Emirates yagoma kuiwekea vikwazo Urusi, safari za ndege zinaendelea kama kawaida

Emirates yagoma kuiwekea vikwazo Urusi, safari za ndege zinaendelea kama kawaida

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Emirates.jpg

Rais wa Emirates, Sir Tim Clarke amekataa kufuata agizo la Nchi za Ulaya kuiwekea vikwazo Urusi kwa kusitisha ndege kwenda Nchini humo, akisema hayo maamuzi yanatakiwa kufanywa na Serikali ya United Arab Emirates (UAE)

"Kama tukiambiwa kusimamisha safari tutafanya hivyo, lakini kwa sasa kila kitu kinaendelea kama kawaida," - Sir Tim Clarke.

Makampuni mengi makubwa ya ndege yalisitisha safari zao kwenda Urusi baada ya taifa hilo kuwekewa vikwazo kwa kuivama Ukraine kijeshi.

Ndege za Emirates ni kati ya chache ambazo bado zinaendelea na safari kuelekea Moscow na St Petersburg.

Sir Tim ameongeza kuwa inatakiwa kufahamika watu wa Urusi wao siyo wahusika wakuu na maamuzi ya vita ya Ukraine.

Source: BBC
 
Wakati wa Corona mashirika mengi ya ndege yalikaribia kufilisika. Kwa Emirates huu ni wakati wake wa kuziba makovu.Japo nina wasi wasi kuwa msimamo huo huenda usiendelee kwani UAE ni miongoni mwa vibaraka wakubwa wa washirika wa NATO.
Hilo ndio tatizo la vita vinavyomuingiza Marekani.Lazima avute na watu wengine wamsaidie kwenye vita vyake.Mbona Urusi halazimishi watu kupigana naye ijapokuwa wanaojiunga kwake kwa hiyari zao anawapokea.
 
Ni kweli hata mimi nakubaliana na Ofsa hapo

Sioni sababu ya kuwawekea vikwazo Urusi wakati waathirika wengi ni wananchi ambao hata wao tunawaona wana protest kupinga uvamizi wa Raisi wao

Kuendelea kuwaminya hawa ni kuzidi kuchochea uadui kwasababu mwisho wa siku wakijikuta Dunia nzima imewatenga hawatakuwa na option zaidi ya kuungana na Raisi wao na kuweka chuki kwa mataifa mengine.
 
Hao Fly Emirates wakumbuke kwamba the west can ban them from their airspace wakati wanaenda au kotoka Russia.
 
Hao Fly Emirates wakumbuke kwamba the west can ban them from their airspace wakati wanaenda au kotoka Russia.
Yaani inaonekana umeumia hadi kijambio ulivyosikia Emarati wataendelea kwenda Urusi, hao mabeberu hawana huo ubavu wakufunga anga maana india, china, Brazil bado wanafanya safari zao kwenda Urusi kama kawa.

umeelemewa na ufinyu mdogo wa uelewa kuhusu dunia hapo ulipo unaamini US/NATO wanaweza kufunga anga lolote duniani kitu ambacho hakipo hebu fikiria hapo ukraine kwa rafiki yao wameshindwa kufunga anga lake na Urusi anaendelea kugawa dose.
 
poor reasoning , kwan watu wa ukraine ni wahusika wa maamuz ya vita ?
 
Wakati wa Corona mashirika mengi ya ndege yalikaribia kufilisika. Kwa Emirates huu ni wakati wake wa kuziba makovu.Japo nina wasi wasi kuwa msimamo huo huenda usiendelee kwani UAE ni miongoni mwa vibaraka wakubwa wa washirika wa NATO...
ushawai kaa upande wa mwizi?
 
Ni kweli hata mimi nakubaliana na Ofsa hapo

Sioni sababu ya kuwawekea vikwazo Urusi wakati waathirika wengi ni wananchi ambao hata wao tunawaona wana protest kupinga uvamizi wa Raisi wao

Kuendelea kuwaminya hawa ni kuzidi kuchochea uadui kwasababu mwisho wa siku wakijikuta Dunia nzima imewatenga hawatakuwa na option zaidi ya kuungana na Raisi wao na kuweka chuki kwa mataifa mengine.
fikiria tena , weak point
 
Watu washachoshwa na US kuwaingiza kwenye ugomvi wake ndio maana middle East akina Saudia na Emirates this time huwasikii wakiunga mkono.
Yeye akigimbana na mtu anataka uwe ugomvi wenu nyote.
kwan kavamiwa USA ? ttzo la team Putin linaanzia hapo , akili zote zipo kwa USA
 
Yaani inaonekana umeumia hadi kijambio ulivyosikia Emarati wataendelea kwenda Urusi, hao mabeberu hawana huo ubavu wakufunga anga maana india...
Mamb ni pole pole , Ghadaf walitoka nae 1980s ila 2011 akaangushwa , subir next election utacheka
 
URUSI wenyewe wamefunga baadhi ya viwanja vyake vya ndege kwa sababu za usalama, hao EMIRATE wanasuburi mpaka wadunguliwe ndiyo wajue kuwa RUSSIA hapafai.
Waache kwanza, kuna kitu ndege ya abiria ilitunguliwa hapo crimea
 
Back
Top Bottom