KERO Eneo la Ilala Sokoni karibu na Ofisi ya RC na DC hali ni mbaya, maji ya kinyesi yanatiririka eneo la kufanyia biashara

KERO Eneo la Ilala Sokoni karibu na Ofisi ya RC na DC hali ni mbaya, maji ya kinyesi yanatiririka eneo la kufanyia biashara

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

BigTall

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2022
Posts
525
Reaction score
1,257
photo_2024-12-11_13-35-04.jpg

photo_2024-12-11_13-35-20.jpg
Kipande cha barabara inayopita kwenye Soko la Ilala Boma Jijini Dar es Salaam, Mtaa wa Tabora hakipitiki kipo kwenye hali mbaya kutokana na kuwa na mashimo makubwa huku maji huku pia majitaka kwenye mashimo hayo.

Lakini katika hali ya kushangaza katika eneo hilo biashara ya vyakula hususani matunda inaendelea ikiwa majitaka ya chemba inayopita maeneo ya karibu.

Wafanyabiashara hususani wa magenge ufika eneo hilo kila siku kuchukua bidhaa mbalimbali ikiwemo nyanya, karoti, nyanya chungu na matunda, lakini kwa hali inavyoendelea naona afya za Wananchi zikiwa hatarini kutoka na bidhaa kupangwa kwenye maeneo machafu huku magari yanayopita maeneo hayo yakiwa yanatimua hayo maji kutokana na barabara kujaa mashimo.

Licha ya changamoto za kiafya njia hiyo ni kero kwa watumiaji wa magari hususani daladala ambazo zinapita kwenye njia hiyo, ambapo mashimo hayo yanaleta foleni pamoja na kupelekea magari kuaribika kutokana na ubovu wa kipande hicho cha daladala.

Nashangaa kwanini mamlaka hazichukui hatua za haraka kuiweka barabara hiyo katika mazingira rafiki pamoja na kuondoa kero ya majitaka yanoyotokea kwenye chemba hasa kipindi mvua zikinyesha.

Rai yangu kwa mamlaka ikiwemo Mkuu wa Mkoa na Mkuu wa Wilaya ambao wapo karibu na eneo hilo wafuatilie changamoto hiyo na kuipatia ufumbuzi wa haraka.
photo_2024-12-11_13-35-01.jpg

photo_2024-12-11_13-34-45.jpg

photo_2024-12-11_13-34-30.jpg

photo_2024-12-11_13-34-18.jpg
 
hii mpaka utokee mlipuko wa kipindupindu ndiyo wanaweza kuona umuhimu wa kushughulikia.
Mwisho wa siku,tutaenda kumpigia goti Mungu atusaidie.Tunapendaga utani sana. Sasa nawazaga magonjwa ya mlipuko yanayoipiga Congo,siku yakivuka mipaka si itakuwa shida.
 
Hivi hakuna tender watu wanalipwa ili kufanya hizi kazi sababu hapo kale kulikuwa hakuna hizi kero za kila ofisi kudaiwa sijui pesa ya taka tena gharama kuna sehemu wanatoa hata zaidi ya kodi ya chumba...

Hii nchi imekuwa shida yaani watu badala ya kupata kazi na kuhudumia wananchi wamekuwa wanahudumia matumbo yao... Uchafu zaidi haupo kwenye mazingira (uchafu unaoonekana) bali ni utendaji ulaji, umimi, rushwa na kukosa uzalendo...

Alafu tunasema tumeendelea na tunawacheka babu zetu waliokuwa vijijini wanaishi sustainably... (kama ni maendeleo labda tunaendelea kurudi nyuma siku baada ya siku)
 
Back
Top Bottom