Elon Musk kuleta Intaneti ni tishio kwa mitandao ya simu, atapora wateja wenye matumizi makubwa na kuteka soko sehemu ambazo network inasumbua

Nadhani kuna masafa (frequency) ambazo watatakiwa kupewa ili kuweza ku access eneo hilo, ila kwa wale wa mipakani nadhani ni possible ku access huduma hiyo kutoka nchi wanazopakana!
Hapana , waulize canal plus serikali inaipinga ila hivyo visimbuzi vipo vya kutosha na mpira tunaona ......unadhani madishi ya starlink tutashindwa kununua??
 
Swali je nape na timu yake Voda Airtel tigo halotel Simba net watakubali hii kitu jibu ni hapana.
If they can't compete, let them join, NI dhambi kuifunga tanzania kwa namna hiyo, huduma hii itakapokuwa inafika kila pahala hata mapoorini itasaidia ku guarantee watalii huko Mbugani, wataweza kufanya lives touring huku wakionekana marekani na kwingineko duniani, WARUHUSIWE TU.
 
Hii ni dunia ya tekinolojia, katika ulimwengu wa biashara, tunasema huu ni ushindani (competition) katika biashara. Kwa wanaoelewa, hii wanaichukulia kama changamoto (challenge), na sio tatizo. Na bila ushindani hatuwezi kupiga hatua katika ubinifu (innovation). Tunaweza kuona nchi kama Japan wanavyoshindana kwa tekinolojia katika mechanics na electronics. Hivyo, makampuni yetu, yajipange kushindana na sio kuogopa tekinolojia mpya inayoingia. Maendeleo duniani yameletwa na mabadiliko ya tekinolojia. Niliwahi kusikia kuwa train ya mwanzo ilikuwa inatumia makaa ya mawe, lakini leo inatumia ninj? Hence, we shouldin't be resistant to changes, but responsive to changes.
 
Hata kwenye simenti za dangote mlisema hivyo lakini haikushuka bei corruption is our great enemy tutabadilisha katiba na mitaala mashuleni na vyuoni lakini Kama tabia zetu na maalezi yetu hayatabadilika umaskini unakuja Kama jambazi
 
 
Si yeye Bali huku kwetu. Wanahitaji mambo kadhaa kutoka kwake kabla hawajamruhusu kuingia soko letu. Ila kama anavyotueleza mleta mada, kuna watu wanachelea maslahi yao yatazimwa kwa ujio huu.
Elon vibali kaomba Tanzania toka mwishoni mwa mwaka jana, anaambia habari za operational standards.

Rwanda wamechangamkia dili, wamempa licence tayari.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…