Emirates yagoma kuiwekea vikwazo Urusi, safari za ndege zinaendelea kama kawaida

Emirates yagoma kuiwekea vikwazo Urusi, safari za ndege zinaendelea kama kawaida

Rais wa Emirates, Sir Tim Clarke amekataa kufuata agizo la Nchi za Ulaya kuiwekea vikwazo Urusi kwa kusitisha ndege kwenda Nchini humo, akisema hayo maamuzi yanatakiwa kufanywa na Serikali ya United Arab Emirates (UAE)

"Kama tukiambiwa kusimamisha safari tutafanya hivyo, lakini kwa sasa kila kitu kinaendelea kama kawaida," - Sir Tim Clarke.

Makampuni mengi makubwa ya ndege yalisitisha safari zao kwenda Urusi baada ya taifa hilo kuwekewa vikwazo kwa kuivama Ukraine kijeshi.

Ndege za Emirates ni kati ya chache ambazo bado zinaendelea na safari kuelekea Moscow na St Petersburg.

Sir Tim ameongeza kuwa inatakiwa kufahamika watu wa Urusi wao siyo wahusika wakuu na maamuzi ya vita ya Ukraine.

View attachment 2191982

Source: BBC
Saaafi wapige pesa
 
Yaani inaonekana umeumia hadi kijambio ulivyosikia Emarati wataendelea kwenda Urusi, hao mabeberu hawana huo ubavu wakufunga anga maana india, china, Brazil bado wanafanya safari zao kwenda Urusi kama kawa, umeelemewa na ufinyu mdogo wa uelewa kuhusu dunia hapo ulipo unaamini US/NATO wanaweza kufunga anga lolote duniani kitu ambacho hakipo hebu fikiria hapo ukraine kwa rafiki yao wameshindwa kufunga anga lake na Urusi anaendelea kugawa dose.
Kwa kawaida waga siwajibu slowpokes kama wewe lakini sitavumilia huu ujinga, NATO wanaweza funga anga zao kwa ndege za Emirates zinazo toka au kwenda urussi. In fact juzi wanadiplomasia wa urussi walibidi kusafiri nusu dunia kuelekea nyumbani kutoka uhispania ili kuavoid airspace ya NATO. Sasa ulivyokua mjinga unadhani Ukraine ni sawa na Marekani au EU au NATO
 
Inawezekana hata baadhi ya nchi za ulaya zinataka kushirikiana na Russia ila tatizo ni US, yaani yy akisema fulani adui yangu basi EU wote inabidi mfuate.
 
Rais
poor reasoning , kwan watu wa ukraine ni wahusika wa maamuz ya vita ?

Raisi wa urusi analitambua hili na ndio maana kabla hajapiga sehemu anatoa tahadhari ya wananchi kuondoka.
 
Ni kweli hata mimi nakubaliana na Ofsa hapo

Sioni sababu ya kuwawekea vikwazo Urusi wakati waathirika wengi ni wananchi ambao hata wao tunawaona wana protest kupinga uvamizi wa Raisi wao

Kuendelea kuwaminya hawa ni kuzidi kuchochea uadui kwasababu mwisho wa siku wakijikuta Dunia nzima imewatenga hawatakuwa na option zaidi ya kuungana na Raisi wao na kuweka chuki kwa mataifa mengine.
Idea ni wananchi wachoke mpaka wamnunie kiongozi wao na kuanzisha rebellion.

Kama watachoka na wataona suluhisho ni kushikamana na Rais basi kitakachotokea itakua ni kinyume cha matarajio ya vikwazo.

Binafsi naona huyu kiongozi wa Emirates anachofanya ni ule mchezo wa bad cop good cop kuwafanya warusi waone kumbe kuna watu bado wanawapambania so wampinge Putin while there is still time.
 
Usilazimishe adui yako wewe awe adui wa wote

Chukulia mahusiano ya kenya na tz yakavurugika, sasa ikawa ni mwendo wa kukomoana. We unayo nguvu ya kumshinikiza marekani amuwekee vikwazo mkenya?
Ngumu kumezaaah hiii!
 
URUSI wenyewe wamefunga baadhi ya viwanja vyake vya ndege kwa sababu za usalama, hao EMIRATE wanasuburi mpaka wadunguliwe ndiyo wajue kuwa RUSSIA hapafai.
Safari za ndege zinapangwa kitaalamu sana.Ndege kinachokwepa ni kupita juu ya anga la Ukraine tu.Njia za kuingia Urusi na kutoka zi tele.Hakuna anayeweza kuazimia kuidungua ndege yoyote ile kwenye njia za salama.Hata mimi kuna siku nilisafiri takriban masaa 17 angani mpaka miguu ikavimba kukwepa anga ya Saudia wakati wa ugomvi wao na Qattar.Nilitalii mataifa kadhaa ya Ulaya kupitia dirisha la ndege na camera mbele yangu nikafika mpaka Urusi kabla kutua Doha.Nilikuwa natoka Ulaya kuja kwetu,
 
