Eneo lile lile: 1998 Magaidi walilipua ubalozi wa Marekani wananchi wakakimbilia kushuhudia leo kaibuka Hamza watu wamekimbia!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Haya ni maendeleo makubwa kwa wananchi kuanza kuelewa maana ya hatari na kuikimbia badala ya kuikimbilia.

Mwaka 1998 ulipolipuliwa ubalozi wa Marekani eneo hilo hilo alilokuwa anatamba Hamza jana wananchi kutoka maeneo ya jirani walikuwa wanakimbilia eneo la tukio kadri milipuko ilipoongezeka ili kushuhudia kwa macho yao.

Jana ilikuwa tofauti maana hata madereva waliacha magari yao na kukimbilia kusikojulikana.

Labda ni kwa sababu ya teknolojia.

Mungu ni mwema wakati wote!
 
Hamza alishikilia hill eneo kwa dakika 30 akiwatafuta police wenye uniform
 
Mkuu unaona raha kuanzisha thread? Huwa huoni hata aibu? Au kuna malipo unayapata kwa kuanzisha thread?
 
Haya ni maendeleo makubwa kwa wananchi kuanza kuelewa maana ya hatari na kuikimbia badala ya kuikimbilia.
Aise tukio hilo nna historia ndefu sana
Wakat wa tukio linatokea 1998

Ova
 
Pale alipolala Hamza picha inaonyesha Ubalozi wa Ufaransa mbele. Picha ingechukuliwa upande wa pili wa barabara ingeonyesha Ubalozi wa Marekani( wa zamani). Kwa hiyo ugaidi umetokea sehemu moja mara mbili. Yaani wewe ungekuwa umesimama pale alipolala Hamza siku ya Agosti saba,ungekufa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…