Eng. Hersi Said usitumie lugha hii tena kwenye usajili

Hivi kweli mleta mada uko serious au unatania?.
Kwahiyo ulitaka Yanga wakisajili kwa mfano mshambuliaji walete mwenye kiwango sawa na mayele au aliyezidiwa kiwango na mayele?.

Unapofanya usajili ni lazima ulete mchezaji mzuri kuliko anayecheza nafasi husika!,sasa hapo kosa la Hersi ni lipi?

Kwahiyo wewe utakuwa na furaha kuona Hersi anasema ataleta mchezaji ambaye hana kiwango kama cha mchezaji aliyepo?
 
Hersi inabidi asaidiane na Mama Mwaikenda kama Vice/Deputy wake. Nimemsikiliza jana bado ana mihemko ya ujana. Vilabu hivi viwili vinahitaji sana busara na uzoefu.
 
Hahahaa inachekesha sana Simba wamegeuka kuwa washauri kwenye uchaguzi huu wa Yanga Ukiangalia wengi wanaoleta agenda zao humu ni majamaa wa Simba.

Kosa la injinia Hersi Said Mr President ni lipi Mbona tunaona makocha Ulaya wanasema Mchezaji flani kiwango kimeshuka Soka limekua zile dhama za kubembelezana zimeisha.

Ni ukweli usiopingika lazima usajili mchezaji mwenye kiwango zaidi ya aliyepo ili kuleta ushindani mfano Yanga hatuna winger wazuri so Morrison is Better than Chiko na Moloko.

Simba tulieni bana.
 
ndio uwezo wako unapoishia. Yaani unamwambia mke wako kuwa nitaoa mke mwingine mzuri na mwenye akili na kujua kupika kuliko wewe. Hiyo labda huko Somalia, congo na kwingine ambako kupigana sio jambo la kutisha sana
 
Kama uwezo umeshuka humpi mkataba mwingine, unamuondoa taratibu bila kusema maneno mengi. Unaweza kumuacha mchezaji ukidhani kuwa ameshuka lakini akaenda timu nyingine akakiwasha. Hivyo, huna sababu ya kumtangaza hadharani kuwa Lukaku kiwango chake kimeshuka. It is very very very unprofessional kusema nitasajili mchezaji bora kuliko Mwamnyeto. Wewe na benchi lako la ufundi fanyeni scouting zenu vizuri, mleteni kisha watu ndio watasema mpya ana uwezo kuliko wa zamani.
 
ndio uwezo wako unapoishia. Yaani unamwambia mke wako kuwa nitaoa mke mwingine mzuri na mwenye akili na kujua kupika kuliko wewe. Hiyo labda huko Somalia, congo na kwingine ambako kupigana sio jambo la kutisha sana
Sawa Mama
 
Sio Simba ni sisi wenyewe wananchi tunaoitazama timu yetu inakoelekea. Tunataka timu ambayo Haina viongozi wa kirafiki, kidini moja, jinsia moja, kabila moja Wala ukanda Wala uchama wa siasa.
 
Manara hata ana elewa basi ye anafuata upepo tu.
 
Mayele anajiona au nyie mashabiki wa Yanga ndio mnaye mkuza na kuonekana yupo juu sana kuliko hata George Mpole?
 
Yanga wenzio washakua mazuzu, kila anachofanya Hersi ni sawa kwao
Kiongozi mkubwa kama Rais anayo lugha yake ya kusema na ni Bora kuliko mwingine. Lugha yake Iko Kwenye mikataba Yao na malipo ya wachezaji TU baasi. Hizi lugha nyingine za mdomoni tuachie sie tuseme.
 
Yanga wenye akili ni kikwete,kavulata na babayangu(Manara,2021).umeongezeka kwenye listi[emoji23][emoji23]
 
Sidhani kama kimataifa pia wako vizuri, maana wasingelazimika kuwasha moto wa kishirikina uwanjani na kumulika vitochi usoni wenzao. Kifupi walitumia fitna za mpira kufika pale walipofika
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…