EPA na mambo yake

Nimesoma post za Muheshimiwa Zitto.

Kwa kweli huenda huyu kijana akawa Obama wetu siku za usoni!

Kwanza nakubaliana naye kabisa kwamba taifa letu linahitaji composition ya national assembly ... kuwa ruling part from 60%-70% na opposition 40%-30%... Hii ndiyo imekuwa hoja yangu milele regardless chama kitakachotawa kinaitwa shetani au malaika.

Kitila utakumbuka haya ndio niliyokueleza siku hile pale Dar es Salaam tulivyokutana kwa moja baridi moja moto.

Tena kwa kufanya mambo yawe matamu zaidi kusiwe na chama ambacho kinaweza unda serikali chenyewe... iwe lazima kitafute mshirika... e.g... chama chochote individually kisiwe na wabunge ambao ni zaidi ya 45% ya wabunge wote. Au kura za urais zaidi ya 50%

with the above composition we shall have health democracy which can bring change to our beloved nation.

Other than that maigizo tu!
 
Hivi is these for real ama changa la macho maana hii serikali yetu siyo ya kuwaamini hata kidogo!
 
hawatoleta chochote.. the only thing that is gonna happen is them being tried and convicted as per the evidence, which in this case is substantial in the sense that the plot was successful and the only thing left to be determined is the level of their involvment, if any... Due to the nature of the said crimes, it is in all likelihood that there is a good amount of documentary evidence implicating the suspects, considering the fact that they authorized the payments in collusion with kina-jettu&co. So lazima watafungwa tuu.

As a lawyer i'm certain that they will have a hard time raising doubt as to their guilt.. The likely defence is probably that 'They did not collude with the criminals and that they were unaware of the forgery' if they can raise that defence to a substantial level then wanaweza get away. But the public policy considerations make that unlikely too.. maybe a few of them will but not all under any circumstances..
 
Kinyambiss kati ya wote watakaofikishwa mahakamani, kesi ya hawa wanne ndiyo ya kuiangalia kwa ukaribu zaidi...
 
Dhamana ni haki ya kila Raia. Kama sheria zikitumika bila woga, haki itatendeka tu na watakaothibitika kuwa ni wakosaji watafungwa. Uchungu tulionao usitufanye tukikuke misingi ya Haki za Raia. Dhamana ni Haki na acha wapate kama wakitimiza masharti

Dhamana ni haki ya raia kwenye haki haki ya raia. Sheria zilishapindwa toka siku wameanza kubembelezwa kurudisha hela kwanza na kwa msingi huo haki ni vigumu kuamini itatendeka. Uchungu ni kweli tunao na tunajua wazi walioathirika kwa namna moja ama nyingine na vitendo vya hawa wezi (wengine kufa kwa kukosa dawa) - wao je hawakuwa na haki ? Wangapi wameswekwa rumande kwa kukosa dhamana, je wao hawana haki ? Kwa nini dhamana ihusishwe na nusu ya fedha walizokwiba, na si hujuma walioifanyia taifa na watu wake ? Hela za dhamana zinatoka wapi kama sio hizo hizo za wizi ambazo hakuna shaka zimezaa faida hata mara tatu. Kwa nini kiasi cha dhamana kisijumuishe na riba. Hapana Mh. Zitto hapa hamna cha haki wala sheria.
 
Press nayo inaonyesha kuridhika na hatua za serikali dhidi ya "vigogo."

Tanzania Daima linadhani linafanya kazi nzuri hapa kwa kuonyesha kwamba vigogo wa CCM nao walikuwemo kwenye ufisadi, lakini wanavyo i-cover story, mwananchi ambaye hayuko well-informed anaweza kuamini kwamba 1) huyu mtu kweli ni "kigogo" 2) Serikali inafanya kazi nzuri ya kukamata pia vigogo 3) vigogo wakweli -the Mgonja's and Mramba's of the world - hawakuhusika.

Crummy press!
 
EPA yakumba vigogo BoT
Shadrack Sagati na Mariam Mogella
Daily News; Friday,November 07, 2008 @19:01

 

Kuhani, waandishi wetu wakati mwingine huweka ushakibiki mbele kuliko ethics za journalism, shinda nyingine wengi ni maripota rather than waandishi, nadhani huyo ripota hajui kigogo ni yupi!
 
Jumla ya watuhumiwa 17 wakamatwa wizi wa mabilioni ya EPA
* DPP asema hakuna maneno, ni vitendo tu
Na Pauline Richard na Ramadhan Semtawa

Source: Mwananchi
 
Kuhani, waandishi wetu wakati mwingine huweka ushakibiki mbele kuliko ethics za journalism, shinda nyingine wengi ni maripota rather than waandishi, nadhani huyo ripota hajui kigogo ni yupi!

Mbali ya ushabiki, either hawajui kuchagua vichwa vya habari au wanaweka makusudi kichwa habari wanachoona kitavutia watu kununua gazeti. Lakini gazeti la Tanzania Daima linanunuliwa sana, hawana sababu yoyote ya msingi ya kuweka vichwa vya habari vya kuwadanganya wananchi, Hivi Wahariri kazi yao ni nini? Mhariri wa Habari ama hata Mhariri Mkuu wa Tanzania Daima hawezi akarekebisha kichwa cha habari pale kinapoonekana hakitoshelezi?
 

