KERO Eneo la Tegeta - Kwa ndevu uchafu unarundikwa eneo la barabara kama dampo, wasimamizi wako wapi?

KERO Eneo la Tegeta - Kwa ndevu uchafu unarundikwa eneo la barabara kama dampo, wasimamizi wako wapi?

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
photo_2025-01-17_07-56-25.jpg

photo_2025-01-17_07-56-28 (2).jpg

Katika eneo la Tegeta kwa Ndevu wahusika wanaosimamia suala la kuzoa taka wanatakiwa kuwajibika kwa uzembe ambao wamekuwa wakiruhusu utokee kwa kubariki Wafanyabiashara wa soko lisilo rasmi lililopo pembezoni mwa Kituo cha Daladala kurundika uchafu kwenye eneo la barabara huku uchafu huo wakati mwingine ukikaa hadi zaidi ya siku tatu.

Uchafu huo unakusanywa kama dampo maeneo yanayozunguka sehemu walipo Wafanyabiashara kwa lengo la wahusika kuja kuubeba, lakini kinachosikitisha unarudikwa eneo ambalo linatumika kwa matumizi ya vyombo vya moto huku ukihatarisha usalama wa afya za Wananchi hususani kupindi hiki ambacho mlipuko wa kipindupindu umekuwa ukitajwa kuwepo kwa baadhi ya maeneo.

Licha hivyo uchafu huo ambao umekuwa ukitundikwa kwenye maeneo ya barabara, imekuwa sehemu ya vyanzo vinavyosababisha uwepo wa foleni wakati magari ya taka yanaposimamishwa kupakia uchafu huo eneo la barabara hasa majira ya asubuhi au jioni

Nitoe wito wangu kwa mamlaka zinazosimamia usafi wa mazingira Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kuwajibika ipasavyo ikiwemo kuweka miundombinu rafiki kwa wafanyabiashara wa eneo hilo kwa ajili ya kumwaga taka badala ya utaratibu wa sasa wa kuzirundika katika eneo la barabara huku zikibaki kuzagaa na kuleta kero zaidi.

Ni vyema kuzingatia suala la usalama wa afya za Wananchi hususani kwenye eneo hilo lenye mkusanyiko wa Watu wengi, wahusika watambue wanahatarisha maisha ya wengi hasa ikitokea kukaibuka magonjwa ya mlipuko.
photo_2025-01-17_07-56-31.jpg

photo_2025-01-17_07-56-29.jpg

photo_2025-01-17_07-56-28.jpg

photo_2025-01-17_07-56-27.jpg

Pia soma:
~
Magari yanayobeba taka eneo la Tegeta-kwa Ndevu yanaleta kero ya foleni, wahusika wameshindwa kuliona hilo?
~ Taka zilizorundikwa barabarani eneo la Tegeta Kwandevu zimezolewa, sasa iwekwe mifumo rafiki ya kuhifadhi taka
 
Duh hatari sana na kipindupindu hiki
 
Mjini kuna mambo.poleni
KAZI ni kipimo cha UTU
 
Back
Top Bottom