Elon Musk ashika tena namba moja kwa utajiri duniani

Elon Musk ashika tena namba moja kwa utajiri duniani

Sasa kumiliki mali zote hizo za nini hamna tija yoyote hawataishi milele watakufa na kuacha. Ni watu waovu na wachoyo wamejipatia hizo Mali kwa umwagaji damu na unyanyasaji tangu kipindi cha utumwa ukoloni hadi leo wanaendelea tu kwa ukoloni mambo leo kwa kuiba rasilimsli nakuleta vita kama Congo na CAR na kusababisha vifo vya wengi.
Ila akili zetu tunazijua wenyewe
 
Ni jambo la muda tu.

Kumbuka Elon ana makapuni kibao ambayo hayajaenda Public kama Space X, Starlink, Boring nk. Hayo yakienda Public Elon mpunga utamuua yule mbwa.
SpaceX na Starlink hayajaenda Public?! Huko "Public" ni wapi?

Otherwise unamaanisha hayo makampuni uliyoyataja ndio yanayofahamika na public na kuna mengine yasiyofahamika.
 
Elon na matajiri wenzake wote ni mapambo tu, matajiri wa kweli wapo nyuma ya paazia na hawawezi kujitokeza kwani utajiri wao unatisha.
Uongo[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Wakati huohuo huku Uswahilini tunazidi kulogana.
 
Ni jambo la muda tu.

Kumbuka Elon ana makapuni kibao ambayo hayajaenda Public kama Space X, Starlink, Boring nk. Hayo yakienda Public Elon mpunga utamuua yule mbwa.
Ina maana starlink na Space x hayapo kwenye NYSE ??
 
Ni kweli hizo ni familia, lakini kuna viongozi wa familia na wasimamizi wa mali zote. Na chimbuko la hizo mali limetokea kwa juhudi binafsi za waanzilishi wa hizo familia. Hao ndiyo matajiri wa kweli haijalishi ni familia au ukoo
Hata Elon miaka kadhaa mbele familia yake itakuwa moja ya familia tajiri zaidi Duniani.
 
SpaceX na Starlink hayajaenda Public?! Huko "Public" ni wapi?

Otherwise unamaanisha hayo makampuni uliyoyataja ndio yanayofahamika na public na kuna mengine yasiyofahamika.
Public maana yake ni kua yanauza hisa zake kwa umma ndio watu wa fedha wanasema kampuni haiuzi hisa zake kwa umma ama not listed in the public stock market.

Mfano, Kampuni ya Bakhressa ni kampuni binafsi ukienda Dar ea Salaam Stock Exchange huwezi kuikuta.

Mfano Tesla ni public maana watu wanamiliki hisa za Tesla.
 
Public maana yake ni kua yanauza hisa zake kwa umma ndio watu wa fedha wanasema kampuni haiuzi hisa zake kwa umma ama not listed in the public stock market.

Mfano, Kampuni ya Bakhressa ni kampuni binafsi ukienda Dar ea Salaam Stock Exchange huwezi kuikuta.

Mfano Tesla ni public maana watu wanamiliki hisa za Tesla.
Nimekupata.

Unazungumzia kampuni nyingi za Elon Musk kuwa Private [Limited] Companies badala ya Public (PLCs). Utambulisho wake ni tofauti kidogo kwa Marekani ukilinganisha na Tanzania.

Ila, issue ni kwamba, kupeleka kampuni public kuna changamoto zake ambazo zinaweza kuingilia ama kuathiri malengo ya mwenye kampuni hasa pale kampuni inapokuwa changa. Shareholders kutoka public mara nyingi huwa na mahitaji na malengo ya muda mfupi.
 
Hizo umetaja ni familia yani ukoo mzima mfano hao rothschild.

Hapa wanaongelea utajiri wa mtu mmoja mmoja.

Ukija list ya familia au koo tajiri ndo hao umetaja hapo
Kwani huyo Bernard huo ni Utajiri wake si wa Family yeye ni msimamizi kama alivyo Mo Dewj
 
Back
Top Bottom