Enzi zetu Serikali ilikuwa inawasisitiza wazazi wawaruhusu watoto kurudi Shule kwa masomo ya ziada, eti leo hii inapiga marufuku

Enzi zetu Serikali ilikuwa inawasisitiza wazazi wawaruhusu watoto kurudi Shule kwa masomo ya ziada, eti leo hii inapiga marufuku

Kingsmann

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2018
Posts
4,805
Reaction score
17,850
IMG-20211201-WA0000.jpg


Tangu lini Serikali yetu ikaanza kujali Afya za Watoto kuliko viwango vizuri vya ufaulu? Hii haijawahi kutokea na haitakaa itokee, tuache siasa kwenye mambo ya msingi, tusiue sisimizi kwa rungu, tutafute solution ambazo hazitawaweka kwenye wakati mgumu walimu wetu (maana watoto wakifeli serikali hii hii huwa inawaangushia zigo wao utafikiri waliofaulu na waliofeli kwenye shule na darasa moja walikuwa wanasoma madarasa tofauti kumbe ni darasa moja).

Sababu kubwa ya watoto kuumia migongo ni hizi 2:

1. Serikali kuongeza masomo(hasa shule za msingi). Enzi zetu tulikuwa na masomo 5 tuu(Kiswahili,English,Sayansi, Hisabati na Stadi za Kazi), wakati sasa kuna masomo 10+.

2. Walimu kulazimisha watoto wanunue counter books badala ya zile daftari nyepesi. Enzi zetu shule ya msingi hakuna aliyekuwa anatumia counter books, hata sekondari ilikuwa siyo lazima kutumia counter books. Mimi mpaka leo nina daftari zangu za sekondari ambazo nyingi ni zile nyepesi, counter books ni chache sana.

3. Walimu kulazimisha wanafunzi kubeba daftari zote waendapo shule badala ya kubeba zile tuu ambazo ratiba ya masomo inaonesha. Unakuta siku hiyo kuna vipindi 4 lakini mtoto analazimishwa abebe counter books zote 10 badala ya 4 tuu.

Hivyo naisihi Serikali na walimu wetu waache siasa kwenye elimu na watafute solution bila kutingisha status quo iliyopo, elimu yetu bila masomo ya muda wa ziada ni ngumu sana watoto wetu kupasua.

Mbona mnawapa homework kama hamtaki wasome muda wa ziada? Kama ni hivo basi pigeni na marufuku walimu kutoa homework, maana zinawatesa sana watoto wanashindwa kupumzika na kuwa na afya njema, si mnajali sana afya bwana!!!

Na nyie madaktari mna vitu vingi sana upande wenu ambavyo vinawashinda, acheni kuhangaika na mambo ya elimu. Ama hamtaki nawanetu wasome kwa bidii wawe madaktari kama nyie?

Huu ushauri wenu utafutieni njia sahihi ikiwemo kuiambia serikali na walimu wapige marufuku counter books maana ndizo zinazoua migongo ya hao watoto mnaojifanya mnawajali sana.

IMG-20211125-WA0016.jpg
 
Pole Mwalimu! Kweli Watoto wanateseke bila sababu za Msingi, hizi Tuition zimezidi, Muda wa Mapumziko ni vizuri ukatumika kwa mapumziko
 
Nakumbuka kipindi nipo form 5 tulikuwa tunaenda mpk siku ya jumapili.

Unaingia shule saa 1 na 30 mpaka saa 1 na 30 usiku ndiyo unatoka.

Watoto wanahitaji mapumziko. Pamoja na kusoma sana lkn bado tuna umeme na maji ya mgao.

Waliofanikiwa kuingia bungeni, wanaangalia matumbo yao.

Vitu vinapanda bei lkn mshahara uko pale pale. Leo hii mawasiliano ni anasa

Hiyo elimu ya kusoma bila mapumziko ina faida gani?
 
Hii limekaaje kwani, ebu nipeni maelezo yasio na mzunguko


Watoto wa advance hasa combination hizo hapa PCM/PCB/PGM/EGM/CBG
itawaumiza sana
 
Upo sahihi kwa asilimia kubwa ila watoto wanahitaji mapumziko jamani. I mean...watakuja kupumzikaga lini tena?? When will they be allowed to be just kids??? We are robbing these kids of their childhood and it's not fair hata kidogo!

Watoto wanakuwa overloaded na vitu ambavyo hata hawapewi muda wa kuvi-digest. Mwisho wake wengi wao wanaishia kukariri....yani for the most part wanakaririshwa na sio kwamba wanafundishwa ili kuelewa wanachojifunza. Na ndio maana mwaka huu matokeo yamesua sua kwasababu mitihani ya taifa ilikuwa competence based.

I really wish hizi shule zingekuwa na ratiba za kueleweka....mwalimu, mwanafunzi & mwanafunzi wote wawe wanajua kinachofundishwa Monday mpaka Friday...that way watoto wanabeba vitu wanavyohitaji tu kuendana na ratiba.
 
Nakumbuka kipindi nipo form 5 tulikuwa tunaenda mpk siku ya jumapili.

Unaingia shule saa 1 na 30 mpaka saa 1 na 30 usiku ndiyo unatoka.

Watoto wanahitaji mapumziko. Pamoja na kusoma sana lkn bado tuna umeme na maji ya mgao.

Waliofanikiwa kuingia bungeni, wanaangalia matumbo yao.

Vitu vinapanda bei lkn mshahara uko pale pale. Leo hii mawasiliano ni anasa

Hiyo elimu ya kusoma bila mapumziko ina faida gani?
Kwa sasa hata hiyo elimu mnataka kunyimwa ili watoto wenu wakose reasoning.

Tuache watoto wapewe elimu kadri ya uwezo wao, ili waweze kuexplore their full potential.
 
Wanafunzi wa primary wakipumzika ni sawa sio wa sekondari ,kwa sekondari mziki ni tofauti ,Wanafunzi wa shule za serikali sekondari ,wakipumzika baada ya muda wa masomo ,wa shule binafsi wanacover syllabus ya form 4 wakiwa form 3 na form 2 wakiwa form 1 ,matokeo ya form FOUR na Form TWO yanaonyesha tofauti ya wanaopumzika hovyo hovyo na wasiopumzika .Nimetoa mfano rahisi tu
 
Wanafunzi wa primary wakipumzika ni sawa sio wa sekondari ,kwa sekondari mziki ni tofauti ,Wanafunzi wa shule za serikali sekondari ,wakipumzika baada ya muda wa masomo ,wa shule binafsi wanacover syllabus ya form 4 wakiwa form 3 na form 2 wakiwa form 1 ,matokeo ya form FOUR na Form TWO yanaonyesha tofauti ya wanaopumzika hovyo hovyo na wasiopumzika .Nimetoa mfano rahisi tu
Kwa hio unaishauri serikali iunganishe syllabus ili wawahi kuimaliza eti ?
Du ! Mwafrika hajawahi kuwa na akili timamu.
 
Hili la Barakoa limemshinda waziri wa afya sembuse wewe katibu mkuu wa elimu!! Tatizo ni kwamba tunatishiwa na tishio la kufikirika!! mabeberu wako kwenye biashara ya chanjo na barakoa!! Mzee wa watu anatumika kama wakala bila kujielewa!! Asante JPM uliacha umetufumbua macho, hawa mawakala wa mabeberu kwa kujua au kutokujua wanatwanga maji kwenye kinu!! Hachanjwi mtu hapa!!
 
Back
Top Bottom