martial jb
JF-Expert Member
- Oct 21, 2021
- 863
- 1,462
Habari JF
Huyu ni mtu na nusu, Yeah! Unaweza kusema hivyo. Elon Reeve Musk mapema wiki hii ameteka vichwa vya habari duniani baada ya kununua mtandao pendwa duniani( Twitter ) kwa dau la $44B, sawa na Trilioni 102.6 kwa pesa za kibongo.
Bilionea huyo namba moja duniani kutokana na takwimu za Forbes na Bloomberg, anakadiriwa kuwa na utajiri (net worth) wa $244B. Hii ina maana dili hilo la ununuzi wa Twitter limekunja takribani asilimia 18 ya utajiri wa Musk.
Elon hana shida na wala hafikirii jambo lolote baya kwenye ununuzi wake wa mtandao huo, kwani alishawahi sema kwenye moja ya kurasa zake za Twitter kuwa kumiliki mtandao huo ni moja kati ya ndoto zake, hivyo anaonekana yuko tayari kuingia costs zozote ili kuiishi ndoto yake.
Elon ni nani?
Kwa kifupi Elon Musk ni raia wa nchi tatu (Marekani, Canada na South Africa). Ameoa mara mbili na kuachika na ni baba wa watoto kumi pia. Ni mmiliki wa makampuni mbalimbali kama Tesla, PayPal, Space X nk.
Kwenye ukuaji wake Elon alipitia vipindi mbalimbali vigumu ikiwemo wazazi wake kutalikiana na hali ngumu ya kimaisha iliyokuwa ikiwakumba. Alianza ujasiriamali katika umri mdogo akishirikiana na kaka yake kwa kuuza bidhaa mbalimbali na kupitisha majumbani.
Alizaliwa South Africa kabla ya baadae kuhamia Canada kwa masomo ya chuo. Licha ya pia kufeli kuendelea na masomo hayo ya chuoni (discontinued). Baada ya kuwa drop out chuoni Elon aliamua kujikita zaidi kwenye biashara huku akipewa ushirikiano mkubwa na mkewe, na kwa shida na tabu Elon Musk alipambania kampuni zake zote mpaka kufikia hapo zilipo.
Mengine
Elon ni muumini mkubwa wa matumizi ya bangi, Na ni bilionea pekee alieweza kukuza utajiri wake kutoka $1B mpaka $244B ndani ya kipindi cha miaka 10.
Huyu ni mtu na nusu, Yeah! Unaweza kusema hivyo. Elon Reeve Musk mapema wiki hii ameteka vichwa vya habari duniani baada ya kununua mtandao pendwa duniani( Twitter ) kwa dau la $44B, sawa na Trilioni 102.6 kwa pesa za kibongo.
Bilionea huyo namba moja duniani kutokana na takwimu za Forbes na Bloomberg, anakadiriwa kuwa na utajiri (net worth) wa $244B. Hii ina maana dili hilo la ununuzi wa Twitter limekunja takribani asilimia 18 ya utajiri wa Musk.
Elon hana shida na wala hafikirii jambo lolote baya kwenye ununuzi wake wa mtandao huo, kwani alishawahi sema kwenye moja ya kurasa zake za Twitter kuwa kumiliki mtandao huo ni moja kati ya ndoto zake, hivyo anaonekana yuko tayari kuingia costs zozote ili kuiishi ndoto yake.
Elon ni nani?
Kwa kifupi Elon Musk ni raia wa nchi tatu (Marekani, Canada na South Africa). Ameoa mara mbili na kuachika na ni baba wa watoto kumi pia. Ni mmiliki wa makampuni mbalimbali kama Tesla, PayPal, Space X nk.
Kwenye ukuaji wake Elon alipitia vipindi mbalimbali vigumu ikiwemo wazazi wake kutalikiana na hali ngumu ya kimaisha iliyokuwa ikiwakumba. Alianza ujasiriamali katika umri mdogo akishirikiana na kaka yake kwa kuuza bidhaa mbalimbali na kupitisha majumbani.
Alizaliwa South Africa kabla ya baadae kuhamia Canada kwa masomo ya chuo. Licha ya pia kufeli kuendelea na masomo hayo ya chuoni (discontinued). Baada ya kuwa drop out chuoni Elon aliamua kujikita zaidi kwenye biashara huku akipewa ushirikiano mkubwa na mkewe, na kwa shida na tabu Elon Musk alipambania kampuni zake zote mpaka kufikia hapo zilipo.
Mengine
Elon ni muumini mkubwa wa matumizi ya bangi, Na ni bilionea pekee alieweza kukuza utajiri wake kutoka $1B mpaka $244B ndani ya kipindi cha miaka 10.