Eneo la chini ya kitovu kuvuta

Eneo la chini ya kitovu kuvuta

Lyandembela1

JF-Expert Member
Joined
May 10, 2013
Posts
277
Reaction score
113
Heshima mbele wakuu na madaktari wote pande hizo.

Huyu ni msichana wa umri wa miaka 28 analalamika kuwa chini ya kitovu panavuta, Wiki moja imepita trh 03/08 alikwenda Muhimbili hosipitali wakampima vipimo vyote, ULTRA SOUND, X-RAY pamoja na full blood picture kulingana na maelezo yake. lakini mwishoe daktari alisema hana atizo lolote zaidi ya vidonda vya tumbo. Na akapewa dawa za kutumia kwa siku tano.

Sasa anasema lile tatizo limeanza kujirudia tena afanyaje ndugu zangu wataalamu, au tatizo litakuwa zaidi ya hilo la ULCERS?

Tafadhali msaada wenu, usiku hapalaliki jamani. full kujinyongorota.

CC: Dr MziziMkavu Dr Preta
 
Last edited by a moderator:
Wamempima na hawakuoan kitu sas hao ma-Daktari wanakisia kuwa ana vidonda vya tumbo na wamempa dawa bado hajapona? Je wamempima kujuwa kama ana vidonda vya tumbo? au ndio wanakisia tu? muulize je amesha wahi kuzaa? isije kuwa ni chango la uzazi. Mwambie akiumwa tena arambe kijiko kimoja cha Asali ikiwa bado arambe tena asali kijiko kimoja kesho yake aende kupima hivyo vidonda vya tumbo kisha uje hapa utupe feedback.cc.@Lyandembela1
 
lakini mwishoe daktari alisema hana tatizo lolote zaidi ya vidonda vya tumbo.

Labda kiswahili changu hakijaeleweka, Baada ya kupima Dakitari kasema anasumbuliwa na vidonda vya tumbo. Na pia hajawahi kuzaa. Linawezekana hilo la chango la uzazi.
Niatmshauri akapime tena Dr MziziMkavu. Na kama nu swala la uzazi tufanye mchakato inawezekana kaka ila tunasubili wakati ndo uzungumze si unajua taratibu za kiafrika. Nipo kwenye mchakato.

Aksante kwa ushauri wako.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom