Endeleeni na mazoezi ya wazi Bunju/Boko, endeleeni na uzungu wenu

Endeleeni na mazoezi ya wazi Bunju/Boko, endeleeni na uzungu wenu

Duh popoma jamaa unajua mengi sana wycliff keto nilimuona akicheza AfC arusha nikiwa dogo kumbe we braza yangu , SAid Tully sijawahi mwelewega kabisa na kwa jinsi uzungu ulivyo wa kutosha pale simba

mwaka huu huyo Barbara watamuharibia left and right maana kwa mwendo huu wa kukataa kushikilia baadhi ya mambo yetu ya "kiswahili" tuwaachie tu utopolo ubingwa wao, wao wame stick na uswahili wao wakiweka pia na huo "uzungu"
Unachopaswa kuelewa Simba na Yanga mmiliki wake ni mmoja, kwahiyo hakuna shida yoyote ukimuona mtu wa Simba yupo Yanga au wa Yanga yupo Simba.

Walioanzisha Sunderland walinyang'anywa timu kitambo na walikuwa Waarabu timu ikakabidhiziwa kina Abunuwasi.

Simba ni jina la kawawa, mambo mazito kama haya huwezi kuyapata kutoka kwa huyo taahira Genta.

Siku utakayosikia Simba inaitwa Simba FC au Yanga FC njoo unidai pesa. Hizo siyo club za football.

Jengo la Simba mtaa wa Msimbazi limejengwa na Karume na jengo la Yanga Jangwani limejengwa na Karume, ndio Yanga wakatoka jengo la mtaa wa Mafia na kuhamia Jangwani.

Huyo Genta ni kinda wa juzi hawezi kuyajuwa haya.
 
Kwa Kukusaidia tu ni kwamba nimesoma nae Said Tully Shighatini Secondary School ( 1993 mpaka 1994 ) kabla sijahama kwenda Kusoma nchi Jirani ya Uganda.

Tukiwa hapo Shighatini Secondary School wakati huo Mwalimu Mkuu wetu akiwa ni Marehemu Thomas Kavuye ( TK ) na Mwalimu wa Michezo akiwa ni Marehemu Mwalimu Maina kila tukicheza Mechi za Simba SC na Yanga SC huyu Said Tully wenu alikuwa si tu ni Mchezaji wa Team Yanga pale Shighatini Secondary School bali pia alikuwa ndiyo Nahodha wao.

Achilia mbali huko pia baada ya kuwa Marafiki na Said Tully kutokea Shuleni hapo Shighatini Secondary School pia nilikuja kuwa nae karibu Kimpira baada ya kuwa tunacheza Wote Ligi za Dar es Salaam na Yeye Timu yake ikiwa ni ya hapo Kwao katika hizo Flats za NHC zinazotazamana na Fire njia panda ya kuelekea Muhimbili Hospitali.

Na nyumba aliyokuwa akiishi Said Tully ilikuwa ikitizama na nyumba ya Kocha wake aliyemkuza Boniface Mkwasa ( Yanga SC Mwenzake ) na Mkwasa ndiyo alikuwa muda wote akienda nae pale Jangwani Kaunda ( Yanga Kids ) na Kumfundisha Soka na pia kumfanya azidi Kuipenda Yanga SC.

Siku nilipomuona na kusikia kuwa Said Tully kaibukia Simba SC tena hadi kupewa Cheo cha Ujumbe na kuwa karibu na Simba SC hasa kwa mambo ya ndani nilishtuka na Kuumia mno na nakumbuka nilionya hata hapa JamiiiForums ila kama Kawaida Watu wanapenda sana Kunichukia 'poa' GENTAMYCINE ila wangejua nina Tunu ( Shani ) gani kutoka Kwake Mwenyezi Mungu wangenishukuru.

Kuna Siku Mimi na Watu wangu Watatu tuliosoma nae Said Tully Shighatini Secondary School Peter ( yuko TBL Ofisi za Ubungo ), Hemed ( yuko TRA Makao Makuu ) na Mchezaji mwenzetu Shighatini Secondary School na baadae akaja Kuchezea Simba SC Wycliff Keto tulikutana naa ( Said Tully ) na Kumhoji na Jibu alilotupa ni kwamba 'tuuchune' kwani nae ana Familia tukabaki Kucheka tu na 'Kuuchuna' Kweli.

Said Tully ni Yanga SC tena 200% zote.
Mkuu umemaliza......huyu kijana ni mamluki hasa
 
Back
Top Bottom