..........FP je unakumbuka Makubo style............na Sembe Chapa Jogoo?.......this time...labda JK mwenyewe aamue kula shubiri........lakini kwa ushahidi uliopo haponi mtu........
 
innocent until proven guilty.....
Ndio maana bail ni haki. Na kama wana wakili mzuri anaweza aka question iyo bail amount iliyowekwa, maana inakuwa sawa na kuwanyima bail. The amount is too high, assuming they are innocent they wouldnt have that much

Mrembo karibu sana jamvini.

Hapo juu Mrembo kweli umeniacha hoi...Hii lazima ni style ya cat walk hiyo maana warembo mambo hayo mnayajuwa zaidi.

Kweli Mrembo tunaweza ku assume kwamba watuhumiwa wako innocent na wamesingiziwa kuwa walichukuwa pesa hizo za EPA.

Hata hivyo mrembo naomba nikukumbushe kuwa uwezekano huo ni finyu sana kwani ushahidi uko wazi na kama ni kusingiziwa basi hawajasingiziwa...Tofauti inaweza kuwa kwenye technicalities tu..Lakini kama ni makosa wamefanya.

Pia amount ya bail kuwa juu inawezekena kushushwa kama unavyodai endapo utaendelea ku assume kuwa pesa zilitochotwa ni ndogo sana.
 
Kama Johson alirudisha hela mpaka akashindwa kurudisha amepata wapi hizo za kujidhamini???????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! !!!!!!!!!!

Mwenye akili afikirie mara mbili.

Mkuu heshima yako, ni kwamba familia ya Lukaza, wanazo hela hata kabla huyu bwana mdogo hajaingia ufisadi, ndio maana ndugu zake ambao nimeongea nao sana wiki hii wanasema hawaelewi nini hasa kilichompeleka huko BOT,

Baba yake alikuwa kibopa toka enzi za awamu ya kwanza, ndugu zake wote ni vibopa longtime, tena wote wake kwa waume, ni yeye tu aliyezidisha tamaa na sasa amechafua sana jina la baba yake na la familia yake kwa ujumla, bila sababu ya msingi wakati wao ni watu wa pesa siku zote, hiyo dhamana ambayo ni ndogo sana wka ndugu zake anaweza kua amelipiwa na sister wake mmoja tu na sio ndugu zake wote, I mean mnyonge mnyongeni lakini haki apewe.

Bwana mdogo aliichokoza serikali yeye mwenyewe, pale aliposhusha Range kwenye ndege ya British Airways, akimuiga Joemaro, hakujua kua huyu ni mkwe wa mkapa!

Tuliambiwa watuhumiwa wa EPA hawataenda mahakamani kwa sababu rais anawaogopa hawa, maana aliiba nao hela za kampeni, sasa hawa wako kizimbani, dhamana ni haki ya kila mwananchi kulingana na makosa yake kisheria, tayari tumeshaambwia kwamba hili ni kundi la kwanza tu, baadye linakuja na lingine la wakubwa, wallahi kuna mtu mzima hapa yupo hatarini, maana according to the dataz hata kesi wa wakulu wa Kiwira ipo tayari na pending.

Dawa ni kuvuta popcorn na kuiachia sheria ichukue mkondo wake.
 

Thanks Zitto,

ila kumsifia DPP wakati serikali haijashinda kesi hapo BIG NO.......Inawezekana kaona wanakesi ya kujibu ili mahakama iwasafishe....Kuwa makini hapa...
 
Mkuu Field Marshall ES, nakuaminia kwa data lakini kwenye hilo la Kina Lukaza uko nje mno ya ukweli.

Ni kijana mwenzetu na mimi binafsi sababu namfahamu toka miaka ya 80, namwombea yeye na familia heri na baraka na apate unafuu na kuepuka jail time. Ni mawazo binafsi tu.
 

...mkuu polepole na tusiharibu taratibu za demokrasi yetu kwa emotions zetu,fair trial kwa raia wote ndani ya jamhuri ndio maana ya uhuru,acha wajitetee,wapewe lawyer wa kuwatetea na dhamana ambayo ni reasonable,hakuna haja ya kukomoana lazima taratibu zifuatwe no matter what happened ili kulinda haki ya kila mtu!
 

Labda kama wako wawili, lakini ninayemjua familia yake iilikuwa inaishi Upanga, dada yake ambaye ameolewa na mshijaki wangu mmoja wa primary school anamiliki kampuni kubwa sana ya Tele/Communications pale jengo la CRDB, na kaka yake mwingine anamiliki kampuni kubwa sana ya kupeleka watalii mbugani kule Arusha na nikiwa majuu nimemsaidia sana kuwaelekeza watalii kwake, I mean a I can go on and on, unless tunawawaongelea Lukaza wawili tofauti!

Hizi sio dataz, ila ni ukweli wa kawaida tu wa familia ninayoifahamu na ndio maana nimekua kwenye communication nao wiki hii nzima, that is all sikusema hizi ni dataz, lakini unakaribishwa sana ila tu yasiwe yale yale maana tayari naona harufu!

Thanxs!
 

Mkuu sasa umejileta wala sikuachii huyo kaka yake mkubwa anaitwa Emanuel Makubo na yeye ndiye aliyemfundisha huo ufisadi
Huyu makuba waliibaga pamoja na Chavda wakati ule
Hamna cha kuwasifia ukoo wao wote wezi tuu Johnson mwenyewe keshafungwa Mwanza Kwa wizi
Hamna lolote zaidi ya kujikuza tuu si unajua mabwenga walivyo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…