Eng Hersi Said Simamia Misingi ya Kanuni na Sheria za Mpira. Mshauri Rais Samia asivuke Mipaka

Eng Hersi Said Simamia Misingi ya Kanuni na Sheria za Mpira. Mshauri Rais Samia asivuke Mipaka

Wamemuuza Fei Kwa chembe ya ubwabwa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] wamuuze wapi?? Anatokaa akiwa free, na mama mjanja alishajua wakati wa usajiri ni huu, ngoja waje ikulu niwapige kwenye mshonooo.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Fei yuko huruuu.
 
rais katoa ombi hajaelekeza wala kulazimisha,yanga watamwita fei na waongee ili wamuuze au alipe gharama za kuvunja mkataba
Kwani kaitwa mara ngap hataki kwenda? Shida Feisal anaamini anaweza kufanya mambo ye mwenyewe bila kukaa na Yanga! Kitu ambacho hakiwezekani
 
Waarabu wapemba hujuana Kwa vilemba...!!
Maza kamaliza kesi Jana[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]
Amemaliza kikatili sanaaa, watu hata pilau halijafika tumboni, mama akawapa kichefu chefu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Hawajui watapike au wamezeee. Nomaaaaaah
 
Gharama za Algeria na kurudi = 200,000,000
+
Ndege hadi Mbeya 30,000,000
+
Ubwabwa wa Ikulu = 20,000,000
+
Goli la Fainali kwa Mkapa = 20,000,000

Jumla = 270,000,000

Gharama za kumuachia Feisal Salum = 270,000,000

P.S. Feisal ataambiwa hata ile pesa aliyotakiwa kurudisha ili avunje mkataba amesamehewa abaki nayo. Kabla msimu haujaisha rasmi, Feisal atakuwa ameanza mazoezi Bunju.
Jidangaye
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] wamuuze wapi?? Anatokaa akiwa free, na mama mjanja alishajua wakati wa usajiri ni huu, ngoja waje ikulu niwapige kwenye mshonooo.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Fei yuko huruuu.
Kuwa free si anunue mkataba wake! Kwani lini limepingwa na Yanga? Si walishasema kama yupo tayar kuondoka ye mwenyewe aje tuyajenge
 
Habari wanajamvi.

Leo amesikika Rais wa Tanzania Akimdadavulia Rais wa Yanga SC Bw Eng Hersi Said kwa lengo la
kumuhimiza ahakikishe Mchezaji Feisal Salum anapata haki yake.

Ninacho fahamu kuwa Mama Samia hana ufahamu sahihi wa kinacho endelea baina ya mgogoro uliopo kati ya Yanga SC na Mchezaji husika. Hisia zake kama Mzanzibar ndizo zimempelekea kusukumwa kutoa mapendekezo yake pasi na kuhitaji kulifahamu zaidi swala hilo.

Ndugu Hersi Said, unapaswa kucheza karata zako makini mno kwenye hilo. Kumbuka Mama Samia ametumia gharama kiduchu sana kwenye kampeni ya zawadi za kila goli, Dinner la Ikulu pampja na usafiri wa ndege. Kumbuka hajafanya haya si kwa mapenzi ya dhati na masuala ya michezo, bali alilenga zaidi kuilaghai taasisi ya michezo ili iache kusimamia misingi ya kisheria na kikanuni ya michezo.

Kwa kawaida, ni muhimu kwa Rais wa nchi kuzingatia majukumu yake kikatiba na kutofautisha majukumu ya mamlaka nyingine za kiserikali na taasisi mbalimbali. Mgogoro kati ya klabu na mchezaji ni suala la kisheria ambalo linapaswa kusuluhishwa na mamlaka husika za sheria na kanuni za michezo.

Rais Samia Anahitaji Elimu zaidi.

Kwa hiyo Rais wa nchi kuingilia kati ktk mgogoro kama huo unaweza kusababisha mchanganyiko wa majukumu na kuingilia uhuru wa mamlaka nyingine. Ni muhimu kwamba kila mamlaka ifanye kazi yake. Kitendo cha Rais kuwapa Incentives mbalimbali basi isiwe sababu ya kuhalalisha kuingiliana ki mamlaka katika mihimili inayo jitegemea kiutendaji.

Rais Samia anahitaji mrejesho, Basi ni wasaa sahihi kuhakikisha anaandikiwa mrejesho wa kumuelimisha kuwa masuala ya migogoro ya kisoka/kimpira yana namna yake ya kutatuliwa. Muelewesheni kuwa zipo sababu za msingi kwanini hili suala linakawia kufikiwa tamati.

Ni vyema akafahamu kuwa uvunjwaji wa taratibu na mchezaji yeyote wa klabu ni lazima kuadhibiwe pasi na kujali kama huyu ni mchezaji wa kizanzibar, wa bara au wa kimataifa. Na hukumu kwa mchezaji wa namna hiyo hautotokwa kwa upendelea wa kibusara eti kwa kisingizio kuwa mchezaji ni mzawa au la.