NATO wanatia huruma !! Putin 10,NATO 1. Mpaka hapo US na NATO wanatakiwa kujua dunia ya Sasa Ina wanadamu welevu na wenye uwezo wa kujua hiki ni sawa na hiki ni hila .inshort dunia imewakataa !!
 
hivi shirika letu ATCL likiwnzisha Safari Dubai -russia ,si tutapiga pesa ndefu!!maana wenzetu Emirates wamekomaa wameona abiria wako kibao
 
Watu washachoshwa na US kuwaingiza kwenye ugomvi wake ndio maana middle East akina Saudia na Emirates this time huwasikii wakiunga mkono.
Yeye akigimbana na mtu anataka uwe ugomvi wenu nyote.
Unajua mtu anayekuhongahonga mara kwa mara, anategemea favour kutoka kwako wakati fulani..

Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
 
Idea ni wananchi wachoke mpaka wamnunie kiongozi wao na kuanzisha rebellion.

Kama watachoka na wataona suluhisho ni kushikamana na Rais basi kitakachotokea itakua ni kinyume cha matarajio ya vikwazo.

Binafsi naona huyu kiongozi wa Emirates anachofanya ni ule mchezo wa bad cop good cop kuwafanya warusi waone kumbe kuna watu bado wanawapambania so wampinge Putin while there is still time.
Hakuna taifa/taasisi inapambania taifa jingine..
Emirates wanapambania maslahi yao(biashara)..
USA nao hivyo hivyo,wapo kwenye huu mgogoro kimaslahi zaidi..
Emirates akiminywa aana, mwishowe anaweza sitisha hizo safari,USA na Washirika wake nao ikitokea huko mbeleni huu wasione manufaa yoyote kwao wataacha tu Urusi afanye anavyotaka.
Kwa ufupi,utu sio jambo la kwanza kwa pande zote mbili

Sent from my SM-A405FN using JamiiForums mobile app
 
Kwani vikwazo vinawekwa na nani? Kila mtu afanye anachoona sio kulazimisha mataifa yaendane na wao. Emirates kanyaga twende
Eti kanyaga twende,na akizuiwa safari zake kwenda US atafanyaje?Sote tunajua wateja wengi wako hizo Nchi na si Russia.Ni swala la muda tu atabow down kama wengine.
 
URUSI wenyewe wamefunga baadhi ya viwanja vyake vya ndege kwa sababu za usalama, hao EMIRATE wanasuburi mpaka wadunguliwe ndiyo wajue kuwa RUSSIA hapafai.
Ndege za China za kwenda Ulaya bado zinatumia Anga ka Urusi, tafuta maarifa wacha kuwa mnafiki
 
Wakati wa Corona mashirika mengi ya ndege yalikaribia kufilisika. Kwa Emirates huu ni wakati wake wa kuziba makovu.Japo nina wasi wasi kuwa msimamo huo huenda usiendelee kwani UAE ni miongoni mwa vibaraka wakubwa wa washirika wa NATO.
Hilo ndio tatizo la vita vinavyomuingiza Marekani.Lazima avute na watu wengine wamsaidie kwenye vita vyake.Mbona Urusi halazimishi watu kupigana naye ijapokuwa wanaojiunga kwake kwa hiyari zao anawapokea.
Mbona unashindwa kutumia Akili?

Hivi unafikili Urusi atamlazimisha Nani ambaye Hana Maslahi Urusi ili aungane naye?

1.Ukiona nchi imeungana na Urusi kwenye huu mgogoro Basi ujue ana Maslahi makubwa ya Kiuchumi na Kiusalama na Urusi. Mfano Ni ERITERIA,NORTH KOREA,SYRIA,MALI,n.K

2.Ukiona nchi Iko Neutral kwenye huu mgogoro Basi ujue Ina Maslahi Sawa ya Kiuchumi na Kiusalama Kati ya Upande wa Marekani na Urusi. Mfano Ni China. China ina Maslahi makubwa ya Kiuchumi na Marekani huku ikiwa na Maslahi makubwa ya Kiusalama na Nchi ya Urusi. Nchi zingine Ni India na Iran.

3.Ukiona Nchi iko upande wa Marekani(Ukraine) kwenye huu mgogoro ujue Ina Maslahi makubwa ya Kiuchumi na Kiusalama na Marekani kuliko Urusi.

Kwahiyo Mzee Hakuna Nchi inayolazimishwa kwenye huu mgogoro,kila Nchi inaangalia Maslahi yake. Ukiona Mataifa mengi yako upande wa Marekani kwenye huu Mgogoro Basi ujue hazina jinsi Bali zinalazimishwa na Maslahi.

Sent from my TECNO BA2 using JamiiForums mobile app
 
Mamb ni pole pole , Ghadaf walitoka nae 1980s ila 2011 akaangushwa , subir next election utacheka
Labda umesahau kuwa waliinfluence hadi Trump akawa rais...
Russia sio Iraq wewe
Kaulize nani alimuua Kennedy
 
Back
Top Bottom