Elon Musk kuleta Intaneti ni tishio kwa mitandao ya simu, atapora wateja wenye matumizi makubwa na kuteka soko sehemu ambazo network inasumbua

Elon Musk kuleta Intaneti ni tishio kwa mitandao ya simu, atapora wateja wenye matumizi makubwa na kuteka soko sehemu ambazo network inasumbua

Elon vibali kaomba Tanzania toka mwishoni mwa mwaka jana, anaambia habari za operational standards.

Rwanda wamechangamkia dili, wamempa licence tayari.
Inashangaza sana. Hivi ni standard gani hizo ambazo wanaona jamaa hana?
 
View attachment 2514852

Bei ya vifaa vyote na kuwekewa ni shilingi laki 9.

kifurushi kinadumu kwa mwezi, nadhani anapanga bei kwa kuangalia uchumi wa nchi, Marekani ni 230,000/= , Nigeria ni 98,000, Hapa Kwetu si ajabu ikawa 70,000.

Ni internet ya kisasa, Speed yake ni kubwa sana, unaweza kushusha file la gb 1 speed ikiwa chini dakika 3 na speed ikiwa poa ni sekunde 50 tu, kwenye kuperuzi ni kugusa tu hakuna kusubiri, kucheki video ama video call hakuna mambo ya kuganda ganda.

Haina kikomo, ukitumia hata gb 20 kwa siku ni wewe.

Inaweza kupatikana mpaka mbugani, milimani, kwenye makorongo na sehemu remote ambazo mitandao ya simu haijaweza kufikia, Ni kama vile dstv.
.....................................................................................

ujio wake unaweza kupora wateja wengi wenye matumizi makubwa, hii ni hatari kwa makampuni ya simu na kama mjuavyo kuna watu wana hisa zao huko. Mbaya zaidi kifaa kimoja kinaweza kutumika hata kwa watu 50 kwa mpigo maana speed ni kubwa hata ikigawanywa, ni hatari ukizaliwa utamaduni wa watu kujichanga huku wakiacha kununua mabando,

Kwa kuwa internet ni ya Satelite hapa itaweza kufika hadi maporini na vijijini ambako maeneo hayo mengi internet huwa ni changamoto, hii itakuwa changamoto kwa mitandao ya simu hasa katika miji inayokuwa wakitaka kuweka minara watakuta tayari watu wameshazoea starlink.
..............................................................................

HITIMISHO

Kwa hali hii nadhani naanza kuelewa kwanini vibali vinacheleweshwa, sitashangaa njia ya kumuondosha ikiwa ni tozo nzito sana zitazofanya hata kifurushi kuwa bei sawa na mitandao ya simu, dana dana za kusaini documents kila uchwao au tukaja sikia kisingizio kwamba huduma inaharibu mazingira, ni hatari kwa usalama, n.k.
Kuna figisu nyingi sana zimeshaanza kuletwa na Vodacom Tanzania pamoja na Tigo

Hii nchi ina kampuni zenye kiburi sana
 
Napataje GB za bure kwa Tigo,Airtel au vodacom??
Njoo DM unifundishe.
 
Serikali ya mafisadi watakuja kusema
1) Hajatimiza vigezo na masharti
2) Ni hatari kwa usalama wa taifa
3) Ametumwa na mabeberu atuchunguze
 
Kuna figisu nyingi saba zimeshaanza kuletwa na Vodacom Tanzania pamoja na Tigo

Hii nchi ina kampuni zenye kiburi sana
Hizi kampuni hazina Huruma na mtanzania mnyonge, mbona Rwanda makampuni yapo na starlink yupo?, same to Mozambique?
 
Hivi unadhani kwanini Bei ya Bundle ni Gharama ? Jibu ni Serikali na TCRA kupenda mapato kwahio hata Starlink wasipokuja TCRA ikawaachia hawa mabwana wacheze na bei wanavyotaka Bei zitashuka (sababu bei zilikuwa chini kabla ya hao madubwana kuna na Bei Elekezi)

 
Back
Top Bottom