Acheni ukabila kwani akiwa mhehe hapaswi kuimba? Ni wivu au nini?
Haka kanalazimisha fani tu muziki hakajui kazi kufanya remix tu mbovu mbovu
Bora auze bangi....
wanawake bana ndo zenu hakuna hata siku moja mkasifiana
Haka kanalazimisha fani tu muziki hakajui kazi kufanya remix tu mbovu mbovu
Bora auze bangi....
Kwanini angeandika kwa Kiswahili ikiwa anaamini na ama anahitaji mashabiki hadi wale wasiozungumza kiswahili? Kwa maoni yangu, ikiwa lengo lake ni kutangaza kazi yake basi yupo sahihi kutumia English.Dah....Si angeandika Kiswahili tu..
Kwanini angeandika kwa Kiswahili ikiwa anaamini na ama anahitaji mashabiki hadi wale wasiozungumza kiswahili? Kwa maoni yangu, ikiwa lengo lake ni kutangaza kazi yake basi yupo sahihi kutumia English.
Tatizo letu Watanzania ushamba umetujaa... yaani mtu akiongea ama kuandika broken English inakuwa ndio issue wakati Kiingereza ni lugha tu kama lugha nyingine yoyote duniani! Ule ushamba wetu wa kudhani mtu anayekifahamu Kiingereza yupo matawi ya juu ndio unaotusumbua! Jambo la kushangaza, hata ukiwaona hao ambao English ni native language, bado nao ni full broken! Watu tunashindwa kufahamu kwamba hata huyo Mwingireza ambae hajasoma English language nae ana uwezekano mkubwa wa kuongea ama kuandika broken! By the way, mbona tukiwaona Wazung wakipiga broken ya Kiswahii hatuwajei zaidi tu ya kuona ni funny?
NguoYaSikuKuu
bado watanzania hatuna identity ya muziki wetu..! na kama ipo bado saaaana!!miaka 25643!
Hivi mtu kama lina anapewa jukumu la kuitangaza nchi? Mbona mnampa jukumu kubwa sana? Aachwe aendelee kufanya mambo yake na kuitangaza pappuchi yake .hilo la kuitangaza nchi wala hapaswi kulauimiwa lina wenyewe na wamelala! Kuhusu kizungu mbona hata wazazi wenu hawakijui?..
wanawake bana ndo zenu hakuna hata siku moja mkasifiana
Video ni nzuri very good directing skills i didnt know that video was shoot in south africa! we are going far keep it up linah sanga.
Kuna vitu hayupo sawa, hata ile nyimbo jinsi ya kutamka maneno you are........ anatamka kama anaongea kibena,kihehe au kikinga. Lakini najua vinarekebishika tu, lakini watu wa humu kwenye forums wanamnanga tena wakikebehi hata kabila lake, kama tuna wema tumuelekeze pale alipokosea. Wengi wanaosema maneno ya ovyo unaweza kukuta hawana hata cha kujivunia zaidi ya kuendekeza porojo tu
Linah ni Msanii mkubwa tu wa Tanzania..Ila hii Description aliyoweka Youtube sio Nzuri!
Hapo kwenye RED english mbovu ,na sikudhani kama kulikUwa na maana wa kuiweka South Africa .
nadhani Anaitangaza South Africa zaidi na GODFATHER
Hivi we kilaza wanaijeria wapo juu sana kwenye moviesSaasa , unamrekebishaje na wimbo kashautoa ? na anadai katumia Milioni sabini? Si huwa kuna sijui wanasema 'listening party"? alikosa mtu wa kumwambia? tatizo Watanzania wenzangu pia ukweli unatuwia mgumu kuu handle na kuambiana lakini anayekukosoa na kukwambia ukweli huyo ni rafiki.
Mi kila siku nikisikia hiyo yuaaaayuaaaaa, yuaaamaidestiniiiiii yaani nakerekwa utadhani nalipia kusikiliza. Nasema jamani, hivi hapa alishindwa hata kuiweka tune iendane na hii lugha ya meli na ndege? au walau angeweka mtu mwingine kwani lazima uimbe wimbo woooote tangu mwanzo hadi mwisho? Mi mwenyewe ukinipa zile verse anavyoimba Ney wa Mitego zile ' heee wananiitaga honey, haaaa, jaribu kushindana nami siogopi haaaa' ( kama anahema kama analima kwenye ule wimbo wake wa Mr Ney) hata unipe milioni hamsini siwezi kukita vile.
Sasa unaimba kiingereza na maneno ya kiingereza unaimba yuaaaaayuaaaaaa ! kaaah jamani.
tusifie palipo pema lakini tukosoe ukweli ili tusonge mbele.
Video nayo ni Mafikizolo tupu, hakuna ubunifu kivile. Kwa maoni yangu 'mbuzi' kwa ile beat ilipasa kiuno kizunguruke fasta maana ni beat ya faster, sio ule uvivu. Na pia, hakuna link kati ya akupendaye hakuachi hivihivi na ile benzi, mara kiti kama cha ufalme wa kale wa Rumi na wale wachezaji wa kilugha... where are the connecting dots?
Samahani lakini kwa para ndefu ila kiukweli!! Yaaya bagosha!
Wala usisumbuke kujibizana nao. Hao ni vijana wa ufipa bange na viroba imekua sehemu yao ya maisha.
Ni mpumbavu pekee anayedhania kuandika broken english ni ujinga
Alicho andika lina hakuna mtu anayejua kiingereza asijue anamaanisha nini
Kama mtafiti kidogo jaribu kutembelea fb page, tweeter na insta za wasanii wakubwa duniani ambo hawatoki nchi zinaongea kiingereza uone wanavyo chapia, but all in all ujumbe ufike