Mshaurini Rais kuwa licha ya kuyafurahia mafanikio haya madogo ya klabu, kuna watu nyuma ya pazia ambao wanawekeza pesa zao na wasingependa kuona wanapata hasara ktk biashara ya mauzo ya wachezaji. Tukiruhusu kuingilia maamuzi ya taasisi huru ambazo zina sheria zake za usuluhishi basi tunajiweka katika nafasi ya kuwafukuza wawekezaji aina ya wakina GSM na Mo Dewji katika mpira wa Tanzania.

Kuna madhara makubwa sana endapo klabu kama klabu itashindwa kusimamia misingi ya taratibu zake na kusuluhisha migogoro na kesi za kimpira kwa kutumia tu mapendekezo ya wana siasa. Je Mama Samia anatoa ushauri kama nani? Je ni kama mtu mwenye ufahamu wa kanuni na taratibu za uendeshaji wa mpira? au Kama
Endelea kumdanganya..

NAANDIKA KWA HERUFI KUBWA....UKIMTOA MUNGU KWA KATIBA HII TULIYO NAYO ANAFUATIA RAIS WA NCHI.....
 
Nyie si mlisema Fei ana haki sasa hamuoni umuhimu wa kutafuta haki kwenye mamlaka za kisoka ili waliomfanyia dhuluma waadabishwe ?
Sisi lengo ni yeye atoke hapo Utopoloni iwe kwa sheria au kinguvu.

Nyinyi ndio mkajidai wasiamamia misingi eti mnalinda brand.

Haya sasa Raisi katoa amri hakuna cha brand wala brandina hapo ni utekelezaji tu.
 
Hana ubavu wa kusimamia misingi wakati hela za kuendeshea Yanga zinatoka Msoga ndio maana wameitwa ikulu kwa sababu kuna rimoti pale Msoga inacontrol kila kitu
 
Usiseme; "Rais hana ufahamu wa kinachoendelea baina ya mgogoro uliopo kati ya Yanga na Faisal"

Rais ni taasisi,anapata information zote,mpaka kufikia kuliongelea hilo,ujue anazo info zote.
Rais wako hana uwezo wa kufalia mambo na kuyachakata! Angekuwa anazo taarifa sahihi basi hiyo issue wala asingeiongelea labda angekaa kimya tu! Kwani hajui kuwa vyombo vya maamuzi vya kisoka ambavyo vipo kwa mujibu wa taratibu za kisoka vilishakaa na kuamua? Yeye kwanini apeleke pressure kwa Yanga na sio kwa huyo mchezajj mwenyewe ambae anataki aufuate taasisi yake wakamalizane?
 
Amemaliza kikatili sanaaa, watu hata pilau halijafika tumboni, mama akawapa kichefu chefu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Hawajui watapike au wamezeee. Nomaaaaaah
Vya Bure ghali siku zote
Mpk mda huu fei 3 yanga 0
 
Kuwa free si anunue mkataba wake! Kwani lini limepingwa na Yanga? Si walishasema kama yupo tayar kuondoka ye mwenyewe aje tuyajenge
Mbna walirudisha zile 112M baada ya kuingiziwa kwa ACC yao?? Au huna kumbu kumbu??

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] imeishaaaa hiyooooo
 
Tena Waambie No free lunch/dinner in Africa specifically Tanzania
[emoji1][emoji1][emoji1][emoji849]Tena tajiri kaambiwa habanwi banwi Sasa ajishaue aone [emoji1][emoji1][emoji1]
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] wamuuze wapi?? Anatokaa akiwa free, na mama mjanja alishajua wakati wa usajiri ni huu, ngoja waje ikulu niwapige kwenye mshonooo.

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Fei yuko huruuu.
Hivi kweli dogo kawa huru na ni msimu wa usajili [emoji3][emoji3] Ubwabwa umewagharimu Uto
 
Amemaliza kikatili sanaaa, watu hata pilau halijafika tumboni, mama akawapa kichefu chefu [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

Hawajui watapike au wamezeee. Nomaaaaaah
Siku nyingine wakiitiwa ubwabwa tena Ikulu hawaendi,wamejifunza vya bure ni gharama pia [emoji3][emoji3][emoji3]
 
Walikuwa wanafakamia masotojo wakajiona wameyapatia maisha kuliko Simba.Wamepigwa ndoige moja tu ya Feisal sasa wamepoteana na pilau lote limekuwa chungu[emoji3][emoji3]
Wanajutaaaa kiherehere Cha vya Bure
Hapanaa chezeyaa mama ndo kashasema na anataka mrejesho
 
Back
Top Bottom