Company, Twitter, Neuralink, na mtandao unaokua kwa kasi ya ajabu wa OpenAl ama ChatGPT na nyingine nyingi.
Hisa zake zilishuka baada ya kununua mtandao wa Twitter na wabaya wake wakawa wanamponda na kumshambulia baada ya yeye kusema ataibadilisha twitter kua mtandao wa haki kwa wote. Hii ilipelekea kampuni yake ya Tesla hisa zake kupoteza ama kushuka thamani kwa karibu 65%.
Kwa vile elon ni akili kubwa, akawaacha wabaya wake wakabwabwaja weee kisha akaamua kuwapiga na kitu kizito kichwani, akashusha bei ya magari ya Tesla, baada ya hapo hisa zimepanda kwa kasi ya ajabu na kupelekea Elon kurudi kwenye nafasi yake ya Tajiri namba 1 Duniani.
Natamani Elon aendelee kua tajiri namba moja Duniani kwa miaka mingi sana.
Elon Musk aambaeni muanzilishi na mmiliki wa makampuni kadhaa ikiwemo Tesla, Starlink, Space X, Boring Company, Twitter, Neuralink, na mtandao unaokua kwa kasi ya ajabu wa OpenAl ama ChatGPT na nyingine nyingi.
Hisa zake zilishuka baada ya kununua mtandao wa Twitter na wabaya wake wakawa wanamponda na kumshambulia baada ya yeye kusema ataibadilisha twitter kua mtandao wa haki kwa wote. Hii ilipelekea kampuni yake ya Tesla hisa zake kupoteza ama kushuka thamani kwa karibu 65%.
Kwa vile elon ni akili kubwa, akawaacha wabaya wake wakabwabwaja weee kisha akaamua kuwapiga na kitu kizito kichwani, akashusha bei ya magari ya Tesla, baada ya hapo hisa zimepanda kwa kasi ya ajabu na kupelekea Elon kurudi kwenye nafasi yake ya Tajiri namba 1 Duniani.
Natamani Elon aendelee kua tajiri namba moja Duniani kwa miaka mingi sana.