Sakata la Feitoto tunajua hizi ni njama za Simba kuivuruga Yanga kupitia pesa za Bakhresa mwanachama wao baada ya kuona Yanga inabeba makombe yote na kuipiga Simba kama mtoto yaani matajiri wa kariakoo furaha imekata mwaka wa pili sasa sura zinakunjamana na uzee unadhihiri , kila muda wana hasira, wanagombeza wafanyakazi ovyo ovyo , wanachapa watoto bila makosa ili kumaliza hasira za Simba kupigwa pigwa kama ngoma na Yanga!! Yani Simba ni ndondo cup ndio kunakowastahili, timu mbovu , viongozi wabovu. Matajiri wa kariakoo gubu limewakaba kuona kila kona jezi za Yanga tu watu wanajidai nazo mtaani kifua mbere!
Huyu Feitoto tunae miaka mingapi mbona matajiri wa chamazi hawakumtaka leo unbeaten 49 na tumeanza tena hesabu ya unbeaten 100 sherehe ikafanyike Arachuga basi makolo wamenuuuna! Hata Azam mumchukue Feisal halafu eti mumtoe kwa mkopo Simba kuiudhi Yanga haitawasaidia lile goli la karne alilowapiga CCM Kirumba litawauma miaka yenu yote hapa duniani! Na kichapo cha wananchi kwa kolo fc kitaendelea bila Feisal maana bado kuna bunduki Aziz Ki na Mayele!