Enyi Serikali hivi vifo visivyoeleweka vya Watanzania wenzetu huko Nje ya Nchi, Muwe mnavifatilia, kila Nafsi ya Mtanzania iwe yenye thamani

Huko OMAN washaambiwa sana
Kuhusu kwenda huko ila hawasiki,hawakomi

Ova
 
Sad. Apumzike kwa amani.

Kabla ya kwenda huko wahusika huwa wanazingatia ushauri wa serikali? Serikali imesema sana watu wachukue tahadhari hasa hizi kazi za ndani huko arabuni.

Wahusika wakifika huko nje huwa wanajitambulisha ubalozini au kutambulika kwa wawakilishi kwa namna yeyote ile?

Nimesikia time and again watu wakisema hawataki ukaribu na wabongo wenzao au ubalozi wawapo ughaibuni. Wanasema wabongo wanoko, wanafki, hawasaidiani nk. Kujitenga si dhambi ila unapoamua kufanya hivyo pia kubali kubeba msalaba wako mwenyewe kwa kila jambo.
 
Kwanini nchi isizuie wananchi wake kwenda kuwa house maid huko nchi za kiarabu?

Na ikiwa wamekubali kupeleka watumwa huko badi waweke sharti la mtumwa kuwasiliana na ubalozi angalau mara moja kwa mwezi kumsikiliza, kama mazingira ya kazi ni mazuri, na treatment kwa ujumla, na iwe tayari kumsaidia kurudi nyumbani muda wowote kama mazingira ya kazi hayamridhishi kwa namna yoyote ile.

Wengi ninewasikia wakilalamika mitandaoni, baada ya kurudi nyumbani, kenya au Tanzania, kwamba mazingira kule siyo salama kabisa, manyanyaso, na mateso ni mengi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…