Loan utapata , nikushauri kwa petroleum geology tena kuna sponsor hawa jamaa wa makampun ya mafuta, kwa mfano mwaka Jana wanafunz kum wa petroleum walipewa ufazili na swala, changamkia fursa kaka, hiki ni kipindi cha geology , c it tena,
Engineering geology in kozi ya geology ambayo lengo lake kuu ni kusaidia kutafsiri geology kwa ajili ya shughuli za ujenzi , uchimbaji madini( Open pits na underground mining) hapa tunaangalia (uimara wa kuta za migodi), kuangalia madhara ya majanga kama matetemeko ya ardhi(earthquake),maporomoko ya mawe (Landslide) , kudidimia kwa ardhi (subsidence) , uaimara wa mabwawa ya maji ( DAM stability) .
Engineering geology imeanza kufundishwa UDSM kuanzia muda mrefu tu ikiwa mojawapo ya kozi ya geology , lakini sasa ni kama kozi inayojitegemea.
Engineering geologist akiwa kama mtafsiri wa geology ,anatakiwa aijue geology vizuri ndipo aweze kutafsiri, lakini lazima ujue unatafsiri kwa ajili ya nini?kwa hiyo kuna pande mbili za engineering geology ,kwanza lazima usome kozi za geology uielewe na pili lazima uelewe engineering inakwendaje kwa hiyo utasoma kozi za civil engineering (muhimu ni Soil mechanics,material, foundation design,survey). kuna kozi moja ambayo ni muhimu kama Rock Mechanics zinafundwa kwenye idara ya geologia.
Kuhusu ajira- tangu kuanzishwa kwake kama kozi inayojitegemea, wanafunzi wameajiriwa sehemu tofauti tofauti, kuanzia kwenye makampuni ya mafuta hadi makampuni ya kuchimba madini, jiunge tu usiwe na wasiwasi na ajira.
Kwa kweli ni kozi nzuri ,itakayokupa changamoto kidogo ,lakini ndio kusoma huko.